Mtu mwenye matokeo haya form four utamshauri asome nini?

Joseph Kasa-Vubu

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2014
Posts
356
Reaction score
550
Kuna dogo kapata matokeo yafuatayo katika mtihani wa form four- 2021 na hataki kwenda advance.

Civics- C
Geography- C
History- C
Kiswahili- B
English-C
Biology-C
Chemistry-C
Physics- F
Maths-D.
Yeye anapenda kwenda chuo kozi za sayansi. Je ni kozi gani anaweza chaguliwa.
 
Hapo labda diploma ya phamacy tatizo ameharibu physics angepata hata D
 
Angefaulu physics tu angesoma koz yoyote
 
Akasome geomatics, forestry au urban and regional planning
 
Dahh Physics imemuharibia kidogo sana, angekula ata D ya Physics hakuna course ya science angeshindwa kusoma

Muulize kwanza yeye anataka kusoma nini au anapenda nini na baada ya hapo unaweza kupata mwanga, hizi habari za kumchagulia mtu kitu Cha kusoma Waga kina changamoto zake pia
 
Mpe hongera kjana kwa ufaulu mzur sana[emoji120]. Ni wazo zuri sana kutotaka kwenda Advance japo Vyuo ni GHARAMA. Yangu ni haya matatu (3):

1. Me ninge mshauri asome kozi ya Afya (PHARMACY) kwa sababu ya ufaulu wake wa masomo kwa ngazi ya kada ya Afya.

2. Asomee kozi za CHUO CHA VETA ambazo zina uhitaji sana katika jamii mfano: Fundi mwashi, umeme, ushonaji, uchomeleaji, utengenezaji wa magari, pikipiki na mashine.

3. Kaa na kuzungumza na kjana vzuri inawezekana kuna kitu anataka kusomea au anakipenda kukifanya, mshauri mpe na idea mbalimbali zaidi za maisha mfano: labda anapenda kuwa MWANASHERIA au MWANAJESHI even MSUSI.


YANGU NI HAYO TU. HOPE ATAPATA KITU KIZURI CHA KUSOMEA AMBACHO KITAMSAIDIA KATIKA FUTURE YAKE[emoji120]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…