Mtuhumiwa wa mauaji ya Kware akamatwa, akiri kuua wanawake wasiopungua 42 ikiwemo mkewe

Mtuhumiwa wa mauaji ya Kware akamatwa, akiri kuua wanawake wasiopungua 42 ikiwemo mkewe

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
atRktkpTURBXy8wMmFiNjQ3NTU5MjRiZTQyMWUzNjk5YTdjZWI0OTI2NC5qcGeSlQMAAM0DhM0B-pMFzQSwzQJ2.jpg

Taarifa za sasa zinasema Muuaji wa Watu waliokutwa kwenye viroba huko Kware amepatikana na anahojiwa na Polisi kujua asili yake na sababu za kufanya Mauaji hayo.

Source: Citizen TV

====

DCI nchini Kenya, Mohamed Amin amesema mtuhumiwa aliyekamatwa ,auaji ya Kware, Collins Khalisia mwenye umri wa miaka 33 kutoka Vihiga amekiri kuua wanawake wasiopungua 42 ikiwemo mkewe kati ya mwaka 2022 na Julai 11, 2024.

Amekutwa na simu na laini za simu wakati anakamatwa Kayole leo.

====
Jomaisi Khalisi (33) amekiri kuwaua wanawake 42, ikiwa ni pamoja na mke wake mwaka 2022 kisha kwenda kuitupa miili hiyo kwenye dampo la Kware- Mukuru jijini Nairobi.​

Julai 13, 2024 ilipatikana miili 9 ya wanawake kati ya umumri 18-30 waliokuwa wameuliwa kwa kukatwa vipande na kisha uwekwa kwenye magunia katika dampo hilo

Baadhi ya vitu vilivyosemekana kupatikana nyumbani kwa mtuhumiwa ni pamoja na simu 10, line 24 za simu, vitambulisho 8 na nguo za wanawake. Pamoja na panga na magunia kadhaa ambayo linashukiwa kutumika kwa ajili ya mauaji hayo

Tukio hili limegundulika baada ya Polisi nchini Kenya kuanza uchunguzi wa watu waliotekwa na kuuliwa wakati wa maandamano yaliyokuwa yakiendelea nchini humo Julai 2024

UPDATE
- Collins Jumaisi Khalusha, akana kufanya mauaji ya Wanawake 42
 
Taarifa za sasa zinasema Muuwaji wa Watu waliokutwa kwenye viroba huko Kware amepatikana na anahojiwa na Polisi kujua asili yake na sababu za kufanya Mauaji hayo

Source: Citizen TV
Pengine atakuwa ametokea kusini mashariki mwa Kenya. Kwani wale waliojaribu kule mbugani tayari walishakamatwa au ndio waliotorokea Kenya?
 
Back
Top Bottom