Hakuna contradiction, Ni Kweli kua Yesu alikuja kwa ajili ya Wana wa Israeli. Kwa maana ya kuzaliwa na kuinjilisha. Injili ambayo hapo baadaye ilitakiwa iwafikie mataifa yote ulimwenguni.
Fahamu kua Zamani zile wana wa Israeli walikua wanatawaliwa moja kwa moja chini ya Utawala wa Mfalme herode ambaye hakua mwisraeli bali Mgiriki. Na pia wote wakilipa kodi kwa utawala Mkubwa wa Roma ya Caesari(Siza/kaisari)..kwasababu Utawala wa Wagiriki ulikua chini ya utawala wa Rumi(Roman Empire).
Mfalme Herode pamoja na kua ni Mgiriki aliwasaidia waisraeli kuwajengea Hekalu la Yerusalemu lililokua limebomolewa na wakaldayo.
Lakini wana wa Israeli waliamini akija Masiha, atakua Mfalme wao. kwa mfano wa akina Mfalme Daudi atatawala kama ilivyo watawala wa Dunia.
Imani hii ilimgusa hadi MFALME Herode ambaye alijaribu kufanya upelelezi Ili amuue Mtoto Yesu Kristo ili kulinda milki yake.
[emoji116] [emoji116]
Mathayo 2:3-4
Basi mfalme Herode aliposikia hayo, ALIFADHAIKA, na Yerusalemu pia pamoja naye. [4]Akakusanya wakuu wa makuhani wote na waandishi wa watu, akatafuta habari kwao, Kristo azaliwa wapi?
ALIPOMKOSA YESU, MAANDIKO YANAELEZA ALIUWA WATOTO WOTE WA KIUME WALIOZALIWA ENEO HILO wa umri wa kufikia hadi miaka miwili, ili kama kuna mtoto ambaye yuko destiny kua mfalme akatize ndoto hizo (Mathayo 2:16).
Waisrseli walishathubutu kumfanya Mfalme vile wanavyoona.
[emoji116] [emoji116]
Yohana 6:1
Kisha Yesu, hali akitambua ya kuwa walitaka kuja kumshika ili wamfanye MFALME, akajitenga, akaenda tena mlimani yeye peke yake.
Madai haya yalikwenda hadi wakati akikaribia kusulubiwa.
[emoji116] [emoji116]
Yohana 18:36
Yesu akajibu, Ufalme wangu sio wa ulimwengu huu. Kama ufalme wangu ungekuwa wa ulimwengu huu, watumishi wangu wangenipigania, nisije nikatiwa mikononi mwa Wayahudi. Lakini ufalme wangu sio wa hapa.
Mtume Petro ni mmoja ya watu waliotaka kupigana vita kumlinda Yesu asikamatwe na wayahudi( Mathayo16:23; 26:52 )
[emoji116] [emoji116]
Na baada ya kusulibiwa
[emoji116] [emoji116]
Mathayo 27:37
Wakaweka juu ya kichwa chake mashitaka yake, yaliyoandikwa HUYU NI YESU, MFALME WA WAYAHUDI. Madai haya yaliendelea hata alipofufuka.
[emoji116] [emoji116]
Matendo ya Mitume 1:6
Basi walipokutanika, wakamwuliza, wakisema, Je! Bwana, wakati huu ndipo unapowarudishia Israeli ufalme?
Lakini maandiko yanaweka wazi nafasi ya Yesu kwa ulimwengu.
[emoji116] [emoji116]
Luka 2:32
Nuru ya kuwa mwangaza wa Mataifa, Na kuwa utukufu wa watu wako Israeli.
Matendo ya Mitume 13:47
Kwa sababu ndivyo tulivyoamriwa na Bwana, Nimekuweka uwe nuru ya Mataifa, Upate kuwa wokovu hata mwisho wa dunia.
[emoji115] [emoji115]
Yohana 1:11-13
[11]Alikuja kwake, wala walio wake hawakumpokea.
[12]Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake;
[13]waliozaliwa, si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu.