Wakati wowote Yesu anapoonekana amekosea na ameshindwa kudhihirisha nguvu zake kubwa akiwa Mwana wa Mungu,
Wakristo wanajikinga kwa kudai ya kwamba yeye alikosea akiwa mtu siyo akiwa mungu.
Kwahiyo tunayo kila haki ya kuuliza na kujua waziwazi sehemu gani ndani yake ilikuwa mtu na ipi mungu.
Kukaa kwa mtu ndani ya Yesu kunataka ubongo wa 'mtu' mbali na ubongo wa 'mungu' ndani yake.
Ubongo ulipohuika basi 'mtu' ndani ya Yesu alihuika, kwani Uungu wa Yesu hauhitaji ubongo wa kiwiliwili ili kumsaidia.
Ubongo huo wa kiwiliwili uliingiwa tu na mungu alipokuwa ardhini mara ya kwanza, jinsi inavyokuwa katika mambo ya roho kwamba kitu fulani kinakuwa chombo ama njia ya kudhihirisha onyesho la kiroho. Basi kuhuika Yesu kutamaanisha kuhuika mtu ndani ya Yesu, kwani pasipo kuwa hivyo haiwezekani roho yake kurejea ndani ya mwili huo.
Kama jambo hilo halikubaliwi, hapo tutalikabili tatizo jingine la kukubali kwamba Yesu alikuwa na bongo mbili mbalimbali za
kujitegemea pindi alipokuwa duniani humu: Ubongo mmoja wa 'mtu' na mwingine wa 'mungu', zote mbili zikikaa mahali pamoja, lakini hazikulingana bali kila mmoja unajitegemea.
Kama ni hivyo, basi suala la kuhuika lichunguzwe upya ili uhakika wake hasa utambulikane. Basi hamna haja tena ya kufikiria ubongo wa kibinadamu kufanyizwa upya ili kuipatia dhamiri mahali pa kukalia. Bali twahitaji kufikiria kwamba Yesu analitembelea tena fuvu la kichwa cha mtu aliyekuwa mwenyeji wake wa zamani, ambamo ndani ya fuvu hilo mna masazo ya ubongo yaliyooza.
Kadiri tunavyochunguza kwa uangalifu zaidi suala hilo, ndivyo yanavyojitokeza matatizo zaidi katika kila daraja la uchunguzi.
Mtu anahitaji ubongo kuwa chombo cha mfuatano wa fikira.
Kuhusu kazi zinazofanywa na mwili wa kiwiliwili ni kwamba kama tukiamini kuwa dhamiri inakuwapo peke yake na inaishi
kwa kujitegemea, basi hiyo itamaanisha kwamba dhamiri na roho ni kitu kilekile kimoja. Waweza kuita dhamiri ama roho lakini
inaishi peke yake hata kama uhusiano wake na ubongo wa mtu unakatika.
Lakini kama dhamiri au roho inahitajika ili kuutawala mwili wa mtu ama inaathirika na yanayotokea katika ufalme wake
wa kiwiliwili, hapo bila shaka unahitajika ufungamano madhubuti baina ya dhamiri na ubongo ama roho na ubongo. La sivyo, hivyo (roho na ubongo) haviwezi kabisa kuathiri, kuhimiza au kutawala mafuatano ya kimwili na ya kiakili ama ya ki-maono katika mtu.
Naona hilo halina haja ya kujadiliwa.
Hilo linatuongoza kwenye tatizo jingine kubwa zaidi: Je, anayefanywa kuwa Mwana wa Mungu anahitaji kuutawala ama
kusimamia mwili kwa njia ya ubongo?
Na je, yeye anautegemea ubongo wa kiwiliwili kwa mfuatano wa fikra zake?
Kama yeye anavuka mipaka yote ya kibinadamu, na kama yeye anao mfumo wa kujitegemea wa mfuatano wa fikira ambao ni wa pekee kwake usiyo na kifani katika ulimwengu mzima aliouumba, hapo kurejea roho ya Mungu katika mwili wa mtu pamoja na dhamiri ya mtu kunaleta natija isiyolingana na akili yaani kupatikana kwa dhati iliyo na mifuatano miwili ya fikra inayopingana, kwani haiwezekani kwa dhamiri na roho ya mtu kulingana kikamilifu na dhamiri na dhati ya Mungu.
Kutakuwa na upinzani wa kudumu baina ya mifuatano hiyo miwili utakaosababisha mapambano ya kusumbua baina ya mawimbi ya ubongo.
Mwenye shida hiyo anafaa kutibiwa na mtaalamu wa utibabu wa maradhi ya roho mwenye uwezo zaidi ya mtu.
Huo pengine ndiyo ugonjwa mpya wa roho uitwao schizophrenia kwa Kiingereza.
INAENDELEA