kimpe
JF-Expert Member
- Jan 26, 2012
- 911
- 862
1). Mtwa Mkwawa hakuwa mhehe na wala hakuwa mtoto wa Mnyigumba (kama historia iliyoandikwa na Wajerumani inavyopotosha); bali Mkwawa alikuwa ni mtoto wa dada wa Mnyigumba aliyeolewa na mtemi wa Waluguru; hivyo Mkwawa alikuwa Mluguru kwa asili.
Akiwa mdogo alikwenda kumtembelea mjomba wake (Mnyigumba) na kutokana na ushujaa wa Mkwawa akafanikiwa kumuokoa mjomba wake katika vita kali dhidi ya Wangoni pale Makambako. Mnyigumba akampenda Mkwawa kuliko watoto wake, na ndio chanzo cha kupewa urithi pamoja na mtoto wa Mnyigumba aliyeitwa Muhenga.
2). Sherehe za kuapishwa Mtwa Mkwawa zilifanyika Dodoma eneo linaloitwa Mpwapwa. Sherehe zilihudhuriwa na wajomba zake Mtemi Mazengo, Kimweri, Lugulu na Mirambo; ambapo walikuwa wakiimba "Mpwa! Mpwa!" na ndipo neno Mpwapwa likazaliwa.
3) Mtwa Mkwawa alikua na vikosi vinne vya majeshi ya vita; kimojawapo kilikuwa cha upelelezi na ushambuliaji [Kiitwacho Vamalavanu] ambacho kilikuwa kikila nyama ya mbwa ikichanganywa na dawa ya tambiko; wakiamini kuwa watakuwa na uwezo wa kunusa maadui na wao kutoonekana. Hivi ndivyo ulaji nyama ya mbwa ulivyoanza.
4). Mtwa Mkwawa alijua kusoma na kuandika kwa ufasaha lugha ya Kiarabu na alikuwa muumini wa dini ya Kiislamu.
5). Mtwa Mkwawa hakujipiga risasi bali alijitumbukiza katika daraja la Kikongoma (lililopo mto Ruaha) mahali ambapo mama yake mzazi pia alijitumbukiza na kujiua pale. Lile fuvu linalodaiwa kuwa la Mtwa Mkwawa inadaiwa ni la mlinzi wake. Hadi leo hakujawahi kufanyika DNA tests kuthibitisha fuvu hilo.
6). Kwenye vita iliyomsambaratisha Mtwa Mkwawa, Wajerumani walifanikiwa kumkamata mdogo wa Mkwawa aliyeitwa Mpangile, walimtundika kitanzini-hakufa, wakampiga risasi-hakufa! Baadae akatoboa siri kuwa wammwagie maji na wamchome mkuki-ndipo akafa! Baada ya kuona hivyo wakampa jina "Mpangelwangindo Mgopisala Sasisinagopi" likimaanisha: Mpangile anaeogopa mkuki risasi haogopi.
7). Kutokana na kuwa Mluguru kwa asili ndio maana Mtwa Mkwawa alikuwa na uhusiano wa karibu na mtemi Mazengo (Ugogo Dodoma) pamoja na mtemi Mirambo wa Unyamwezini Tabora. Mazengo, Mirambo na mtemi wa Uluguru walikuwa ndugu wa damu na walikuwa Wajomba wa Mkwawa.
8) Mtwa Mkwawa alikuwa na rada za asili alizozitega milimani ambazo zilikuwa zikimjulisha hali ya vita na ujio wa maadui katika himaya yake. Rada hizi zilizoitwa "Kimwanyula" zilopoangushwa na Wajerumani ndio ulikuwa mwanzo wa kushindwa kwa Mtwa Mkwawa katika vita.
9). Askari mkuu wa kikosi cha usalama wa ufalme wa Mtwa Mkwawa aitwae Chavala ndie aliesababisha anguko la Mkwawa mbele ya Wajerumani baada ya kuanika siri zote za kijeshi, kimizimu na kiganga alizokuwa akitumia Mkwawa. Chavala alishawishika kumuasi Mkwawa baada ya kupewa rupia 5,000 na Wajerumani.
10). Mtwa Mkwawa alikuwa na wake 63, waliokuwa wakiishi Ipamba na mamia ya watoto aliowajengea makazi eneo la Tosamaganga