Mtwa Mkwawa hakuwa muhehe

Mtwa Mkwawa hakuwa muhehe

mdogo wa mkwawa alikufa kwa kuchomwa na mkuki wenye makali juu na chini na alinyongewa mtaa unaitwa kitanzini Iringa
 
5). Mtwa Mkwawa hakujipiga risasi bali alijitumbukiza katika daraja la Kikongoma (lililopo mto Ruaha) mahali ambapo mama yake mzazi pia alijitumbukiza na kujiua pale. Lile fuvu linalodaiwa kuwa la Mtwa Mkwawa inadaiwa ni la mlinzi wake. Hadi leo hakujawahi kufanyika DNA tests kuthibitisha fuvu hilo.

Enzi za mkwawa kulikuwa na daraja hapo mtoni?,unakumbuka mkwawa aliwashinda wajerumani wakati wanajaribu kuvuka mto ruaha,fanya utafiti wa kutosha,wajerumani wamepotosha historia kwa masilahi ya nani.zambi zingine bwana.
 
historia ina mambo mengi. Nimeamini baadhi ya statement ila huwezi kuniaminisha kuwa yule mwamba hakuwa muhehe. uislamu naamini coz generation ya mtwa wanaotawala now ni waislamu
 
Sawa kweli wajeruman waliupotosha ukweli wa historia ya Mtwa Mkwawa je wewe uliyesema ukweli tunaamini enzi za Mkwawa haukuwepo hizi habari umezipata wapi na je umewaamini vipi waliosema habari hizo na kwann wajerumali walipindisha ukweli!!? mtoa uzi
 
Last edited by a moderator:
#6 nitakuwa wa mwisho kuamini kabisaaaa


Sent from my iPad Air using JamiiForums
 
Source? in actualfact ulichoandika kinaweza kuwa factual ikiwa tu kitaweza kubomoa historia ambayo kila mmoja anaijua,hizo DNA tests unazosema sijui ni zipi Kwani ukoo wa mkwawa umethibitisha kupitia Chief Adam Sapi kwamba ile skull ni ya babu yao,so cite source uaminike:what:
 
Hii habari ina uwongo mwingi kuliko ukweli. Nia yako nzuri lakini ulihitaji maandalizi ikiwemo kupata taarifa sahihi. Vinginevyo, uwongo huu haukujengi wewe, wahehe, wala warugulu.

1. Unaweza kuelezea kabila la wahehe lilianzaje? Maana kumbuka hapakuwahi kuwa na kabila la wahehe.

2. Unaweza kuelezea uhusiano uliokuwepo baina na Mkwawa na Mwambande?

3. Eti radar za asili, uwongo gani huu?

4. Mkwawa alienda Dodoma kwa chief Mazengo kuapishwa kweli? Mbona wewe mwongo hivi?

KWA UJUMLA HISTORIA YAKO IMEBUMBWA BUMBWA SANA. UNAPOKOSA TAARIFA UNALAZIMISHA USHIRIKINA ILI WATU WASIHOJI. ACHA HIZO. HISTORIA SAHIHI YA MKWAWA TUNAIJUA JAPO HUWA IKO TOFAUTI KIASI NA YA WAJERUMANI LAKINI NA YA KWAKO IKO KIVYAKO VYAKO SANA.





1). Mtwa Mkwawa hakuwa mhehe na wala hakuwa mtoto wa Mnyigumba (kama historia iliyoandikwa na Wajerumani inavyopotosha); bali Mkwawa alikuwa ni mtoto wa dada wa Mnyigumba aliyeolewa na mtemi wa Waluguru; hivyo Mkwawa alikuwa Mluguru kwa asili.

Akiwa mdogo alikwenda kumtembelea mjomba wake (Mnyigumba) na kutokana na ushujaa wa Mkwawa akafanikiwa kumuokoa mjomba wake katika vita kali dhidi ya Wangoni pale Makambako. Mnyigumba akampenda Mkwawa kuliko watoto wake, na ndio chanzo cha kupewa urithi pamoja na mtoto wa Mnyigumba aliyeitwa Muhenga.

2). Sherehe za kuapishwa Mtwa Mkwawa zilifanyika Dodoma eneo linaloitwa Mpwapwa. Sherehe zilihudhuriwa na wajomba zake Mtemi Mazengo, Kimweri, Lugulu na Mirambo; ambapo walikuwa wakiimba "Mpwa! Mpwa!" na ndipo neno Mpwapwa likazaliwa.

3) Mtwa Mkwawa alikua na vikosi vinne vya majeshi ya vita; kimojawapo kilikuwa cha upelelezi na ushambuliaji [Kiitwacho Vamalavanu] ambacho kilikuwa kikila nyama ya mbwa ikichanganywa na dawa ya tambiko; wakiamini kuwa watakuwa na uwezo wa kunusa maadui na wao kutoonekana. Hivi ndivyo ulaji nyama ya mbwa ulivyoanza.

4). Mtwa Mkwawa alijua kusoma na kuandika kwa ufasaha lugha ya Kiarabu na alikuwa muumini wa dini ya Kiislamu.

5). Mtwa Mkwawa hakujipiga risasi bali alijitumbukiza katika daraja la Kikongoma (lililopo mto Ruaha) mahali ambapo mama yake mzazi pia alijitumbukiza na kujiua pale. Lile fuvu linalodaiwa kuwa la Mtwa Mkwawa inadaiwa ni la mlinzi wake. Hadi leo hakujawahi kufanyika DNA tests kuthibitisha fuvu hilo.

6). Kwenye vita iliyomsambaratisha Mtwa Mkwawa, Wajerumani walifanikiwa kumkamata mdogo wa Mkwawa aliyeitwa Mpangile, walimtundika kitanzini-hakufa, wakampiga risasi-hakufa! Baadae akatoboa siri kuwa wammwagie maji na wamchome mkuki-ndipo akafa! Baada ya kuona hivyo wakampa jina "Mpangelwangindo Mgopisala Sasisinagopi" likimaanisha: Mpangile anaeogopa mkuki risasi haogopi.

7). Kutokana na kuwa Mluguru kwa asili ndio maana Mtwa Mkwawa alikuwa na uhusiano wa karibu na mtemi Mazengo (Ugogo Dodoma) pamoja na mtemi Mirambo wa Unyamwezini Tabora. Mazengo, Mirambo na mtemi wa Uluguru walikuwa ndugu wa damu na walikuwa Wajomba wa Mkwawa.

8) Mtwa Mkwawa alikuwa na rada za asili alizozitega milimani ambazo zilikuwa zikimjulisha hali ya vita na ujio wa maadui katika himaya yake. Rada hizi zilizoitwa "Kimwanyula" zilopoangushwa na Wajerumani ndio ulikuwa mwanzo wa kushindwa kwa Mtwa Mkwawa katika vita.

9). Askari mkuu wa kikosi cha usalama wa ufalme wa Mtwa Mkwawa aitwae Chavala ndie aliesababisha anguko la Mkwawa mbele ya Wajerumani baada ya kuanika siri zote za kijeshi, kimizimu na kiganga alizokuwa akitumia Mkwawa. Chavala alishawishika kumuasi Mkwawa baada ya kupewa rupia 5,000 na Wajerumani.

10). Mtwa Mkwawa alikuwa na wake 63, waliokuwa wakiishi Ipamba na mamia ya watoto aliowajengea makazi eneo la Tosamaganga

 
Ni kweli Mkwawa alikuwa mwislamu na kuna simulizi za ajabu kuna mahali nilielezwa kuwa alikuwa ni mjahidina wa mwanzo kabisa ambaye alitumiwa kama proxy na waarabu kupigana na wajerumani kuwazuia wasieneze dini yao ya kilutheli kwenye maeneo yake ya utawala ambako uislamu ulikuwa ukijaribu kuyafikia.

Silaha zake za vita inasemekana alikuwa akipata toka kwa waarabu ushahidi ni aina ya bunduki alizotumia vitani ni zile ambazo waarabu walikuwa nazo.

'Inasemekana alikuwa mwislamu' chanzo cha fununu!! na alikuwa akiswali msikiti gani!!
 
Huyu jamaa mwongo sana tu. Uhehe halikuwa kabila. Ilikuwa ni sauti waliyokuwa wakitoa askari wa kitoka vitani na mikuki wakiruka juu na kudua wakisema HE HE HE HE. Na hawa wahehe leo asili yao ni mkusanyiko wa vikabila vingi vidogo vidogo wilivyoungana na kwa ajli ya hiyo common phenomena ya kufanya HE HE HE HE He ndipo walipoitwa wahehe kwa ujumla wao. Haka kajamaa haka, kamepotosha habari nyingi sana.

historia ina mambo mengi. Nimeamini baadhi ya statement ila huwezi kuniaminisha kuwa yule mwamba hakuwa muhehe. uislamu naamini coz generation ya mtwa wanaotawala now ni waislamu
 
La usilamu siwezi kulisemea lakini ni kweli warabu walitangulia kufika Iringa kabla ya wajerumani. Waarabu walifanya urafiki na mkwawa lakini mkwawa hakuwaruhusu wachukue mtumwa kutoka uheheni. Kwamba alikuwa mjahidina hilo halipo kwa sababu hakuwa brainwashed na ndiyo maana hakukubaliana nao katika masuala likiwemo na kuchukua watumwa.

Vita ya mjerumani na mkwawa haikuwa vita ya kidini kama kamjamaa kanavyotaka kutuaminisha hapa. Ilikuwa ni vita ya sovereignty. Na wala si kweli kwamba mkwawa alizidiwa kwa sababu ya kuvuja siri za mizimu na uganga. Huu ni uwongo. Mkwawa alizidiwa mbinu za medani. Na kwa ajili ya ukatili wake, alijitengenezea maadui wengi wa ndani na miongoni mwao wakaweza kuwapa ramani wajerumani namna ya kumfikia mkwawa bila intelligencia yake kufahamu. Na hivyo akavamiwa kwa kushitukizwa.

'Inasemekana alikuwa mwislamu' chanzo cha fununu!! na alikuwa akiswali msikiti gani!!
 
Namba 2,kabla ya kuitwa Mpwapwa kulikuwa kunaitwaje?
Nalog off
 
Huyu jamaa mwongo sana tu. Uhehe halikuwa kabila. Ilikuwa ni sauti waliyokuwa wakitoa askari wa kitoka vitani na mikuki wakiruka juu na kudua wakisema HE HE HE HE. Na hawa wahehe leo asili yao ni mkusanyiko wa vikabila vingi vidogo vidogo wilivyoungana na kwa ajli ya hiyo common phenomena ya kufanya HE HE HE HE He ndipo walipoitwa wahehe kwa ujumla wao. Haka kajamaa haka, kamepotosha habari nyingi sana.

Santeee,ingekuwa vizuri ungetuorodheshea majina ya hivyo vikabila vidogo vidogo na je bado vipo au ndio vimepotea?
Nalog off
 
Back
Top Bottom