Haifiki tarehe 15 wana pokea 300,000/ mwisho wa mwezi 275,000Ni 7 kwa mwez
Yaani hawa mbwa bila hofu ya Mungu unawaroga wote tena wafe vile vifo vya kukiri walichofanya kabla ya kukata roho!Kila siku mauaji ya raia yanayofanywa na polisi yanaongezeka . Na imekuwa too much maana hatuoni IGP akichukua hatua.
=====
View attachment 2095921
JESHI la Polisi Mkoani Mtwara limewakamata na kuwafikisha mahakamani Maafisa wa Polisi saba kwa tuhuma za mauaji ya Mussa Hamisi Hamisi (25) mkazi wa Kijiji cha Ruponda wilayani Nachingwea Mkoani Lindi aliyekuwa akiwadai askari hao zaidi ya Sh milioni 33.7.
Inadaiwa maafisa hao wa polisi walijipatia kiasi hicho cha pesa wakati wakimfanyia upekuzi mfanyabiashara huyo. Taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mtwara, ACP Marck Njera imesema mauaji hayo yalifanyika Januari 5, 2022 na mwili wa marehemu ulitupwa kitongoji cha Majengo kijiji cha Hiari Wilayani Mtwara.
Maafisa wanaoshikiriwa ni Mrakibu wa Polisi Gilbert Kalanje -Mkuu wa Upelelezi wa wilaya ya Mtwara, Mrakibu Msaidizi wa Polisi Charles Onyango - Mkuu wa Kituo cha Polisi Mtwara, Mrakibu wa Polisi Msaidizi Nicholaus Kisinza - Mkuu wa Kikosi cha Intelejensia ya Jinai mkoa wa Mtwara, Mkaguzi wa Polisi John Msuya Mganga - Mkuu wa Zahanati ya Polisi Mtwara, Mkaguzi wa Polisi Msaidizi Marco Mbuta, Mkaguzi wa Polisi Shirazi Mkupa na Koplo Salimu Juma Mbalu.
Uchunguzi wa tukio hilo bado unaendelea.
Chanzo: Habari leo
Pia soma: Mtwara: Askari Polisi mmoja kati watuhumiwa wa mauaji ya mfanyabiashara alikutwa mahabusu akiwa amejinyonga tarehe 22 Jan 2022
kuna police alikuwa anaitwa Benadi kama sikosei.kikosi chao kilikuwa na askari kazaa pale Morogoro ila nisingependa kuwataja.
hawa police walikuwa wakifanya unyang'anyi wa kiujambazi kwa wa2 wengi sana.Ila uyu benad ambae aliingia kazini kwa kipaji cha kucheza mpila alipatwa na shida ya kuifiwa na mke wake.Ila cjajuwa kilichomuuwa mkewe.
kutokana na kifo cha mkewake ambae alikuwa anafanya kazi SUA uyu askari akaamuwa kuokoka.
Sasa basi katika kuokoka kwake ilimbidi aanze kutubu matendo yote ambayo alikuwa wakiyafanya.
Apo ndio alikuwa anaamuwa kuyasema adhalani matendo ambayo alikuwa wakiyafanya na askali wenzake.siwezi kuelezea sana mambo ambayo walikuwa wakiyafanya ila hayatofautiani na aya waliyofanya askali wa mtwala akina Zombe.
Mwisho waliamua kutangaza kama yule askali amechanganyikiwa na wakampeleka dodoma milembe ila bado mshikaji alikoamaa na msimamo wake na kuamuwa kuandika vijalada kuutangazia uma kwa matendo yao waliyokuwa wakiwafanyia rahia hasa wafanya biashala wenye hela.
Mwisho kabisa uyu askali walimkuta amejinyonga ila kwanye mazingila yanaonyesha kuwa aliuwawa ila kwakuwaa upelelezi wanafanya wao hivyo walifanikiwa kumpoteza.
Kati ya maaskari waliobaki ni yule ambae niliona you tube amejitengenea kabuli.Nazani damu za wasio na hatia zishaanza kumtafuna...
Nazani damu za watu wasio na hatia.. 76 nazani anaitwa.
naomba nisiongee sana maana zama za jiwe bado zinaendelea...Matendo yanayo tendeka sasa c mageni kwenye idala hii😭😢!!
Hata wao huwa hawafanyi poa..Kuliwa naniliu tena? Hiyo siyo poa kiongozi!
Ndugu wa MAJALIWANdugu waendelee kukomaa
RCO nae sijui kachukuliwa hatua gani hadi sasa?!Ishu tangu tarehe tano ni kwa vipi RPC anakosekana kuwa ndani? Jee OCD Yuki wapi? Kiufupi hao wote ni wahusika wanatakiwa kuwa ndani mahabusu na kesi yao iendeshwe mapema na haraka wanyongwe ili kuleta nidhamu kwa jeshi la polisi.
Nilikuwa mtwara toka ijumaa ndio stori imezagaa mjini , kwa kweli hawa polisi wamefanya tendo la kikatili sana akiongozwa na mkuu wa kituo
Sent from my JKM-LX1 using JamiiForums mobile app
Dhambi kubwa sanaKila siku mauaji ya raia yanayofanywa na polisi yanaongezeka . Na imekuwa too much maana hatuoni IGP akichukua hatua.
=====
View attachment 2095921
JESHI la Polisi Mkoani Mtwara limewakamata na kuwafikisha mahakamani Maafisa wa Polisi saba kwa tuhuma za mauaji ya Mussa Hamisi Hamisi (25) mkazi wa Kijiji cha Ruponda wilayani Nachingwea Mkoani Lindi aliyekuwa akiwadai askari hao zaidi ya Sh milioni 33.7.
Inadaiwa maafisa hao wa polisi walijipatia kiasi hicho cha pesa wakati wakimfanyia upekuzi mfanyabiashara huyo. Taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mtwara, ACP Marck Njera imesema mauaji hayo yalifanyika Januari 5, 2022 na mwili wa marehemu ulitupwa kitongoji cha Majengo kijiji cha Hiari Wilayani Mtwara.
Maafisa wanaoshikiriwa ni Mrakibu wa Polisi Gilbert Kalanje -Mkuu wa Upelelezi wa wilaya ya Mtwara, Mrakibu Msaidizi wa Polisi Charles Onyango - Mkuu wa Kituo cha Polisi Mtwara, Mrakibu wa Polisi Msaidizi Nicholaus Kisinza - Mkuu wa Kikosi cha Intelejensia ya Jinai mkoa wa Mtwara, Mkaguzi wa Polisi John Msuya Mganga - Mkuu wa Zahanati ya Polisi Mtwara, Mkaguzi wa Polisi Msaidizi Marco Mbuta, Mkaguzi wa Polisi Shirazi Mkupa na Koplo Salimu Juma Mbalu.
Uchunguzi wa tukio hilo bado unaendelea.
Chanzo: Habari leo
Pia soma: Mtwara: Askari Polisi mmoja kati watuhumiwa wa mauaji ya mfanyabiashara alikutwa mahabusu akiwa amejinyonga tarehe 22 Jan 2022
Wale wazee wenzangu ambao macho yetu yanaelekea ukingoni, nimedokoa kwa Muhtasari;
-Alitiwa mbaroni akiwa nyumbani kwake mjini Nachingwea kisha kupelekwa Mtwara Mjini
-Baadae aliachiwa baada ya kuchukuliwa maelezo lakini alirudi Polisi kudai fedha zake zilizoshikiliwa
-Tangu aliporudi kituoni hapo kudai fedha zake alishikiliwa tena na kuhojiwa na baada ya hapo hakuonekana tena
-Taarifa Zaidi zinadai kuwa mfanyabiashara huyo aliondolewa kituoni hapo na kupelekwa eneo lingine, inadaiwa kuwa alichomwa sindano ya sumu kisha kutupwa Baharini
Hao ndio Polisi wetu wenye jukumu la kulinda raia na mali zao!
Mungu Ibariki Tanzania.
Yapo kitambo hayo mkuu,halafu tamaa ya polisi wachache ndio inaharibu sifa nzuri ya jeshi zima,chanzo cha yote vikosi vya madefender vile,wale wazee wa kuning'ia wana good time babu kubwa,na 90% ya chanzo cha mapato yao ni raia,uwe mhalifu au usiwe mhalifu,ukiingia kwenye 18 zao utajua kama hujuiPolisi nao wameanza kuunda magenge ya uhalifu.
Kila mbuzi atakula urefu wa kamba yake