Mtwara: Maafisa Saba(7) wa Polisi wafikishwa Mahakamani kwa tuhuma za mauaji ya Kijana aliyekuwa akiwadai zaidi ya Tsh milioni 33.7

Bora hata polisi kuliko lile kabila linaloua mama mzazi kisa shamba la mbege.
 
Wewe ni polisi? Au baba yako ni polisi acheni dhuluma na ujambazi.
 
Hivi hili jeshi lina sifa nzuri?
Kuua na kutesa Kwa jinsi wanavyojisikia na kuwapora marehemu pamoja na kuwabakikia makosa raia na kutoa ushahidi mahakamani Kwa kesi walizochunguza na kushtaki wenyewe! Sifa nyingine ni kupora kura! Maa mbali nao!
 
Lazima wawe hivyo..sehemu kubwa ya maisha yao..ni uonevu..na dhuluma...Mungu gani atakufanikisha iwapo unawadhulumu watu wake!!
Nimeona wengi wakistaafu na asset na pesa..baada ya muda vianakauka vyote. Bse sio utajiri utokanao na haki..huwezi rithisha vizazi...utakula na vitakupita ..ila haviishi muda mrefu.

Polisi wote mliko humu..fahamuni kuwa..mali ya dhuluma ni laana...kula lakini ujue inakutafuna mdogomdogo...
 
Kwa kashfa hizi IGP Sirro kwa hiari yake ajiuzuru na kama hatafanya hivyo alazimishwe kuondoka!! Mahita ilibidi aondoke baada ya ujambazi aliohusishwa nao wa wakina Zombe kushamiri sana nchini; sasa ni zamu ya Sirro kuachia ngazi.
Alafu kamera ya itv inammulika ajibu tuhuma anakimbia kanishangaza. Angesema hata mfuateni rpc
 



Jeshi la Polisi Mkoani limewakamata na kuwafikisha mahakamani Maafisa wa Polisi saba (7) kwa tuhuma za kufanya mauaji ya kijana Mussa Hamisi Hamisi (25) mkazi wa Kijiji cha Ruponda wilaya ya Nachingwea Mkoani Lindi.

Mauaji hayo yamefanyika baada ya marehemu Mussa Hamisi kudai fedha zake shilingi Milioni 33,748,980 ambazo maafisa hao wanadaiwa kuzichukua kutoka kwa kijana huyo baada ya kumfanyia upekuzi.

Kulingana na taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mtwara, ACP Marck Njera amesema mauaji hayo yalifanyika Januari 5, 2022 na mwili wa marehemu ulitupwa kitongoji cha Majengo kijiji cha Hiari wilaya ya Mtwara.

Maafisa wanaoshikiriwa ni Mrakibu wa Polisi Gilbert Kalanje -Mkuu wa Upelelezi wa wilaya ya Mtwara, Mrakibu Msaidizi wa Polisi Charles Onyango -Mkuu wa Kituo cha Polisi Mtwara, Mrakibu wa Polisi Msaidizi Nicholaus Kisinza -Mkuu wa Kikosi cha Intelejensia ya Jinai mkoa wa Mtwara, Mkaguzi wa Polisi John Msuya Mganga- Mkuu wa Zahanati ya Polisi Mtwara, Mkaguzi wa Polisi Msaidizi Marco Mbuta, Mkaguzi wa Polisi Shirazi Mkupa na Koplo Salimu Juma Mbalu.
Uchunguzi wa tukio hilo bado unaendelea.

Source: Kusiniyetu Online Tv.
 
Hao inaonesha hata MAHARAMIA wa msituni wanawavusha wao. Wakipewa pesa tu wanawapakia kwenye magari yao..
Wahojiwe vizuri hicho kikundi kitakuwa kimefanya mengi zaidi
 
Polisi wengi ni wauaji sana wa raia wema ila basi tu mambo yao mengine yanaishia chini ya kapeti
Yule jamaa hamza aliyeuliwa pale ubalozi wa ufaransa lazima kulikuwa na kitu kama hiki ila aliamua kuchukua njia yake nyingine kulipiza kisasi labda naye angekwenda kudai madini yake angeuwawa akaamua afanye vile alivyofanya.
Polisi jirekebisheni mnazulumu sana raia wema
 
Mwanzo zilisikika habari za 70 milioni now 33 milioni. Kwa jinsi hawa jamaa wasivyohaminika ukute kabisa zilikuwa 70 kweli na 40 zimepotelea kwenye hizi press release. Anyways yote heri tu na Pole nyingi sana kwa familia na jamaa ya Musa Hamisi.

Yaani mnamuua kijana mdogo kabisa wa miaka 25 na kukatili maisha yake na ndoto za familia yake. Inaumiza sana yaani. Badala ya polisi kulinda watu na kuwa kimbilio la watu mnageuka kuwa madhulumati na wauaji. Inauma sana
 
Ukifwatilia kesi ya Mbowe utaona kiasi gani jeshi la polisi linahitaji overhaul ya kufa mtu..maana wanafanya kazi nje ya utaratbu sana..wanaonewa ni wengi sema hawana pakusema.Sio sehem sahihi sana kuapata msaada
 
Ni jambo la kusikitisha sana kuhuzunisha sana kuona matendo yanayofanywa na Polisi wetu. Kwa nini Mhe. Rais asitengue IGP aliyopo kutokana na matendo yanayotokea kwenye taasisi yake. Kweli inahuzunisha sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…