GeoMex
JF-Expert Member
- Jan 10, 2014
- 5,431
- 19,913
ina maana huo uchumi umekua kwa usiku mmoja ...baada ya mapumuziko marefu!?
Watu wamenunua magari kwa wingi kwenye sikukukuu...magari mengi= Uchumi umekua....Source Rais mpendwa Jeikei
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
ina maana huo uchumi umekua kwa usiku mmoja ...baada ya mapumuziko marefu!?
Shughuli za serikali zote peleka Dom, pale Magogoni pawe nyumba ya makumbusho walau Dar itapumua huku ikibaki na biashara pamoja na bandari.
Ahsante sana mkuu, nadhani inabidi ifike kipindi tuache haya magari yetu na mjini tuwe tunatumia alternative transport, maana Parking nayo ni changamoto nyingine.
Ni kweli mkuu.... Ni bora kutumia public transport kama bajaj na bodaboda ili kuwahi maana unaweza kukaa kwenye foleni ukiwa na private mpk ukatamani kuliacha gari ukapanda bodaboda ila ndo huezi!!!
Ni wakati muafaka sasa kujitambua na kubadilika kwa manufaa ya jamii ya watanzania na maendeleo ya nchi yetu, nasema hili kwa sababu nami nilikuwa kama wengi wa wanaolalamika bila kutafuta suluhisho la kudumu, Dar ina tatizo la miundombinu muda mrefu na kila mmoja analifahamu fika, serikali imeshanyoosha mikono juu kutuhakikishia kuwa imeshindwa kupata suluhisho na hivyo imebaki ni kwa wajanja wachache kubuni vijimiradi feki vya kudai kuwa wanatatua tatizo la foleni huku wakijinufaisha na nyumba ndogo zao! Sasa basi, baada ya kumwaga utangulizi huo natoa suluhisho la kweli kwa maisha ya foleni za DAR, watu tuamue kutumia usafiri wa pikipiki na baiskeli kama mbadala wa haya magari yetu ya starehe tuendeshayo! Mimi natumia pikipiki, inahitaji kiwango cha kati mpaka cha juu cha adabu kuitumia katika jiji kama la Dar, kuwa makini na madereva wazembe, waenda kwa miguu na vyombo vyote vinavyotumia barabara huku ukiwa na vifaa vya kujikinga na hatari ya aina yoyote kwa suala zima la afya na usalama wa mtumia pikipiki! Najua kuna wataodhani ni utani lkn nakuhakikishia ukiweza kuwa mtumiaji wa pkpk kwa Dar basi utafaulu sana katika suala zima la kuokoa muda wako na wa mwajiri, hivyo kuongeza uzalishaji kwako na kwa mwajiri huku ukiiongezea nchi kipato na kukuza uchumi wetu hohehahe!
Ndo nimemaliza
Jiji Limeongezeka idadi ya watu pia bado ofisi nyingi zimejikusanya sehemu moja , posta na kariakoo , hz ofisi zetu zingeendelea kutawanywa na kuhamishwa , mfano wizara zingine ziwepo gongolamboto , tegeta , mbagala na tabata maana asubuh watu wengi wanatoka maeneo hayo kuelekea posta au kariakoo.
Solution ni highways tu
ina maana huo uchumi umekua kwa usiku mmoja ...baada ya mapumuziko marefu!?
umemaanish flying over?
kama ni hivyo kwa kweli kwa mji ulivyopangwa dar sijui itawezekanaje labda sehemu kubw ya makazi ya watu huduma za kijamii zibomolewe!
mfano nilielezwa kuwa ili kuweka flying over pale ubungo ni lazima ile petrol/diesel filling station lazima iondoke kwz mfano kama huo utaona ni jinsi gani sehemu kubwa ya dsm itaathirika.
tatizo la mango yetu ni ya miaka mitano wakati wenzetu mbele wanapanga miaka 50-100 mbele!
Wakitufikisha hapa, sijui itakuwa lini?
Hapo tutafika soon!! Wanaanza Ubungo na Tazara, sasa hv wapo kwenye kipindi cha kuandaa michoro!!
Mkuu, nilisikia kuwa ile plan ya michoro ya Fly- over/ Fly over, imeshahauliwa(kwamba huo mpango haupo tena na Rapid Bus Transport, ndio itakuwa mbadala, ma uwezekano huo(wa kuweka flyover ni katika mikoa ya Lindi na Mtwara, ina ikiwezakana hapa Dar iwe Kigamboni tu, sijui kama lina ukweli hili.