Muda wa Che Malone kukaa bench umefika

Kaokoa mangapi.
 
Kile KICHWA alicho piga alitakiwa awepo mtu afanye cover....!!!
Kwenye mpira timu Ina jikinda kwa kanuni beki akikaba au kucheza mpira ana takiwa awepo mtu wa kucover hiyo nafasi Kisha ana kuwepo mtu mwingine wa kutengeneza balance.
Sasa kwa mantinki hii Che Malone alicheza mpira kwa KICHWA je nani alikwenda cover kwa mshambuliaji?
Swali langu nani alikwenda kucheza drop ball Baada ya KICHWA Cha Che Malone ? Balance nani alifanya.

Karibu tujadili kiufundi ndugu yangu.

Hoja ya tackle ambayo aliifanya kule Libya....!!! Kwanza Ile ilikuwa behind the opponent hivyo Che alicheza kwanza mpira Kisha acheza mguu na mwili wa mshambuliaji wa Al ahly Tripoli.
Nakusaidia tu, hakuna mtu ambaye ana weza kucheza tackle behind the opponent aka cheza mpira asiguse mwili wa mtu.Kwa sababu wakati aliye cheza Tackle ana shuka chini lazima balance yake iwe ni mwili wa aliye pembeni.
Kwaiyo refa ana angalia tukio la kwanza,Je alicheza mpira kwanza ? Au mguu aidha mwili wa opponent?
Kwa sababu haujui mpira kwako Hilo ni kosa ndugu mtaalamu!!
Duniani beki wa kati ana takiwa awe anajua kucheza standing tackle, behind tackle kwa usahihi na hizi Che ana zifanya kwa ustadi mkubwa.
Ndugu taja makosa mengine nikuelekeze kitaalamu.

KIFUPI KIKOSI KIZIMA CHA SIMBA HAKUNA BEKI ANAE WEZA KUMWEKA BENCHI CHE MALONE.
HUYU NDIYE BEKI BORA WA KISASA.
 
Huko kujiamini kupita kiasi ndio kosa lenyewe. Kunguru mwoga anaishi siku nyingi
Ndugu yangu mpira sio sehemu Yako changua kitu kingine.Dunia nzima Ina hitaji beki anae jiamini alafu Wewe una taka beki mwenye hofu daaah.
Kujiamini kwa beki ndio Kuna tengeneza uwiano mzuri wa timu kujenga mashambulizi!!! Hebu jifunze kwanza mpira ndio uje uchangie kwanza.
 
Che Malone and Bacca wa yanga wote wanahitaji kupumzika,akili zinatoka lkn miili imechoka mno
 
Kama si Hongo kwa refa, Jana akustahili kuendelea na mchezo, Red card ya wazi ilimuhusu.
Bahati ni mechi za shirikisho hakuna anaye jali kwakua Zina hadhi ya Ndondo cup.
Ww ni Chakubanga
 
Mbona una andika maoni binafsi bila kuweka fact hata kidogo...!!!
Ngoja nikusaidie ndugu yangu....!!!
Siku hiyo Coastal Union walikuwa Wana kaba kwenye LOW BLOCK Yani Wana kabia kwenye Eneo lao ndani ya box.
Coastal Union walikuwa na wachezaji nane kwenye box lao huku wakiweka watu wawili wakiwa kwenye Eneo la Winga.
Sasa Simba kwa sababu nao walikuwa nahitaji ushindi Ili kuwafungua Coastal Union nao wakawa wanashambulia kwa watu nane kwenye box la Coastal Union.
Pia Simba wakawa Wana cheza kwenye High Line maana yake Wana kuwa wako kwenye Eneo la Coastal Union kwa muda mwingi.

Timu yoyote inayo cheza kwenye high Line Kuna mambo una takiwa kutayaona uwajani.
1.Eneo la ushambuliaji Lina kuwa juu muda wote.
2.Eneo la kiungo Lina sogea Karibu na Eneo la ushambuliaji.
3.Eneo la beki nalo Lina sogea juu Karibu na Eneo la kiungo.
#kwa kuwa Eneo la beki Lina sogea juu zaidi Karibu na Eneo la kiungo Wana acha Eneo kubwa nyuma ya migongo Yao na hivyo kuacha Eneo kubwa kati ya Ulinzi na kipa.
Mpira ukipigwa nyuma ya migongo Yao lazima wapate tabu kwa sababu ya umbali kati Yao na kipa.
Hii sio kwamba mabeki ni wabovu bali ni umbali waliopo una mpa Eneo kubwa mshambuliaji kukimbia kwa urahisi.
Kwa kuwa hajui mpira una ona beki ndio shida.Dunia nzima timu yoyote inayo kaba kwenye High Line Ina fungwa magoli ya Namna hii kwa sababu mshambuliaji ana liangaloa goli wakati mabeki wamelipa mgongo goli kwaiyo mpaka wageuze mwili kuanza kukaba mshambuliaji ana kuwa kasogea umbali mrefu.
Kwa upande wa takwimu za ligi kuu Simba ndio timu ambayo imefungwa goli chache tu goli 3.
NASISITIZA KARIBU TENA KWA MJADALA WA KITAALAMU.
LETE TENA HOJA NYINGINE JUU YA UDHAIFU WA BEKI YA SIMBA.
 
Che Malone and Bacca wa yanga wote wanahitaji kupumzika,akili zinatoka lkn miili imechoka mno

Mchezaji ana takiwa kucheza mechi angalau 50 kwa msimu,Je tayari wamefika mechi hizo ? Ndio kwanza tuna mechi 13 au 12 za ligi na za Kimataifa 3.Kumbuka wachezaji wametoka off season walikuwa wamepumzika. Una taka kusema wamechoka mwanzo wa Msimu daaah basi itakuwa balaa.
 
Ujenge utamaduni wa kuwa mwenye subra. Mara ngapi Che Malone ameipambania Simba mkuu. Ungeniambia kufanyiwa rotation sawa lakini sio bench kwa maana ya kiwango.
 
Shida ya malon anajikutaga bonge la beki kumbe n wakawaida tu safu nzima ya ulinz n wazito ukienda viungo wazito sana ndomana simba inacheza taratibu sana
 
Mimi nimecheza mpira siyo wa kutazama tu. Kwa mfano, kocha alikuwa anasema, ni kosa kubwa kugeuzia ndani, ni lazima ugeuzie nje na ukishindwa toa mpira nje ili wenzako wasogee mjipange upya.

Makosa anayofanya Malone ni ya kitoto si ya kufanywa na mtu mwenye jina kama lake. Kwanini hakugeuzia nje bali akageuzia ndani kwa pasi fupi? Tofautisha kati ya confidence (kujiamini) na over confidence (kujiamini kupita kiasi). Over confidence ina hasara pia. Malone akiendekeza over confidence atakuwa anachomesha tu!

Malone alikuwa na uwezo wa kugeuzia nje na kupiga volley au kutoa nje ila volley ndio ilikuwa sahihi
 
Che Fondoh Malone ni beki mzuri lakini lazima tukubali beki huyu huwa anafanya makosa yanayojirudia rudia karibia kila mechi na hasa za kimataifa.
Makocha wakae naye ili kujaribu kurudisha uwezo wake.
Maana mchezaji wa ulinzi kama yeye kosa lake moja tu linatosha kuamua hatma ya timu msimu mzima.
 
Kama si Hongo kwa refa, Jana akustahili kuendelea na mchezo, Red card ya wazi ilimuhusu.
Bahati ni mechi za shirikisho hakuna anaye jali kwakua Zina hadhi ya Ndondo cup.
Nyooooko
 
Tambala mbovu unaongea kitaalam Sana

Kuwa na utulivu kijana, kunywa Maji na ushushe Sukari.Kucheza mpira hakukupi kibali Cha kufahamu mpira !!! Kucheza mpira ni kipaji na ukocha ni taaluma...hapa tuna jadili jambo la kitaalamu.Alafu usitafute huruma ya kusema eti nimecheza, Sasa ukiwa umecheza ndio hoja Yako iwe imara ?
Hivi back pass ngapi kipa Kacheza mechi hiyo ? Kunaswa hiyo ndio una taka kuhalalisha kwamba Che ni beki mbaya au wa kawaida ?
 
Nakusaidia tu kama hautaki kuona makosa kwenye mpira kaangalie mbio za Baiskeli kule hakuna makosa ya kujirudia rudia.
Mpira wa miguu sifa yake ni uwepo wa makosa ambayo ndio msingi wake.
Nitajie beki mzuri nchi hii kuliko Che Malone kwa sifa zote unazo taka.
1.Libero
2.Sweeper
Aina zote za beki wakati na sifa zao hakuna kama Che Malone Labda mpira una angalia ukiwa na mawazo kichwani.

#Jicho la kitaalamu sio jicho la kishabiki....!!! Mfano wakati Tanzania tuna sema Baka wa Yanga ni beki Bora nchini.Aliye kuwa kocha wake Nabi akiwa Far Rabat wakati ana hitaji beki wa kati aliomba timu imesajili Inonga na akisema ndio beki Bora kwa Sasa Tanzania, Je hakumuona Baka ambaye alimfundisha ?
Ukifatilia Interview ya Nabi ameongea kitaalumu Sana kuhusu ubora wa Inonga na sio Baka wetu.
Sasa basi tuna shida ya kuelewa mpira na misingi yake.
 
Labda mpe mfano wa goli la pili la Alhilal vs Yanga ataelewa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…