SoC02 Muelekeo hasi kwa Wanafunzi katika Elimu

SoC02 Muelekeo hasi kwa Wanafunzi katika Elimu

Stories of Change - 2022 Competition

Lapluto

Member
Joined
Jul 14, 2022
Posts
80
Reaction score
129
UTANGULIZI.

Elimu ni mfumo wa mafunzo utolewao mashuleni na hata katika jamii zetu tunazoishi.Elimu ni moja ya nguzo kubwa sana iletayo mapinduzi makubwa kwa kuirahisishia jamii kupambana na changamoto za kila siku ambazo huchochea maendeleo chanya kwenye sekta mbalimbali iwe kisiasa, kiuchumi, kisayansi na kiteknolojia. Mfumo wa elimu kwa Tanzania hutokewa kwa ngazi tofauti kuanzia chekechea hadi chuo kikuu, mfumo huu humuandaa mwanafunzi kupata maarifa ili atimize ndoto zake na kuisaidia jamii.

Katika kipindi cha masomo wanafunzi hukutana na changamoto nyingi sana za kielimu iwe kiujumla au kwa mtu mmoja mmoja. Kila mwanafunzi huwa na ndoto yake amvayo hutamani kuifikia kama vile kuwa mwalimu, mwanasheria, daktari pamoja na mhabdisi. Hata hivyo kuna baadhi waliofanikiwa na wengine kutofanikiwa kwa sababu mbalimbali kama vile ada, miundombinu, kufeli au kusimamishwa shule. Hivyo, muelekeo wa elimu kwao huenda kinyume na matarajio yao ambayo huzaa majuto na lawama ndani ya nafsi yake na jamii inayomzunguka. Kwa wanafunzi waliifaulu kuendelea husona masomo iwe kwa bidii au la bila kuzingatia ni masomo yapi yatanifikisha ninapokwenda ili ayashike vilivyo kwa kuyaelewa zaidi.

Baadhi ya mifano halisi ni Kama ifuatavyo :



Chando : Jukwaa la elimu

Sababu ziletazo muelekeo hasi kwa wanafunzi.
1. Kuchaguliwa mchepuo au fani (diploma) asizozitarajia, kwa mfano mwanafunzi kuchaguliwa mchepuo wa sanaa badala ya sayansi au fani ya ufundi badala ya afya(kwa ngazi ya diploma).

2.Uelewa finyu juu ya michepuo na fani husika, hapa mwanafunzi hujua baadhi ya michupuo Kama vile PCB, PCN, EGM, HKL na CBG au kozi fulani kwa mfano ualimu, udaktari na sheria.

3.Kufuata mkumbo wa wanafunzi wenzake (marafiki), mwanafunzi hushindwa kuwa na maamuzi binafsi (madhubuti) kwa kuzingatia hitaji lake. Kwa mfano kuacha baadhi ya masomo kwa kufuta mkumbo.

4. Upeo mdogo wa wazazi, ndugu na hata marafiki kuhusu uhusu masomo na kozi au fani husika. Baadhi ya wazazi au walezi hukosa au huwa hawana maarifa juu ya kipi mwanafunzi akipe kipaumbele zaidi ili afanikiwe kutimiza ndoto zake na mwanafunzi afikie malengo yake. Hivyo , wazazi wengi hukosa maarifa zaidi kutokana na kuishia ngazi za chini za elimu kama vile darasa la saba, kidato cha nne au kutokuwa na elimu kabsa.

5. Kukosa mshauri sahihi, katika maisha ya mwanadamu tunaishi kwa kutegemea. Hivyo, kuwa na mtu wa kukushauri unapokwama ni muhimu sana. Mwanafunzi hukosa mshauri sahihi mwenye maarifa juu ya masomo au fani husika iwe mzazi na hata mtu mwalingine. Kwa mfano mwanafunzi ana ndoto ya kuwa mhandisi, hivyo ili apate ushauri mzuri au mwongozo anapaswa kupata mtu sahihu mwenye uelewa wa hiyo fani.

6. Kushindwa kujua uhusiano wa masomo na fani zake kwa kina. Kutokana na kukariri mwanafunzi hujua baadhi ya miunganiko ya masomo kwa mfano PCB, PCM au HKL na kushindwa kuelewa kwa kina fani zipi zinafaa kwa mchepuo fulani.

Matokea yake kabla na baada ya kumaliza elimu.
1. Kushindwa kusoma mchepuo au fani aipendayo, kutokana na kukosa muelekeo sahihi baadhi ya wanafunzi hushindwa kusomea kitu wakitakacho. Hivyo, huishia kusoma kwa unyonge ili amalize au kuhitumu.

2. Kukosekana kwa wataalamu wenye uweledi juu ya kile walichosomea, uwajibikaji wa wataalamu huwa ni mdogo na ubunifu hutoweka kabisa. Hivyo, watatuzi wa changamoto huwa ni wachache.

3. Kuibuka kwa maswali mbalimbali kutoka kwa wanafunzi baada ya kuhitimu ngazi fulani, baadhi ya maswali hayo ni kama vile kozi ipi ina soko ?, nikisoma mchepuo huu baadae naweza somea nini ?, Je, mchupuo huu naweza soma fani hii ?. Hapo ujue mwanafunzi hana muelekeo sahihi.

4. Kurudia kusoma upya, kuna baadhi yao huweza kurudia au kusoma fani aitakayo kwa kuanza ngazi ya chini kama vile diploma na hapa huwa kashapoteza mda mwingi sana hadi kuamka.

5. Kupatwa na matatizo ya kisaikolojia, kutokana na majuto pamoja na lawama huishia kupata msongo wa mawazo na magonjwa mengine. Dharau na kutengwa na jamii nayo huwa inachochea maradhi kwa mhusika.

6. Lawama kwa jamii na hata serikali, mwanafunzi au mhitimu huanza kulaumu juu ya fani au kozi zitolewazo kwa kudai mbona wanatoa kozi ambazo hawaajiri na kusahau suala la utafutaji wa maarifa.

Mapendekezo yangu kwa jamii pamoja na serioali.

1. Kuwepo na somo litakalowapa uelewa wa uhusiano wa michupuo na fani husika. Itawasaidia wanafunzi kutambu kwa kina ni masomo yapi ayatilie mkazo zaidi kuepusha taharuki wakati wa jujiunga kidato cha tano au chuo. Somo au mafunzo haya yanaweza kutolewa mwanzoni nwa muhula wa Kwanza akiwa kidato cha kwanza na kuhakikisha wameelewa hasa muongozo wa Nacte na TCU.

2. Kila mwanafunzi anapaswa apate mshauri sahihi. Mshauri huyo anaweza kuwa ni mwalimu au mfanyakazi (aliyehitimu fani husika) wa masomo husika, kwa kufanya hivyo wanafunzi ataandaliwa kusaikolojia juu ya masomo na fani azipendazo kipindi akiwa mwanafunzi .

3. Kuwapa mda wa kutosha wa kubadili michepuo au fani, hii itapunguza hofu na jazba kwa mhusika na kupata mda wa kutosha kufikiri na kuamua kipi achague kwa wakati huo. Pia ushauri muhimu unapaswa uwepo inaweza ikawa yupo sehemu sahihi ila hana uelewa wa kutosha.

4. Kushirikisha wazazi na walezi juu ya kile ukipendacho. Katika jamii zetu kuna baadhi ya familia kama baba au mama ni mwalimu basi mtoto atalazimishwa kusomea ualimu au Kama ni nesi napo ni hivyo hivyo. Hii nayo huishia pabaya kwani mtoto atasoma kwa kinyongo bila bidii yoyote.Chanzo cha matokeo mabovu ya uwajibikaji kazini hutokana na kufanya kazi asiyoipenda , furaha yake ni siku ya mshahara tu ila siku zingine mawazo yote ni kuwaza mda wa kutoka kazini.

Hitimisho.
Napenda kuwashuru jamii na serikali kwa kuhakikisha elimu inaendelea kutolewa ijapokuwa changamoto hazikosekani lakini mafanikio yameonekana. Ukilinganisha idadi ya wasomi kwa sasa na zamani ni tofauti kwani tumeweza kupata wasomi wengi kuliko kipindi cha nyuma. Juhudi na ubunifu huanza kwa mtu mwenyewe kwa kufuata mkondo husika lakini vitu hivi hukosekana miongoni mwa wahitimu.
 
Upvote 99
Hapo ulipowataja wazazi nakubaliana na wewe kabisa katika kusoma kwangu nilisoma na binti mzazi anataka asome sayansi mtoto anataka asome biashara mwisho mtoto akapotea.

Hapo kurudia masomo upya naona umenigusa mimi kabisa lakini kurudia kwangu kulitokana na chuo wenyewe maana kozi ya chaguo langu nilipata vigezo wakati nikiwa chuoni tayari ikabidi niache nifate hisia zangu na sijawahi kujutia maamuzi yangu.

Sent from my TECNO K7 using JamiiForums mobile app
 
Siku hizi serikali imeamua wote wafaulu.
NECTA pale kuna tatizo kubwa
 
Elimu yetu kwa sasa ipo kisiasa
Ni nalo ni tatizo maana tukiwa na uongozi mbovu katika suala zima la elimu ni changamoto kubwa sana. Na ndio maana huku ngazi za chini wanashindwa kutimiza wajibu wao ipasavyo. Kingine ingawa elimu kwa asilimia kubwa ipo chini ya serikali, hivyo wazazi au walezi nao wamesahau kwenda na mwanao (mwanafunzi) bega kwa bega kuhakikisha yupo kwenye mstari sahihi. Kwa mfano mimi kama Mimi nilipaswa kuwa katika masuala ya teknolojia ila nilikosa mtu wa kuniguide nifike huko. Hata kusema kwamba PCM ndio ilinipasa nikomalie napo sikujua kabsa.
Mwisho serikali inaanza na mtu, familia hadi jamii hivyo nasi wazazi au walezi tuamke na tuhakikishe mwanafunzi anatimiza tarajio lake.
Shukrani Kama maoni yako na karibu sana.
 
Siku hizi serikali imeamua wote wafaulu.
NECTA pale kuna tatizo kubwa
haha ha, hili nalo sikupingi maana siku hizi kusikia division 1.7 au 1.3 kwa advance ni kawaida. Haoa tunaondoa uhalisia na ndio maana tunazalisha wahitimu wenye upeo mdogo.
Hi ishanikuta kwenye somo la geography nilishangaa nimepass grade kubwa kuliko nilivyotegemea.
Hivyo, tunahitaji mfumo mzuri wa elimu pamoja na washauri (sijui wanawaita role model) kwa kila fani. Kama ni afya mfano udaktari basi daktari flani apewe wanafunzi kadhaa wenye passion yako daktari, waanze kuandaliwa kisaikolojia mapema zaidi.
Ni Kama chuo utakuta kila mwanachuo ana mshauri wake basi na ngazi za chini za elimu iwe hivyo na ifanyike kwa ufasaha, hapa tutaibua product nzuri Sana.
 
UTANGULIZI.

Elimu ni mfumo wa mafunzo utolewao mashuleni na hata katika jamii zetu tunazoishi.Elimu ni moja ya nguzo kubwa sana iletayo mapinduzi makubwa kwa kuirahisishia jamii kupambana na changamoto za kila siku ambazo huchochea maendeleo chanya kwenye sekta mbalimbali iwe kisiasa, kiuchumi, kisayansi na kiteknolojia. Mfumo wa elimu kwa Tanzania hutokewa kwa ngazi tofauti kuanzia chekechea hadi chuo kikuu, mfumo huu humuandaa mwanafunzi kupata maarifa ili atimize ndoto zake na kuisaidia jamii.

Katika kipindi cha masomo wanafunzi hukutana na changamoto nyingi sana za kielimu iwe kiujumla au kwa mtu mmoja mmoja. Kila mwanafunzi huwa na ndoto yake amvayo hutamani kuifikia kama vile kuwa mwalimu, mwanasheria, daktari pamoja na mhabdisi. Hata hivyo kuna baadhi waliofanikiwa na wengine kutofanikiwa kwa sababu mbalimbali kama vile ada, miundombinu, kufeli au kusimamishwa shule. Hivyo, muelekeo wa elimu kwao huenda kinyume na matarajio yao ambayo huzaa majuto na lawama ndani ya nafsi yake na jamii inayomzunguka. Kwa wanafunzi waliifaulu kuendelea husona masomo iwe kwa bidii au la bila kuzingatia ni masomo yapi yatanifikisha ninapokwenda ili ayashike vilivyo kwa kuyaelewa zaidi.

Baadhi ya mifano halisi ni Kama ifuatavyo :



Chando : Jukwaa la elimu

Sababu ziletazo muelekeo hasi kwa wanafunzi.
1. Kuchaguliwa mchepuo au fani (diploma) asizozitarajia, kwa mfano mwanafunzi kuchaguliwa mchepuo wa sanaa badala ya sayansi au fani ya ufundi badala ya afya(kwa ngazi ya diploma).

2.Uelewa finyu juu ya michepuo na fani husika, hapa mwanafunzi hujua baadhi ya michupuo Kama vile PCB, PCN, EGM, HKL na CBG au kozi fulani kwa mfano ualimu, udaktari na sheria.

3.Kufuata mkumbo wa wanafunzi wenzake (marafiki), mwanafunzi hushindwa kuwa na maamuzi binafsi (madhubuti) kwa kuzingatia hitaji lake. Kwa mfano kuacha baadhi ya masomo kwa kufuta mkumbo.

4. Upeo mdogo wa wazazi, ndugu na hata marafiki kuhusu uhusu masomo na kozi au fani husika. Baadhi ya wazazi au walezi hukosa au huwa hawana maarifa juu ya kipi mwanafunzi akipe kipaumbele zaidi ili afanikiwe kutimiza ndoto zake na mwanafunzi afikie malengo yake. Hivyo , wazazi wengi hukosa maarifa zaidi kutokana na kuishia ngazi za chini za elimu kama vile darasa la saba, kidato cha nne au kutokuwa na elimu kabsa.

5. Kukosa mshauri sahihi, katika maisha ya mwanadamu tunaishi kwa kutegemea. Hivyo, kuwa na mtu wa kukushauri unapokwama ni muhimu sana. Mwanafunzi hukosa mshauri sahihi mwenye maarifa juu ya masomo au fani husika iwe mzazi na hata mtu mwalingine. Kwa mfano mwanafunzi ana ndoto ya kuwa mhandisi, hivyo ili apate ushauri mzuri au mwongozo anapaswa kupata mtu sahihu mwenye uelewa wa hiyo fani.

6. Kushindwa kujua uhusiano wa masomo na fani zake kwa kina. Kutokana na kukariri mwanafunzi hujua baadhi ya miunganiko ya masomo kwa mfano PCB, PCM au HKL na kushindwa kuelewa kwa kina fani zipi zinafaa kwa mchepuo fulani.

Matokea yake kabla na baada ya kumaliza elimu.
1. Kushindwa kusoma mchepuo au fani aipendayo, kutokana na kukosa muelekeo sahihi baadhi ya wanafunzi hushindwa kusomea kitu wakitakacho. Hivyo, huishia kusoma kwa unyonge ili amalize au kuhitumu.

2. Kukosekana kwa wataalamu wenye uweledi juu ya kile walichosomea, uwajibikaji wa wataalamu huwa ni mdogo na ubunifu hutoweka kabisa. Hivyo, watatuzi wa changamoto huwa ni wachache.

3. Kuibuka kwa maswali mbalimbali kutoka kwa wanafunzi baada ya kuhitimu ngazi fulani, baadhi ya maswali hayo ni kama vile kozi ipi ina soko ?, nikisoma mchepuo huu baadae naweza somea nini ?, Je, mchupuo huu naweza soma fani hii ?. Hapo ujue mwanafunzi hana muelekeo sahihi.

4. Kurudia kusoma upya, kuna baadhi yao huweza kurudia au kusoma fani aitakayo kwa kuanza ngazi ya chini kama vile diploma na hapa huwa kashapoteza mda mwingi sana hadi kuamka.

5. Kupatwa na matatizo ya kisaikolojia, kutokana na majuto pamoja na lawama huishia kupata msongo wa mawazo na magonjwa mengine. Dharau na kutengwa na jamii nayo huwa inachochea maradhi kwa mhusika.

6. Lawama kwa jamii na hata serikali, mwanafunzi au mhitimu huanza kulaumu juu ya fani au kozi zitolewazo kwa kudai mbona wanatoa kozi ambazo hawaajiri na kusahau suala la utafutaji wa maarifa.

Mapendekezo yangu kwa jamii pamoja na serioali.

1. Kuwepo na somo litakalowapa uelewa wa uhusiano wa michupuo na fani husika. Itawasaidia wanafunzi kutambu kwa kina ni masomo yapi ayatilie mkazo zaidi kuepusha taharuki wakati wa jujiunga kidato cha tano au chuo. Somo au mafunzo haya yanaweza kutolewa mwanzoni nwa muhula wa Kwanza akiwa kidato cha kwanza na kuhakikisha wameelewa hasa muongozo wa Nacte na TCU.

2. Kila mwanafunzi anapaswa apate mshauri sahihi. Mshauri huyo anaweza kuwa ni mwalimu au mfanyakazi (aliyehitimu fani husika) wa masomo husika, kwa kufanya hivyo wanafunzi ataandaliwa kusaikolojia juu ya masomo na fani azipendazo kipindi akiwa mwanafunzi .

3. Kuwapa mda wa kutosha wa kubadili michepuo au fani, hii itapunguza hofu na jazba kwa mhusika na kupata mda wa kutosha kufikiri na kuamua kipi achague kwa wakati huo. Pia ushauri muhimu unapaswa uwepo inaweza ikawa yupo sehemu sahihi ila hana uelewa wa kutosha.

4. Kushirikisha wazazi na walezi juu ya kile ukipendacho. Katika jamii zetu kuna baadhi ya familia kama baba au mama ni mwalimu basi mtoto atalazimishwa kusomea ualimu au Kama ni nesi napo ni hivyo hivyo. Hii nayo huishia pabaya kwani mtoto atasoma kwa kinyongo bila bidii yoyote.Chanzo cha matokeo mabovu ya uwajibikaji kazini hutokana na kufanya kazi asiyoipenda , furaha yake ni siku ya mshahara tu ila siku zingine mawazo yote ni kuwaza mda wa kutoka kazini.

Hitimisho.
Napenda kuwashuru jamii na serikali kwa kuhakikisha elimu inaendelea kutolewa ijapokuwa changamoto hazikosekani lakini mafanikio yameonekana. Ukilinganisha idadi ya wasomi kwa sasa na zamani ni tofauti kwani tumeweza kupata wasomi wengi kuliko kipindi cha nyuma. Juhudi na ubunifu huanza kwa mtu mwenyewe kwa kufuata mkondo husika lakini vitu hivi hukosekana miongoni mwa wahitimu.
Mtoa mada yuko sahihi sana. Ni vyema tukafanya jambo juu ya mfumo wa elimu uli kujenga kizazi chenye uwezo wa kufanya mabadiliko kwa kutumia rasilimali tulizo nazo.
 
UTANGULIZI.

Elimu ni mfumo wa mafunzo utolewao mashuleni na hata katika jamii zetu tunazoishi.Elimu ni moja ya nguzo kubwa sana iletayo mapinduzi makubwa kwa kuirahisishia jamii kupambana na changamoto za kila siku ambazo huchochea maendeleo chanya kwenye sekta mbalimbali iwe kisiasa, kiuchumi, kisayansi na kiteknolojia. Mfumo wa elimu kwa Tanzania hutokewa kwa ngazi tofauti kuanzia chekechea hadi chuo kikuu, mfumo huu humuandaa mwanafunzi kupata maarifa ili atimize ndoto zake na kuisaidia jamii.

Katika kipindi cha masomo wanafunzi hukutana na changamoto nyingi sana za kielimu iwe kiujumla au kwa mtu mmoja mmoja. Kila mwanafunzi huwa na ndoto yake amvayo hutamani kuifikia kama vile kuwa mwalimu, mwanasheria, daktari pamoja na mhabdisi. Hata hivyo kuna baadhi waliofanikiwa na wengine kutofanikiwa kwa sababu mbalimbali kama vile ada, miundombinu, kufeli au kusimamishwa shule. Hivyo, muelekeo wa elimu kwao huenda kinyume na matarajio yao ambayo huzaa majuto na lawama ndani ya nafsi yake na jamii inayomzunguka. Kwa wanafunzi waliifaulu kuendelea husona masomo iwe kwa bidii au la bila kuzingatia ni masomo yapi yatanifikisha ninapokwenda ili ayashike vilivyo kwa kuyaelewa zaidi.

Baadhi ya mifano halisi ni Kama ifuatavyo :



Chando : Jukwaa la elimu

Sababu ziletazo muelekeo hasi kwa wanafunzi.
1. Kuchaguliwa mchepuo au fani (diploma) asizozitarajia, kwa mfano mwanafunzi kuchaguliwa mchepuo wa sanaa badala ya sayansi au fani ya ufundi badala ya afya(kwa ngazi ya diploma).

2.Uelewa finyu juu ya michepuo na fani husika, hapa mwanafunzi hujua baadhi ya michupuo Kama vile PCB, PCN, EGM, HKL na CBG au kozi fulani kwa mfano ualimu, udaktari na sheria.

3.Kufuata mkumbo wa wanafunzi wenzake (marafiki), mwanafunzi hushindwa kuwa na maamuzi binafsi (madhubuti) kwa kuzingatia hitaji lake. Kwa mfano kuacha baadhi ya masomo kwa kufuta mkumbo.

4. Upeo mdogo wa wazazi, ndugu na hata marafiki kuhusu uhusu masomo na kozi au fani husika. Baadhi ya wazazi au walezi hukosa au huwa hawana maarifa juu ya kipi mwanafunzi akipe kipaumbele zaidi ili afanikiwe kutimiza ndoto zake na mwanafunzi afikie malengo yake. Hivyo , wazazi wengi hukosa maarifa zaidi kutokana na kuishia ngazi za chini za elimu kama vile darasa la saba, kidato cha nne au kutokuwa na elimu kabsa.

5. Kukosa mshauri sahihi, katika maisha ya mwanadamu tunaishi kwa kutegemea. Hivyo, kuwa na mtu wa kukushauri unapokwama ni muhimu sana. Mwanafunzi hukosa mshauri sahihi mwenye maarifa juu ya masomo au fani husika iwe mzazi na hata mtu mwalingine. Kwa mfano mwanafunzi ana ndoto ya kuwa mhandisi, hivyo ili apate ushauri mzuri au mwongozo anapaswa kupata mtu sahihu mwenye uelewa wa hiyo fani.

6. Kushindwa kujua uhusiano wa masomo na fani zake kwa kina. Kutokana na kukariri mwanafunzi hujua baadhi ya miunganiko ya masomo kwa mfano PCB, PCM au HKL na kushindwa kuelewa kwa kina fani zipi zinafaa kwa mchepuo fulani.

Matokea yake kabla na baada ya kumaliza elimu.
1. Kushindwa kusoma mchepuo au fani aipendayo, kutokana na kukosa muelekeo sahihi baadhi ya wanafunzi hushindwa kusomea kitu wakitakacho. Hivyo, huishia kusoma kwa unyonge ili amalize au kuhitumu.

2. Kukosekana kwa wataalamu wenye uweledi juu ya kile walichosomea, uwajibikaji wa wataalamu huwa ni mdogo na ubunifu hutoweka kabisa. Hivyo, watatuzi wa changamoto huwa ni wachache.

3. Kuibuka kwa maswali mbalimbali kutoka kwa wanafunzi baada ya kuhitimu ngazi fulani, baadhi ya maswali hayo ni kama vile kozi ipi ina soko ?, nikisoma mchepuo huu baadae naweza somea nini ?, Je, mchupuo huu naweza soma fani hii ?. Hapo ujue mwanafunzi hana muelekeo sahihi.

4. Kurudia kusoma upya, kuna baadhi yao huweza kurudia au kusoma fani aitakayo kwa kuanza ngazi ya chini kama vile diploma na hapa huwa kashapoteza mda mwingi sana hadi kuamka.

5. Kupatwa na matatizo ya kisaikolojia, kutokana na majuto pamoja na lawama huishia kupata msongo wa mawazo na magonjwa mengine. Dharau na kutengwa na jamii nayo huwa inachochea maradhi kwa mhusika.

6. Lawama kwa jamii na hata serikali, mwanafunzi au mhitimu huanza kulaumu juu ya fani au kozi zitolewazo kwa kudai mbona wanatoa kozi ambazo hawaajiri na kusahau suala la utafutaji wa maarifa.

Mapendekezo yangu kwa jamii pamoja na serioali.

1. Kuwepo na somo litakalowapa uelewa wa uhusiano wa michupuo na fani husika. Itawasaidia wanafunzi kutambu kwa kina ni masomo yapi ayatilie mkazo zaidi kuepusha taharuki wakati wa jujiunga kidato cha tano au chuo. Somo au mafunzo haya yanaweza kutolewa mwanzoni nwa muhula wa Kwanza akiwa kidato cha kwanza na kuhakikisha wameelewa hasa muongozo wa Nacte na TCU.

2. Kila mwanafunzi anapaswa apate mshauri sahihi. Mshauri huyo anaweza kuwa ni mwalimu au mfanyakazi (aliyehitimu fani husika) wa masomo husika, kwa kufanya hivyo wanafunzi ataandaliwa kusaikolojia juu ya masomo na fani azipendazo kipindi akiwa mwanafunzi .

3. Kuwapa mda wa kutosha wa kubadili michepuo au fani, hii itapunguza hofu na jazba kwa mhusika na kupata mda wa kutosha kufikiri na kuamua kipi achague kwa wakati huo. Pia ushauri muhimu unapaswa uwepo inaweza ikawa yupo sehemu sahihi ila hana uelewa wa kutosha.

4. Kushirikisha wazazi na walezi juu ya kile ukipendacho. Katika jamii zetu kuna baadhi ya familia kama baba au mama ni mwalimu basi mtoto atalazimishwa kusomea ualimu au Kama ni nesi napo ni hivyo hivyo. Hii nayo huishia pabaya kwani mtoto atasoma kwa kinyongo bila bidii yoyote.Chanzo cha matokeo mabovu ya uwajibikaji kazini hutokana na kufanya kazi asiyoipenda , furaha yake ni siku ya mshahara tu ila siku zingine mawazo yote ni kuwaza mda wa kutoka kazini.

Hitimisho.
Napenda kuwashuru jamii na serikali kwa kuhakikisha elimu inaendelea kutolewa ijapokuwa changamoto hazikosekani lakini mafanikio yameonekana. Ukilinganisha idadi ya wasomi kwa sasa na zamani ni tofauti kwani tumeweza kupata wasomi wengi kuliko kipindi cha nyuma. Juhudi na ubunifu huanza kwa mtu mwenyewe kwa kufuata mkondo husika lakini vitu hivi hukosekana miongoni mwa wahitimu.
Kazi nzuri brother
 
Mkuu nioneshe ni sehemu gani hapo kuna hako kaalama?View attachment 2299356
Maxence Melo inabidi ifike hatua mtusikilize na sisi watu wa Mobile App. Kuna baadhi ya features kwetu hazipo kabisa, Yani ni kama vile kipaumbele chenu ni Web users.

Katika ili jukwaa, watu wa Mobile hatuwezi kabisa kupiga kura. Yani ni mpaka tukalogin kwenye website. Tunaomba mtuangalie
 
Maxence Melo inabidi ifike hatua mtusikilize na sisi watu wa Mobile App. Kuna baadhi ya features kwetu hazipo kabisa, Yani ni kama vile kipaumbele chenu ni Web users.

Katika ili jukwaa, watu wa Mobile hatuwezi kabisa kupiga kura. Yani ni mpaka tukalogin kwenye website. Tunaomba mtuangalie
tumia app ya sasa mkuu
 
Back
Top Bottom