Muendano wa kimawazo katika ndoa.

Muendano wa kimawazo katika ndoa.

Shanily

JF-Expert Member
Joined
Nov 4, 2024
Posts
856
Reaction score
1,662
Ndoa nyingi za sasa zinavunjika kwakua watu wanaoa au kuolewa na watu ambao hawaendani nao.

Mnaweza nyote mkawa na dini, tabia nzuri lakini ndoa ikafa kwakukosa muendano wa kimawazo.

Kuna wanaume wao ndo wanataka wawe dominate kwa 100% yaani huna Cha kumwambia, neno lake ndo katiba huyu akitaka adumu ndoani aoe yule mwanamke wa tumeskia na tumetii, Chochote hewala.
Shida inakuja kakuta bint ana tabia zake nzuri lakini ni 50/50, anapenda ushirikishwaji katika mambo, maoni yangu yaheshimiwe pia , hapo lazima watasumbuana na ikafikia talaka maana mke atahisi kaachwa nyuma, vinyongo vinaanza.

Au mwanamke anataka yeye ndo awe mwenye kauli ya mwisho, anaenda kuolewa na mtu anaetaka kuwa mwenye kauli ya mwisho pia, hapo kizaazaa kinaanza, halafu shida tunajipa moyo atabadilika. Tabia ni kama ngozi ya mwili vigumu kuibadili.

Kwahy katika vigezo vya mwenza umtakae muhimu pia kuongeza kigezo cha muendano wa kimawazo ili tupunguze hizi talaka za Kila siku katika zama hizi za teknolojia.
 
Hakuna kitu mtawaambia kataa ndoa wakawaelewa, 400 wake za watu tena mabosii🤔
 
Kujua mtizamo au mawazo ya mtu ni hadi ukae upige nae story ambazo majibu yake yanahusu fikra za msingi katika maisha.

Sasa kibaya wadada wakiwa wanatongozwa wanawaza Mengine kabisaaaa, kengine unakuta hakana hata story kenyewe ni kuitikia tu, ndio, asante, nimependa, nitakumiss, me to story hadi mwanaume aanzishe.
 
Kujua mtizamo au mawazo ya mtu ni hadi ukae upige nae story ambazo majibu yake yanahusu fikra za msingi katika maisha.

Sasa kibaya wadada wakiwa wanatongozwa wanawaza Mengine kabisaaaa, kengine unakuta hakana hata story kenyewe ni kuitikia tu, ndio, asante, nimependa, nitakumiss, me to story hadi mwanaume aanzishe

Kujua mtizamo au mawazo ya mtu ni hadi ukae upige nae story ambazo majibu yake yanahusu fikra za msingi katika maisha.

Sasa kibaya wadada wakiwa wanatongozwa wanawaza Mengine kabisaaaa, kengine unakuta hakana hata story kenyewe ni kuitikia tu, ndio, asante, nimependa, nitakumiss, me to story hadi mwanaume aanzishe.
Waweza mjua mtu kwa maongezi yake hayo hayo kwamba ni wa karba gani. Mfano huyo ni wale wa tumeskia na tumetii, Hana mawazo yake binafsi Bali yeye ni kuitika tu.
 
Ndoa nyingi za sasa zinavunjika kwakua watu wanaoa au kuolewa na watu ambao hawaendani nao.
Tatizo unaempenda hata hathamini huo upendo....lazima tuangukie pua
 
Back
Top Bottom