Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM


Mkandara
Mkuu ulianza vyema sasa naona mnatupeleka kwenye malumbano.
swala la siasa na dini zinaharibu mwanzo/msingi mzuri wa hoja ambazo ulikuwa umezianzisha. Kama kweli CCM ndo ina msimika mufti hilo litakuwa ni tatizo la waumini wenyewe maana ninaimani CCM siyo ya wakristo tu
na wala siyo ya waislamu tu.
tuzungumzie faida na hasara za mahakama hii ili kwa wale wasiokuwa na mwanga walione wawe na maamzi sahihi.
Maswala ya UWT ni ya kisiasa zaidi.
 
..OK, fainally nimepata sehemu ambako kuna MCHANGO WA KITAALAMU.

..ni muhimu suala hili likaangaliwa kitaalamu kuliko kulumbana na kunyoosheana vidole kuhusu Vatican, OIC, etc etc.

..nawaomba wanachama mbonyeze hapa kupata maoni ya kitaalamu.

Huko bado hakuna msaada wa kisheria kwani mchambuzi yupo ndani ya box, haoni nje ya box alilomo. hapo hakuna msaada wala maoni ya kitalaam.
 
Hapa ndio tulipasubiri. Ama kwa hakika imechelewa sana kutokea hii incident. sisiemu inatakiwa ifie mikononi kwa Mungu kwa kuwa Lucifer au shetwani mkuu ana share humo hataweza kutoa hukumu ya haki. After all shetani si mtoa hukumu. Any how sisiemu kwishne! Na walivyo wamero utasikia hili swala tumeliundia tume, ili tu wapate kura baada ya waislamu kuikataa sisiemu. wait and see and see their strategy. Ni huligans hawa tuwapige chini tu. Bado wale wanaodai ndoa za jinsia moja waje n.k. yao. SISIEMU red light ya kwishne. End of the road and magic tricks! Ila pia chama kingine kitakachotawala hakitakubali hiyo mahakama ya kadhi pia badala yake kitarekebisha/kubadilisha katiba na waislamu watakuwa roho kwatu
 
Nziku said:
Huko bado hakuna msaada wa kisheria kwani mchambuzi yupo ndani ya box, haoni nje ya box alilomo. hapo hakuna msaada wala maoni ya kitalaam.

Nziku,

..of course mtoa mada ktk hiyo website ni Muislamu. ni vigumu kupata mchangiaji asiyekuwa na dini katika suala hili.

..ninaweza nisikubaliane na conclusions zake lakini kilichonivutia ni kwamba ana nukuu vifungu vya sheria na katiba yetu.

..binafsi nadhani huo ni mwanzo mzuri kuliko kujadili suala hili kwa hisia-hisia tu.

..mpaka sasa hivi majadiliano haya yamekosa maoni[hata yaliyo ndani ya boksi] yenye uzito wa kitaalamu.
 
Hili suala linakuwa gumu sababu linajadiliwa kidini zaidi. Waislamu kwa kuweka dini mbele wengi watasema mahakama ya kadhi ni muhimu. Wakristu nao obvius hata mtoto mdogo ambaye hajui ili wala lile ukimuuliza atakuambia mahakama ya kadhi kwa ajili ya waislamu ni NO. Na ukija kwa mkristu au muislamu muadilifu ambaye yuko kwenye decicsion making ya sheria ya serikali ambayo haina dini naye atakuambia NO kwa mahakama ya kadhi

Lakini sasa ukweli ulio wazi ukiondoa mtazamo wa kidini kwa dhati kabisa jibu lako pia litakwenda kule kwa wakristu ambako ni NO kwa mahakama ya kadhi.

Ni logical kwa nini uweke mahakama kwa ajili ya dini fulani wakati serikali haina dini? Inaweza kuwa na faida kwa waislamu tena faida kubwa lakini je itakuwa na effect kwa watatakiwa kuhukumiwa na mahakama hii ambao si waislamu.

Hili jambo ni vigumu zaidi kusukumw ana rais ambaye ni muislamu . Akija rais mkristu akimua anaweza kuchukua risk hiyo. Ni risk kubwa zaidi kwa rais muislamu kuchukua risk hiyo.

Ukweli ni kuwa ukiondoa mtazamo wa kidini na kuwa na mtazamo wa kiserikali isyokuwa na dini hili suala la mahakama ya kadhi halitekelezeki na ni tatizo.
 
Zing,

..waziri wa sheria na katiba ametoa uamuzi wa serikali bungeni.

..maana yake ni kwamba huo ndiyo uamuzi wa Baraza la Mawaziri, na Raisi Kikwete ndiye mwenyekiti wa baraza hilo.

..kwa kuwa jibu la serikali ni NO kwa mahakama ya Kadhi, basi RAISI KIKWETE ana nafasi nzuri zaidi ya kutumia busara zake kuwaelewesha na kuwatuliza Waislamu ambao hawajaupokea uamuzi huo vizuri.

..suala hili ni kipimo cha maturity na uwezo wa kisiasa wa Raisi wetu.
 
Zing,

Ni vigumu sana kujadili suala la kidini halafu hisia za kidini zisiingie. Labda tuwaachie walijadiri watu wasio na dini. Kimsingi dini ni taasisi ambazo zina ubinafsi uliokithiri. Kwa sababu kila dini inaamini kuwa yenyewe ndo sahihi. Hili linaingia kwenye mioyo ya wana dini, ndo maana kwa kweli wanakuwa wafuasi wa dini hii.

Huwezi ukapata objectivity yoyote unapojadili suala la kiislam wakati wewe ni mwislam halafu unayejadili naye si mwislam. Mwislam husimama katika uislam ndo akatoa hoja. Vivyo hivyo mkristo naye husimama katika ukristo wake. Hapo mjadala huwa ni kati mbwa na mbuzi. Huwezi kuwaelewa hata kama wewe huna dini!!
 

Shingo,

..uko sahihi 100%.

..lakini tunapaswa kujifunza kuyajadili masuala ya KIDINI kwa hekima na ustaarabu na kufikia muafaka kwa manufaa yetu SOTE.

NB:

..kama umeufuatilia mjadala huu, na ukawajua wachangiaji wake, basi utagundua kwamba wengi mawazo na misimamo yao haijabadilika kwa miaka kama 2 sasa.

..kwa maana nyingine hakuna walichojifunza toka kwa wachangiaji wenzao.
 
Shingo,

Ndio maana wanashangaa kwa nini rais muislamu halisukumi suala hili. Ukweli ni kuwa hata kama ni musilamu awe rais , PM au mwansheria mkuu akiweka uadilifu mbele na dini pembeni basi jibu litakuwa NO.

Na kama ni kuamua kutokuwa muadilifu basi JK atamuachia rais asiye muislamu ili aje apindishe na kufumba macho. Nionavyo mimi kuna risk kubwa zaidi rais muislamu akisema yes kwa mahakama ya kadhi kuliko mkristu.

Hivyo hivyo kutakuwa risk au impact kubwa zadi kwa CCM rais mkrisru akisema NO to mahakama ya kadhi.
 
Mzee Mwanakijiji,

Mkuu pengine nianze kwa kusema samahani ikiwa nimekukwaza.. Kalini siku zote mimi huandika with Authority ktk swala nalolifahamu - hoja zenye Critics huzijibu kwa critics sikuanza mimi kuuliza hayo..

Naam!

Nimetumia UWT kama mfano na ajabu wewe umerukia UWT kwa sababu tu unafahamu hicho ni chombo cha CCM.. kisha ukaendelea kusema, wewe ukiwa mwana CCM una haki ya kuuliza.

Ni kweli.


Tatizo si mimi; ni wao waislamu hawataki sisi wengine tuwaachie suala hilo walizungumzie wenyewe. Wanajitahidi kwa kila hali kutuhusisha sisi wengine.

Na unaposema CCM ndio hugharamia UWT una maana gani?, hizo fedha wanazipata toka wapi ikiwa CCM haina miradi ya kukiendesha chama hicho bila nguvu ya Watanzania wote..

CCM ina miradi yake na inapata ruzuku kama chama cha siasa. Mambo yao ya ndani ya chama na jumuiya zao ni wanachama wao ndio wanatakiwa kufuatilia na pale yanapokuja masuala ya ruzuku inayotoka serikalini kuna vyomo vinavyofuatilia hilo kwa niaba yetu na tusiporidhika tunatumia wawakilishi wa watu Bungeni kufuatilia masuala hayo na hata kubadili sheria.


Mkuu vyama vyote nchini mkuu vinaendeshwa na sisi wananchi iwe CCM, Chadema, CUF na kadhaliika.

Hili si kweli isipokuwa kwa maana pana sana. Vyama vya siasa vinaendeshwa kwa mujibu wa katiba zao na kwa mujibu wa sheria ya vyama vya siasa. Mtu asiye mwana CCM hawezi kwenda kupiga kura kuchagua kiongozi wa CCM au mtu asiye NCCR hawezi kwenda kupiga kura kuchagua viongozi wa NCCR ati kwa vile yeye ni Mtanzania tu.

Pinda, majibu yake huyo si mjali sana kwa sababu moja ana mazoea ya kutoa kauli za kinyume cha sheria na ndio maana tayari nimeshampinga mara kadhaa. HIvyo, kwangu si mfano mzuri.

Kifupi ni lazima ukubali kwanza kwamba unaandika ukiwa kabatini hivyo ni vigumu kwako kuweza kuona nje ya kabati hilo..

na wewe unaandika kutokea wapi, kwenye droo ambamo hutaki kutoka?
Maneno yako ni mazito sawa na viongozi wa CCM ambao malalamiko ya vyama vingine kama Chadema, CUF na TLP huyaona upuuzi mtupu na malalamiko ya watu waliochioka..

Ukiangalia sana utaona kuwa mimi ninatetea uhuru wa Waislamu kushika dini yao kuliko wewe au watu wengi humu. Waislamu wana hoja nzito na ambazo kama jamii hatuwezi kuzipuuza au kuzitupa pembeni. Kama tunataka kujenga taifa la watu wamoja kweli ni lazima tuondoe haya mazoea ya kujitenga kwa minajili ya kidini.


Wanaweka dharau badala ya kuzingatia kwamba kikatiba, kuwepo kwa demokrasia ndiyo inawapa wao nafasi ya kuongoza..Sasa

Kuna ukweli hapo.
ubaya wako ni pale unaposhindwa kuelewa kwanza malalamiko ya Waislaam na chombo chao kama vile CCM na viongozi wake wanapofumba macho ktk maswala ya vyama vinginevyo, hata kama hakuna haki ama utaratibu mzuri.

Sikujua kuwa CCM ni chombo cha Waislmu. Kama ni hivyo basi wana haki ya kuilalamikia; lakini kama CCM ni chombo cha Wakristu, Waislamu, wenye imani na wasio na imani, basi Waislamu wanapoleta malalamiko kwa CCM wanalazimisha na wasio waislamu kuyatolea maoni, isipokuwa kama CCM iwaweke nje wasio waislamu ili ishughulikie matatizo ya Waislamu kitu ambacho kitakuwa ni kinyume na Katiba ya kwao na ya Taifa.

Je, unafikiri malalamiko mengi ya vyama kama Chadema ni uzushi mtupu? Sii kweli vyombo vya Usalama, NEC na vyombo vya serikali husimama upande wa CCM ktk chaguzi za Kitaifa?.

irrelevant.

.Na pengine mawaziri khutumia fedha na mali za serikali ktk kampeni za chama CCM..Kwa nini unaona hakuna haja ya CCM kuyatazama maswala haya au mapendekezo ya vyama vingine..

Immaterial.
NMi kwa sababu CCM wanafikiria kwamba wao ndio watawala milelel huu mfumo wa vyama vingi ni geresha tu kwa nchi za magharibi..

Tukikubali itakuwa hivyo.
Hivyo wewe pia unaona uhuru kwa waislaam ni geresha tu nchi yetu ni ya Kikristu na itaendeshwa kikristu..

Huo ni mtazamo wako si wangu.

Restriction ziendelee kama kawaida, hawataki wajikate wakaunde serikali yao. Siji wapi huko! ndio maneno yenu toka tuanze mada zinazohusu Waislaam..

Hakuna mtu anayeweza kufanya jambo lolote wakati wowote na kwa namna yoyote in pluralistic society. Hivyo restrictions zitakuwepo ili kuhakikisha jamii inaishi kwa amani.
Mkuu umeuliza hapo juu maswali ya A na B, kisha ukatoa suluhu ya C bila kufahamu kwamba Magistrate Court Act ya nchi yetu ina restrict matumizi ya islamic law ktk mahakama zetu.

Sasa unataka Islamic laws zote zitumike kwenye mahakama zetu? Maana nimemuuliza mtu mmoja hapo nyuma wanaposema "islamic laws" wanazungumzia nini kwa maana tafsiri yake ni pana mno. Je, Mahakama zetu ziruhusu the full extent of islamic jurisdiction and juriprudence pasipo kuweka mipaka yoyote? Kama ni Ndio, kwanini tusitangaze tu kuwa tuna dual legal system ambapo tuna Sharia Laws na Western Laws?

.Kisha unahoji kwa nini waislaam wasitumie sheria zao. Hapa unafikiri nitakujibu vipi kama sii kuwa open minded (kutoka ktk kabati la udini) ukaelewa hoja ya Waislaam.

Waislamu tayari wanatumia sheria zao katika Tanzania. Jinsi inavyozungumzwa ni kana kwamba Waislamu hawatumii sheria zao kwamba wanazuiliwa. Nimeshatoa mfano wa Ndoa na Talaka ambapo sheria za Kiislamu zinatambuliwa na sheria za Tanzania.

Swala hili ni sawa na lile la Bakwata kama unakumbuka tuliwahi kujadili mwka jana.. nikasema Bakwata ni chombo kilichoanzishwa na serikali. yaani sisi wote kwa mjumuiko wetu tunahusishwa moja kwa moja na Bakwata ktk matumizi yake..

Miaka 40 iliyopita lilifanyika hilo na leo kuna Mamilioni ya Waislamu, kwanini wasiivunje na kuunda chombo chao wanachokitaka wao? Leo hii kuna vyombo vingine vya Waislamu kwanini wasiamue kuachana na Bakwata na kukisababisha kife halafu wakajiunga na kupromote vile vingine. Kama Waislamu wanajiunga na kuikubali Bakwata hili si la mtu mwingine kulaumiwa.

we ask for that (Muslims and Christians), sasa ikiwa kuna swali waulize serikali na sii Waislaam ambao wangependa sana kujiongoza wao wenyewe bila baraka za serikiali.

Hapa ndipo tatizo. Hamtaki serikali iingilie lakini wakati huo huo mnaitaka serikali iingilie. Isipoingilie mnasema serikali inatupuuza, ikiingilia mnasema serikali imetuingilia mambo yetu. Serikali ikivunja Bakwata kuna watu watalalamika kwanini wavunje chombo chetu, na ikiachilia watu wanasema kwanini Bakwata imeundwa na serikali. Serikali iunde mahakama ya kadhi watu wanadai, watu wanaohusika na uundwaji huo serikalini wakianza mijadala watu wanauliza hatutaki wakristu watolee maoni na wasishiriki kwani hili ni suala la WAislamu!

Wewe kama Mkatoliki unajua fika kwamba Pengo hachaguliwi wala kuteuliwa na serikali ama Rais na hata ukitazama dini nyingine zote isipokuwa Waislaam.

Ndiyo, kwa sababu Ukatoliki una muundo wake na kanuni zake ambazo zinaongoza Kanisa hilo pote duniani. Waislamu na wenyewe wangekuwa na muundo wao. Lakini leo hii Mufti hachaguliwa na serikali hupigiwa kura kwa mujibu wa Katiba ya Bakwata. Kama Waislamu hawaridhiki na muundo huo wabadilishe.

serikali au niseme CCM, imeingiza mkono wake ndani ya dini hii kiasi kwamba hata Mufti ni pandikizi la chama. Huyu anapewa nguvu ya kuchagua na kufukuza kiongozi yeyote wa dini kama atajisikia kufanya hivyo..

Waislamu wanakuwa wapi Mufti akifanya hivyo?

Unakumbuka mara ya mwisho alipokuwa India alifukuza uongozi wote wa Bakwata na kuweka mpya bila vigezo vya kidini isipokuwa maamuzi yake yalitokana na hitilafu za uongozi wa chama Bakwata. Bakwata ni chama under CCM zaidi ya kuwa jumuiya ya Waislaam.

Waislamu wapo ambao wamejiunga na Bakwata. Wapo waislamu ambao wanakubali hilo na wanaendelea kuffanya hivyo. Na wapo Waislamu ambao hawakubaliani na hilo na wameanzisha jumuiya zao wenyewe. Sasa nani awaunganishe Waislamu? serikali? Kwanini Waislamu wa Tanzania kama vile walivyokutana kutoa tamko lao juu ya Mahakama ya Kadhi wasiamue kukutana na kusema tunaamua kuvunja Bakwata na kuunda jumuiya mpya ya Waislamu ambayo itakidhi mahitaji yetu, halafu tuone kama serikali itawakatalia.


Kwa hiyo wale walioko Bakwata siyo Waislamu? Kule Zimbabwe kina Morgani hawakumkubali Mugabe kwa muda mrefu hadi walipolazimisha mabadiliko. Ni makosa kwa watu wenye utashi wao kulazimishwa kukubali kitu ambacho mioyoni mwao hawakikubali. Kama Bakwata haiwakilishi maslahi ya Waislamu basi Waislamu wajitoe an kujitenga nacho na kuunda chombo wanachokiona kinafaa. Hii ndiyo demokrasia na huu ndio uchaji.

Ni hayo tu mkuu wangu ikiwa utakuwa open minded ukaelewa matatizo ndani ya Uislaam nchini ni rahisi sana kuweza kuona point nayozungumzia lakini unapokuja na hoja zilizopigwa mhuri ni vigumu kwako kuweza kuelewa.

Ninaulewa Uislamu vizuri sana kuliko watu wengi humu. Siyo kwa juu juu.


Ukristu umeshambuliwa tangu mwanzo hivyo, hata ukiikosoa na kuushambulia siyo jambo geni. Kwa miaka 2000 ukristu umepitia kila aina ya madudu na ukosoaji hivyo ukijisikia kuukosoa ukosoe tu.

Na kutokuwa kwangu Mkristu haina maana najitenga na wakristu wote, mambo yao yote na siwezi kula nao sahani moja..Nikifikia hapo ni upofu na hakikka nitakuwa nimejifungia ktk kabati la Udini.

Nadhani umeshajifungua tatizo huoni kama umejifungia kwani la kwako yawezekana ni la kioo!
 

Mkuu haya maneno mekundu ndio mtazamo wa wengi wenu hapa na ndio sababu nikasema mtoke ktk hilo box.. Tunapolalamikia serikali au niseme CCM hatuna maana ni chombo cha Wakristu au Waislaam..Hakuna hata sehemu moja nimeihusisha dini ya Kikristu na CCM au serikali isipokuwa nimesema sheria nyingi zinazotumika ktk kesi za madai, huko Kortini (Primary Court), zinafuata sheria tulizopandikizwa na nchi za Magharibi ambazo kwa kiasi kikubwa zimefuata misingi ya Kikristu..
Je, ni vibaya Waislaam kuomba sheria zao zitumike pia? sidhani kama ni kosa kikatiba na hakuna mtu aliyesema sheria za zamani ziondolewe kwa sababu ni za Kikristu - hakuna. Na binafsi nina hakika ingekuwa ni kinyume yaani sheria za sasa hivi ni za kiislaam, basi Wakristu wasingekubali kabisa. Wangetaka sheria zote zibadilishwe na sii kuomba sheria zao zitumike pia ktk maswala ya ndoa na mirathi yao. Kwa hiyo ni vizuri kuangalia Waislaam wanataka kitu gani badala ya kuanza kpayuka ovyo bila kuelewa nini hasa kinachowazuia.

Sheria hizi zitakubalika tu ikiwa nchi yetu inafuata dini moja nayo ni ya Kikristu lakini maadam tumetoa uhuru kwa dini nyinginezo kama alivyosema Mwakanakijiji ktk swali lake la A na B iweje maamuzi ya maswala hayo yasifanywe kwa sheria za Kiislaam zilizowafungisha ndoa na kadhalika..Binafsi iwe mahakama ya kadhi au sio kinachonipa shida kuelewa ni uhuru waliopewa waislaam ktk maswala ya ndoa, mirathi na kadhalika wafuate mafundisho ya dini lakini inapofikia maamuzi ktk matatizo, hizo sheria za dini hazitambuliwi..Nina tatizo kuelewa hapa! na ndio muda wote nimekuwa nikizungumzia.

Binafsi sina malumbano ya kidini kuhusiana na maamuzi ya seriakali. Wapo wanaoamini kwamba kanisa Katoliki lina mkono ndani ktk maamuzi mengi ya serikali.. hao ni wao sii mimi, hivyo nihukumiwe kwa maandishi yangu..

Jokakuu,

Mkuu swala hili ni Ibada kwa Waislaam kutokana na sababu zile zile walizopewa kuabudu mwanzoni..Ibada haikomei pindi wanapooana tu ila huenda hadi kuachana, mirathi na hata kuingia kaburini.. Waislaam wanalipeleka swala hili Bungeni kwa sababu ndiko kwenye sheria kikatiba inayowapa ruksa kuendesha mambo yao ya dini kama walivyopewa wengine..

Hivyo maamuzi yote ya Sheikh au Ulamaa ktk maswala haya yanatakiwa kutambuliwa kisheria. Ikiwa MCA haitambui maamuzi ya nayotokana na islamic law unategemea naniu ataweza kukubali hukumu au settlement zilizofikiwa..
Sheria ni mwongozo mkuu wangu, leo hii tunalazimika Waislaam kuitambua Bakwata kama chombo cha Waislaam.. unataka wafanye nini kinyume kama sii kuitwa magaidi ambao wanahatarisha Usalama wa taifa. Unamkumbuka Sheikh Kassim Bin Jumaa alichokuwa akipinga ni uhalali wa Bakwata na akaanzisha chombo cha Waislaam kwa waislaam toka kwa Waislaam (Balukta), unajua yaliyomkuta!.. alitiwa Lupangoi akafanyiwa mambo mengi machafu hadi akatuondoka hivi hivi tu...Wengi walisherehjekea sana kukamatwa na hata kufa kwake..

Kwa hiyo, ikiwa Bunge litaweza kutambua sheria za kiislaam ktk maswala wanayoyataka iwe kwa kupitia vyombo vyetu vya sheria ni lazima MCA itawapa vifungu vya kutumia..Huo ndio mwongozo wa nchi, sheria yoyote ni lazima ikubalike Bungeni laa sivyo basi tutakuwa tunarudi nyuma katika sunia ya Wagagagigikoko!
Bunge letu wakiingiza baadhi ya sheria ambazo zinahusiana na ndoa, mirathi na mengineyo toka kwa waumini wake - binafsi, sidhani kama kuna haja ya kuwa na mahakama ya kadhi. Naamini kabisa kwamba kjazi inayotakiwa kufanywa na chombo hicho inaweza kabisa kutumika na kufanya kazi ktk mahakama zetu..Haijalishi kama Liwali ni mkristu au Muislaam, kwa sababu hadi leo tunahukumiwa na sheria au watu wenye imani za dini tofauti haina maana makosa mengi ktk hukumu hutokana na imani ya hakimu ktk dini.. Sheria ya Katiba ndiyo inamwongoza Liwali, Makimu au mtu yeyote ktk kutoa maamuzi..Alichojaribu kusema huyo Naibu Mufti ni kwamba 2+2 inaweza kuwa na jibu tofauyti ikiwa waumini ni dini tofauti, wakati uwezo wa kutoa hukumu hufuatana na elimu na sii imani ya mtu..
 
Last edited:


mimi ni mtoto wa nje na nina haki sawa kama watoto wa ndani na hapo ndio tunapotaka mambo ya mirathi yote yashughulikiwe na serikali na sio dini na ndugu...


Kuna akina mama waliozaa na akina baba wa kiislaam nao wanafungua kesi wapate mirathi !
ni haki yao kudai kila siku umuoni JK na wanawake wakitaka usawa

kama matatizo ya misikiti mnashindwa kuyatatua ndio mtayaweza matatizo mengine kweli, mzigo uliokuwa na kichani unakushinda bado unataka uongeze uzito. Hiyo ya ugomvi wa misikiti ni ref tosha kwamba mambo inabidi yaende kiserikali...


hii ni dhairi kwamba wewe unapenda sana sheria za ukandamizaji
kesi zinachukua mda mrefu ni kwa ajili ya resource ndogo za mahakama, na pili kesi zikienda maakamani nyingine ni straight forward na nyingine zinachukua mda mrefu kutokana na complication na hii ni kawaida, kitu kingine ni mawakili wa pande zote mbili
wacha kuongea kama huna akili kwani wakifyatuka unadhani ni hasara kwa nani, hizo vurugu unazotishia kila mtu anapenda amani na kama vurugu kila mtu atadhurika hata hao wanaonzisha vurugu
 
Semilong,
Mkuu sheria zetu nchini zinachukua kila upande isipokuwa toka sheria za Kiislaam. Kama wewe ni mtoto nje ya ndoa lakini wazazi wako ni Waislaam hapo ndipo napoingia mimi kupinga mahakama ya kadhi ..Nikasema maswala ya ndoa, mirathi na kadhalika ni maswala ambayo yanatakiwa kutazama WATU na MAZINGIRA kabla ya kutoa au kupitisha sheria..Ni bora zaidi kutumia sheria zao ktk vyombo vyetu kuliko kufungua mahakama ya kadhi ambayo viongozi wake hubariki ndoa za kiujanja ujanja. Hubariki vitu vingi visivyofuata Uislaam, leo kwa sababu kuna ulaji wanataka tuwape jukumu kubwa la kuchezea maisha ya watu..

Ili sheria zitakazotungwa ziweze ku cover sehemu zote za imani ktk maswala haya kwa faida ya Wanawake na watoto. Kwa sababu hata dini ya Kikristu haitambui mtoto wa nje ya ndoa.. hivyo sii swala la Uislaam au Ukristu ila ni swala la kuingiza baadhi ya sheria za kiislaam kuhusiana na maswala ambyo hadi leo hii yameleta utata mkubwa ktk jamii za kiislaam.
Ikiwa dini ya Kiislaam/Kikristu haziruhusu mtoto wa nje ya ndoa kuchukua urithi lakini inaruhusu mtoto asiyekuwa wa damu (wa kulelewa) awe na mkono ndani ya urithi hapo tunaweza kurekebisha kwa madhumuni maalumya kuwalindfa watoto hao ama kuwaadhibu wazazi (settlement kuwa against them) wanaotembea na kuoa nje ya ndoa..Lakini hatuwezi ku brush off our shoulders kila kitu Waislaam wanachoomba.. kuna sehemu ambazo haki haitumiki na hasa tunapofuata sheria ambazo hazitambui ndoa ya pili au mke nje ya dini yako..
 
unajua haya mambo ya mahakama ya kadhi lazima muyafikirie kuanzia juu mpaka chini na sio kijuu juu tu

lazima mjue kwamba mahakama ya kadhi itahitaji infrastructure

1. lazima mjue kwamba mahakama ya kadhi mahakimu wa kadhi waliohitimu na mawakili wa kadhi, je hawa mahakimu wa kadhi ambao wote watakuwa waislamu kwa ajili makafiri hawatakiwi, watasomeshwa vipi, inamaanisha leo hii serikali iwe na darasa la waislamu ambao wanasomea kupractise kadhi na darasa jingine la makafiri + waislamu ambao wanasome kupractise kikawaida. embu fikirieni huu mgawanyiko madhara yake

2. tanga kuna waislamu wengi kwa hiyo waamue tanga iwe na mahakama ya kadhi (tiyari utakuwa umeubatiza mkoa wa tanga kuwa wa kiislamu), je mikoa isiyokuwa na mahakama ya kadhi mtaibatiza mikoa ya kikristu?? Je raisi akimteua mkuu wa mkoa wa tanga mkristu si watasema hafai kwa ajili aelewi matatizo ya waislamu??

3. Je mahakimu wa kristu hawataanza ubaguzi na kuhakikisha mahakimu wa kiislamu wanagandamizwa kwa kuwaambia kuwa nyinyi mnamahakama yenu na hamtu ruhusu sisi kuja huko. (mahakimu wa kikristu na wana roho kama wenzao wa kiislamu ambao wana mahakama zao , na wao pia wangependa kuwa na mahakama zao how do u say no to them??)
 
Semilong,
Mkuu hata sikuelewi kabisa....Kwa akili yako unafikiri Waislaam hawakusoma elimu ya dini ktk maswala ya Kadhi au una maana gani? Hivi mnawaona vipi waislaam nyie maanake hata siwaelewi.
 
Semilong,

Mkuu hata sikuelewi kabisa....Kwa akili yako unafikiri Waislaam hawakusoma elimu ya dini ktk maswala ya Kadhi au una maana gani? Hivi mnawaona vipi waislaam nyie maanake hata siwaelewi.

mzee unazungumza na mtu mmoja hivyo; mbane huyo huyo.
 
Semilong,

Mkuu hata sikuelewi kabisa....Kwa akili yako unafikiri Waislaam hawakusoma elimu ya dini ktk maswala ya Kadhi au una maana gani? Hivi mnawaona vipi waislaam nyie maanake hata siwaelewi.
hujanielewa mkandara
kabla ya mtu kuanza ku practise lazima usomee
kwa hiyo hao watu watawekwaje madarasani

au unamaanisha kila muislamu anaweza kuwa hakimu wa kadhi bila kusomea, kama unasema watu waliosoma elimu ya dini wanaweza kuwa mahakimu bila kusomea hii mimi na kupinga kabisa
hata nchi za kiislamu zina law school
 
Last edited:

Mkuu unachekesha..Sasa wameweza vipi ku pratice dini yao ikiwa hawana elimu ya dini. Hivi kweli unaweza kuwa Muislaam ukaomba mahakama ya kadhi wakati huna elimu!.. come on now, U better than that..
 
Mkuu Calpso,
naomba kuuliza tafsiri ya mtu kuropoka,nadhani mkuu hiyo lugha si ya mtu muugwana.hapa tunajadiliana tunajaribu kujenga hoja mbalimbali katika kueleweshana,ndugu yangu mkandara katika kunijibu moja ya hoja yangu ameniambia ninakurupuka nadhani si uugwana hakuna mtu anayekurupuka katika kutenda jambo labda mtu nanye kurupuka ama kuropoka ni yule asiyechukua muda wa kutafakari hoja ya mwenzie.
tumieni lugha za kiungwana,ndo utakapo sema swala la kuheshimiana kama ulivyolitanguliza hapo juu waungwana watakuelewa.
 
Mkuu unachekesha..Sasa wameweza vipi ku pratice dini yao ikiwa hawana elimu ya dini. Hivi kweli unaweza kuwa Muislaam ukaomba mahakama ya kadhi wakati huna elimu!.. come on now, U better than that..

hata nchi za kiislamu zina law school kwa nini basi wasitumie viongozi wa dini tuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…