Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Katiba ya nchi ni kanuni ambazo jamii imejiwekea ili zifuatwe katika maisha yao ya kila siku. Kama suala ni kuingizwa kwenye katiba sioni ubaya ili mradi iwekwe wazi kuwa halazimishi mtu kwenye hilo. Mbona Hiyo BAKWATA Ilipoanzishwa wakati wa Nyerere maaskaofu hawakupinga?.

Halafu kama issue ni kuingizwa kwenye katiba, huoni kuwa kwa sheria hizohizo kuingizwa kwenye mahakama za kawaida zinakuwa tayari zimeingizwa kwenye katiba ( Sheria mama?). hoja yako bado imeelemea upande mmoja. Ndoa imefungishwa na Sheikh kwa sheria za dini yao ya kiislamu wewe hakimu Brown Christian unatumia sheria za dini isiyokuhusu kuhukumu wapi na wapi?. Huku ndiyo mwanzo wa kutafuta patashika. Kwa hili serikali imekosea inabidi watu waache idiology zao na kufanya kazi ya nchi sio maaskofu.

Hoftsede;

a. Je Mahakama ya Kadhi ni sehemu ya ibada ya Waislamu kama inavyodaiwa?

b. Je, Katiba imetoa uhuru wa kuabudu.

c. Kama a na b ni kweli, kwanini Waislamu wasitekeleza ibada yao kwa uhuru wao kama dini inavyosema bila kutaka wakristu na wasio wakristu waingilie kati ibada hiyo?

Mkandara kasema kitu kimoja muhimu sana. Sisi kama taifa tunatakiwa kujifunza na kuchukua yaliyo mema katika tamaduni mbalimbali. Tayari tunafanya hivyo. Sheria zetu zinaakisi tamaduni za jadi, dini ya kikristu na kiislamu. Ukisoma Sheria ya Ndoa ya mwaka 71 utaona kwa hata kadhi anatajwa. Hivyo, kuchukua yaliyo mema kwenye dini fulani na kuyaweka kwenye sheria zetu si jambo la ajabu. Ni kitu kinachoitwa secularization.

Nitakuambia binafsi ni sheria gani za Kiislamu ningependa ziingizwe kwenye sheria zetu na kuwa sehemu ya sheria zetu; ni zile zinazohusiana na masuala ya fedha na biashara. Wenzetu wana sheria na taratibu nzuri ambazo kuzifuata zingepunguza sana madeni yasiyo na lazima.

Sasa, kama binafsi ningependa kushawishiwa ni mambo gani yaliyo katika sheria ya Kiislamu ambayo yanaweza kumfaa kila Mtanzania hata asiye na dini? Tukiiyapata hayo tuone ni jinsi gani tutayasecularize ili yatumike kama secular laws na hivyo ni binding?
 
Mwanakijiji,
Mkuu nitaendelea kukujibu kwa sababu bado kabisa majibu yako ni ndani ya kabati hilo ulojifungia... hutaki wala husikii sauti nje ya kabati hilo..
Mkuu binafsi sikubaliani na swala la mahakama ya kadhi kwa sababu za msingi ambazo hazihusiani kabisa na dini zetu.. Ni mahakama yenyewe ya kadhi nikitazama WATU na MAZINGIRA tunayoishi ndipo nakuja na hoja zangu..lakini wewe umeshikilia Udini tuuuu kiasi kwamba maswali yako ni ya kidini tupu... ukiwaona wao ni waislaam na wewe Mkristu.. mambo ya CCM na Chadema..kwa ufinyu huo ndio maana Pinda kajibu ujenzi wa barabara Kigoma umefanywa na chama chake - CCM..

Hivi nikuulize mambo ya wanawake mathaln UWT mbona huulizi nani alaipia gharama zake. kwa nini usiwaambie wanawake wachukue dhamana ya matumizi ya chombo hicho badala ya taifa zima kulipa hali sisi sii wote wanawake..Watoto Yatima, vilema, budget ya mikoa, wilaya kwa nini tunahusishwa sote wakati wengine haituhusu!..Haya ndio mawazo yako mkuu wangu unajaribu kutuvisha lakini huyo huyo Mwanakijiji inapofikia siasa huichambua CCM kama vile yeye sii mkristu anayepinga mambo mengine..
Mkuu, unapofikiria tu kuwa waislaam ni WAO, wale, na kadhalika tayari wewe umeshaweka utengano, yaani hao wana mabaya fulani ambayo wewe hutaki kuhusishwa, hivyo hoja yako haiwezi kujenga Umoja unataka kuutangaza hapa.bali kujitenga kama unavyojitenga na Ufisadi.

Wewe unajua fika kwamba Magistrate Court Act yetu ina restrict matumizi ya Islamic law ktk maswala yote ya personal matters ya waislaam ambao Kikatiba wanaruhusiwa kufanya ibada hizo..Sasa jiulize inakuwaje unamruhusu mtu kufanya ibada zake lakini inapofikia matatizo settlement ya dispute baina ya wahusika haifanyiki kufuata misingi ya dini..

Toka wakoloni Tanzania tulikuwa na mahakama za kadhi, toka Mreno, Mjarumani, Muingereza na hata baada ya Uhuru sheria nyingi za kiisilaam ziliendelea kutumika ktk legal framework..
Nitarudia kusema, kuwa mimi binafsi natazama nje ya box na nafanya hivyo sii kwa sababu ni Muislaam isipokuwa natazama wahusika na mustakabali wa nchi nzima kwa ujumla wake kwani binafsi sina mke zaidi ya mmoja, mirathi yangu ipo ktk will na kadhalika. Binafsi nimejitahidi kadri ya uwezo wangu kuweka vitu vyangu kulingana na mazingira ya hapa, nchi ambayo haitambui Uislaam zaidi ya dini ya Waarabu (Axis of evil)..kwangu poa vile vile lakini sii nyumbani ambaklo tunadai ati sisi ni nchi isiyokuwa na dini wakati tunatoa maamuzi mengi kufuata mfumo wa dini moja..

Kingine naelewa fika kwamba Tanzania ni Democratic secular State, imetoa ruksa kwetu sote yaani kila dini kuendesha shughuli zetu tofauti ktk maswala ndoa, Talaka, guardianship, Urithi na kadhalika lakini serikali hiyo hiyo inakataa (restrict)kutambua sheria za dini moja ktk maswala ambayo imeruhusu..Sasa jiulize kweli unawapa uhuru waislaam kuabudu au unawakaanga kwa mafuta yao wenyewe.
.
Hii ndio point ya hao Masheikh kutaka mahakama ya kadhi na kama utatumia sabnbabu zako mkuu unazidi kujenga hoja zao vizuri kwani unaonekana wewe ni Mdini..
Kinachotakiwa ni empirical and objective information. Tuwapingew kwa hoja nzito ambazo zinahusu wananchi wenyewe wanaotakiwa kupewa suluhu. mahakama ya kadhi haifungi mtu, ni mahala pa kutoa suluhu, Upatanisho kulingana na dini na wanachokiomba wao ni kutambuliwa kisheria kwa mahakama hizi ili maamuzi yao yaweze kutumika hata High Court itakapo bidi..kinyume chas kutambulika mtu anaweza kupuuza mahakama na hapo ndipo tutakapo anza kuuana ovyo..
Hivyo kabla ya kutoa suluhu Liwali anatakiwa kuzijua sheria za dini zinasema nini ktk swala husika, sio kuvuta sheria za kikristu ktk personal matters za Waislaam..tunakuwa hatujengi demokrasia ila tutagawanyika. Haya mmefikia hadi kusema waislaam wapewe kisha wagharamie, mbona leo hii tunahukumiwa kikristu na sisi waislaam tunagharamia..Hizo Biblia zilizoko Kortini, maofisi, magereza na kwingineko mnalipia nyie pekee yenu..

Wakuu sii swala la gharama tujenge hoja tuombe serikali ichukue baadhi ya sheria kuziweka ktk vipengele kwa maamuzi.. kipengele kisomeke ikiwa mhusika ni Muislaam solution ya tatizo hilo inatakiwa kuwa hivi au vile..hatuwezi sote kukumbatia culture yanu mkwa sababu tu imeletwa na Muingereza au Nyerere..Changes ni mwanzo wa kwenda mbele tusipokubali hili ni sawa na CCM anayefikiria kwamba atatawala milele..
Na believe me, huko CCM wanakuona wewe mchawi tu pamoja na kwamba unaangusha vigongo kisawasawa..Sababu kubwa, CCM nao wamejifunguia katika kabati lao (kisiasa) vile vile.
 
Last edited:
umesema kitu ambacho kinaitwa "bottom line". Suala la kadhi ni suala la fedha. Nani afadhili na kugharimia mahakama hizo? Uongozi wa Waislamu wanasema serikali! lakini at the same time hawataki serikali kuingilia kati!? So hilo litawezekana vipi?


Baniani mbaya kiatu chake dawa!
 
Madrasa ni kaaazi kweli kweli.

Madrasa si kaazi bwana, nafikri developing countries kazi kwelikweli.... Kua mkweli haya ni matokeo ya be developing country , kwani asikudanganye mtu bwana hamna anae weza toa maamuzi yoyote juu ya nchi yake ikiwa kuna pressure za dunia ya kwanza.
 
Katiba ya nchi ni kanuni ambazo jamii imejiwekea ili zifuatwe katika maisha yao ya kila siku. Kama suala ni kuingizwa kwenye katiba sioni ubaya ili mradi iwekwe wazi kuwa halazimishi mtu kwenye hilo. Mbona Hiyo BAKWATA Ilipoanzishwa wakati wa Nyerere maaskaofu hawakupinga?.

Halafu kama issue ni kuingizwa kwenye katiba, huoni kuwa kwa sheria hizohizo kuingizwa kwenye mahakama za kawaida zinakuwa tayari zimeingizwa kwenye katiba ( Sheria mama?). hoja yako bado imeelemea upande mmoja. Ndoa imefungishwa na Sheikh kwa sheria za dini yao ya kiislamu wewe hakimu Brown Christian unatumia sheria za dini isiyokuhusu kuhukumu wapi na wapi?. Huku ndiyo mwanzo wa kutafuta patashika. Kwa hili serikali imekosea inabidi watu waache idiology zao na kufanya kazi ya nchi sio maaskofu.


Sasa inakuwa vipi kina Brown Christian wanapotakiwa kuchangia (kodi) uendeshwaji wa hiyo mahakama?! Kwa nini kina Alhaji Idd Al-Muslim wasichukue jukumu lote la kuendesha mahakama ikiwa ni pamoja na funding?! This is the main PUZZLE!!!!!! And, only Islams (BAKWATA) can answer it!
 
Madrasa si kaazi bwana, nafikri developing countries kazi kwelikweli.... Kua mkweli haya ni matokeo ya be developing country , kwani asikudanganye mtu bwana hamna anae weza toa maamuzi yoyote juu ya nchi yake ikiwa kuna pressure za dunia ya kwanza.

Duh! Basi tuna safari ndefu. Kama hata mahakama ya kadhi ni kufanya maamuzi kutokana na pressure ya dunia ya kwanza mh.
 
Mwanakijiji,
Mkuu nitaendelea kukujibu kwa sababu bado kabisa majibu yako ni ndani ya kabati hilo ulojifungia... hutaki wala husikii sauti nje ya kabati hilo..
Mkuu binafsi sikubaliani na swala la mahakama ya kadhi kwa sababu za msingi ambazo hazihusiani kabisa na dini zetu.. Ni mahakama yenyewe ya kadhi nikitazama WATU na MAZINGIRA tunayoishi ndipo nakuja na hoja zangu..lakini wewe umeshikilia Udini tuuuu kiasi kwamba maswali yako ni ya kidini tupu... ukiwaona wao ni waislaam na wewe Mkristu.. mambo ya CCM na Chadema..kwa ufinyu huo ndio maana Pinda kajibu ujenzi wa barabara Kigoma umefanywa na chama chake - CCM..

Mkandara, tatizo lako unachodai wengine wanfanya ndicho wewe unafanya. Hoja zako japo ni nzuri lakini haziwezi kusimama hadi umshambulie mtu. Mara kabati, mara droo, mara hili mara lile. Inafanya vigumu kweli kukusoma bila kukerwa na mashambulizi binafsi ya mtu. Uzuri wa hoja na nguvu ya hoja haiji kwa kulazimisha hivyo isipokuwa kwa kuitetea na kuonesha ukweli wake.

Hivi nikuulize mambo ya wanawake mathaln UWT mbona huulizi nani alaipia gharama zake.

Sina sababu ya kuuliza kwa sababu UWT ni jumuiya ya wanawake wa CCM. Mimi si mwana CCM na si mwanamke; lakini pia kwa sababu fedha za walipa kodi wa Tanzania kinadharia haziingii kule. Nikiwa mwana CCM nitahoji.
kwa nini usiwaambie wanawake wachukue dhamana ya matumizi ya chombo hicho badala ya taifa zima kulipa hali sisi sii wote wanawake..

Ungesema Wizara ya Wanawake, Jinsia na Watoto hilo tutalizungumzia; lakini UWT haiendeshwi kwa fedha za serikali. Period.
Watoto Yatima, vilema, budget ya mikoa, wilaya kwa nini tunahusishwa sote wakati wengine haituhusu!.

sijui unazungumzia nini hapa. Kama UWT basi haituhusu; kama ni mambo ya serikali yanatuhusu.
.Haya ndio mawazo yako mkuu wangu unajaribu kutuvisha lakini huyo huyo Mwanakijiji inapofikia siasa huichambua CCM kama vile yeye sii mkristu anayepinga mambo mengine..

sijakuelewa.
Mkuu, unapofikiria tu kuwa waislaam ni WAO, wale, na kadhalika tayari wewe umeshaweka utengano, yaani hao wana mabaya fulani ambayo wewe hutaki kuhusishwa, hivyo hoja yako haiwezi kujenga Umoja unataka kuutangaza hapa.bali kujitenga kama unavyojitenga na Ufisadi.

wewe unaona "wakristu" na "waislamu" mimi naona Watanzania. Mambo ya Waislamu hayanihusu. Bahati mbaya wao wanayafanya ya Watanzania wote.

Wewe unajua fika kwamba Magistrate Court Act yetu ina restrict matumizi ya Islamic law ktk maswala yote ya personal matters ya waislaam ambao Kikatiba wanaruhusiwa kufanya ibada hizo.
.

sasa kama ni suala la ibada, kwani wamekatazwa na nani kuitekeleza? Hivi kuna Muislamu aliyeenda kwa Shehe na kutaka jambo lake liamuliwe kidni akakataliwa?

Sasa jiulize inakuwaje unamruhusu mtu kufanya ibada zake lakini inapofikia matatizo settlement ya dispute baina ya wahusika haifanyiki kufuata misingi ya dini..

sasa hilo ni swali la kidini siyo la serikali. Kwanini Waislamu kwa mambo ambayo yako katika dini yao hawafanyi kile dini yao inataka hususan masuala haya ya kisheria?


Toka wakoloni Tanzania tulikuwa na mahakama za kadhi, toka Mreno, Mjarumani, Muingereza na hata baada ya Uhuru sheria nyingi za kiisilaam ziliendelea kutumika ktk legal framework..

hili mbona halina utata. Lakini wakati wa Mkoloni tulikuwa na mambo mengi ambayo leo hatuendelei nayo. Sasa kama wakoloni walikuwa wanafanya basi na sisi tufanye? Hii hoja haina nguvu, kuna sheria ambazo tulizirithi toka kwa wakoloni na tumeeendelea kuzifuta kila inapobidi. Suala la Mahakama ya Kadhi liangaliwe kwa mwanga wa leo na mahitaji ya taifa zima.

ndiyo maana sina tatizo la mahakama za kadhikuwepo au sheria za Kiislamu ambazo zinatufaa Watanzania wote kuingizwa kwenye sheria zetu. Lakini sheria za kikundikimoja tu cha dini kuingizwa kwenye sheria zetu ili zifae kikundi hiko kimoja cha dini hilo nalikataa kwani zinafunza non-discrimination clause ya Katiba yetu.

Nitarudia kusema, kuwa mimi binafsi natazama nje ya box na nafanya hivyo sii kwa sababu ni Muislaam isipokuwa natazama wahusika na mustakabali wa nchi nzima kwa ujumla wake kwani binafsi sina mke zaidi ya mmoja, mirathi yangu ipo ktk will na kadhalika.

Sijui kama ni kweli unataza nje ya box. Kauli zako zimejaa mashambulizi ya kidini,kejeli za kidini na kudhalilishana kidini kwa sababu tu wewe si mtu wa dini hiyo.

Binafsi nimejitahidi kadri ya uwezo wangu kuweka vitu vyangu kulingana na mazingira ya hapa, nchi ambayo haitambui Uislaam zaidi ya dini ya Waarabu (Axis of evil)..kwangu poa vile vile lakini sii nyumbani ambaklo tunadai ati sisi ni nchi isiyokuwa na dini wakati tunatoa maamuzi mengi kufuata mfumo wa dini moja..

nakusikia.

Kingine naelewa fika kwamba Tanzania ni Democratic secular State, imetoa ruksa kwetu sote yaani kila dini kuendesha shughuli zetu tofauti ktk maswala ndoa, Talaka, guardianship, Urithi na kadhalika lakini serikali hiyo hiyo inakataa (restrict)kutambua sheria za dini moja ktk maswala ambayo imeruhusu..Sasa jiulize kweli unawapa uhuru waislaam kuabudu au unawakaanga kwa mafuta yao wenyewe.

hili si kweli. Hivi ni muislamu gani aliyetaka mirathi yake iendeshwe kwa minajili ya dini ya kiislamu akakataliwa? Ni nani aliyetaka talaka au kutoa talaka kwa mujibu wa mafundisho ya dini ya Kiislamu akakataliwa au talaka yake kutotambuliwa?

je, Muislamu akitoa talaka kama inavyosemwa katika Uislamu, talaka yake serikali yetu haiitambui? Kama inaitambua je siyo huko kutambua sharia za kiislamu?
.
Hii ndio point ya hao Masheikh kutaka mahakama ya kadhi na kama utatumia sabnbabu zako mkuu unazidi kujenga hoja zao vizuri kwani unaonekana wewe ni Mdini..

well inamhitaji mtu mmoja mdini kumjua mwingine.

Kinachotakiwa ni empirical and objective information.

sidhani kamahili linawezekana kwa mtindo huu wa kuongozwa na dini.

 
Tatizo hapa nimekuta wengi wa wanao chambua kadhia hii wapo nje ya nchi halafu wanataka waonekane wanajua sana masuala ya nchi vilivyo.Hivi nyie mnao jadiliana hapa mnajua kesi ngapi za mirathi zipo mahakamani zinazo husu Waislam na familia zao?Kwa mujibu wa sheria za kiislaam mtoto wa nje ya ndoa harithi lakini kuna kesi nyingi zimefunguliwa na hao waliozaliwa nje ya ndoa kudai mirathi kutoka kwa baba wa kiislaam ambao mahakama zetu zinachukua muda kutoa maamuzi ?Kuna akina mama waliozaa na akina baba wa kiislaam nao wanafungua kesi wapate mirathi !Kuna kesi za uongozi wa nyumba za ibada na wakfu zipo mahakamani yanatakiwa yahakumiwe kwa mujibu sheria za kiislaam,Kuna kipindi nilikuwa Iringa kulikuwa na mgogoro wa uongozi msikiti mmoja wakapeleka mahakama kuu iliyopo Iringa Jaji katika kutoa maamuzi aliwaeleza "sijaona sheria za nchi zitakazo niwezesha kutoa hukumu ya kesi yenu nawashauri mjaribu kuwatumia Masheikh wenu kutatua suala lenu".Kesi hiyo ilikuwa ya muda mrefu sana mahakamani.
Kuna kesi nyingi zinazo husu kadhia za waislam ambazo zinahitaji sheria za kiislaam kuzitatua zimechukua miaka kuamuliwa na mahakama zetu .Ndipo hapo Waislaam wanapodai mahakama za kadhi kutokana na hayo matatizo wanayo kabiliana nazo.Takriban kila familia ya kiislaam wameshaguswa na matatizo hayo yanayohusiana mirathi ,ndoa nk na matatizo ya uongozi kwenye taasisi mbali mbali za kiislaam.
Mia nipo mitaani nimetembea mitaa na maeneo mengi ya Dar es salaam .Tanga na Pwani nk nimeongea na Waislaam wengi hili suala lina wagusa sana.
Naami naawambia msiwabeze viongozi wa kiislaam wa tasisi mbali mbali hapa nchini ndiye wanao tuliza amani siku wakiwaambia waumini wao wafyatuke hapatakalika .Nyie mliopo kwenye deskptop ku type na kukujeli waislaam tutakuja kukumbushana hapa siku moja hayo mnae yakejeli.
Mungu Ibariki Tanzania
 
Waarabu na wazungu tabia yao ya kulazimisha tushike dini zao ndiyo iliyotufikisha ha pa.
Ndiyo maana kwa hili nawapenda wahindi walikuja kuchukua pesa tu huku Afrika na siyo na imani zetu. Hivi na wahindi nao wangelazimisha imani zao naona nchi ingekuwa masikini zaidi duh! afadhali hawakufanya hivyo, yaani nchi isingekuwa na ng'ombe hata mmoja kwenye mabucha!!!!
Watu wanaweza kudhani ni utani, lakini sisi tulivyo? watu wangekuwa wanaandamana kupinga ulaji wa nyama ya Ng'ombe!!
Hebu angalia aibu hii, majitu mazima yanajiona bora kwa imani za kufikia!!!
 
Waarabu na wazungu tabia yao ya kulazimisha tushike dini zao ndiyo iliyotufikisha ha pa.
Ndiyo maana kwa hili nawapenda wahindi walikuja kuchukua pesa tu huku Afrika na siyo na imani zetu. Hivi na wahindi nao wangelazimisha imani zao naona nchi ingekuwa masikini zaidi duh! afadhali hawakufanya hivyo, yaani nchi isingekuwa na ng'ombe hata mmoja kwenye mabucha!!!!
Watu wanaweza kudhani ni utani, lakini sisi tulivyo? watu wangekuwa wanaandamana kupinga ulaji wa nyama ya Ng'ombe!!
Hebu angalia aibu hii, majitu mazima yanajiona bora kwa imani za kufikia!!!

Asilimi 60 ya Watanzania wana imani za dini zilizoletwa na Waarabu na Wazuungu kama unalichulikia jambo hili jepesi hebu siku moja jitose mskitini au kanisani uyatamke haya maneno unayo yaeleza hapa kwenye net huenda wakauelewa.
Ukisha ingia mskitini au kanisai sehemu yeyote ya Tanzania uambie "jamani eeh hivi ninyi mna akili kweli ninyi mijiti mizima mna jiona bora kwa imani za kifikia?"mie nahisi watakuelewa tu !
 
Asilimi 60 ya Watanzania wana imani za dini zilizoletwa na Waarabu na Wazuungu kama unalichulikia jambo hili jepesi hebu siku moja jitose mskitini au kanisani uyatamke haya maneno unayo yaeleza hapa kwenye net huenda wakauelewa.
Ukisha ingia mskitini au kanisai sehemu yeyote ya Tanzania uambie "jamani eeh hivi ninyi mna akili kweli ninyi mijiti mizima mna jiona bora kwa imani za kifikia?"mie nahisi watakuelewa tu !

We Sie lee hutaki mwenzio aioene kesho! am sure hatatoka pale atakapo kuwa anayaongelea hayo kabla title yake haijabadilika na kuwa mgeni wa malaika!

Japo hoja yake ina ukweli mwingi tu!
 
Mufti Simba hana haja ya kuhamaki. Sera ya CCM sasa hivi ni kuhakikisha waislam wanasaidiwa kupata sheria zao wenyewe, mahakama zao wenyewe na mahakimu wao wenyewe. Hii imo ndani ya manifesto ya CCM. CCM watatekeleza tu sera yao. Awape muda!!
 
Mzee Mwanakijiji,

Mkuu pengine nianze kwa kusema samahani ikiwa nimekukwaza.. Kalini siku zote mimi huandika with Authority ktk swala nalolifahamu - hoja zenye Critics huzijibu kwa critics sikuanza mimi kuuliza hayo..
Nimetumia UWT kama mfano na ajabu wewe umerukia UWT kwa sababu tu unafahamu hicho ni chombo cha CCM.. kisha ukaendelea kusema, wewe ukiwa mwana CCM una haki ya kuuliza. Ajabu ktk swala la mahakama ya kadhi wewe sii mwanachama,(Muislaam) wala mhusika wa Bakwata kwa njia yoyote ile, lakini umerukia kuuliza matumizi yake wakati huna unanachama ktk chombo hiki wala Uislaam..Kwa nini usiwaachie wana CCM (Waislaam) kuuliza kama ulivyojibu hapo nyuma!

Na unaposema CCM ndio hugharamia UWT una maana gani?, hizo fedha wanazipata toka wapi ikiwa CCM haina miradi ya kukiendesha chama hicho bila nguvu ya Watanzania wote.. Mkuu vyama vyote nchini mkuu vinaendeshwa na sisi wananchi iwe CCM, Chadema, CUF na kadhaliika. Pamoja na hayo naikubali hoja yakoi kama ulivyoandika na kujaribu kukutaarifu zaidi. Na kama umesoma vizuri nimeorodhesha taasisi nyinginezo ambazo umeziruka ukachagua moja kukidhi hoja yako.. U still wrong mkuu wangu. Ndio maana nikakupa mfano wa Pinda na majibu yake huko Kigoma.. huu ndio mtazamo wako ktk swala hili.

Kifupi ni lazima ukubali kwanza kwamba unaandika ukiwa kabatini hivyo ni vigumu kwako kuweza kuona nje ya kabati hilo.. Maneno yako ni mazito sawa na viongozi wa CCM ambao malalamiko ya vyama vingine kama Chadema, CUF na TLP huyaona upuuzi mtupu na malalamiko ya watu waliochioka..Wanaweka dharau badala ya kuzingatia kwamba kikatiba, kuwepo kwa demokrasia ndiyo inawapa wao nafasi ya kuongoza..Sasa ubaya wako ni pale unaposhindwa kuelewa kwanza malalamiko ya Waislaam na chombo chao kama vile CCM na viongozi wake wanapofumba macho ktk maswala ya vyama vinginevyo, hata kama hakuna haki ama utaratibu mzuri.

Je, unafikiri malalamiko mengi ya vyama kama Chadema ni uzushi mtupu? Sii kweli vyombo vya Usalama, NEC na vyombo vya serikali husimama upande wa CCM ktk chaguzi za Kitaifa?..Na pengine mawaziri khutumia fedha na mali za serikali ktk kampeni za chama CCM..Kwa nini unaona hakuna haja ya CCM kuyatazama maswala haya au mapendekezo ya vyama vingine..NMi kwa sababu CCM wanafikiria kwamba wao ndio watawala milelel huu mfumo wa vyama vingi ni geresha tu kwa nchi za magharibi.. Hivyo wewe pia unaona uhuru kwa waislaam ni geresha tu nchi yetu ni ya Kikristu na itaendeshwa kikristu.. Restriction ziendelee kama kawaida, hawataki wajikate wakaunde serikali yao. Siji wapi huko! ndio maneno yenu toka tuanze mada zinazohusu Waislaam..

Mkuu umeuliza hapo juu maswali ya A na B, kisha ukatoa suluhu ya C bila kufahamu kwamba Magistrate Court Act ya nchi yetu ina restrict matumizi ya islamic law ktk mahakama zetu..Kisha unahoji kwa nini waislaam wasitumie sheria zao. Hapa unafikiri nitakujibu vipi kama sii kuwa open minded (kutoka ktk kabati la udini) ukaelewa hoja ya Waislaam.

Swala hili ni sawa na lile la Bakwata kama unakumbuka tuliwahi kujadili mwka jana.. nikasema Bakwata ni chombo kilichoanzishwa na serikali. yaani sisi wote kwa mjumuiko wetu tunahusishwa moja kwa moja na Bakwata ktk matumizi yake.. we ask for that (Muslims and Christians), sasa ikiwa kuna swali waulize serikali na sii Waislaam ambao wangependa sana kujiongoza wao wenyewe bila baraka za serikiali.

Wewe kama Mkatoliki unajua fika kwamba Pengo hachaguliwi wala kuteuliwa na serikali ama Rais na hata ukitazama dini nyingine zote isipokuwa Waislaam. serikali au niseme CCM, imeingiza mkono wake ndani ya dini hii kiasi kwamba hata Mufti ni pandikizi la chama. Huyu anapewa nguvu ya kuchagua na kufukuza kiongozi yeyote wa dini kama atajisikia kufanya hivyo.. Unakumbuka mara ya mwisho alipokuwa India alifukuza uongozi wote wa Bakwata na kuweka mpya bila vigezo vya kidini isipokuwa maamuzi yake yalitokana na hitilafu za uongozi wa chama Bakwata. Bakwata ni chama under CCM zaidi ya kuwa jumuiya ya Waislaam.
Hivyo haya malalamiko yao ni ktk kujikomba kwa serikali wakitaka wapewe ulaji mwingine wakati Waislaam wenyewe wanahoji uhalali wa chombo hicho Bakwata..Huyo Mufti ni kiongozi wa Bakwata sii wa Waislaam isipokuwa tunalazimika kumkubali kama vile Mugabe na Zimbabwe kwani ndiye anayetambulika.

Ni hayo tu mkuu wangu ikiwa utakuwa open minded ukaelewa matatizo ndani ya Uislaam nchini ni rahisi sana kuweza kuona point nayozungumzia lakini unapokuja na hoja zilizopigwa mhuri ni vigumu kwako kuweza kuelewa.

Toka naandika hapa hujanisikia nikiwa critic na dini ya Kikristu isipokuwa waumini wenye kutazama nje ya mafundisho ya dini yao..Haina maana sina tofauti zangu au kutokubaliana na Ukristu lakini siwezi kuingilia mfumo wa dini yako wala ku question mambo ya ndani ya dini yako kwani hizo sababu ndizo zilinifanya nisiwe Mkristu..
Na kutokuwa kwangu Mkristu haina maana najitenga na wakristu wote, mambo yao yote na siwezi kula nao sahani moja..Nikifikia hapo ni upofu na hakikka nitakuwa nimejifungia ktk kabati la Udini.
 
Last edited:
Bakwata hawana ubavu huo wanabwaka tu, wao wenyewe credibility yao ni questionable wasafishe nyumba yao kwanza.

Hawana jipya zaidi ya kutafuta njia ya kutokea na kuficha madudu yao. Ni ukweli usio na shaka uislam haupo kitaasisi kama ukristo na madhehebu yake catholics, Lutheran, Anglican nk. Bakwata ni kikundi cha wajanja wachache wasio na mandate yeyote kwa waislam ndio maana no body is taking them serious.

Jambo ninalo amini ndugu zangu waislamu wanamsimamo usiyoyumba wanapo kuwa wanadai jambo lao tofauti na ndugu zangu wakristo.
Mara zote jambo lao likihubiriwa wakalikubari na kuliamini hawayumbishwi kama wakristo.Na ndo maana walibatizwa watu wenye msimamo mkali
Kama wakristo wangeacha unafiki kwa sehemu fulani tungeweza kupiga hatua.Ni rahisi sana kumyumbisha mkristo tofauti na mwislamu kwa lile analo liamini.wako tayari kufaa mwembechai,kuvaa mabomu na kujilipua ilimradi ameamini analo fanya hatakama siyo sahihi.kwa hilo ninawasifu na mchngo mkubwa wa pressure kwa watawala wetu mara nyingi umekuwa ukitokea kwao.
Hivyo basi hawa watu wakiivishwa watakitema chama cha mapinduzi.
 
Mwanakijiji, Mkandara,

..ni vizuri tukapata maoni ya MTAALAMU WA SHERIA ktk suala hili.

..binafsi sielewi kwanini Shekhe anayefungisha ndoa, na kushughulikia mazishi, bila kuwepo Mahakama ya Kadhi, ashindwe kushughulikia talaka, mirathi,... kwa kisingizio kwamba hakuna mahakama hiyo.

..pia maelezo ya Waislamu ni kwamba suala hili ni IBADA. sasa hawaoni kwamba kulipeleka bungeni/serikalini likajadiliwa na kushughulikiwa na Watanzania wote bila kujali imani zao ni kukiuka taratibu za ibada ya dini yao?

..vilevile haya masuala ya ndoa,talaka,na mirathi, kwa ndugu zetu Waislamu yamekuwa yakishughulikiwa namna gani tangu Mahakama ya Kadhi iondolewe ktk sheria za Jamhuri? kuna mapungufu gani ktk utaratibu ulioko sasa hivi?

..pia hakuna anayetoa maelezo ya kina Mahakama hii ya Kadhi itafanya kazi namna gani in a secular and polarized country kama Tanzania.

..Mahakama za serikali zinategemea Jeshi la Polisi na Magereza kuhakikisha utekelezwaji wa hukumu na mahakama hizo. Je, ni chombo kipi kitakuwa enforcer wa hukumu za mahakama ya Kadhi?

..je, mwenye shauri ktk mahakama ya Kadhi asipokubaliana na maamuzi ya mahakama hiyo ana haki ya kwenda kushitaki ktk mahakama ya raia wote?

..je, ikitokea mahakama ya kiraia ikatoa hukumu tofauti na mahakama ya Kadhi, hukumu ipi inapaswa kutekelezwa kati ya hizo?

..kwa kifupi mpaka kati ya mahakama ya Kadhi na mahakama za kiraia utakuwa wapi? Mpaka huo utawekwa na kusimamiwa na nani?
 
nimezipenda sana hizi analysis by mukandara
big up Mkuu
hizi information zingekuwa published kwenye news zingefaa sana kuikumbusha jamii ili tuweze kuwa pamoja kwani huku mitaani tunalopoka tu bila kujua tunataka nini

Mkandara
Asante kwa elimu hii.
 
..OK, fainally nimepata sehemu ambako kuna MCHANGO WA KITAALAMU.

..ni muhimu suala hili likaangaliwa kitaalamu kuliko kulumbana na kunyoosheana vidole kuhusu Vatican, OIC, etc etc.

..nawaomba wanachama mbonyeze hapa kupata maoni ya kitaalamu.
 
Tutabishana sana lakini naamini kuwa botom line ni kuwa hili ni sula la waislamu na ni vema waislamu wakaachiwa waliendeshe kwa mujibu wa taratibu zao. Serikali, kwa namna yoyote ile haipaswi kujihusisha na suala hili. Period
 
Back
Top Bottom