Muharami Abdallah (Chonji) na wenzake wahukumiwa kifungo cha maisha jela kwa makosa ya kusafirisha dawa za kulevya

Muharami Abdallah (Chonji) na wenzake wahukumiwa kifungo cha maisha jela kwa makosa ya kusafirisha dawa za kulevya


Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imewahukumu kifungo cha maisha jela washtakiwa watano baada ya kutiwa hatiani kwa makosa ya kusafirisha dawa za kulevya aina za heroini gramu 5,309.57 na kokeni zenye uzito wa gramu 894.28.

Hukumu imetolewa Julai 11, 2024 na Jaji Awamu Mbagwa, aliyesikiliza kesi hiyo ya jinai namba 58/2023.

Waliohukumiwa ni Muharami Abdallah, maarufu Chonji, Abdul Chumbi, Rehan Umande, Tanaka Mwakasafule na Maliki Maunda.

Baada ya kusikiliza ushahidi wa pande zote mbili, Jaji Mbagwa aliwahukumu kifungo cha maisha jela washtakiwa wote watano akieleza upande wa mashitaka umethibitisha makosa hayo bila kuacha shaka yoyote.

Washtakiwa walidaiwa kusafirisha dawa za kulevya kinyume cha kifungu cha 16 (1) (b) cha Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2012.

Katika shitaka la kwanza, walidaiwa Oktoba 21, 2014 eneo la Magomeni Makanya, Wilaya ya Kinondoni, Dar es Salaam, walisafirisha dawa za kulevya aina ya heroini ambazo iwapo zingeuzwa zingekusanya Sh265.47 milioni.

Shtaka la pili, walidaiwa siku hiyohiyo na katika eneo hilo, walisafirisha dawa za kulevya aina ya kokeni za Sh62.59 milioni.

Katika kesi hiyo upande wa mashitaka uliwakilishwa na mawakili watano wakiongozwa na Wakili wa Serikali Mkuu, Saraji Iboru, huku washtakiwa wakitetewa na mawakili wanane wakiongozwa na Juma Nassoro.

Upande wa mashitaka ulikuwa na mashahidi 10 na vielelezo 12, ikiwamo mizani tatu za kupimia, bastola aina ya Browing iliyokuwa na risasi nane, ripoti ya mkemia, simu, cheti cha kukamata na ripoti ya kitaalamu ya taarifa ya uchunguzi na uthibitisho wa picha mjongeo (video).
Hv hayo madawa polisi wanayaharibu kweli?...au ndo yanarudishwa kwenye mzunguko!!
 
Siku hizi pwani za huku bongo hawaji.....wanadakwa sana
Wenyewe wanakuambia tunaenda kuvua 😄
Ununio kipindi fulani walishushiwa sana maboom...baadhi ya wavuvi walipopewa mchongo wengi wakahamia huko na uvuvi wakaacha,kwa kina dallas huko
Any way kitengo bongo kinajitahidi kupiga kazi aise..pongezi wapewe
Na sahivi wao wanataka wakikudaka wakudake na kidhibiti
Ukidakwa ukitoka we kidume...
Ile OP ya awamu ile nyingi zilikuwa na ulakini,kila mtuhumiwa akidakwa anakutwa na grm 200
Kama ulinotice...kulikuwa na kuchomekeana

Ova
Uko sahihi Mkuu, hakuna kipindi ambacho Kitengo kimejitahidi kama Kwa miaka ya hivi karibuni...!
 

Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imewahukumu kifungo cha maisha jela washtakiwa watano baada ya kutiwa hatiani kwa makosa ya kusafirisha dawa za kulevya aina za heroini gramu 5,309.57 na kokeni zenye uzito wa gramu 894.28.

Hukumu imetolewa Julai 11, 2024 na Jaji Awamu Mbagwa, aliyesikiliza kesi hiyo ya jinai namba 58/2023.

Waliohukumiwa ni Muharami Abdallah, maarufu Chonji, Abdul Chumbi, Rehan Umande, Tanaka Mwakasafule na Maliki Maunda.

Baada ya kusikiliza ushahidi wa pande zote mbili, Jaji Mbagwa aliwahukumu kifungo cha maisha jela washtakiwa wote watano akieleza upande wa mashitaka umethibitisha makosa hayo bila kuacha shaka yoyote.

Washtakiwa walidaiwa kusafirisha dawa za kulevya kinyume cha kifungu cha 16 (1) (b) cha Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2012.

Katika shitaka la kwanza, walidaiwa Oktoba 21, 2014 eneo la Magomeni Makanya, Wilaya ya Kinondoni, Dar es Salaam, walisafirisha dawa za kulevya aina ya heroini ambazo iwapo zingeuzwa zingekusanya Sh265.47 milioni.

Shtaka la pili, walidaiwa siku hiyohiyo na katika eneo hilo, walisafirisha dawa za kulevya aina ya kokeni za Sh62.59 milioni.

Katika kesi hiyo upande wa mashitaka uliwakilishwa na mawakili watano wakiongozwa na Wakili wa Serikali Mkuu, Saraji Iboru, huku washtakiwa wakitetewa na mawakili wanane wakiongozwa na Juma Nassoro.

Upande wa mashitaka ulikuwa na mashahidi 10 na vielelezo 12, ikiwamo mizani tatu za kupimia, bastola aina ya Browing iliyokuwa na risasi nane, ripoti ya mkemia, simu, cheti cha kukamata na ripoti ya kitaalamu ya taarifa ya uchunguzi na uthibitisho wa picha mjongeo (video).
Hizo dawa ziko Wapi? Wakishahukumiwa mzigo wao unakua chini ya Nani? Au ndio unaozunguka mtaani?
 
Chonji si ndo yule aliyekamatwa na wa marekani? Akapelekwa mtwara akatoroka wakamkamata tena au ni yupi? Kama ni yeye umrinwake ni mkubwa sana na hiyo miaka sijui kama atakaa mingi atajifia zake gerezani tu.
Yule wa underground ya hapo magomeni yeye alitoka au vipi?
Yule alishamaliza kifungo chake Marekani yupo huru, siyo huyu Chonji.

Yule Don anaitwa Skuba.
 
Duh huyu cambiasso hii ngoma ya sahvi ngumu ni kuicheza
Maana kesi nyingi alikutana nazo alizichezesha...anyway ngoja tuone

Ova
Toka maktaba :

2022 21 November
Kambi Zubery Seif, mmiliki wa kituo cha Cambiasso Sport Academy na wenzake watano wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kusomewa mashtaka mawili ya kusafirisha dawa za kulevya kilogram 27 eneo la Kiluvya kinyume na Sheria ya Kuzuia na Kupamba na Dawa za Kulevya.


View: https://m.youtube.com/watch?v=JPTClkY3Ntk

SARAH MWENYE KESI ya DAWA ZA KULEVYA kilo 34.89 inayomkabili pamoja na Muharami Sultan, Cambiasso na wenzanke kadhaa AWATAJA WATOTO WAKE MAHAKAMANI - ''SIELEWI WANAISHIJE''...

View: https://m.youtube.com/watch?v=Dh02jQsSM_Y
2023 16 February
SARAH MWENYE KESI ya DAWA ZA KULEVYA heroine zenye uzito wa kilo 34.89. AWATAJA WATOTO WAKE MAHAKAMANI - ''SIELEWI WANAISHIJE''...Kutoka katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ni kuhusu mshtakiwa Sarah Joseph anayekabiliwa na kesi ya kusafirisha dawa za kulevya, ameieleza Mahakama hiyo kuwa haelewi watoto wake wanaishi maisha gani huko walipo.Mshtakiwa huyo ametoa madai hayo leo baada ya Wakili wa Serikali Caroline Matemu kuieleza mahakama hiyo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Mary Mrio kuwa upelelezi wa shauri hilo bado unaendelea, hivyo wanaomba Mahakama ipange tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa.

Hakimu Mrio baada ya mahakama kuelezwa hayo, ameahirisha kesi hiyo hadi Machi 2, 2023 itakapotajwa na washtakiwa wamerudishwa rumande kutokana na kesi inayowakabili haina dhamana kwa mujibu wa sheria.

Mbali ya Sarah pia katika kesi hiyo kuna washtakiwa wengine watano akiwemo aliyekuwa kocha wa Makipa wa Timu ya Simba, Muharami Sultan(40), ambapo kusafirisha dawa za Kulevya aina ya heroine zenye uzito wa kilo 34.89.
 
Atayajua wapi haya huyo boya..mtu akiishavaa shati la kijani anajiona eti Na yeye ni mtu wa systems😀😀😀😀
Sasa hivi ukienda huko visiwani wavuvi wanavua samaki kwa njia haramu na hatarishi sana, yaani ni mwendo wa mabaruti tu na hakuna anayejali wala kufuatilia.

Bangi na mirungi jamaa zangu wanavusha tu kwenda Kenya kupitia Sirali na hawana wasi wasi wowote.... bila kusahau wazee wa kupanga magogo barabarani kwenye mipaka ya burundi.

Halafu leo hii eti kuna mlamba asali mmoja akiwa na kilaki mbili chake mfukoni alichokipata kwa njia ya rushwa, anakuja kuanza kumsifia sifia Samia kwamba anadhibiti bishara za haramu huku akipondea awamu zilizopita...!?? Shenzy zake
 
K
Chonji ni Tajiri maarufu kule Nagomeni MwembeChai ni The Doni hasa.
Tangu mwaka 2010 alikuwa akiwika kama tajiri anayeibuka kwa kasi.

Kesi hii imekaa muda mrefu sana..
Hongera Dr Samia kwa kusimamia ukweli kuliko wale wenzako walioshindwa kazi wakaishia kubambikia watu madawa kwa chuki tu.
Kwan samia ndiyo ametoa hukumu
Mpumbavu wewe
Hata ukinya utasema asante samia

Mijitu mijinga kama wewe unafikir raisi ndiyo anafanya kila kitu
 
Chonji ni Tajiri maarufu kule Nagomeni MwembeChai ni The Doni hasa.
Tangu mwaka 2010 alikuwa akiwika kama tajiri anayeibuka kwa kasi.

Kesi hii imekaa muda mrefu sana..
Hongera Dr Samia kwa kusimamia ukweli kuliko wale wenzako walioshindwa kazi wakaishia kubambikia watu madawa kwa chuki tu.
Kazi ya kamishna wa kwanza Rogers Sianga.
 
K

Kwan samia ndiyo ametoa hukumu
Mpumbavu wewe
Hata ukinya utasema asante samia

Mijitu mijinga kama wewe unafikir raisi ndiyo anafanya kila kitu
Mkuu unanitukana bure tu. Kwa Tanzania hii hata leo Dr Samia akiamua Chonji atolewe anatoka na huna la kufanya na hakuna atakayekohoa.

Tuendelee kupambania katiba bora inayowajibisha watu bila Rais kulazimika kutia mkono wake.

Bado tuna shukuru utashi wa Dr Samia kuamua magwiji hao wakamatwe.
 
Kwa hiyo kwa akili yako unaona hii serikali ya samia ndio ina umadhubuti wa kupambana na vita ya madawa ya kulevya??

Kwamba kukamata hao akina choji ambao hata sio main supplier ndio kunakufanya uwe excited namna hii kiasi cha kubwabwaja maneno ya mipasho kama kimama cha uswahilini chenye asili ya kizanzibari?

Wewe nakuona umevimbiwa asali na haujui kinachoendelea, na kwa taarifa yako tu ni kwamba hakuna kipindi ambacho biashara haramu zinafanyika sana tena kwa uwazi kama awamu hii... weka hilo akilini.
Kaka unanisakama bure tu mimi sina hata huo uchawa na wala asali ya ccm sijawahi na siitaki.
Jambo moja unalosahau kujua ni kwamba kwa Katiba Yetu Tanzania bila Rais kutaka hakuna kitu chochote kinawezekana.

Si umemsikia Nape Nauye? Je Tume ya Taifa ya Uchaguzi ina nguvu yoyote juu ya kina Nape?
 
Kaka unanisakama bure tu mimi sina hata huo uchawa na wala asali ya ccm sijawahi na siitaki.
Jambo moja unalosahau kujua ni kwamba kwa Katiba Yetu Tanzania bila Rais kutaka hakuna kitu chochote kinawezekana.

Si umemsikia Nape Nauye? Je Tume ya Taifa ya Uchaguzi ina nguvu yoyote juu ya kina Nape?
Haaa nimekuelewa sasa, ila comment yako ya awali ilikuwa imekaa kichawa zaidi na kilamba asali.... maana walamba asali wanachojua wao ni kutoa sifa za uongo kwa mama yao huku wakipondea awamu iliyopita...

Kuhusu akina Nape Nnauye kuwa na nguvu kuliko tume pamoja na Samia mwenyewe hilo liko wazi wala sio la kushangaza na ndio maana mimi nawachukia sana machawa sababu wanaowakingia kifua ndio wanufaika wakuu wao wanarushiwa mifupa tu.
 
Back
Top Bottom