Muhudumu wa Bar alivyowaabisha jamaa wa "mupe muruke, mupe muruke"

Muhudumu wa Bar alivyowaabisha jamaa wa "mupe muruke, mupe muruke"

Alvin A.

JF-Expert Member
Joined
Oct 14, 2016
Posts
2,865
Reaction score
3,633
Good morning fellas, long time no see

Jana majira ya saa kumi nimeenda Bar fulani ambayo ni hot sana mtaani kwangu, nilikuwa na miadi ya kukutana na jamaa yangu ambaye alikuwa semina so nikawa namsubiri maana nlikuwa na vyeti vyake. Hii bar mi ni regular cuctomer [emoji482][emoji482][emoji482] so meneja na wahudumu wananifahamu vilivyo.

Nikawa nimekaa kwenye meza iliyopo kivulini ina viti vitano ila nilikuwa alone napiga zangu giness smooth bariiiiiidioi[emoji481] meza zingine zilikuwa juani na ndani kulikuwa na kelele na kama kumejaa fulani hivi. Mara wakaja jamaa wawili na madem zao na Alteza[emoji594] yao wamevaa miwani nyeusi[emoji41] na vipensi wakakaa mezani kwani wala sikujali nikaendele kuperuzi kwenye simu yangu [emoji336][emoji336]sina habari.

Wakaagiza vinywaji vya viwili viwili wakaendelea na stori za kwa sauti ya juu hadi wateja wengine wakaanza kututolea macho, walipomaliza mmoja akaropoka "we malaya njoo huku akimpungia muhudumu kwa ishara ya kumuita" alipofika akamwambia lete bia mbili mbili ina muruke huyu jamaa, nikamwangalia nikatabasamu zangu nikaendelea na shughuli zangu.

Yule muhudumu akaja na kapu lina bia 10 akaziweka katikati ya meza akaanza kuzipanga akawapa mbilimbili mi akaniwekea bia 6, wale jamaa wakamuuliza "jamaa hajaagiza hizi bia analipa nani?" Muhudumu kwa lugha ya nyodo na vidole juu kama anawasuta[emoji1305][emoji1305][emoji1305] akawaambia "hizi ni kwa bili yangu upo nyonyo"?

Nikatabasamu kwa jeuriii jamaa wakakasirika wakahama meza na kwenda kukaa juani wateja wengine wakaanza kucheka kile kicheko cha kero na cha kugugumia kwa kwi kwi [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787].

Nikapiga bia tatu mchizi wangu akaja tukaendeleza vinywaji mwisho wa siku nikamlipa dada zile bia sita na zingine tulizokunywa tukasepa.

View attachment 1946817
 
Good morning fellas, long time no see

Jana majira ya saa kumi nimeenda Bar flan ambayo ni hot sana mtaani kwangu, nilikuwa na miadi ya kukutana na jamaa yangu ambaye alikuwa semina so nikawa namsubiri maana nlikuwa na vyeti vyake. Hii bar mi ni regular cuctomer so meneja na wahudumu wananifahamu vilivyo.
😂😂😂
 
Mkuu bia zenyewe hunywi utajulia wapi mambo ya Bar we endelea kupiga umbea na mkeo hao ndani wazee wa mupe muruke tumaelewa hichi alichofanya muhudumu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nalijua sana hilo neno na mimi mdau mkubwa kwenye hayo mambo pengine hata kukuzidi wewe. Ila sijaona cha ajabu hapo mpaka jamaa alete uzi. Inawezekana mpo wengi sana washamba wa biere humu
 
Good morning fellas, long time no see

Jana majira ya saa kumi nimeenda Bar flan ambayo ni hot sana mtaani kwangu, nilikuwa na miadi ya kukutana na jamaa yangu ambaye alikuwa semina so nikawa namsubiri maana nlikuwa na vyeti vyake.
nikapiga bia tatu mchizi wangu akaja tukaendeleza vinywaji mwisho wa siku nikamlipa dada zile bia sita na zingine tulizokunywa tukasepa.
View attachment 1946817
Mwamba naona umeambatanisha na picha kabisa...kama uko na video tupia tuburudike 😂😂😂
 
Nalijua sana hilo neno na mimi mdau mkubwa kwenye hayo mambo pengine hata kukuzidi wewe. Ila sijaona cha ajabu hapo mpaka jamaa alete uzi. Inawezekana mpo wengi sana washamba wa biere humu
Kama umeelewa good for you, sioni tunabishana nini?
 
Back
Top Bottom