Mulika: Hali ya usalama Dar es Salaam ni tete, Kova amelala fofofo

Mulika: Hali ya usalama Dar es Salaam ni tete, Kova amelala fofofo

Tofauti ya mwanzo na kubwa iliyopo baina ya ughaibuni na nchini kwetu sio hatua ya maendeleo ya majengo na miundombinu mingineyo, bali ni utofauti wa usalama wa raia. Polisi wa ughaibuni hana taim na asiye mhalifu, na hawana taim na watu, polisi wetu hawana taim na wahalifu ila na wasio wahalifu. Unatembea usiku kucha hakuna mtu wala polisi atakayekuuliza kama huna shida. Tembea saa tano nchini kwetu na mkeo uone polisi watakavyoona dili. Hili ni jambo la kushangaza sana na linatutoa akili watu weusi, why? why polisi wanakosa maadili kiasi hiki why?. Likitokea tukio la kihalifu litakuwa gumzo na vyombo vyote vya habari, ukisahau japo simu klabuni jua utaikuta au itapelekwa kituo cha polisi. Wakikuona usiku wa maneno unatatizika na jambo, polisi wako tayari kukusaidia si kukutisha,
 
Maelezo yako ni mazuri sana, na hakuna ubishi juu ya mambo hayo,
sasa toa mawazo yako nini kifanyike kama ulivo diclare intrest yako.

soma pale aliposema the way forwad utaona mkuu
 
Wadau

Mambo mengi ya kimafia yalikua yanatokea behind the scene but WATU walikuja kustuka baada ya unyama aliofanyiwa Dr. Ulimboka.....kabla hata machungu ya Dr. Ulimboka hayajaisha.....mara ya Absalom Kibanda yakafuata.....mbaya zaidi wahalifu wa matokeo yote hayo mawili either hawajakamatwa or kufikishwa mahakamani....hakika hili jeshi la Polisi ni la KINGESE sana na linatia hasira( Natamani Kutukana Hapa).....

Kova amelala wakati bosi wake Mwema naye amelala......Kinachotia hasira zaidi THEY ACT LIKE EVERY THING IS OKAY....nakumbuka wakati wa Alfred Tibaigana huu upuuuzi haukuwepo......nakumbuka mm nilikua nalaza gari yangu nje na asubuhi nikiamka nakuta every thing is okay.....leo hata gari ulaze ndani bado hawa MAFIA wanaweza kuingia na kuchukua kila kitu kuanzia taa za gari mpaka power windows......hawaogopi kwasababu huu mtandao unahusisha POLISI wetu FAKE......haya juzi juzi hapa mmiliki wa maduka ya Home Shopping Center Said Mohamed Saad naye yamemkuta yanayowakuta wakazi wengi wa Dar na utasikia Polisi wakiongea their usual Blah Blah " Upelelzi bado unaendelea ukikamilika tutoa taarifa zaidi" Nyambafff upelelezi gani huo usioisha....mbona hadi leo upelelezi wa tukio la Dr. Ulimboka haujakamlika....yaani hili la Jeshi La Polisi limejaa wasanii tu hakuna professionalism wala work ethics.....wanachojua wao ni kusumbua wamachinga na kina mama wauza gongo wa uswahilini....wakati WAUZA UNGA, WAMWANGA TINDIKALI, WATEKAJI NA WEZI WA MAGARI wakitesa jijini hapa na BENZ na HAMMER.

Ndugu zangu wa Dar hapa hakuna cha jeshi la Polisi wala nn kilichobaki ni kila mtu kutafuta mbinu za kujilinda yeye na mali zake......kama ni wafanyabiashara nawashauri aanzisheni vikundi vyenu vya ulinzi.......wasaniii pia aanzisheni vyenu pia.....wakazi wa mtaa na nyinyi pia.....vyama vya siasa nawashauri muwe na brigade zenu kabisa because hakuna kitu kinaitwa Jeshi La Polisi hapa Tanzania.......


Nina hasira hapa mpaka nataka kulipuka


Nawasilisha
 
wauza unga,watekaji,wezi na wamwagia tindikali ni mtu mmoja.
Serikali ikiamua itamaliza hili genge la wahalifu kwa mgongo wa wafanyabiashara.
JK anawafahamu na aliishawahi kukiri,mbona akina ighondu walitajwa na vielelezo kibao lkn ikapigwa kimya.
Ila nahisi unayetafutwa sasa ni wewe maana hauwezi kuwafichua hawa watu na ukabaki salama,nakwambia unaweza kupigwa risasi mbele ya ikulu iwapo utaingia anga za hawa wafanyabiashara wa ikulu.
 
Jeshi limeoza! Rafik yangu mmoja aliwah porwa simu majengo dodoma na anasoma capital collage ualim,tulilipoti polis wakauliza eneo gan mmeporwa tukawaeleza cha ajabu tukaambiwa nenden chuon mtaletewa kwan wale wez tunawafaham, sikuamin kwan siku iliyofuata tulipigiwa sim kuwa kuna mtu katumwa kuileta na kweli tuliipata na mpaka leo wiz pale haujaisha, pia nilikuwa mbeya nikiwa line polis karibu na magereza nilikuwa nikipiga story na maaskar weng walisema wapo kiajira na kipesa hawako tayar kufa mapema kwa kupigwa na majambaz wanajeshi weng wakasema maisha magum ndio maana tumekuja huku, na huku wanabana mshahara tufanye nini kwa hili mwema kala hasara,nilicheka japo yanaumiza.hiyo ndio polis yetu.
 
Nakubaliana na wewe 100% cku hz wananchi tunajilinda wenyewe mfano watu wengi wameajili walinzi kwenye nyumba zao
 
Kwa Dar es salaam kama huwezi kujilinda umekwisha , hawa akina kova na wenzake wapo kwa ajili ya kuwalinda viongozi tu .
 
Ametoa kwenyw way foward au unacomment bila kumaliza kusoma habari yote



maelezo yako ni mazuri sana, na hakuna ubishi juu ya mambo hayo,
sasa toa mawazo yako nini kifanyike kama ulivo diclare intrest yako.
 
Sijaona cha maana ulichozungumza mkuu ni majungu mwanzo mwisho,...kama polisi kachukua mkeo acha kukimbilia jf najibu hoja...

1...Sio kweli kuwa kikaratasi cha Report book kikipotea hauwezi kupata msaada maana kesi zote huwa zinakuwa na mpelelezi na mlalamikaji hvyo basi watarudi kumbu kumbu na utapata msaada.....

2....Moja ya Sifa ya upolisi ni jamii kukuchukia ndo maana polisi wanakuwa close wao kwa wao..,..haitokei Raia kukubali polisi labda tu awe na shida hiyo inaeleweka.
 
kaka kweli umetoka america!unasema siku za hivi karibuni wakati hayo yapo miaka nenda rudi hiyo gerezani watu wanakwenda na kukuta mali zao walizoibiwa na wananunua tena na hakuna wa kumkamata mtu!si bora uibiwe taa,watu wanaibiwa magari na madereva wao kuuawa halafu gari inapelekwa "theater" kubomolewa kila kitu kinauzwa kimoja kimoja hapa hapa mjini faida mara mbili gari ya mil 8 vifaa vyake vyote vikiuzwa watu wanapiga mil 8 mara mbili yake, na soko kubwa ni huko huko kkoo especially mitaa uliyotaja! huenda hata bar unayokunywa huyo mwenye bar ana ofisi yake gerezani!hawa polisi wetu sio wa america kaka,we umesikia ulinzi shirikishi tu hujawahi kujua kuna ujambazi shirikishi?welcome to bongo,devil's playground!hali ni mbaya kaka!naongea si kwa ushabiki,bali masikitiko!serikali yetu ni simba wa kwenye picha,haumi,hang'ati,haparui,hangurumi,hawindi..yupo ukutani tu anapendezesha sebule!
 
Kudhibiti upinzani wanaweza kupitia kikosi cha intelejinsia kwenye uhalifu wanashindwa kwa nini?
 
Mkuu,

Kwanza nikupongeze kwa uzi wako wenye mashiko, kwani suala la usalama ni kipaumbele cha serikali ya CCM.

Pia kuhusu mapungufu uliyo yasema hasa kwenye mazingira ya kazi kwa askari wetu ni sahihi kabisa, hii inatokana na uwepo wa vituo vingi vya polisi kwenye maeneo mbalimbali hapa Dar.

Tuje kwenye kiini cha hoja yako, huo mtandao uliosema ni kweli upo, ila ni ngumu kuweza kuwadhibiti wahalifu hao kwa kuwa parts hizo za magari mara nyingi haziwekwi eneo ambalo wanafanyia kazi hao wahalifu.

Katika kudhibiti uhalifu wa namna hii ina hitajika ushirikiano mkubwa kati ya jamii na polisi, na kwa kulifanikisha hili la ushirikiano ndio tukapata kitu kinachoitwa polisi jamii.

Mkuu, hii nchi yetu ni moja, watanzania ni wamoja, dhamira yetu ni moja ya kuhakikisha ulinzi na usalama vinalindwa. Si vyema kwa wewe kusema hautaki kuwa sehemu ya juhudi za polisi za kupambana na uhalifu, nadhani ni vyema utumie utaalamu wako huo uwe karibu na polisi ili tuweze kufikia azma yetu ya Tanzania bila uhalifu inawezekana.

Ni nani aliyekuteua wewe kuwa msemaji wa serikali ya CCM na jeshi la polisi? Kama jeshi la polisi limeshindwa kuthibiti huo wizi IGP anasubiri nini kujiuzuru au Kova anasubiri nini kujiuzuru? Eti unasema vifaa vinauzwa sehemu tofauti na vinakoibiwa? This is a very silly excuse! Vifaa vinaibiwa keko vinauzwa karume, hivi panahitaji siku ngapi kwa polisi kusafiri na kwenda kufanya investigation pale?

Unasema eti polisi hawana vifaa, kama serikali haina uwezo wa kuwapa vifaa vya kazi polisi ili kuwahakikishia watanzania usalama wao basi ijiuzuru. Sasa umhimu wake wa kuwepo madarakani ni nini? Nilitarajia kwamba kama uki-file kesi yako kituo cha polisi cha Chang'ombe basi hiyo issue iwe kwenye system kiasi cha kwamba hata polisi wa kituo cha Oysterbay au Makambako aweze kuiaccess hiyo kesi na kuishughulikia kama ataona mazingira yanayotoa ushahidi juu ya kile kilichopo kwenye system.

Kwanini serikali inaacha jeshi la polisi lifanye kazi kwa mfumo wa kizamani kiasi hiki? Hovyo kabisa na serikali yenu mahututi ya CCM.
 
Kaka hapa hakuna usalama wowote hebu fikiria ulimboka katekwa toka mwka gani mpka leo hakuna aliekamtwa... Mabom ya arusha mpka leo hakuna taarifa yoyote... Ni nchi gani utaripo tukio uulizwe ushqhidi zaidi ya hapa.. Mtu kamqliza kayumba kafaulu bila kujua kusoma na kuandika kaenda kata nako kafaulu baada ya matokeo kusahihishwa upya baada ya kupata zero ... Then ccp miezi 6 kweli hayo c majanga....
 
Kaka hapa hakuna usalama wowote hebu fikiria ulimboka katekwa toka mwka gani mpka leo hakuna aliekamtwa... Mabom ya arusha mpka leo hakuna taarifa yoyote... Ni nchi gani utaripo tukio uulizwe ushqhidi zaidi ya hapa.. Mtu kamqliza kayumba kafaulu bila kujua kusoma na kuandika kaenda kata nako kafaulu baada ya matokeo kusahihishwa upya baada ya kupata zero ... Then ccp miezi 6 kweli hayo c majanga....

hayo matukio ya kimafia inafanya serikali yenyewe ndio maana inashindwa kukamata waliohusika,kingine ni kuwa huku kushuka kwa uwezo wa jeshi letu kulinda raia na mali zake kumechangiwa kwa kiasi kikubwa na jeshi hilo kuacha majukumu yake ya msingi badala yake kujiingiza kwenye siasa mfu za nchi hii,jeshi la polisi limekuwa sawa na branch ya ccm elsewhere na hapo ndipo tatizo la msingi la jeshi letu lilipoanzia.
 
Nasikia kuna mganga wa jadi anafanya majamboz gari haiibiwi spear kudadeeki.
 
mpelelezi huru umeleta mada nzuri,japo jambo hili lilikuwepo muda mrefu lkn sasa linaonekana kuhalalishwa ba Polisi,mimi nitoke nje ya vifaa vya gari,kuna siku nilikuwa pale kariakoo mtaa wa agrey nikasikia story ya stationary moja iliyovunjwa jamaa wakachukua printer 2,inasemekana za ukweli,aliyeibiwa akaripoti hilo tukio polisi na kama kawaida wakaandika kwenye hizo daftari unazosema,inaaemeka mwenye stationary akaanza kutembeza hela kwa askari mzigo urudi,cha kushangaza ni kuwa askari walimpeleka kwa jamaa mmoja mwizi kweli kweli na huyo jamaa akasema yy hakufanya hilo dili ila akipiga simu mbili,tatu atapata jibu, na kweli ndicho kilichotokea.....mwwnye duka akapata vifaa vyake na askari wakalamba cha juu na wezi hawakukamatwa eti wamemsaidia......hapo wizi utaisha kweli.
 
Back
Top Bottom