Mume aua hausigeli kwa kipigo akimlazimisha amwambie mchepuko wa mke wake ni nani

Mume aua hausigeli kwa kipigo akimlazimisha amwambie mchepuko wa mke wake ni nani

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Picha

JESHI la Polisi wilaya ya Igunga mkoani Tabora linamshikilia Ezekiel Jonas (37), mkazi wa mtaa wa stoo Kata ya Igunga mjini, kwa tuhuma ya mauaji ya binti wa miaka 16, Ester Mahona.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Barnabas Mwakalukwa alithibitisha mauaji hayo na kusema kuwa tukio hilo ni la Mei 5 mwaka huu saa nne usiku katika mtaa wa stoo Kata ya Igunga mjini.

Mwakalukwa alisema mtuhumiwa, Ezekiel Jonas alikuwa anaishi na binti huyo aliyekuwa mfanyakazi wa ndani. Alisema baada ya yeye kutengana na mke wake, alimwita ndani binti huyo na kumuuliza amwambie mwanaume anayetembea na mke wake.

Alisema binti huyo alipoulizwa na mtuhumiwa, alidai yeye hajui kitu chochote, ambapo mtuhumiwa hakuridhika na majibu ya binti huyo, hivyo alianza kumshanbulia kwa kumpiga kichwani na kitu chenye ncha kali hadi kusababisha kifo chake.

Alisema mtuhumiwa alipoona ameua, alichukua mfuko wa sandarusi na kuuweka mwili wa marehemu kwenye mfuko huo.
“Polisi tulipata taarifa kutoka kwa raia wema wakisema kuna binti anapigwa vibaya na tajiri yake.

Sisi tulifika eneo la tukio majira ya saa nne usiku, ambapo tulikuta mtuhumiwa ameshamuua binti huyo huku akiwa amemuweka kweye mfuko wa sandarusi” alisema.
Mtuhumiwa atafikishwa mahakamani wakati wowote. Alisema chanzo cha mauaji hayo ni wivu wa mapenzi.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Igunga, Merchades Magongo alithibitisha kupokea mwili wa Ester Mahona Mei 5 majira ya saa 4:30 usiku. Alisema baada ya kuufanyia uchunguzi, waliwakabidhi ndugu zake kwa ajili ya mazishi.

Chanzo: Mtanzania
 
R.I.P Angel,
Hao washenzi wamekatisha maisha yako bila huruma, Dunia itawanyoosha.

Boost your Immune System to fight a Covid-19.
 
Mbunge wa Chadema mollel alisema swala la lissu ni inside job, hapa dereva wa lissu akirudi Chadema inaweza kupata jinai
Kemea pia wa tundu lissu,azory gwanda,na wengine wengi waliodhuriwa na kuuwawa na ccm
 
Back
Top Bottom