Mume kizimbani kwa kutishia kumuua mke kisa kupeleka chakula kwa mchungaji

Mume kizimbani kwa kutishia kumuua mke kisa kupeleka chakula kwa mchungaji

Ila hii nchi bana, wanawake wa nchi hii sijui wamepatwa na nini! Jamaa katishia kumuua mke wake kisa mama watoto anamplekea nyama mchungaji
[emoji23][emoji23]

“Mheshimiwa hakimu huyu mwanamke anakera sana, yaani tukichinja kuku, vipaja na vidari vyote anapelekewa mchungaji, alafu mimi ninayetafuta pesa kwa shida napewa vipapatio."

“Hii tabia imeota mizizi kiasi kwamba nahisi anatoka naye kimapenzi, kwanza mchungaji mwenyewe hana mke. Hivi hata ungekuwa wewe usingehisi vibaya?”

- Joseph Moses mkazi wa Mbeya anayedaiwa kutisha kumuua mkewe
 
Ila kuna wanawake sijuagi wana akili gani, kuna mwingine nae huku kaachika kisa hakai kabisa nyumbani anashinda kanisani.
 
Japo kutishia kuua ni kosa, ila alilofanya huyu dada ni ujinga na upumbavu kwa wakati mmoja. Hatukatai mtu kumtolea Bwana sadaka ila aina hizi za sadaka ni dhambi si sadaka tena.


---
Joseph Moses dereva wa ‘bodaboda’ mkazi wa Mbeya anayekabiliwa na shtaka la kutishia kumuua mkewe kwa maneno, Irene Mwaikana, ameiambia mahakama kuwa chanzo cha ugomvi huo ni tabia ya mkewe kupeleka chakula kwa mchungaji.

Moses ametoa madai hayo katika Mahakama ya Mwanzo mjini Mbeya chini ya Hakimu Upendo Moshi alipokuwa akitoa ushahidi wake mahakamani hapo.

Ameiambia mahakama kuwa anafanya kazi kwa shida na kukutana changamoto nyingi hususani ajali za barabarani, lakini pindi anaporudi nyumbani anakuta mkewe amepika chakula na kukipeleka kwa mchungaji.

“Mheshimiwa Hakimu huyu mwanamke anakera sana, yaani tukichinja kuku, vipaja na vidari vyote anapelekewa mchungaji, alafu mimi ninayetafuta pesa kwa shida napewa vipapatio,” amedai.

“Hii tabia imeota mizizi kiasi kwamba nahisi anatoka naye kimapenzi, kwanza mchungaji mwenyewe hana mke, hivi hata ungekuwa wewe usingehisi vibaya?” amehoji.

Moses anadaiwa kutenda kosa hilo Agosti Mosi mwaka huu usiku, na ndipo mkewe alipomfikisha mahakamani akidai kutishiwa kuuawa.

Chanzo: Swahili Times
Huyu ni wakutandika tu makofi ya masikioni na kumdurisha kwao, au unamkabidhi kwa "mchungaji"
 
Church woman wengii ni hatari kwa ustawi wa ndoa..na wengi wamevuruga mpk familia zao kisa huko kanisani na wachungaji wao
 
Hao ndiyo baadhi ya wanawake yaani, hapo usikute ameamua kwenda mahakamani kabisa ili jamaa afungwe yeye aendelee kula maisha na mchungaji, maana kama si dhamira yake kumfunga wangemalizana polisi then angeachana na jamaa maisha yaendelee

Kitendo cha mume kukesha akiitafuta pesa ya kulea familia, halafu mke naye anakuwa busy kulea mchungaji inaumiza sanaaaa
 
Hawa wanawake na wachungaji wao sijui wameumbwaje sijui akili zao zinawaza nini.. ukute huyo mchungaji ndiyo kamshauri aende mahakamani kumshtaki waachane
Hili lidini la kipumbavu sana. Na watu/wanawake wanavyopenda upumbavu, basi wanamiminika huko.
 
Tuna mahakama za hovyo sana,
Badala ya kusuhisha ndoa, wanataka kuivunja ndoa.

Hili suala lilitakiwa liishie huko serikali za mitaa au ustawi wa jamii.

Hivi wanategemea wakishamshughulikia uyo mume, kutakua na ndoa Tena hapo?

Vipi kuhusu hao watoto wa hiyo familia?
Mahakama itatoa malezi na matunzo?

Ujinga mtupu[emoji3525]
 
“Mheshimiwa Hakimu huyu mwanamke anakera sana, yaani tukichinja kuku, vipaja na vidari vyote anapelekewa mchungaji, alafu mimi ninayetafuta pesa kwa shida napewa vipapatio,” amedai.

“Hii tabia imeota mizizi kiasi kwamba nahisi anatoka naye kimapenzi, kwanza mchungaji mwenyewe hana mke, hivi hata ungekuwa wewe usingehisi vibaya?” amehoji.
Mchungaji kajifanya ndege wa angani halimi, havuni wala kuweka ghalani lakini muumini wake anamlisha
 
Back
Top Bottom