Mume kumgeuza rafiki ndio kila kitu kwake

Mume kumgeuza rafiki ndio kila kitu kwake

Zumarudi

Member
Joined
Jan 12, 2023
Posts
5
Reaction score
39
Habari zenu wapendwa,

Mwenzenu nina changamoto nipo kwenye ndoa miaka 13. Mimi na mume wangu tulikuwa tunapendana sana tulikuwa marafiki wazuri ila baada ya kuhamia Dar mwaka 2015 kuanza maisha mume wangu akapata Rafiki uyo Rafiki yake ni wale watu wenye uswahili mwingi maisha yakaendelea tukapata maisha biashara nzuri tuna mafanikio sasa hivi, ila yule Rafiki wa mume wangu Hana kazi kwa hiyo muda wote anafatana na mume wangu.

Muda mwingine mume wangu anaacha kazi kwenda kuzurura na rafiki yake nikawa namwambia mume wangu shughuli za kazi zetu ni mjini wewe unashinda Mbagala huku biashara nani anaendesha, basi anakuwa mkali.

Yaani nikitaka kumuongelea huyo rafiki yake vibaya anakuja juu. Mume hanywi pombe havuti sigara hapendi mpira ila siku akiwa na rafiki yake kurudi nyumbani ni saa 7 au saa 8 usiku msg za wanawake kama zote kwenye simu ila wakitengana na Rafiki yake kama miezi miwili au mitatu anawahi kurudi simu anaacha peupe anashinda mazingira ya kazini.

Mwanzo nikasema labda mimi namchukia huyu Rafiki yake ngoja nianze kuongea naye, ukikaa naye ni kama mtu Mwenye chuki na wanawake haoni thamani ya mwanamke anamwambia mume wangu

1) Mwanamke akikupenda anakuwa kama mzigo bora kuishi na mwanamke asiyekupenda

2) Hii alinambia mimi yaani wewe usipokuwa karibu na mimi nina uwezo kumharibu mumeo kumpeleka kwenye makundi mabaya na urafiki wangu na mumeo wakutenganisha Bado hajazaliwa

3) Mke kitu gani, wangapi tunasikia huyu alikua mke wa fulani kwa hiyo kuachana na mke sio ishu.

Mume wangu kila kitu cha ndani ya ndoa anamwambia hakuna kitu hajui nilimwambia mume wangu vitu vingine ni siri yetu haelewi.

Mume wangu nampenda ila nahisi ye anampenda zaidi rafiki yake kuliko Mimi. Imefikia hatua nawaza niondoke nimuache na Rafiki yake au niendelee kumvumilia huyo Rafiki yake maana hata akipiga simu huyo Rafiki yake anaenda kuongelea nje.

Nahisi ndoa imekuwa ya watu wa tatu sio wawili tena naomba mnisaidie ushauri.
 
Ndio baadhi ya wanaume walivyo hatuwezi kuamini ke percent 100 no way lazima utafute rafiki mwenzako wa kiume mshauriane kiume zaidi au umesahau sir God alituasa tuishi nanyi kwa akili hivyo simpingii mshkaaji yupo very right hivyo tulia tu ndani Mambo yasije yakawa mengi hapa 🤣🤣🤣🤣 utaisoma namba safari hii.
 
Muombe sana Mungu lakini pia tumia chumvi ya mawe kumfukuza huyo shetani maana keshaiingilia ndoa yenu na hakuna mchawi anaweza kumtoa mpaka mfilisike kabisa.

Ameshapata pa kuponea kwahiyo usimuoneshe kabisa kwamba unamchukia, maana kwa jinsi alivyomkamata mumeo anaweza kumuamrisha chochote naye akafanya.
 
Ndo baadhi ya wanaume walivyo hatuwezi kuamini ke percent 100 no way lazima utafute rafiki mwenzako wa kiume mshauriane kiume zaidi au umesahau sir God alituasa tuishi nanyi kwa akili hivyo simpingii mshkaaji yupo very right hivyo tulia tu ndani Mambo yasije yakawa mengi hapa 🤣🤣🤣🤣 utaisoma namba safari hii
Huu ni ushauri mbovu kuuona tangu mwaka huu uanze ukiachana na nyuzi za kisiasa za wana-CCM.Umeambiwa uishi na mke kwa akili na siyo umpe jirani au rafiki akili akushikie.Simama kama mwanaume.Kwani lazima utumie akili za rafiki uliyekutana naye tu mjini kuiendesha familia yako?Huo ni udhaifu daraja la juu sana.Badilika!
 
Ndo baadhi ya wanaume walivyo hatuwezi kuamini ke percent 100 no way lazima utafute rafiki mwenzako wa kiume mshauriane kiume zaidi au umesahau sir God alituasa tuishi nanyi kwa akili hivyo simpingii mshkaaji yupo very right hivyo tulia tu ndani Mambo yasije yakawa mengi hapa 🤣🤣🤣🤣 utaisoma namba safari hii
Na wewe umetoa bonge la ushauri!🤣🤣 "utafute rafiki wa kiume mshauriane kiume zaidi"...hata mambo ya faragha we umshirikishe rafiki, hata ya kiuchumi we mwambie tu kila kitu.

We jamaa bwana!!
 
Ndo baadhi ya wanaume walivyo hatuwezi kuamini ke percent 100 no way lazima utafute rafiki mwenzako wa kiume mshauriane kiume zaidi au umesahau sir God alituasa tuishi nanyi kwa akili hivyo simpingii mshkaaji yupo very right hivyo tulia tu ndani Mambo yasije yakawa mengi hapa [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] utaisoma namba safari hii
Huu ni uandishi wa kijana ambaye bado yupo chuo au amemaliza hivi karibuni bado hajaanza kusota na vibahasha,
Kuna mada zingine zinakua kubwa unaachana nazo tu.
 
Muombe sana Mungu lakini pia tumia chumvi ya mawe kumfukuza huyo shetani maana keshaiingilia ndoa yenu na hakuna mchawi anaweza kumtoa mpaka mfilisike kabisa

Ameshapata pa kuponea kwahiyo usimuoneshe kabisa kwamba unamchukia, maana kwa jinsi alivyomkamata mumeo anaweza kumuamrisha chochote naye akafanya
Umemshauri vizuri kaka mkubwa.

Story ya huyo dada inafanana na ya Aunt yangu, ndoa yake ili vamiwa na kidudumtu akamshika Anko kichwa akawa anamtafutia wanawake, kila kitu anamshirikisha, nyumba ikawa haina amani, hajali tena familia yeye ni wa kupelekeshwa na huyo rafiki aliyemuamini kuliko nafsi yake, Aunt alikonda sana, alihangaika sana kuwatenganisha vikao na vikao viliwekwa lakini wapiiii.

Siku moja huyo kidudumtu akamtambulisha Anko kwa mwanamke akadai alikua anaishi Uingereza ameachana na mume wake amerudi Tz, basi wakaanza mahusiano penzi lilinoga akawa harudi nyumbani hata wiki, nguo akahamishia kwa huyo Muingereza, si akaanza kumjengea nyumba bhana, unaambiwa Anko alitumia pesa zake zote na mikopo juu kujenga nyumba ya kifahari, nyumba ilijengwa kwa shinikizo la huyo huyo rafiki mtu akamshawishi ajenge nyumba ya kifahari amuoe huyo mwanamke waishi wote.

Kufupisha story, siku moja anko, kidudumtu na yule mwanamke walikua hoteli moja maarufu kwenye live band, mmoja wa waimbaji wa ile Band anawafahamu wote watatu si ndio akaenda kuwasalimia bhana akawa anamuita yule mwanamke shemeji, kwa kuzuga ikawa hana namna ilibidi aitikie na kulazimisha uchangamfu, baada ya yule muimbaji kuondoka kidudumtu na Mwanamke wa UK hawakua na furaha baada ya muda wakaondoka, lakini Anko akabaki na alama nyekundu vipi yule muimbaji amuite yule Mwanamke Shemeji? Alijua ni Mwanamke wa nani wakati yeye mke wake anajulikana na yule hawara anamficha kama bangi sura yake haitambuliki isipokua kwa rafiki yake? na Rafiki yake hana Mke? Hakutaka kupuuzia hilo.

Weekend iliyofata akaenda peke yake akamuomba muimbaji wazungumze pembeni, alipomuuliza kama yule mwanamke anamjua muimbaji akashangaa sana akamjibu mbona yule ni mke wa rafiki yako? Ina maana pale kwenye meza nyie mlikaa bila kujuana au ina maana hujui kama rafiki yako ana mke na watoto na yule mwanamke! Anko alipoteza fahamu hapo hapo.

Anko aliwajengea Mume na Mke nyumba nzuri huku yeye akibakiwa na madeni na msongo wa mawazo alirudi kwa mke wake suruali imetepeta, zombie si zombie ilichukua miezi 6 kurecover, nyumba hakuipata na huo ndio ukawa mwanzo na mwisho wa urafiki wao.

Kuna tetesi zilisema alikua anaenda kuitizama nyumba yake kwa mbaaali huku analia ndio familia ikaazimia imuhamishe Mkoa.
 
Dunia imeshapinduka sasa hivi angalia na chunguza vizuri mambo yafuatao kati ya mme wako na huyo rafiki yake:-
1. Ushoga
2. Ushirikina
3. Dawa za kulevya
Kati ya hayo matatu hutokosa moja, haingii akilini mtu mpaka anaacha shughuli za uzalishaji na kwenda ku mfuata mwanaume mwenzie Mbagala!!!!!!
 
Umemshauri vizuri kaka mkubwa,
Story ya huyo dada inafafa na ya Aunt yangu, ndoa yake ilavamiwa na kidudumtu akamshika Anko kichwa akawa anamtafutia wanawake, kila kitu anamshirikisha, nyumba ikawa haina amani, hajali tena familia yeye ni wa kupelekeshwa na huyo rafiki akiyemuamini kuliko nafsi yake, Aunt alikonda sana, alihangaika sana kuwatenganisha vikao na vikao viliwekwa lakini wapiiii,

Siku moja huyo kidudumtu akamtambulisha Anko kwa mwanamke akadai alikua anaishi Uingereza ameachana na mume wake amerudi Tz, basi wakaanza mahusiano penzi lililonoga akawa harudi nyumbani hata wiki, nguo akahamishia kwa huyo Muingereza, si akaanza kumjengea nyumba bhana, unaambiwa Anko alitumia pesa zake zote na mikopo juu kujenga nyumba ya kifahari, nyumba ilijengwa kwa shinikizo la huyo huyo rafiki mtu akamshawishi ajenge nyumba ya kifahari amuoe huyo mwanamke waishi wote,

Kufupisha story, siku moja anko, kidudumtu na yule mwanamke walikua hoteli moja maarufu kwenye live band, mmoja wa waimbaji wa ile Band anawafahamu wote watatu si ndio akaenda kuwasalimia bhana akawa anamuita yule mwanamke shemeji, kwa kuzuga ikawa hana namna ilibidi aitikie na kulazimisha uchangamfu, baada ya yule muimbaji kuondoka kidudumtu na Mwanamke wa UK hawakua na furaha baada ya muda wakaondoka, lakini Anko akabaki na alama nyekundu vipi yule muimbaji amuite yule Mwanamke Shemeji? Alijua ni Mwanamke wa nani wakati yeye mke wake anajulikana na yule hawara anamficha kama bangi sura yake haitambuliki isipokua kwa rafiki yake? na Rafiki yake hana Mke? Hakutaka kupuuzia hilo,

Weekend iliyofata akaenda peke yake akamuomba muimbaji wazungumze pembeni, alipomuuliza kama yule mwanamke anamjua muimbaji akashangaa sana akamjibu mbona yule ni mke wa rafiki yako? Ina maana pale kwenye meza nyie mlikaa bila kujuana au ina maana hujui kama rafiki yako ana mke na watoto na yule mwanamke!,
Anko alipoteza fahamu hapo hapo,

Anko aliwajengea Mume na Mke nyumba nzuri huku yeye akibakiwa na madeni na msongo wa mawazo alirudi kwa mke wake suruali imetepeta, zombie si zombie ilichukua miezi 6 kurecover,nyumba hakuipata na huo ndio ukawa mwanzo na mwisho wa urafiki wao

Kuna tetesi zilisema alikua anaenda kuitizama nyumba yake kwa mbaaali huku analia ndio familia ikaazimia imuhamishe Mkoa.
Kuna tetesi zilisema alikua anaenda kuitizama nyumba yake kwa mbaaali huku analia ndio familia ikaazimia imuhamishe Mkoa.[emoji23]

Mkishakuwa familia kwa maana ya mume na mke mnapaswa kuwa makini sana na outsiders
 
1. Muombee kwa Mungu sana huyo mume wako, afunguke macho na masikio yake atambue na kujali thamani na hisia zako kwake. Tumia meditation- unamwomba Mungu muda wote na kwa ukimya kabisa. Asijue mtu unachokiwaza.

2. Usimjali, usimwogope, usimnyenyekee hata kidogo wala usimwoneshe chuki directly huyo rafiki yake. Kuwa bold. Akijichekesha shem shem we kuwa serious usimkenulie meno au kumjibu..aone tofauti flani.

3. Badilika katika mambo yako na tabia zako flani flani positively, na yeyote asijue kwanini umebadilika ghafla. Kama ulizoea kuamka saa moja, amka saa 12 asbh. Kama ulizoea kulala na vyombo vichafu au jikoni rafu.. ongeza usafi zaidi. Hali kadhalika na usafi binafsi (in case haukuwa 100%)

  • Acha kumwongelea huyo rafiki wa mumeo kwa mumeo, acha kabisa tena kwa ghafla. Endelea tu na meditation kwa Mungu wako kuwa waachane/ mumeo afunguliwe.
  • Ikitokea siku mumeo akasema jambo flani baya alilokerwa na huyo jamaa, usikimbilie kuchangia moja kwa moja, kuwa "si nilikwambia!" au "ndio matokeo ya ubishi wako!" No, No! Usije kufanya jambo hilo. Badala yake toa jibu la general kama vile " uwe makini na marafiki" basi.
  • Kila la kheri.
 
Back
Top Bottom