Mume kumgeuza rafiki ndio kila kitu kwake

Mume kumgeuza rafiki ndio kila kitu kwake

Huu ni uandishi wa kijana ambaye bado yupo chuo au amemaliza hivi karibuni bado hajaanza kusota na vibahasha,
Kuna mada zingine zinakua kubwa unaachana nazo tu.
Siyo mwanandoa na bado yupo chini sana kwenye mahusiano yaki jamii, Serikali inabidi iwekwe somo la mahusiano yaki jamii mashuleni ili kuokoa jamii, sisi watanzania atujui mipaka ya mahusiano ya ndugu jamaa na marafiki.
 
Habari zenu wapendwa,

Mwenzenu nina changamoto nipo kwenye ndoa miaka 13. Mimi na mume wangu tulikuwa tunapendana sana tulikuwa marafiki wazuri ila baada ya kuhamia Dar mwaka 2015 kuanza maisha mume wangu akapata Rafiki uyo Rafiki yake ni wale watu wenye uswahili mwingi maisha yakaendelea tukapata maisha biashara nzuri tuna mafanikio sasa hivi, ila yule Rafiki wa mume wangu Hana kazi kwa hiyo muda wote anafatana na mume wangu.

Muda mwingine mume wangu anaacha kazi kwenda kuzurura na rafiki yake nikawa namwambia mume wangu shughuli za kazi zetu ni mjini wewe unashinda Mbagala huku biashara nani anaendesha, basi anakuwa mkali.

Yaani nikitaka kumuongelea huyo rafiki yake vibaya anakuja juu. Mume hanywi pombe havuti sigara hapendi mpira ila siku akiwa na rafiki yake kurudi nyumbani ni saa 7 au saa 8 usiku msg za wanawake kama zote kwenye simu ila wakitengana na Rafiki yake kama miezi miwili au mitatu anawahi kurudi simu anaacha peupe anashinda mazingira ya kazini.

Mwanzo nikasema labda mimi namchukia huyu Rafiki yake ngoja nianze kuongea naye, ukikaa naye ni kama mtu Mwenye chuki na wanawake haoni thamani ya mwanamke anamwambia mume wangu

1) Mwanamke akikupenda anakuwa kama mzigo bora kuishi na mwanamke asiyekupenda

2) Hii alinambia mimi yaani wewe usipokuwa karibu na mimi nina uwezo kumharibu mumeo kumpeleka kwenye makundi mabaya na urafiki wangu na mumeo wakutenganisha Bado hajazaliwa

3) Mke kitu gani, wangapi tunasikia huyu alikua mke wa fulani kwa hiyo kuachana na mke sio ishu.

Mume wangu kila kitu cha ndani ya ndoa anamwambia hakuna kitu hajui nilimwambia mume wangu vitu vingine ni siri yetu haelewi.

Mume wangu nampenda ila nahisi ye anampenda zaidi rafiki yake kuliko Mimi. Imefikia hatua nawaza niondoke nimuache na Rafiki yake au niendelee kumvumilia huyo Rafiki yake maana hata akipiga simu huyo Rafiki yake anaenda kuongelea nje.

Nahisi ndoa imekuwa ya watu wa tatu sio wawili tena naomba mnisaidie ushauri.
Ushauri wangu wagombanishe anza mahusiano na huyo rafiki yake ikiwezekana mtongoze kama akikubali ukikaa nammeo uwe unamsifusifu jamaa tu mala ana gaden lov zili mala yupo strong mmeo ataanza kukata mahusiano na rafikiake kwa speed
Endapo ya kwanza itafeli kama anakulaga chakula unacho pika anza kumjali kupitiliza mpigie simu za njoo tule mala kwa mala ikiwezekana una over the game maisha sio lele mama

Sent from my TECNO B1f using JamiiForums mobile app
 
Duh, ndugu hiki kisa hakipaswi kuwa comment. Hii ilitakiwa iwe katika uzi unaojitegemea. Kuna somo kubwa mno hapa.
Unataka kusema amemfunika mtoa mada..?? Ni kawaida hyo mbna. Umesahau uzi wa Rikiboy watu walitoa Visa Mara mia vizuri kuliko cha kwake.. na uzi ukatembea Kama fire.jf ukiona stor imeandikwa focus Kwa wachangiaji utapata Madini ya kutoshaa
 
Umemshauri vizuri kaka mkubwa.

Story ya huyo dada inafanana na ya Aunt yangu, ndoa yake ili vamiwa na kidudumtu akamshika Anko kichwa akawa anamtafutia wanawake, kila kitu anamshirikisha, nyumba ikawa haina amani, hajali tena familia yeye ni wa kupelekeshwa na huyo rafiki aliyemuamini kuliko nafsi yake, Aunt alikonda sana, alihangaika sana kuwatenganisha vikao na vikao viliwekwa lakini wapiiii.

Siku moja huyo kidudumtu akamtambulisha Anko kwa mwanamke akadai alikua anaishi Uingereza ameachana na mume wake amerudi Tz, basi wakaanza mahusiano penzi lilinoga akawa harudi nyumbani hata wiki, nguo akahamishia kwa huyo Muingereza, si akaanza kumjengea nyumba bhana, unaambiwa Anko alitumia pesa zake zote na mikopo juu kujenga nyumba ya kifahari, nyumba ilijengwa kwa shinikizo la huyo huyo rafiki mtu akamshawishi ajenge nyumba ya kifahari amuoe huyo mwanamke waishi wote.

Kufupisha story, siku moja anko, kidudumtu na yule mwanamke walikua hoteli moja maarufu kwenye live band, mmoja wa waimbaji wa ile Band anawafahamu wote watatu si ndio akaenda kuwasalimia bhana akawa anamuita yule mwanamke shemeji, kwa kuzuga ikawa hana namna ilibidi aitikie na kulazimisha uchangamfu, baada ya yule muimbaji kuondoka kidudumtu na Mwanamke wa UK hawakua na furaha baada ya muda wakaondoka, lakini Anko akabaki na alama nyekundu vipi yule muimbaji amuite yule Mwanamke Shemeji? Alijua ni Mwanamke wa nani wakati yeye mke wake anajulikana na yule hawara anamficha kama bangi sura yake haitambuliki isipokua kwa rafiki yake? na Rafiki yake hana Mke? Hakutaka kupuuzia hilo.

Weekend iliyofata akaenda peke yake akamuomba muimbaji wazungumze pembeni, alipomuuliza kama yule mwanamke anamjua muimbaji akashangaa sana akamjibu mbona yule ni mke wa rafiki yako? Ina maana pale kwenye meza nyie mlikaa bila kujuana au ina maana hujui kama rafiki yako ana mke na watoto na yule mwanamke! Anko alipoteza fahamu hapo hapo.

Anko aliwajengea Mume na Mke nyumba nzuri huku yeye akibakiwa na madeni na msongo wa mawazo alirudi kwa mke wake suruali imetepeta, zombie si zombie ilichukua miezi 6 kurecover, nyumba hakuipata na huo ndio ukawa mwanzo na mwisho wa urafiki wao.

Kuna tetesi zilisema alikua anaenda kuitizama nyumba yake kwa mbaaali huku analia ndio familia ikaazimia imuhamishe Mkoa.
Hapa ndio huwa naikumbuka ngoma ya Proff Jay - Bongo Dar Es Salaam, ukiwa afya lege lege unakata moto unajiona hivi hivi
 
Usimwamini......

Mwanamke........cos ni wabinafsi
Mume akiwa na rafiki shida ila marafiki awe nao yeye wew hubaki kama sanamu no friend no friend...............
Mwanaume yeyote hua na ukomo kwenye urafiki hasa huu urafiki wa ukubwani hua tunaweka limit mara nying urafik wetu hua unapande mbili yaani kila mmoja atanufaika kwenye urafiki huo.....(fighting spirit)........
 
Hapa ndio huwa naikumbuka ngoma ya Proff Jay - Bongo Dar Es Salaam, ukiwa afya lege lege unakata moto unajiona hivi hivi
"Aliyeuza Cheni ameuza Cheni bandia na aliyeuziwa Cheni ametoa hela bandia, tuliozoea jiji tunasema ngoma droo"..... Ila kwa huyu Anko wa Mari, alipigwa na kitu chenye ncha kali, amejifunza kwa kweli, lol
 
Unataka kusema amemfunika mtoa mada..?? Ni kawaida hyo mbna. Umesahau uzi wa Rikiboy watu walitoa Visa Mara mia vizuri kuliko cha kwake.. na uzi ukatembea Kama fire.jf ukiona stor imeandikwa focus Kwa wachangiaji utapata Madini ya kutoshaa
Nadhani alimaanisha story nzuri kama ile yenye funzo imefichwa kwenye comment ilipaswa iwe na uzi wale ili iwafikie wengi kwa urahisi wajifunze..... Mimi mwenyewe kanisimulia kwa kirefu aisee inatishaa kuna watu wauaji, imebidi huyo mjomba nimuonee tu huruma.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] ina maan docs za nyumba na ardhi zilikua jina la nani?
Khaaaaaaah.
We acha tu babe, unaambiwa mjomba alikua anamwaga mihela tu yeye si ndio alikua anamjengea mwanamke kwa hiyo docs majina ya huyo mwanamke..... ila angekua ni mjomba angu ningebeba panga nikadai jasho letu 🤣
 
Nadhani alimaanisha story nzuri kama ile yenye funzo imefichwa kwenye comment ilipaswa iwe na uzi wale ili iwafikie wengi kwa urahisi wajifunze..... Mimi mwenyewe kanisimulia kwa kirefu aisee inatishaa kuna watu wauaji, imebidi huyo mjomba nimuonee tu huruma.
Njoo tusimulie na Sie basi...
 
Habari zenu wapendwa,

Mwenzenu nina changamoto nipo kwenye ndoa miaka 13. Mimi na mume wangu tulikuwa tunapendana sana tulikuwa marafiki wazuri ila baada ya kuhamia Dar mwaka 2015 kuanza maisha mume wangu akapata Rafiki uyo Rafiki yake ni wale watu wenye uswahili mwingi maisha yakaendelea tukapata maisha biashara nzuri tuna mafanikio sasa hivi, ila yule Rafiki wa mume wangu Hana kazi kwa hiyo muda wote anafatana na mume wangu.

Muda mwingine mume wangu anaacha kazi kwenda kuzurura na rafiki yake nikawa namwambia mume wangu shughuli za kazi zetu ni mjini wewe unashinda Mbagala huku biashara nani anaendesha, basi anakuwa mkali.

Yaani nikitaka kumuongelea huyo rafiki yake vibaya anakuja juu. Mume hanywi pombe havuti sigara hapendi mpira ila siku akiwa na rafiki yake kurudi nyumbani ni saa 7 au saa 8 usiku msg za wanawake kama zote kwenye simu ila wakitengana na Rafiki yake kama miezi miwili au mitatu anawahi kurudi simu anaacha peupe anashinda mazingira ya kazini.

Mwanzo nikasema labda mimi namchukia huyu Rafiki yake ngoja nianze kuongea naye, ukikaa naye ni kama mtu Mwenye chuki na wanawake haoni thamani ya mwanamke anamwambia mume wangu

1) Mwanamke akikupenda anakuwa kama mzigo bora kuishi na mwanamke asiyekupenda

2) Hii alinambia mimi yaani wewe usipokuwa karibu na mimi nina uwezo kumharibu mumeo kumpeleka kwenye makundi mabaya na urafiki wangu na mumeo wakutenganisha Bado hajazaliwa

3) Mke kitu gani, wangapi tunasikia huyu alikua mke wa fulani kwa hiyo kuachana na mke sio ishu.

Mume wangu kila kitu cha ndani ya ndoa anamwambia hakuna kitu hajui nilimwambia mume wangu vitu vingine ni siri yetu haelewi.

Mume wangu nampenda ila nahisi ye anampenda zaidi rafiki yake kuliko Mimi. Imefikia hatua nawaza niondoke nimuache na Rafiki yake au niendelee kumvumilia huyo Rafiki yake maana hata akipiga simu huyo Rafiki yake anaenda kuongelea nje.

Nahisi ndoa imekuwa ya watu wa tatu sio wawili tena naomba mnisaidie ushauri.
Hii ni hoja nzito sana best.

Hapo ulipo, upo njiapanda bila kufahamu uelekeo halisi. Hebu tuangalie haya mambo kidogo.

1.
Mtu anayechukia wsnawake inawezekana ni mhanga wa downsyndrome aliyetokana na malezi ya kufanyiwa ukatili na wsnawake labda mama wa kambo, mashangazi au upande wa mama ambao walimtesa sana hadi kikua.
Au labda ameshaumaliza mwendo na sasa anafanya mambo sambamba na wanawake hivyo hawezi kukubali kuzidiwa na wanawake.

2.
Hana kazi na anazurura kutwa na mumeo, inawezekana anatumia uchawi kumnasa mumeo ili kuchuma mali kutoka kwenu. Jaribu kuchunguza kama ana watoto na wanatunzwaje? Hizi zipo sana mjini yaani mtu hana kazi lakini mboga saba hazikosekaniki mekoni

3.
Jamaa labda ni dalali wa wsnawake na hivyo anamuonesha mumeo viwanja vipya vya matumizi.

4.
Shetani ameingilia ndoa yako.

USHAURI
1.
Usiache kumuomba Mungu wako atengeneze ndoa yako

2.
Tafuta watu wenye busara wakae na ninyi wawili muanze kuyajenga. Na ikiwezekana viongozi wa dini wenye kuthamini na kuheshimu ndoa wahusishwe

3.
Ukiona hakuna ni vyema unaruhusiwa kuchukua hatua za kisheria dhidi ya huyo rafiki wa mumeo kwa sababu anaingilia mahusiano yenu halali

Usiache kusali
 
Acha kulalamika kwa vitu vya kupita

Wanawake mko na njaa Sana inawatesa Mimi binafsi Sina Muda kumsikiliza Mwanamke wengi waongo waongo plus roho mbaya .

Hii nimeona Sana wanawake hawapendi mtu Apate hata Muda wa kufurahi na marafiki ni upuuzi mtupu kid

Hamna shetAni hapo
 
Back
Top Bottom