Mume wa ndoa akikujibu hivi utajisikiaje?

Mume wa ndoa akikujibu hivi utajisikiaje?

...uhudumiwe kwani wewe mtoto ?!..jihudumie mwenyewe
Una mume mnaishi pamoja kama mwaka hivi, hamjabahatika kupata mtoto. Tangu umeolewa jamaa amekuwa mzito sana kukuhudumia na akitokea amekuhudumia, ni mpaka kumetokea ugomvi mkubwa.

Yeye anachojua ni kuhemea chakula ndani tu.

Unavyojaribu kumuuliza mbona mimi hanihudumii anajibu "Nilisoma kwa ajili ya ndugu zangu tu, na ninatafuta pesa kwa ajili ya ndugu zangu tu"

Je, kama wewe ni mke utajisikiaje, na utachukuwa maamuzi gani?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
....constructive advice,..MTU mzima unalalamika kuhudumiwa kweli ?!
Alisoma kwa ajili ya ndg zake, hapo ni kuchakarika kutafuta zako ili ujihudumie na uhudumie ndg zako, mimi binamu yangu kaoa muda kidogo, wifi akawa analalamika hasaidii ndg zangu, kuja kulalamika kwa mama yangu, na kufunguliwa akili wewe upo home umekaa tu toa cherehani yako upinde kanga upate hela usaidie ndg zako. Hadi saiz ndg zake wakija anawasaidia fresh tu haya mambo ya kumtegemea mwanaume binafsi siyawezi.

FANYA MPANGO WA KUTAFUTA PESA YAKO, USIMTEGEME

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bidada anamaduka yake ya dawa 2 jamaa anahakikisha anasimamia

Kama alikutwa na duka lake kwa nini asibaki kulisimamia Hilo ili apate mahitaji yake asiboreke na majibu ya jamaa?

Kuna mama mmoja ni mke wa Doctor wa chuo kikuu kimoja maarufu , huyo Doctor Ana mashule pia Tena yanajaza kweli kweli so pesa iko ndefu. Yule mama amepewa kumsimamia ishu za makusanyo ya Ada kwa kuwa wafanyakazi wakiwekwa wanaiba mno kwa kushirikiana na management iliyopo. Cha kushangaza Yule Doctor huwa hamhudumii mkewe kwa chochote zaid sana Mara moja kwa week atampatia elf 2 ya nauli jioni ambayo haitoshi mafuta ya Corolla anayotumia (ambayo alinunua mwenyewe kwa kuwa ni mfanyakazi pia). Yule mama anachofanya anaiba mbayaaaa kwenye makusanyo ya mumewe. Hapo anafanya yake na anapata mahitaji . Yule Doctor ni Malaya mbaya na anahonga hatari. So bi dada ajiongeze kikubwa asikamatwe tu maana ukute michepuko inafaidi Kama kawaida Ila yeye ndo anateseka
 
Kiwango Cha chini ambacho anaweza pata ni 2m icho nikiwango Cha chini
Hiyo 2m ni hela anayoingiza kwa mwezi?Kama ni hivyo anajimudu vizur.
Lakini pia inategemea tena mwanzoni ulianza naye kwa staili gani,Kama ulianza kwa kumbughuzi kwa kuomba misaada ya kila siku isiyokuwa na mwisho wanaume huwa tunachoka na kuzira.
Jitahidi kuwaseti ndugu zako kwamba inapotokea shida ya msingi tu ndio waombe msaada.
Kwa mfano Kama Kuna mgonjwa amelazwa na inahitajika pesa ya matibabu hii ni shida ya msingi.
Au imetokea mzazi ameishiwa kodi ya nyumba na vyombo vinataka kutolewa nje,hii ni shida ya msingi.
Au imetokea mdogo wako anasoma na anadaiwa ada hadi inapelekea anataka kufukuzwa shule hii ni shida ya msingi.
Ila usipende mme wako aombwe pesa kila siku hadi za kwenda kufanyia starehe,itakuwa fedheha.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Una mume mnaishi pamoja kama mwaka hivi, hamjabahatika kupata mtoto. Tangu umeolewa jamaa amekuwa mzito sana kukuhudumia na akitokea amekuhudumia, ni mpaka kumetokea ugomvi mkubwa.

Yeye anachojua ni kuhemea chakula ndani tu.

Unavyojaribu kumuuliza mbona mimi hanihudumii anajibu "Nilisoma kwa ajili ya ndugu zangu tu, na ninatafuta pesa kwa ajili ya ndugu zangu tu"

Je, kama wewe ni mke utajisikiaje, na utachukuwa maamuzi gani?

Duh, muda mrefu sana ulipumzika kuleta thread za namna hii.
 
Tatizo ninaloliona hapo ni majibu yake machafu hilo la kutokutoa mahitaji lipo ndani ya ndoa nyingi.Wanaume wengi hawajui majukumu yao,yeye anataka wewe utimize yake lakini yeye hapana.Na ukimkumbusha majukumu yake ugomvi unaanzia hapo.Kuna haja ya vijana kupewa semina na kuelezwa majukumu yao kwenye ndoa na sio kupenda papuchi tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hilo ni simango kubwa mno. Hivi wanaume wenzetu wa hivi mlilazimishwa kuoa au? Ningekuwa huyo mwanamke naondoka mchana jua likiwa katikati ya dunia na sitageuka nyuma. Nitaapa nikigeuka nibadilike kuwa mnara wa chumvi.

Dada jipange huyo mwanaume labda ulilazimisha kuelewa naye au ana mwanamke pembeni hivyo hana haja na wewe. Chapa lapa.
 
Back
Top Bottom