Mume wa shangazi kwa Kiswahili sahihi anaitwaje?

Mume wa shangazi kwa Kiswahili sahihi anaitwaje?

Tanga wabondei wanaita Mtumba na maana yake walisema ni mjomba kule kwetu sisi hakuna mkaza wala nn ni Mjomba tu
 
Kitu mkaza shangazi hicho. Kama mkaza mwana tu. Ila kiswahili kiboko huu utaratibu wa kutumia mkaza sijui waliwaza nini!!!
 
Mimi niliwahi kumwuliza mume wa shangazi yangu mimi nimwiteje? Akaniambia mimi ni shemeji yako. Kwa hiyo ninavyofahamu mume wa shangazi ni shemeji yangu na tulikuwa tunaitana hivyo!!
 
Wanaomwita mume wa shangazi kuwa ni baba shangazi ni makosa!! Unaposema baba shangazi unamaanisha ni baba wa shangazi. Lakini baba wa shangazi ni babu mzaa baba yako na mzaa shangazi yako,
 
Karibuni tujadili mume wa shangazi tumwiteje? Vinginevyo tumbatize jina fulani na uwe ni mchango wa jamii forum kwenye kukuza msamiati wa kiswahili. Nawaza tumtize kumwita SHANGAMU. (kifupi cha shangazi mumewe!)
 
Back
Top Bottom