Mume Wangu Ametishia Kuniua, Sababu, Urafiki na Mzungu na Kutembelea U-turn

Mume Wangu Ametishia Kuniua, Sababu, Urafiki na Mzungu na Kutembelea U-turn

Acha ushamba wa kushobokea wazungu!!!Hauwafahamu vema hao watu wewe!!!Kwanza unaonekana bado mshamba ana haujakua.Vitu unavyovitetea ni upumbavu mtupu ukilinganisha na thamani ya ndoa na heshima kwa mume.Wanawake mnakosea sana kuchanganya u beijing(Kujifanya nawe jeuri) katika mambo ya kidini.Kama uliolewa kidini(sio kuwekwa tu ndani) ni lazima uliapa kumheshimu na kumtii mumeo!!Yeye ndo kichwa cha familia,analosema litii.Eti u turn mara rafiki yangu mara mzungu wewe WANAKUSAIDIA nini hawa zaidi ya mume.Nina wasiwasi kuwa uliolewa kwa kusikilizia upepo wa kutoka kimaisha sasa umeona matarajio finyu wataka kujaribu bahati kwa mzungu.Aibu kwako.UKIMALIZA KUSOMA HAPA RUDI HOME MUOMBE MSAMAHA MUMEO
 
Wanasema ukiwa muongo usiwe unasahau ulichokisema rejea post zako za nyuma ulivyosema kuhusu UTURN.

CPU tukumbushe kidogo alichosema, nimeamini JF kuna vichwa maana hapo juu kuna mtu alishatoa angalizo kwa zionist juu ya hili
 
Zionist,
Sio haki kabisa,urafiki na mzungu zidisha ukiweza kalale na kwake kabisa,U-turn usiikose hata sekunde moja ili usinyanyasike kijinsia..afu matokeo uturudishie..,
 
Maskini yutani inashika kasi...kila anaeitembelea anatamani kuwa na uhusiano na mzungu! hiki sio kisa cha kwanza wala cha pili kinachohusishwa na U-Turn blog
mimi ni mshabiki wa blogu ya u-turn, ila mume wangu kwa muda wa miezi minne sasa amekuwa na kisirani kweli heti, kisa mimi kuitembelea hiyo tovuti ya uturn. sababu zake ni kwamba nina ujeuri. basi kuna rafiki yangu mmoja ambaye ameolewa na mzungu aliniita nyumbani kwake. shemeji yake ambaye pia ni mzungu alikuwepo hapo. tukapata vinywaji kidogo, na kubadirishana namba za simu na huyu shemeji yake. mara kadhaa tumewasiriana kama marafiki tu, mume wangu akatokea kuona text moja niliyotumiwa na huyu mzungu mabayo ilikuwa tu ni knijulia hali, matokeo yake kaja juu na kunipiga sana. Alinifukuza kwa siku 4, pia ananitishia kuniua iwapo sitasitisha mawasiliano na huyu mzungu pamoja na kuacha mara moja kutembelea blogu ya uturn. Hataki hata urafiki wangu na yeyote ambaye ana uhusiano na huyo dada mwenye blog ya u-turn. Anasema heti nikiendelea kutokumsikiliza ataniua na huyu mzungu, wakati mzungu wa watu hana hatia yoyote? Jmani huu si ni ubaguzi wa rangi? kwa nini anifukuze au kuniua, kisa urafiki na mtu wa rangi tofauti, hii kweli ni haki? mm urafiki na mzungu siachi, na uturn siondoki, huu ni unyanyasaji wa kijinsia
 
Nndoa ni sacrif,e sometimes, unatakiwa uache vitu fulani ambavyo mwenzi wako havifurahii.usidhani wenye miaka miingi kwa ndoa ua wana experience raha pekeyake! kuna changamoto sana. sioni tatizo kwa wewe kuachana na huo urafiki wako na huyo mzungu kwa manufaa ya ndoa yako! lakini kama we unadhani hutaki endelea ila iko siku unawez kujuta sana.
 
mumeo kashakupa masharti ayatakayo ila wewe hutaki kutimiza. huo ndio ujeuri ulionao. kwa upande wangu sina cha kukushauri zaidi ya kukwambia utimize yale ayatakayo mumeo. lakini kwa kuwa u mjeuri na pia unawasiliana na mzungu sidhani kama nitakuwa nimefanikiwa kukushauri. kila la kheri ila ndo wapi sijui,norway au denmark au holland? popote kule ili mraadi mzungu.
 
Wanawake wajinga wajinga kama wewe hayo ndo mnayostahili. Inaelekea wewe ni kichwa maji na dawa yako ndo hiyo dozi anayotoa mumeo
 
Mfuate huyo mzungu kondoo wewe....! Unaonywa, halafu unabaki kujadili na kuonesha kiburi chako hata huku JF....! Kweli wewe hadi hapo hufai tena....!
 
......mm urafiki na mzungu siachi na uturn siondoki, huu ni unyanyasaji wa kijinsia

huyo mzungu si mume wa rafiki yako, ni hawara yako. you are just stupid, disclosing your stupidity.
Kipigo cha mbwa mwizi na talaka ni dawa stahiki kwako. ili umgande huyo mzungu na ikiwezekana hata rafikiyo ajue kuwa unatembea na mumewe ili naye akuanzishie.
 
Nakukumbusha tu nadhani umesahau wewe ni mke wa mtu, kwa nini una fikiri kiuchanga hivyo?
Maelezo yako 100% yanaonesha una intrest na mzungu, kama umepigwa na unakiri hutakomesha iyo tabia, inaonesha umejitoa kwa mzungu kwa gharama yoyote hata kuisaliti ndoa yako.
Usipokomesha iyo tabia na kufuata ya mumeo, naona mambo mawili,
1. Mumeo atakuacha
2. Utadhani utakuwa huru na mzungu lakini baada ya muda mfupi atakuacha kwani anae anayempenda kwanza ni mwaribifu huyo.
Unapaswa kufanya yafuatayo:
1. Leo mkiwa chumbani na mumewako mwombe msamaha kwa upendo na umuahidi kuzingatia yote aliyokuelekeza mara moja.
2.funga iyo acount, sahau ao marafiki kwa ajili ya amani na furaha ya ndoa yako.
3.muombe MUNGU WA MBINGUNI sana akupe ujasiri na hekima ya kumtii mumewako na kuondolea tamaa za mali.
4.usifanye jambo lolote wala kuingia urafiki na mtu bila kukubaliana na mumeo, nyie ni mwili mmoja, ndipo mtapata furaha.
 
naomba niongee kwa lugha ya kuonya

haya ndio huwa nayakataa kila siku hapa jf...huwez kuja na hoja za kijinga na kipuuzi kama hizi wewe....sasa hapa unatafuta nini kama hutaki kuacha kile unachoambiwa na mume wako?

acha upuuuuzi na tuondelee mapepe yako hapa....hebu tuekee hapa hiyo sms ya huyo mzungu ilikuwa inasemaje...kuwa muwazi...
 
Duh! Ama kweli JF kiboko....kumbe humu unatakiwa upost mada ambazo ni well researched, evidence based.....wee mdada tafadhali waombe wanaJF msamaha halafu mengine yatafuata
 
haswaaa!!!
sasa huyu hajateleza, amekuja humu kuchafua hali ya hewa!!
aende zake akapige U Turn kule kwa Mashosti wake


Kweli mkuu nadhani mtoa mada amekosea njia alifikiri ni uturn hapa... pumb**u zake!!!
 
Wewe endelea kuingia huko uturn na endelea na huyo mzungu wako na mwisho wake utauawa kama si kuachwa.. Baadae sijui utaijutia uturn au mzungu... UTAJUUUUUTA kuzaliwa!!!
 
Q1. Choose the corect answer.
(a) kuacha kutembelea u-turn
(b) kuuliwa:hatari:
(c) kuachwa
 
Wewe huna lolote kwa jinsi ulivyojiapia hapo mwisho, ni wazi uko tayari kuachana na mumeo na kuolewa na mzungu kila la heri, hivi ukiambiwa mume wako huwa anakutana mahali na rafiki yake na mke wake na pembeni kuna kademu ambako hukaelewi then ukagundua huwa wanawasiliana utaona poa tu ee
Nimependa Avatar yako, Duuh hicho kitambiiiiiiii !!!!!!!!!!
 
Ok tusimlaumu zionist nahisi sio yeye kai copy mahali kaileta hapa tuchangie,zion tujulishe kama hii inakuhusu wewe.
 
Achana nayo!Kwani usipotembelea itakuaje?

mume ni kichwa cha familia!! mtii, hayo si maneno yangu bali Biblia takatifu!!

hivyo chagua moja, umtii mumeo Mungu akuheshimu, au kutomtii shetani akugeuze kitoweo!!
 
ushehe yahaya wangu unaniambia lazima huyu atakuwa kala mkorogo tu afanane na wazungu. ningekuwa mod ningempiga ban yeye na shangazi yake. nimekasirika kweli, yaani kama hii laptop si ya kuazima ningevunjilia mbali kwa hasira. (naomba unitulize mzuka keren)

Mmmmmmh, punguza nzuka!
 
Back
Top Bottom