Mume wangu hapendi kula nyumbani

Mume wangu hapendi kula nyumbani

Ni chakula gani hicho ambacho mumeo hula kwa kijiko?

Nadhani wewe unajua kupika, lakini hujui ni aina gani ya chakula upike. So unapika chakula ambacho mumeo hali! Lazima ale kidogo ashibe.

Ukweli ni kuwa wanaume wengi tunakula huko mtaani kama nyumbani hakipikwi kitu ambacho tunapenda. Tena ukute mumeo ni mtu wa asili ya kutosema kwa haraka kama kitu hakipendi, yaani hawezi kukwambia moja kwa moja kuwa hapendi kitu flani, anaona atakuudhi kukwambia moja kwa moja. Hivyo wewe ndio tumia maarifa.

Cha kufanya, nenda out na mumeo (wewe ndo umtoe na ikiwezekana mlale huko huko), mwache aagize yeye kwanza chakula, chunguza ataagiza nini! Chunguza pia kama ni breakfast ataagiza nini. Baada ya hapo utajua unapaswa kupika vyakula gani kwa mumeo.
Ah jamani
Mambo ndio magumu hivo
🤣🤣🤣
 
Kwa mentality uliyo nayo utaendelea kuteseka sana.
Heshima gani umepata hadi sasa? kuliwa huliwi na sasa hali chakula unachopila

Huna ubavu wa kuwa single.
[emoji1][emoji1][emoji1][emoji1]jamani mnampa makavu live daahhh!!
 
..ila wanawake waliokulia mbali na bahari kupika chakula kizuri chenye radha bado ni changamoto!
...... from my own experience.
Uongo yani jamii ya pwani inayojua kupika ni wazaramu na wandeleko lakini wazazibar ndiyo wabovu wakupika sana kupika mboga hawajui wanapika michuzi ya maji, kupika pilau hawajui pia kupika Samaki haaajui.
 
Tukiandika tunaonekana walokole. Anyways kama wewe ni Mkristo..Omba. Yani simama kwenye maombi na kumuamini Mungu kweli kweli. Ninachoona hapa unalengwa wewe kuondolewa kwenye nafasi.

Kuna maneno umeyaandika hapa tayari shetani kashakudaka. Katika Mith 6:2 neno linasema "umetegwa kwa maneno ya kinywa chako, umekamatwa kwa maneno ya kinywa chako." Shetani anachofanya kakungoja utype.."sometimes ndoa hizi bora uwe single..umeolewa kwa ajili ya heshima tu". Usifikiri ulichotype kimeenda bure. Maana si unaona bora uwe single ok fine, haujakiri anything positive rather comments za humu zinazidi kukuvuruga kihisia na kiufahamu.

Wewe tena....unazidi kuharibu kwa maneno yako mwenyewe. Mungu aliumba dunia kwa neno, neno lako lina uwezo mkubwa wa kujenga ama kuharibu. Ukijiita wewe ni masikini..kweli utakuwa..what do you speak over your life, marriage, children, in laws, relatives??...jifunze kuwa na positive affirmations.

Nakuambia hili kwa sabbu mm ni mhanga. Nilikuwaga naongea negative kila mara katika maisha yangu. Sikuwahi kusogea. Kila ukurasa ulikuwa umefungwa. Nilipoanza kukiri kushinda kila siku mambo yakaanza kubadilika moja baada ya jingine.

Ni muda wa kumconsult Mungu miss. Ni muda wa kwenda kuongea naye what is happening and the changes you want to see happen in your marriage. God is able..I know it for sure. Mume wako ni mdogo sana mbele ya baba yake aliye mbinguni. Kama hilo agano mlilifunga mbele za Mungu, uwe na uhakika ni Mungu huyohuyo anaeweza kuirestore hiyo ndoa. Lakin sasa usiende mbele zake huku unajihesabia haki. Nenda mbele zake huku unatubu kabisa kutoka moyoni. Maana neno linasema wote tumetenda dhambi hata kupungukiwa na utukufu.

Utukufu wa Mungu ukiondoka lazima furaha na amani viondoke. Mimi ni shuhuda wa hii statement. Ilinichukua mwaka kugundua hili. Ask God where did you go wrong? Maana mpaka shetani kuingia hapo kuna mlango ulifunguliwa..na wewe kama mlinzi wa familia hukusimama nafasi yako. Naweza kuandika mengi lakin for consultation zaid am available PM. Ila kama utaona naongea nonsense please usimind..potezea hii comment..achana nayo madam. All the best.
Dear pitia thread zake kwanza kuhusu uchumba mpk ndoa
 
Habari zenu wapendwa?

Naombeni msaada Mume wangu amekuwa pasua kichwa hapendi kula nyumbani, najua kupika nampikia vyakula vizuri lakini akija anakula tu kidogo anaacha wakati mwingine hali kabisa ukimuliza hana sababu.

Mwanzo nilijua labda napika vibaya lakini siyo maana watu wengine wakila hata wageni wanakifurahia sana chakula mpaka wananisifia najua kupika Ila mme wangu ndo tatizo anaweza akala hata vijiko 5 akasema ameshiba.

Hii hali kwakweli inaniumiza sana akili na uzuri ana mwili nahisi labda atakuwa anakula uko nje akija anakuwa labda ameshiba maana ka jinsi anavyokula hapa ndani alitakiwa awe hana hata afya yani kwa kifupi ni Kama tu hali Ila anagusagusa Kuna wakati hadi nawaza sijui kalogwa.
Kama anapiga mitungi, jua tu tu anakula Bar na kuhusu wageni hao lazima wasifie maana ni wageni ila all in all maada anatimiza mahitaji ya nyumbani na ya ndoa, mengine achana nayo. mi mwenyewe kula home huwaa weekend tu maana nikitoka job napitia sehemu napiga kamnyweso na nyama au mchemsho ndio narudi home ila weekend nashinda home hadi sa11 ndio natoka.
 
Imebidi nipitie nyuzi zake
Sina uhakika kama alifosi ndoa lakini ndoa yake ilikuwa inaonekana itakuwa chungu kabla hata haijafungwa

Yes yaani ishara zilianza mapema Sana kabla ya ndoa yake, namuonea huruma mnoo
Mungu ampe faraja siku Moja ktk ndoa yake
 
Kuna watu hawana adabu humu, anaandika kitu unamuonea huruma kabisa kumbe anadanganya kuinjoi watu[emoji28]
Hahaha...hadanganyi huyuu anasema Kweli nachomshauri APAMBANE kusali snap na kuomba kwa Imani yake
 
Nimeisoma itakua kuna tabia mbaya alizionyesha baada ya yy kutolewa mahari labda dharau...thats why mama mkwe akawa hataki tena...na kaka amefosi kuoa naona labda sasa na yy ndo anayaona...itakua huyu bi dada hana heshima ana mdomo mchafu...
[emoji1][emoji38][emoji38][emoji125][emoji125][emoji125]kalpana Mungu anakuona
 
Nendeni Msalato ukamshauri
[emoji1][emoji1][emoji1]
[emoji38][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1]depal aje ajifunze nyama choma
Miss chuga Mungu ampe hekima na busara ktk hili
Nilisusiwa kula siku Moja Tena ilikua hivi katoka kachelewa kurudi akakuta nshakula(utaratibu ni kula pamoja)we akagoma kula kasusa,dogo nilitupa sahani na vyakula nikapiga teke bwana wee[emoji38][emoji38][emoji38]nilikumbatiwa Kwa nguvu nkaombwa msamaha na sikussusiwa Tena ht nitoe boko
 
Mumeo kama ni mnywaji wa pombe mpikie vyakula vya kilevi.

Cheza na vitu vya kukaanga.. kama ndizi za kukaanga;, viazi na nyama za kukaanga.

Pia mpikie michemsho chemsho kama ndizi za kuchemsha na masupu supu ya nyama nyama za kuchemsha .

Kutegemea mtu alietoka kunywa bia ale wali maharage kisa umeunga na nazi ni upumbavu.

Hata mpishi atoke mbinguni kuna vyakula mtu alietoka kunywa pombe hawezi kula
[emoji23]
 
Back
Top Bottom