Mume wangu hapendi ndugu zangu

Mume wangu hapendi ndugu zangu

Mkuu, amini maneno yangu. Ikitokea siku mumeo na mdogo wako wakaja kupatana na kucheka pamoja.

Elewa umeshachelewa. Ameshapigwa mtu tako 3000.

Mimi ni mwanaume na nimeshapitia yote hayo. Kuanzia kutongoza mashemeji na hata marafiki wa mke.
Hapo mumeo katoswa na mdogo wako hilo ndy tatizo. Hamisha mdogo wako, au kubali kushare mapenzi.

Ukweli mchungu.
Dada najidai anamjua sana mume wake mara ooho sio muhuni yani anachekesha sana kiukweli MME WAKE ANAMTAKA MDOGO WAKE... NA HUENDA AMESHAKULA MARA MOJA SASA DOGO ANABANA. akiweza amuamishe hapo nyumbani.
 
Hili ni tatizo kwa kizazi hiki cha shetani, wao walisaidiwa waliishi kwa watu lakini wakipata awataki watu waishi kwao. Wengine ufikia mbali zaidi awataki ndugu zao wala wa upande wa pili. Yaani mtu ataki ndugu wa upande wa kike wala upande wa kiume.
 
Ka
Kasema uwezo wa hostel hana

Ndio aendelee hivyohivyo kuvumilia kwani atakaa hapo milele. Degree ni miaka 3-5 avumilie.

Hapo sio kwao, sio kwake.
Hivyo avumilie yote.

Huyu Dada asitake mdogo wake akae Kwa ku-relax kama yupo Nyumbani.
Kwanza hiyo sio nzuri Kwa Afya ya ndoa.
Ni rahisi kuibiwa Mume na mdogo MTU.
 
Huyo ni mbinafsi aliyepitiliza,
Ukishamjua mtu hakusumbui Tena,
Anza kutomchukulia serious kweye hayo mambo yake ya uselfish, mpuuze na usiruhusu moyo wako uumie simply umeshamjua, act matured and normal anapokupa changamoto kama hii.

Akiona haujali atabadilika mwenyewe na kuacha ubinafsi japo itachukua muda ila matunda utayaona.

Ubinafsi ni roho ya kurithi
 
Hili ni tatizo kwa kizazi hiki cha shetani, wao walisaidiwa waliishi kwa watu lakini wakipata awataki watu waishi kwao. Wengine ufikia mbali zaidi awataki ndugu zao wala wa upande wa pili. Yaani mtu ataki ndugu wa upande wa kike wala upande wa kiume.

Huko Kwa watu walikoishi hawakupata changamoto?
Hizo ni changamoto za kawaida.

Kizazi cha sasa ndio kinataka kuishi Kwa Watu Kwa ku-relax bila ya kuwa na changamoto Jambo ambalo haliwezekaniki
 
Kama mda umebakia mchache amalize chuo bora mvumilie hivyo hivyo tu sometimes, mtu mbinafsi ni kumpuuza kwa kumkomoa. Ndoa ni pamoja na ndugu.
 
Hili ni tatizo kwa kizazi hiki cha shetani, wao walisaidiwa waliishi kwa watu lakini wakipata awataki watu waishi kwao. Wengine ufikia mbali zaidi awataki ndugu zao wala wa upande wa pili. Yaani mtu ataki ndugu wa upande wa kike wala upande wa kiume.
Na wengi unakuta walilelewa kwa ndugu hivyo hivyo. Ila wakioa hawawataki ndugu. What a selfish race!
 
Ukisema hanipendi nanyong’onyea maana ananijali yani kuna vitu ananifanyia naridhika so nikimuhukumu kwa hili ntakua nakosea. Roho ya kimaskini siwezi Kupinga ila naikemea tu kwa jina la Muumba. Na ntafanyeje sasa ndo mume wangu wa ndoa
Pole sana, Wenye roho ya kokoto wapo wengi sana na wabinafsi, yaani anampenda mke au Mme tu, ndugu zake wakija sawa lakini wa upande wa pili ananuna hiyo pia ni roho mbaya, hata mtu akikaa kwenye sofa anaona kama analiharibu, kuna mdada mtoto wa ndugu yake aliletewa pale Mama yake alipata matatizo mtoto wa miaka 3, mmewe hataki akae kwenye sofa, na kulalamika anamaliza chakula na alipelekwa kwa muda tu, huyo Baba ni wawapi, kuna familia moja wao kwa Dada yao wanajazana hata usafiri wanaendesha, ila yeye ndugu wa mkewe akija ananuna hawezi kukaa sebule kama karudi kazini hawezi msalimia anapitiliza chumbani na anataka kupelekewa chakula huko, ni tabia tu ya uchoyo na roho mbaya
 
Huyo wa shemeji kumjibu mume wala haihusiki kwanza mume wangu hata jamii forum account hana. Angekua ana jeuri ningeshamcharaza mwenyewe na anamuogopa mume wangu kweli.

Na kwa bahati nzuri mdogo wangu hadi leo anaamini mimi ndo mkorofi nna mcontrol kuliko shemeji yake😃 nimeona bora nibebe mimi ubaya. Ye anaaamini shemeji yake ni mkimya hana shida. Na mimi naendeleza imani hiyo so hiyo story yako hapa wala haiingii
Mimi ni mwanaume na nakupa ushauri kutokana na experince kubwa niliyo nayo kutokana na kuwa na shida kama yako. Yalinipata mimi na nimeshaona yakipata familia kadhaa. Mimi nilikuwa natuhumiwa tuhuma kama ulizoandika. Ni hivi: wanawake wengi wenye tuhuma kama zako, hupofushwa na undugu, wakajiona kuwa wanalofanya wao ni sahihi kabisa, pia wakaona wanalofanya ndugu zao ni sahihi kabisa, kumbe ukichukuwa mtu neutral anaona kabisa wana makosa.
 
Kanuni za kuishi kwa watu usirelax, watendee wema wafadhili wako wataona umuhimu wako watakuthamini ni nature. Laws of attraction. Amka kabla yao somba maji, piga deki, fagia Uwanjani, safisha mazingira, safisha magari, waandae watoto kwenda shule, fanya nao homework. Sio unaamka saa tatu unawahi gombea rimoti na watoto. Unarudi mda uutakao. Unapolelewa nawe lipia gharama kwa kutoa nguvu na mda wako.
 
Vipi kuhusu hao ndugu wengine wanaokuja hapo kusalimia na anawatosa? Mimi siamini kwamba binti kamkataa, hapo issue ni gubu la mwamba, hataki ndugu wa mke waishi hapo.
Huyo baba kweli ni gubu na huenda hiyo tabia kairidhi kwa wazazi sasa kuitoa ni kazi sana na tabia nikama ngozi ya mwili, halafu utakuta yeye anataka mkewe awafanyie mema ndugu zake ni ujinga na upumbafu kabisa halafu ukute eti msomi duu Mungu amsaidie huyo dada.
 
Asante kwa ushauri,

naweza kuwapa benefit of doubt katika kugegedana, mdogo wangu amefata nyayo zangu na ananijua vizuri tu na kiukweli uhuni hana.

Mume wangu kusema anatembea nae naweza kumtetea kwa sasa, mimi ni mtu mfatiliaji sana wa hisia so kama kuna mahusiano kati yao ntakuwa wa kwanza kujua ila kwasasa ntakua natenda dhambi kumuhukumu mume wangu siku akinipa
Hiyo sababu ntajua tu.

Sababu ambayo nahisi ni kwamba mume wangu hajawahi kuishi na familia kubwa yenye ndugu mchanganyiko kama mimi nilivyokua wazazi wetu maisha yao yoye wamekua wakiishi na ndugu zao so nilijifunza huko kuwa kila mtu ni mwanadamu mwenye uwezo wa kukosea.

Kilichonileta natamani mume wangu awe na amani na mdogo wangu naumia kuwa katika position ya kumfukuza mdogo wangu wakati mimi ndo nilishadadia aje hapa ili awe karibu na chuo. Leo namwambiaje nenda nyumbani? Ni mbali sana kutokea nyumbani kwenda chuoni kwao. So kwa hapa kwangu anarahisisha.
Wanaume wachache sana wenye hizo mambo za kuchukia ndugu wa ukweni tena mwanafunzi atleast angekua hana ramani yupoyupo tu, mi nadhani huyo shemeji yetu aliomba mchezo akanyimwa jaribu kufatilia kiundani.
 
Huyo mwanaume anashinda nyumbani mda wote hadi apate huo mda wa kuchukizwa na shemeji.
Au alimtaka akachomolewa so anasaka sababu. Tabia za kuchukia ndugu nilidhani ni wanawake pekee. Kumbe na wanaume nao wapo
 
Huyo mwanaume anashinda nyumbani mda wote hadi apate huo mda wa kuchukizwa na shemeji.
Au alimtaka akachomolewa so anasaka sababu. Tabia za kuchukia ndugu nilidhani ni wanawake pekee. Kumbe na wanaume nao wapo
Wanaume wapo wengi sana wenye roho ya hivyo wanawake huwa tunazuga kama mwanaume ana roho ya hivyo unafunika funika ili kuficha aibu
 
Habari wakuu, nahitaji ushauri,

Mimi ni binti nimeolewa naishi na familia, mume wangu pamoja na mdogo wangu wa kike. Tatizo ni kwamba mume wangu amekuwa na kisirani sana juu ya huyu mdogo wangu wa kike. Kila anachofanya lazima mwanaume alalamike.

Na wala sijawahi kuwa na mawazo labda anamtaka, ndiyo maana anafanya hivi visirani vyote. Mazingira niliyomlea mdogo wangu namjua na ana tabia njema sana.

Mume wangu pia siwezi kumuhukumu kwa uhuni, hajanipa sababu ya kufanya hivyo. Kwahiyo kinachonichanganya ni kwanini ananipa wakati mgumu wa kumfanya mdogo wangu aishi kama yuko kwa mtu baki wakati mimi ni dada yake wa kuzaliwa naye kabisa?

Kila kitu ni lazima aseme kana kwamba huyu mtoto anamkwaza. Kinachoniuma mimi ni kwamba kila siku namuuliza hivi kama angekuwa anaishi hapa ndugu yako halafu mimi namfanyia hivi
Ungejiskiaje? Si ningeonekana mimi ndiyo mbaya sipendi ndugu wa mume?

Na kinachonishangaza, kuna kijana tunaishi naye hapa siyo ndugu wa damu wa mume wangu lakini anatusaidia kazi za hapa nyumbani, ametokea kijijini kwao. Sasa huyu hata akosee vipi mume wangu ukimwambia huyu kakosea hiki na hiki wala hutomuona akijigusa kwenda kumfokea wala kumsema.

Sana sana atajibaraguza tu ili uone ame 'react' na hii siyo mara ya kwanza. Chochote kinachomuhusu mtu wa kwao hutomuona mume wangu amekasirika, lakini ikiwa ni swala la kuhusu ndugu yangu atafoka haswa.

Inafika hatua anamnyima hadi vitu vya kutumia ndani ambavyo hata yeye anavitumia. Hiyo siyo shida, naumia kwasababu mimi huyu mtoto namchukulia kama mwanangu wa kumzaa, nimelichukua hilo jukumu kwa mama yangu tangu mdogo na kwa sasa mama haishi Dar na hatujawa na mahusiano mazuri sana na baba yetu kwa sababu ya mambo ambayo amekuwa akifanya kwetu sisi kama familia.

Kwahiyo najitahidi sana mdogo wangu asijihisi mpweke wala asione kuna pengo la kuumizwa kimalezi na baba yetu.

Na kuna siku ilikuwa sikukuu, nilimwambia mume ndugu zangu wanakuja kwasababu wazazi wetu hawaishi hapa Dar naomba sisi hapa tuwafanyie kitu kama kuwaalika wale hata chakula cha kawaida tu, akasema yeye hana hela.

Wala sikukasirika, nikajikokota nikanunua vyakula nikapika nioneshe kama mume wangu ndiyo amewaalika na wao waone wana kaka hapa mjini. Mume wangu wala hakuonesha ule ushirikiano ambao mimi huwa nautoa wakija ndugu zake, maana huwa napika haswa hadi kwenye kuni.

Nahangaika, napanga, naandaa, nikijua ndugu wa mume wangu wanakuja ila siku wamekuja wadogo zangu sikupata ushirikiano huo. Nilisema acha tu nivumilie kwasababu namheshimisha mume wangu mwenyewe.

Mara nyingine aliniliza na nikamwambia mimi huwa silii lakini unanitenda kama vile sisi kwetu ni masikini, yaani wadogo zangu walipita kutusalimia wakawa sebuleni akaniita chumbani akaniambia nataka kuja kukaa sebleni, naomba nikute siti ya kukaa. Kanakwamba wadogo zangu wamejaa pale maana walikuja kusalimia.

Kinachoniuma ni kwamba, sisi katika kukua kwetu hatujawahi kulelewa na ndugu, kama wadogo zangu wanakaa nje ya kwa baba na mama basi kwangu ndiyo pa kwanza, kwahiyo nikiona wanatendewa hivi naona kama ni mimi ndiyo napitia, sitamani wajione watu baki.

Na kuna muda huwa nawaza, ningekuwa na uwezo ningejenga nyumba yangu niwaweke wadogo zangu hadi watakapokuja kuolewa. Atakae tawanyika sawa, ila kwakuwa mzazi wetu ana uwezo ataona nampokonya wanae. Ila natamani sana wadogo zangu waishi maisha niliyotamani kuishi.


Ushauri unaohitajika;

1. Ni kosa mimi kumtetea mdogo wangu? Kwasababu ninapo jaribu kuuliza kwani tatizo lipo wapi hadi ufoke juu ya jambo dogo hivi, naonekana mkorofi au nataka kumpanda mume kichwani?!

2. Kiubinadamu, huyu mdogo wangu amekosea kuja kuishi kwangu? Nimemlea na hana tabia mbovu kwahiyo namjua, na kila siku namwambia mdogo wangu ikitokea leo dada yako nimedondoka, watoto wangu hutowaacha naamini.

Nampenda sana huyu mtoto, Mungu pekee ndiyo anajua. Kuna muda namwambia mume wangu basi nisamehe mimi naomba vumilia kidogo huyu mtoto akipata kazi ataondoka.

Kwasababu siyo kwamba kwetu tuna shida ya kifedha na wala mume wangu hamgharamii chochote zaidi ya chakula ninachokula mimi ndiyo anachokula huyu mtoto. Ni anakaa kwangu kwasababu ni karibu na chuoni anaposoma yeye.

Kwa upande wa nauli na gharama za kujikimu anatoa mzazi na mimi nikipata huwa nampa kidogo, nashindwa hata kusema namuhudumia maana biashara niliyokuwanayo ilishavurugika baada ya kumuomba mume tusimamie wote ili asiwe na wivu na wateja (stori ndefu haihusiki na mada).

Kwahiyo sina uwezo wa kumgharamia mdogo wangu kwa asilimia mia ila nikipataga 20, 30 nampa ajisogeze. Na mdogo wangu najua ananijali sana, kuna vitu ananifanyiaga huwa nahisi kama nina binti wa kike kabisa.

Yaani kiufupi sipo tayari ndoa yangu iingie doa kwasababu ya mimi kumtetea mdogo wangu na sipo tayari kugombana na mdogo wangu kwasababu yoyote, sijui kama nimeeleweka hapa?

3. Nifanyeje ili mume wangu awe na amani, mdogo wangu pia awe na amani na asijue kwamba shemeji yake huwa analalamika? Kwasababu kila ambacho mume huwa analalama mimi huwa natafuta namna ya kumuelekeza mdogo wangu kama vile mimi ndiyo nataka iwe hivyo, namwelekeza ili asije akafanya tena mume asione tunamdharau.

Na kibaya ni kwamba kuna siku mdogo wangu alisikia nikilalamika sana kwamba hii hali ya yeye mume wangu kukosa amani inaninyima raha, nataka anisaidie mawazo nifanyeje ili awe na furaha na nimuelewe ili niwe namrekebisha mdogo wangu na mimi niwe na amani, hakunijibu! Kesho yake mdogo wangu alikosa raha na sikutaka tena kuibua hiyo mada.

Kiukweli ndoa yetu haina miaka mingi lakini naumia, nilitamani sana mume wangu amlee mdogo wangu kama ambavyo mimi ningelea wa kwake. Lakini inanipa wakati mgumu sana kwamba isije ukatokea mtafaruku kati yao. Nitakae kuwa kwenye wakati mgumu ni mimi.

Uadui huwa hauishi ikiwa mmoja akijua mwengine anamchukia. Na kuna muda huwa namwambia mume, natamani hata na wewe aje ndugu yako hapa akae nikuoneshe jinsi inavyokua kuishi na familia, kuna vitu unavichukulia kama ni mwanao kafanya. Na mume kwangu ana upendo, anajitahidi sana kwakweli, kama kuna makosa ni madogo ya kiubinadamu, ndiyo maana nafukia mengine yoote.

Ninachotamani ni ushauri tu wa kumfanya mume wangu amuone mdogo wangu kama mdogo wake. Niwe na amani pia.

Naombeni ushauri.
mumeo ana chuki binafsi kwa mdogo wako hawezi kufikia hatua ya kufuatilia hadi mashuka ya kulalia. Siku ukipata muda wa kukaa nae akiwa na furaha mwambie kama kiutani kuwa nimeota unatembea na mdogo wangu ili ajue kuna kitu unahisi kwake. Pia, wala usimrudishe dogo kaa na mumeo mweleze ukweli kama hataki ukae na mdogo wako akwambie badala ya kuleta visa nyumbani.
 
Pole sana mkuu. Bila shaka mdogo wako kashamaliza chuo.
 
Huyo mumeo nimpe hongera japo hii ni chai yaani mtu atoke chuo alipwe hivyo pia hongera umechangamsha genge
 
Wanawake Huwa mnakosea sana KULETA ndugu zenu Kwenye familia, huendq hata hukumashirikisha mumeo ujio wa mdogo wako, au kama ulimshirikisha basi hakuridhia Kwa moyo mweupe mdogo wako kuishi hapo. NDUGU wanachangia sana kuharibu familia, ndoa ikiwa changa inahitaji utulivu na mnapaswa kukaa peke yenu kabla ya KUANZA KULETA ndugu , Kuna muda mkiwa peke yenu mnaenjoy sana hata sebuleni MNAWEZA kunyanduana , bafuni nk ila wakishaanzn kujazana ndugu , watoto, housegirl ni privacy inaanza kupotea unakuta inakuwa ngumu hata kumhug mkeo mbele za watu ukitoka kazini na pia mapenzi mnaanza kuviziana hadi watoto walale au ndugu watoke sebuleni wengine ni wabishi unakuta wanakaa sebuleni hadi saa Saba USIKU kisa tamthilia !
Ushauri
Mume wako hana tatizo , tatizo ni wewe uliyeletq ndugu Yako hapo, na Kwa maelezo Yako unatamani ndugu zako wangehamia hata hapo kwako, mke ataacha wazazi wake na ataambatana na Mume wake na sio ndugu zake! Elewa mume wako anataka Nini na Nini hataki ,
 
Back
Top Bottom