Mume wangu hapendi ndugu zangu

Mume wangu hapendi ndugu zangu

Kuna uzi fulani mwamba anacomplain mdogo wa mke wake anadharau sana,anamjibu anavotaka na anamuambia ni bora wagawane mali na dadaake waachane,ni kama dada huwa anamsimulia mapungufu ya mwamba kwa mdogo wake..pia mwamba alikuwa hashirikishwi ujio wa baba mkwe,anashtukia tu anapewa taarifa baba mkwe anakuja maana alikwisha tumiwa na nauli kbs

Nakonekti doti tu jameni[emoji16][emoji16][emoji16]
Mkuu kwaiyo huyu ni mke wa yule mwamba amejibu mapigo
 
Kuna uzi fulani mwamba anacomplain mdogo wa mke wake anadharau sana,anamjibu anavotaka na anamuambia ni bora wagawane mali na dadaake waachane,ni kama dada huwa anamsimulia mapungufu ya mwamba kwa mdogo wake..pia mwamba alikuwa hashirikishwi ujio wa baba mkwe,anashtukia tu anapewa taarifa baba mkwe anakuja maana alikwisha tumiwa na nauli kbs

Nakonekti doti tu jameni[emoji16][emoji16][emoji16]
Huyo wa shemeji kumjibu mume wala haihusiki kwanza mume wangu hata jamii forum account hana. Angekua ana jeuri ningeshamcharaza mwenyewe na anamuogopa mume wangu kweli.

Na kwa bahati nzuri mdogo wangu hadi leo anaamini mimi ndo mkorofi nna mcontrol kuliko shemeji yake😃 nimeona bora nibebe mimi ubaya. Ye anaaamini shemeji yake ni mkimya hana shida. Na mimi naendeleza imani hiyo so hiyo story yako hapa wala haiingii
 
Dada, fanya hata vibiashara ili uondokane na hii low self esteem.
Yaan kumbe unahofia ukija fukuzwa,hakuna atakaye kupokea kwenu kwa kuwa hukuishi nao? Huoni kama huo ni wajibu wao kukupokea kwa kuwa ni ndugu yao wa damu..lakini mumeo siyo ndugu yao.
So chagua ndoa ama ndugu zako.
Mimi huwa na support mahitaji ya nyumbani, vitu vingi tunavyotumia na mume wangu nimetoka navyo kwenye hustle zangu kabla ya ndoa so sijaja hapa kizembe mkuu, kuanzia mali hadi usafiri na hilo wala sijawahi kulitaja wala sihesabii so ukisema niko hapa kitegemezi sio kweli. Siwezi kuelezea career yangu na sitaki kujionesha kwa mume kwamba nnataka kutake over majukumu ya familia I tried that once tuligombana sana, ukinunua gesi anaona unatamba, ukienda kujifanyia shopping anaona unamdharau sijui kama unaelewa. So saizi nafanya biashara zangu online sio kwamba niko apeche alolo ila uwezo niliokua nao sio wa mimi kuja kumtambia mume.


Na kwa kusema hivyo watu watasema kwanini nisimpangie dogo hostel, hivi mnajua gharama za mtoto kukaa hostel kuanzia malazi, chakula na huduma zingine.? Saizi napambana kujiwekea akiba ya mipango yangu ya baadae. Na kingine kumtoa huyu mtoto ni kumpeleka home tu maana hizo cost ni sawa na yeye kutoka kwetu kwenda chuo
 
Thubutu kumfukuza ndugu yako kwa kuwa mwanaume ni baba yako hatokuja kuku cheat wala kukuacha. Hao wanaokushauri ni wapumbavu eti mfukuze dogo. Wa kwao wamewafukuza? Miroho mibaya tu.

Ndo nyie mkiumwa mnaenda kusumbua marafiki wawachangie hamna hata wa kukusogezea kopo la kutemea mate. Na ukute mume kaenda kuoa mke wa pili au mke kaenda kufanya yake hukooo we umebaki huna hata kumsumbua.

Dada mtoa mada nilichoona unataka ushauri jinsi ya kumfanya mume aelewe kuishi na watu ila watu wameacha kushauri wana attack.

Usifukuze ndugu. Huyo mume aache roho mbaya siku atakufanyia kibaya hutoamini
 
Wa kusalimia akija hamalizi masaa mawili wala matatu wanarudi nyumbani. Atawafurahia yaani hata ndugu zangu wanampenda sana tena sana na nimewaruhusu wanione mimi mkali kuliko yeye ili wampende zaidi. Sasa akiendelea hivi watakuja kujua ukweli na staki mume wangu aonekane mbaya sijui nifanyeje
pamoja na yote dada yangu inaonekana unalazimisha Sana hio ndoa lakn utabaki kuwa ukweli tu huyo mwanaume ni WA ajabu huwezi kusema mtu anakupenda alafu hampendi ndugu Yako wa damu hapo una mume Bali unaishi jitu la hovyo hakupendi na ndio maana haogopi kumchukia ndugu Yako Huku akikuonyesha. mkatae haraka
 
Ifike mahala tuache tabia ya kuishi na ndugu, ww umeoa au umeolewa hakuna sababu ya kuishi na ndugu kama hakuna ulazima, hicho ndo chanzo cha matatizo mengi.
 
Shida ni kwamba huyo mdogo wako hana faida naye halafu na wewe pengine unamjibu hovyo mme wako na hamkujadiliana wakati wa kumleta
 
Habari wakuu, nahitaji ushauri,

Mimi ni binti nimeolewa naishi na familia, mume wangu pamoja na mdogo wangu wa kike. Tatizo ni kwamba mume wangu amekuwa na kisirani sana juu ya huyu mdogo wangu wa kike. Kila anachofanya lazima mwanaume alalamike.

Na wala sijawahi kuwa na mawazo labda anamtaka, ndiyo maana anafanya hivi visirani vyote. Mazingira niliyomlea mdogo wangu namjua na ana tabia njema sana.

Mume wangu pia siwezi kumuhukumu kwa uhuni, hajanipa sababu ya kufanya hivyo. Kwahiyo kinachonichanganya ni kwanini ananipa wakati mgumu wa kumfanya mdogo wangu aishi kama yuko kwa mtu baki wakati mimi ni dada yake wa kuzaliwa naye kabisa?

Kila kitu ni lazima aseme kana kwamba huyu mtoto anamkwaza. Kinachoniuma mimi ni kwamba kila siku namuuliza hivi kama angekuwa anaishi hapa ndugu yako halafu mimi namfanyia hivi
Ungejiskiaje? Si ningeonekana mimi ndiyo mbaya sipendi ndugu wa mume?

Na kinachonishangaza, kuna kijana tunaishi naye hapa siyo ndugu wa damu wa mume wangu lakini anatusaidia kazi za hapa nyumbani, ametokea kijijini kwao. Sasa huyu hata akosee vipi mume wangu ukimwambia huyu kakosea hiki na hiki wala hutomuona akijigusa kwenda kumfokea wala kumsema.

Sana sana atajibaraguza tu ili uone ame 'react' na hii siyo mara ya kwanza. Chochote kinachomuhusu mtu wa kwao hutomuona mume wangu amekasirika, lakini ikiwa ni swala la kuhusu ndugu yangu atafoka haswa.

Inafika hatua anamnyima hadi vitu vya kutumia ndani ambavyo hata yeye anavitumia. Hiyo siyo shida, naumia kwasababu mimi huyu mtoto namchukulia kama mwanangu wa kumzaa, nimelichukua hilo jukumu kwa mama yangu tangu mdogo na kwa sasa mama haishi Dar na hatujawa na mahusiano mazuri sana na baba yetu kwa sababu ya mambo ambayo amekuwa akifanya kwetu sisi kama familia.

Kwahiyo najitahidi sana mdogo wangu asijihisi mpweke wala asione kuna pengo la kuumizwa kimalezi na baba yetu.

Na kuna siku ilikuwa sikukuu, nilimwambia mume ndugu zangu wanakuja kwasababu wazazi wetu hawaishi hapa Dar naomba sisi hapa tuwafanyie kitu kama kuwaalika wale hata chakula cha kawaida tu, akasema yeye hana hela.

Wala sikukasirika, nikajikokota nikanunua vyakula nikapika nioneshe kama mume wangu ndiyo amewaalika na wao waone wana kaka hapa mjini. Mume wangu wala hakuonesha ule ushirikiano ambao mimi huwa nautoa wakija ndugu zake, maana huwa napika haswa hadi kwenye kuni.

Nahangaika, napanga, naandaa, nikijua ndugu wa mume wangu wanakuja ila siku wamekuja wadogo zangu sikupata ushirikiano huo. Nilisema acha tu nivumilie kwasababu namheshimisha mume wangu mwenyewe.

Mara nyingine aliniliza na nikamwambia mimi huwa silii lakini unanitenda kama vile sisi kwetu ni masikini, yaani wadogo zangu walipita kutusalimia wakawa sebuleni akaniita chumbani akaniambia nataka kuja kukaa sebleni, naomba nikute siti ya kukaa. Kanakwamba wadogo zangu wamejaa pale maana walikuja kusalimia.

Kinachoniuma ni kwamba, sisi katika kukua kwetu hatujawahi kulelewa na ndugu, kama wadogo zangu wanakaa nje ya kwa baba na mama basi kwangu ndiyo pa kwanza, kwahiyo nikiona wanatendewa hivi naona kama ni mimi ndiyo napitia, sitamani wajione watu baki.

Na kuna muda huwa nawaza, ningekuwa na uwezo ningejenga nyumba yangu niwaweke wadogo zangu hadi watakapokuja kuolewa. Atakae tawanyika sawa, ila kwakuwa mzazi wetu ana uwezo ataona nampokonya wanae. Ila natamani sana wadogo zangu waishi maisha niliyotamani kuishi.


Ushauri unaohitajika;

1. Ni kosa mimi kumtetea mdogo wangu? Kwasababu ninapo jaribu kuuliza kwani tatizo lipo wapi hadi ufoke juu ya jambo dogo hivi, naonekana mkorofi au nataka kumpanda mume kichwani?!

2. Kiubinadamu, huyu mdogo wangu amekosea kuja kuishi kwangu? Nimemlea na hana tabia mbovu kwahiyo namjua, na kila siku namwambia mdogo wangu ikitokea leo dada yako nimedondoka, watoto wangu hutowaacha naamini.

Nampenda sana huyu mtoto, Mungu pekee ndiyo anajua. Kuna muda namwambia mume wangu basi nisamehe mimi naomba vumilia kidogo huyu mtoto akipata kazi ataondoka.

Kwasababu siyo kwamba kwetu tuna shida ya kifedha na wala mume wangu hamgharamii chochote zaidi ya chakula ninachokula mimi ndiyo anachokula huyu mtoto. Ni anakaa kwangu kwasababu ni karibu na chuoni anaposoma yeye.

Kwa upande wa nauli na gharama za kujikimu anatoa mzazi na mimi nikipata huwa nampa kidogo, nashindwa hata kusema namuhudumia maana biashara niliyokuwanayo ilishavurugika baada ya kumuomba mume tusimamie wote ili asiwe na wivu na wateja (stori ndefu haihusiki na mada).

Kwahiyo sina uwezo wa kumgharamia mdogo wangu kwa asilimia mia ila nikipataga 20, 30 nampa ajisogeze. Na mdogo wangu najua ananijali sana, kuna vitu ananifanyiaga huwa nahisi kama nina binti wa kike kabisa.

Yaani kiufupi sipo tayari ndoa yangu iingie doa kwasababu ya mimi kumtetea mdogo wangu na sipo tayari kugombana na mdogo wangu kwasababu yoyote, sijui kama nimeeleweka hapa?

3. Nifanyeje ili mume wangu awe na amani, mdogo wangu pia awe na amani na asijue kwamba shemeji yake huwa analalamika? Kwasababu kila ambacho mume huwa analalama mimi huwa natafuta namna ya kumuelekeza mdogo wangu kama vile mimi ndiyo nataka iwe hivyo, namwelekeza ili asije akafanya tena mume asione tunamdharau.

Na kibaya ni kwamba kuna siku mdogo wangu alisikia nikilalamika sana kwamba hii hali ya yeye mume wangu kukosa amani inaninyima raha, nataka anisaidie mawazo nifanyeje ili awe na furaha na nimuelewe ili niwe namrekebisha mdogo wangu na mimi niwe na amani, hakunijibu! Kesho yake mdogo wangu alikosa raha na sikutaka tena kuibua hiyo mada.

Kiukweli ndoa yetu haina miaka mingi lakini naumia, nilitamani sana mume wangu amlee mdogo wangu kama ambavyo mimi ningelea wa kwake. Lakini inanipa wakati mgumu sana kwamba isije ukatokea mtafaruku kati yao. Nitakae kuwa kwenye wakati mgumu ni mimi.

Uadui huwa hauishi ikiwa mmoja akijua mwengine anamchukia. Na kuna muda huwa namwambia mume, natamani hata na wewe aje ndugu yako hapa akae nikuoneshe jinsi inavyokua kuishi na familia, kuna vitu unavichukulia kama ni mwanao kafanya. Na mume kwangu ana upendo, anajitahidi sana kwakweli, kama kuna makosa ni madogo ya kiubinadamu, ndiyo maana nafukia mengine yoote.

Ninachotamani ni ushauri tu wa kumfanya mume wangu amuone mdogo wangu kama mdogo wake. Niwe na amani pia.

Naombeni ushauri.
Ndo umeona uje kunielezea huku mtandaoni????
Huu ni ushahidi [emoji35][emoji35][emoji35]

Sasa ikifika tarehe 1 mwezi wa 12 sitaki kumwona huyu mdogo wako vinginevyo ntawafukuza wote.

Na unajua kabisa kuwa huwa sitaki ujinga wa kutangazwa kwenye mitandao.
 
dada anajiamini eti mume wake hawez omba Tunda[emoji23][emoji23].

mimi mwenyew hapa nilishawahi omba tunda la mama mdogo wa wife, mbna ishue ni simple kama ni mzuri basi unaomba.

ila tunda nilinyimwa na nkapewa onyo, baada ya hapo nilimchukia na sitaki kumuona kwangu,

wife akiuuliza kwanini namchukia mama ake mdogo?
huwa sina majibu zaidi ya kufoka tu[emoji23]
Hahah

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
 
mimi was reverse. mama mdogo alianza kuniapproach nilipomgiga chini alinichukia. wife akanijia juu kuwa namchukia mama yake mdogo. baada ya miaka zaidi ya mitano ndipo nikamwambia siwezi kuoa mtu na mama yake.....alichoka, hajarudia kuniuliza tena
Hukutakiwa kusema hii Mzee,hizi tunakufa nazo

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
 
Pole sana kwa changamoto za maisha mama, kwa jinsi ninavyoona hapo uyo mumeo kwa vyovyote inawezekana kwa asilimia kubwa kamtongoza mdogo wako ndio mana kamuwekea gumu fulani hivi, afu kingiine yawezekana aujazaa nae mumeo bado hamjapata mtoto bado ndio mana itakuwa inampa shida aje ndugu yako badala ya kumpatia mtoto ili na yeye apate raha ya kuwa na mtoto, ayo ni mawazo yangu suala la kisirani sidhani mama ila Kaa kwa kutulia ukweli utaujua tu.
 
Mdogo wangu ana akili sana huwa tunakaa tunapiga sana story na tuna viakili flani vinafanana. Ni mtu ambae ukimuuliza swali straight forward anajua unataka kumaanisha nini. Na hata mimi ndo nilivyo. Ukija ukiniuliza swali flani, ntajua unataka information gani au unanishutumu. Naona bora nisali tu Mungu ali sort
Unavypmuamini sana mdogo ako lol. Tunza akiba ya imani kidogo

Sent from my SM-N960F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom