Mungu ndiye shetani(?)

Mungu ndiye shetani(?)

Mtu akiteseka wanasema ni mapenzi ya Mungu, Ina maana ana uhusiano na shetani. Mimi ninaona Mungu na shetani ni vitu viwili vinavyofanya kazi pamoja. Ni sawa na mwanga na Giza. Wakati wa mchana mimea inatumia jua kutengeneza ule ukijani wake na usiku mimea inatoa hewa kwa binadamu.
Kuna watu niliwahi kuwambia Mungu na Shetani ni marafiki sana. Wakaniona kama nakufuru.

Sisi ndio tunawagombanisha ila wao wanaelewana vizuri.

Rejea tukioa la Ayoub. Pia wakati Babeli inaenda kuvamia Wayahudi ktk kitabu cha Yeremia Mungu akasema nilimtumia Mtumishi wangu Nebukadineza awatie mikononi mwake........

Inawezekana vipi Shetani apigane vita Mbinguni dhidi ya Mungu?

Na bado akafanikiwa kushawishi 1/3 ya malaika zake?

Inawezekana vipi Shetani aliye na nguvu kiasi hiki aletwe duniani kupamna na sisi viumbe dhaifu tulioumbwa na udongo na utegemee ushindi??

Why Mungu asingemalizana na shetani kabisa? Sasa mlolongo wa matukio ukaanza mara namtuma Yesu aje kuwakomboa, mara chinjeni kafara toeni sadaka ziwasafishe dhambi.....huu mzunguko wa nini wakati anatakiwa kufyekelea mbali shetani?
Duniani tunakadiriwa kuwa 7bn. Watakaoenda mbinguni hawafiki 1mIlioni.

Iweje 6bn inapotea hivi hivi sababu ya shetani mmoja?
 
Nikisoma historia ya ukoloni baran Africa,
Hasa role ya wamisionari na waarabu ktk kutuletea huu ukoloni.

Nakosa kabisa imanj na hizi dini zilizokuja na meli Islamic& Christianity [emoji22]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mtu akiteseka wanasema ni mapenzi ya Mungu, Ina maana ana uhusiano na shetani. Mimi ninaona Mungu na shetani ni vitu viwili vinavyofanya kazi pamoja. Ni sawa na mwanga na Giza. Wakati wa mchana mimea inatumia jua kutengeneza ule ukijani wake na usiku mimea inatoa hewa kwa binadamu.
Hata ukifa kwa kupigwa risasi,
Watasema Ni mapenzi ya mungu[emoji22]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Palikuwa na darweshi mmoja wa tarika ya uzururaji (kalanda) aliyetembea jangwani Kwa muda wa siku kadhaa, akiwa mwenye njaa na kiu nusura ya kufa alifika Hadi katika mji mmoja na kuanza kuparamia vyakula na maji...wenyeji walipomwona walimkamata na kumpiga sana Kwa sababu ilikuwa ni kipindi cha ramadhani...alipopata ahueni yule darweshi alisema kuwa kwa wakati ule chakula na maji vilikuwa ndio ibada kubwa kwake ila waliompiga walifanya hivyo Kwa sababu maana ya kufunga haikujulikana kwao...

Inawezekana na sisi, fumbo la "Mungu na Shetani" hatulijui au hatutaki kulijua...
 
Ukisoma kwa umakini biblia Mwanzo mpaka ufunuo utaelewa kuwa kitabu kimebadilisha wahusika, Sehtani ameitwa Mungu na Mungu ameitwa shetani.

Mungu wa kwenye biblia anaelezewa kuwa Mungu mwenye wivu anayechukia kuona unamsifu au kumfuata mungu mwingine, Anataka wewe tokea unaamka hadi unalala uwe unamuwaza yeye tu na kufanya kila kitu anachotaka yeye...wakati biblia haijaonesha kama Shetani ana wivu au anataka watu wafuate itikadi zake lasivyo atakasirika.

Kutokana na huu wivu, Mungu wa kwenye biblia ukihesabu ameua wanaume takribani millioni na ushee.....2, 345, 439 (Hapa hatujahesabu wanawake na watoto)
Ukiconsider na source za nje ya biblia idadi inafika mpaka 22, 743, 746

Watu alioua mungu ni wengi, kama wale vijana 42 aliowaua kwasababu walimtania Elisha kuwa ana upaa...
Watu 147, 000 aliowaua kwasababu walitaka demokrasia maana walichoka kupelekeshwa na Mussa
Nk. Nk.

Lakini Shetani wa kwenye biblia ameua watu 10 tu, tena hao 10 aliwaua kwasababu alishinikizwa na Mungu...Mungu alimbinya vidole shetani awaue wale watoto wa Ayubu.

Na muda huo huo, Mungu anasema atakuja siku ya mwisho kuchukua watu wake wachache tu na Kuwachoma kwa moto mkali wengine wote ambao hawakumsikiliza mchana na usiku.

Nani ni shetani apo? Na nani ni Mungu?
Una matatizo gani kwanza
 
Alivyooandika umemuelewa? Biblia haisomwi km gazeti na waliojaribu kusoma km gazeti walishindwa kujua maana yake.
Alichoandika ni kama masimulizi ambayo hayana ukweli 100% ndani yake.
Biblia inakutaka unapoielezea uoneshe vifungu kwa mfano ni Mwanzo sura ya 1, mstari wa 4 inasema hivi ndiyo maana imeandikwa kwa lugha nyingi ili watu waeielewe.
Ukweli usiojificha angekuwa ameisema hivyo quran, kuna masheh wangekuwa wanamsomea Albadili sasa hivi, angefahamika ilikuwa ni kuuliwa au kuhukumiwa kifo kwenye mahakama ya kadhi.
Mfano hai
Iran, mwanamke wa dini ya kiislam hakufunika kichwa aliuliwa
Kuna shekh hapo naijeria amehukumiwa kifo. Uzi wake humu JF
Kuna sheh mwingine Uarabuni alihukumiwa kifo
Kuna mwanamke hapo jirani alimbusu mwanaume hadharani alihukumiwa kifo ila kwa kuona watu wa haki za binadamu wataingilia kati wakabadili hukumu na kufungwa jela miezi 6
Siyo kama wakristo wanatetea dhambi
1. Mungu wao ni mwenye nguvu na anaweza kujitetea ndiyo anayetoa hukumu.
2. Usihukumu usije ukahukumiwa. Ambaye hana dhambi awe wa kwanza kumtupia mawe huyu mtoa uzi? Utaenda mbingu ya nani ukimuua mwenzako
Zilongwa mbali,, zitendwa mbali, hapa hatuko kujadili Iran, Quran, wala kadhi. Mleta uzi ni mgala mwenzenu na amesoma biblia na kukiona hicho alichokiona, suala la kusema biblia aisomwi kama gazeti usiniambie mimi bali mwambie huyo mgala mwenzio kwa kuwa yeye ndio alieleta uzi,, shida yangu mimi kwako ni kuingiza Quran, iran, kadhi, sijui albadir kwenye uzi ambao hata hivyo vitu havihusika, na ukitaka kujadili hayo fungulia uzi wako kama alivyofanya mleta uzi,, ila kwa leo jadiliana na mgala mwenzio juu ya kile alichokiona kwenye biblia.
 
Hata ukifa kwa kupigwa risasi,
Watasema Ni mapenzi ya mungu[emoji22]

Sent using Jamii Forums mobile app
Elimu yako na uelewa wako juu yako ya Mungu uko limited na sio wewe ni tatizo la watu wengi, mwanadamu kupitia adamu alimkataa Mungu na mfumo wake wa maisha ndo maana wewe na wenzako mnatukana Mungu na hawafanyi chochote sababu Mungu hawez shindana na binadamu ambaye atakufa
 
Zilongwa mbali,, zitendwa mbali, hapa hatuko kujadili Iran, Quran, wala kadhi. Mleta uzi ni mgala mwenzenu na amesoma biblia na kukiona hicho alichokiona, suala la kusema biblia aisomwi kama gazeti usiniambie mimi bali mwambie huyo mgala mwenzio kwa kuwa yeye ndio alieleta uzi,, shida yangu mimi kwako ni kuingiza Quran, iran, kadhi, sijui albadir kwenye uzi ambao hata hivyo vitu havihusika, na ukitaka kujadili hayo fungulia uzi wako kama alivyofanya mleta uzi,, ila kwa leo jadiliana na mgala mwenzio juu ya kile alichokiona kwenye biblia.
Huwez mpangia mtu acomment kama unavyotaka wewe na je kama mleta uzi ni muislamu
 
Yesu akajibu, akamwambia, Mtu akinipenda, atalishika neno langu; na Baba yangu atampenda; nasi tutakuja kwake, na kufanya makao kwake. Yohana 14:23

Maisha yetu yana shughuli nyingi na vizuizi vingi.Ni rahisi sana kushikika katika shughuli, wasiwasi na majukumu hadi tukasahau kile kilicho cha muhimu zaidi.

Kuna hadithi fupi ya kupendeza mwishoni mwa Luka 2 wakati Maria na Yusufu walimpeleka Yesu Yerusalemu kwa pasaka akiwa umri wa miaka 12. Baada ya sherehe walianza safari kurudi nyumbani wakidhani kwamba yuko nao.

Nami najiuliza, ni mara ngapi tunadhani Mungu yuko nasi ilhali tumeenenda katika shughuli zetu wenyewe.

Sasa jambo la kushangaza ni hili; Maria na Yusufu walikuwa wamesafiri siku nzima kutambua kuwa Yesu hakuwa nao na iliwachukua siku tatu kumpata. Siku tatu! Sasa ujumbe hapa ni huu; ni rahisi sana kwetu kuupoteza uwepo spesheli wa Mungu kuliko kuupata tena tunapoupoteza.

Inafaa tuwe waangalifu kusalia katika uwepo wa Mungu. Tunapofanya hivyo, Mungu hupata maskani mioyoni mwetu.

Hii huanza kwa kuwa watiifu kwa neno la Mungu. Njia moja ya kuonyesha ukomavu wa kiroho ni kuachana na tabia ambazo hazimpendezi Mungu, hii huonyesha kwamba unayajali yale anayofikiria.

Hii inamaanisha unakuwa mkarimu kwa watu, unajifundisha kusamehe, unaachana na migogoro na unaishi kwa amani. Tunapojifunza kuwa makini na maneno yaetu, kumshukuru Mungu na kuwainua wengine, tutazidi kuwa katika uwepo wa Mungu siku nzima.

Ombi La Kuanza Siku
Baba, asante kwa kufanya moyo wangu makao yako. Ninahitaji uwepo wako leo. Nisaidie nikuheshimu kwa mawazo na maneno yangu, na kuwa wa Baraka kwa wale walio karibu nami.
 
Alivyooandika umemuelewa? Biblia haisomwi km gazeti na waliojaribu kusoma km gazeti walishindwa kujua maana yake.
Alichoandika ni kama masimulizi ambayo hayana ukweli 100% ndani yake.
Biblia inakutaka unapoielezea uoneshe vifungu kwa mfano ni Mwanzo sura ya 1, mstari wa 4 inasema hivi ndiyo maana imeandikwa kwa lugha nyingi ili watu waeielewe.
Ukweli usiojificha angekuwa ameisema hivyo quran, kuna masheh wangekuwa wanamsomea Albadili sasa hivi, angefahamika ilikuwa ni kuuliwa au kuhukumiwa kifo kwenye mahakama ya kadhi.
Mfano hai
Iran, mwanamke wa dini ya kiislam hakufunika kichwa aliuliwa
Kuna shekh hapo naijeria amehukumiwa kifo. Uzi wake humu JF
Kuna sheh mwingine Uarabuni alihukumiwa kifo
Kuna mwanamke hapo jirani alimbusu mwanaume hadharani alihukumiwa kifo ila kwa kuona watu wa haki za binadamu wataingilia kati wakabadili hukumu na kufungwa jela miezi 6
Siyo kama wakristo wanatetea dhambi
1. Mungu wao ni mwenye nguvu na anaweza kujitetea ndiyo anayetoa hukumu.
2. Usihukumu usije ukahukumiwa. Ambaye hana dhambi awe wa kwanza kumtupia mawe huyu mtoa uzi? Utaenda mbingu ya nani ukimuua mwenzako
Badala ujibu hoja za mleta mada unahangaika hangaika tu..
Unasema Biblia haisomwi kama gazeti halafu wewe ulichoandika ni EMPTY SET.
 
Huwez mpangia mtu acomment kama unavyotaka wewe na je kama mleta uzi ni muislamu
Hata kama awe muislam au mkiristo kwa kuwa ameleta hoja kwa vifungu vya mistari ya kitabu kitakatifu ajibiwe kwa hoja za vifungu pia..
Porojo za sijui huwezi mpangia mtu accoment nini inaonyesha kichwa kimebebe uzito gani wa kichwa.
 
Wafia dini kawaida hawajui kujibu hoja, ni huwa wanakuja na tu vitisho twao walivyokaririshwa kutoka kwenye vitabu vya wakoloni....
 
Ukisoma kwa umakini biblia Mwanzo mpaka ufunuo utaelewa kuwa kitabu kimebadilisha wahusika, Sehtani ameitwa Mungu na Mungu ameitwa shetani.

Mungu wa kwenye biblia anaelezewa kuwa Mungu mwenye wivu anayechukia kuona unamsifu au kumfuata mungu mwingine, Anataka wewe tokea unaamka hadi unalala uwe unamuwaza yeye tu na kufanya kila kitu anachotaka yeye, wakati biblia haijaonesha kama Shetani ana wivu au anataka watu wafuate itikadi zake lasivyo atakasirika.

Kutokana na huu wivu, Mungu wa kwenye biblia ukihesabu ameua wanaume takribani millioni na ushee; 2, 345, 439 (Hapa hatujahesabu wanawake na watoto). Ukiconsider na source za nje ya biblia idadi inafika mpaka 22, 743, 746.

Watu alioua mungu ni wengi, kama wale vijana 42 aliowaua kwasababu walimtania Elisha kuwa ana upaa... Watu 147, 000 aliowaua kwasababu walitaka demokrasia maana walichoka kupelekeshwa na Mussa n.k.

Lakini Shetani wa kwenye biblia ameua watu 10 tu, tena hao 10 aliwaua kwasababu alishinikizwa na Mungu, Mungu alimbinya vidole shetani awaue wale watoto wa Ayubu.

Na muda huo huo, Mungu anasema atakuja siku ya mwisho kuchukua watu wake wachache tu na Kuwachoma kwa moto mkali wengine wote ambao hawakumsikiliza mchana na usiku.

Nani ni shetani apo? Na nani ni Mungu?
Umekufuru.Adhabu yako ni kufanya toba/tubu.
 
Back
Top Bottom