Muonekano mpya wa Chidi Benz baada ya kutumia unga

Akiongea kwa uchungu kwenye kipindi cha Da Weekend Chat Show cha Clouds TV jana, Chidi ambaye mwili wake umepungua kwa kiasi kikubwa, amesema bado uwezo kimuziki anao lakini wale aliowaita wadau walioushikilia muziki wamemtupa.

Amesema wakati wa kilele chake, alikuwa akifanya show kila siku katika wiki, lakini kwa sasa mambo yamebadilika kabisa.


“Matatizo yangu na stress zangu ambazo niko nazo zinanisababishia mwili wangu unapungua kwasababu siko okay, siko poa, siko sawa yaani,” alisema.

Katika hatua nyingine Chidi alisema pamoja na afya yake kuzorota, hivi karibuni alipiga show kwa masaa mawili hadi mama yake akalia.

“Mama yangu akaniambia mwanangu unafanya show two hours, show kali watu wanapenda unachokifanya lakini sioni mwamko wa watu kutokea kukusaidia, kwahiyo tufanye mpango watu wakusaidie’ na mimi namuambia nataka watu wanisaidie, natamani kusaidiwa, natamani kupata mafanikio anayopata Diamond,” alisisitiza.

 

Msaada ni muhimu sana.
 
nilishangaa jana eti anaomba msamaha kwa kula unga... km ray c bla
the
 
Hana discipline acha dunia imfunze, pesa inahitaji adabu huwez jua dhahiri airport kuna mitambo kushika drugs then we wapita nayo, hiyo ni dharau, I wonder ile kesi aliachiwa vp vurugu wewe, madawa wewe, mademu wewe ,
 
kwasasa chidi benz hamkuti dogo janja kwa afya,asaidiwe na nani badala ya kujisaidia mwenyewe kwanza kuacha upuuzi.
niliwahi kuwa mvutaji mzuri wa sigara,nikapata kansa ya mapafu nikatibiwa nikapona.daktari siku ananiaga alisisitiza kunywa pombe moshi achana nao.mpaka leo niko poa kwani kweli sijagusa.
Nilikua namkubali sana chid kwa rap zake kwakweli angeendelea angefika mbali sana.nafkiri Nay kidogo anafuatia lakini kwa Chid yuleeee Nay bado sana.
 
Dah! Siku za Dar es salaam stand up haziwezi kurudi tena, huwa kuna nafasi moja Tu huwa inatokea, Chid yule anafanya show moja ya Kilimanjaro award then T.I Kama msanii mkubwa toka Marekani anaalikwa kwenye utoaji tuzo ule, wakati unafanya show ya nguvu kwa ngoma zako kali Naitwa nani! Babe ft Ray C, T.I ananukuliwa akiwauliza wenyeji wake alokaa nao.... "Huyu Ni nani?"...anaambiwa huyo Ni mwana Hip Hop anayekimbiza bongo, Na baadaye unashinda tuzo, T.I mwenyewe anakupatia tuzo, Na uhakika uliambiwa jinsi T.I alivyouliza kuhusu wewe, Leo kina Diamond wakipata nafasi Kama hizo wanazitumia hapo hapo, Ni vipi ungefanya ngoma Na T.I wakati ule, bila shaka ungekua mbali, all in all madawa yamekupoteza, sidhani Kama utapata msaada kwenye muziki wako tena, Sana Sana makosa yako wacha yatumike Kama funzo kwa vijana wengine, Na wenyewe wasipojifunza kwako! Wacha yawakute Tu, hatuna namna....sorry Chid Benz, fulsa huwa Ni Mara moja Tu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…