Kuna mdau fulani anahusika sana na magari aliniambia kama unataka gari ya kununua hapa bongo bora ununue kwa wahindi au waarabu wa kkoo. Wale jamaa wanatunza sana magari yao halafu pia hayapati dhoruba sana kama haya mengine. Utakuta gari inazunguka hapohapo kkoo au posta na upanga.
Na pia hao jamaa wanauza gari nzuri sana kwa bei chee kwasababu wanataka kuleta nyingine mpya zaidi.
na pia naomba kujua mkuu, hivi ni kwel wale wafunga miziki kwenye magari vile vifaa ni aghali sana au nao ni wezi tu.
wapi wanafunga mziki kwa bei reasonable kwenye gari.
Kaka uzi mzuri sana huu, big up kwako umetoa mambo ya msingi na itasaidia watu wengi sana.
Kuna kuangali kama gari inadaiwa na TRA AMA LA kwa kuandika ujumbe mfupi ukiandika namba ya gari mfano T 200 ASS kwenda namba 153 41 watajibu sms yako na makadirio ya madai ama muda ambao hayo malipo yanaisha
Sina uhakika zaidi ila kama unapenda mziki mnene kwenye gari yako gharama ipo very reasonable:
inategemea unataka nini na nini kwenye muziki wa gari yako. kuna vifaa gharama na vingine bei ya kawaida. mafundi mara nyingi ukija kichwakichwa unapigwa! shop around ujue bei za mafundi tofauti. nipe bajeti yako nimuulize fundi wangu,yuko vizuri sana.
******
akupe bei zake mkuu utuwekee hapa kwa faida ya wengi
ukipata gari kwa muhindi ni bingo! gari inatumika posta tu na ni kweli wengi wanauza kwa sababu haina kazi na si njaa au kibiashara.
***********
mhhhh sio wote mkuu, kuna mmoja mhindi alikuwa k/koo alitaka kuniuzia GAIYA, mhhh imechoka bt anapiga parefu.
cha msingi pata gari iloshushwa bandarini haijatumika bongo, yan ww ndo uiwekee plate number...daaah unaenjoy gari unakuta kila kitu kinashine,,,dashbord inang'aaa...ndani pasafiiiiii.
mhhh raha sana unapoikabidhiwa unaanza kuelekea nyumbani unaona hufiki, ukifika napo hukai unasema ngoja nielekee tegeta niitest.
******all in all huu uzi safi sanaaaa****
*********
wapi mkuu ambapo wanaweka mziki kwa reasonable price, maana am planing kuuza hii nilonayo nipate kitu kipya, masuala ya kukaa na gari hadi ikuzeekee mikononi hilo halipo siku hizi,
tumia mwaka then enjoy kitu kingine
tupo pamoja kaka.....ila namba ya gari yako imenivunja mbavu! T200 ASS
Nimeipenda sana hiyo ya kutobebe hela cash. Madalali wengi hwan si na ri wana record mabaya. Wengi ni majambazi na utaona wanavyokusukumia gari kwa nguvu ili ununue.
Nimecheka mpaka jino la X-massimagine mwenye gari yuko goba huko anakwambia mkamalize biashara kwake!
Mi breki ya kwanza ilikuwa Bagamoyo. Mafuta niliweka Full Tank. Nimefika Bagamoyo,napata bia huku funguo za gari nazichezea mezani. Kurudi nikajaza tena Full Tank ndo nikapaki.ha ha ha ha tabia ya first time owner hii........
very useful....naomba ruhusa kuchukua mstari kwenye hii post.