Jodoki Kalimilo
JF-Expert Member
- Feb 12, 2012
- 12,559
- 11,180
Kama amesema atamfukuza Ngasa as an individual hapo sawa naweza kuhoji mamlaka ameyatoa wapi otherwise kama amesema kwa niaba ya taasisi yupo rightHujamuelewa Muro wewe!! Amesema atamfukuza Ngasa!.. yaani yeye kama yeye wala hajatumwa kutoa tamko hilo
Deni sio laki 5, Ngasa alikopa pesa bank, mwajiri wake ambaye ni Yanga akamdhamini kwa makubaliano ya mshahara wa Ngasa upite bank kwa makato ya laki tano kila mwezi (ambayo wewe ndio umesema anadaiwa laki tano) ama kwa makusudi ama vipi, mwajiri ambae ni Yanga hakupeleka mshahara wa Ngasa bank kwa muda wa mwaka mmoja. Bank wakaiandikia Yanga ambae ni mwajiri na mdhamini wa Ngasa na kuchukua hatua ya kuingiza mshahara wa Ngasa bank na makato yakawa makubwa kwa kuwa mwaka mzima deni halikulipwa. Ngasa akatangaza mgogoro na Yanga (migogoro yetu watz si unaijua ile ya kusema chini chini wakati ukweli wewe ndio tatizo)unadhani ni busara kuita waandishi wa habari kuzungumzia makato ya deni la laki tano mlilokubaliana kwenye vikao vyenu vya ndani? busara zenu ndio zimeishia hapo?
Rage akukosea kuwaita mbu3
Hivi kati ya Ngasa na Muro nani yuko juu ya mwenzake? AU Muro ndiyo mwajiri wa Ngasa?Jana nimemsikia ktk Sports Leo ya Radio One, nikashangaa jinsi anavyoongelea suala la Ngassa, anaongea kwa mamlaka makubwa kana kwamba ana uwezo na mamlaka juu ya Ngasa.
Mbumbumbu hawezi kumpiga mtu bao 5 bila, lazima Yanga watakuwa mambumbumbu waandamizi daraja la I.
Kama magoli 5 ni miaka nenda rudi je bao 2 bila nazo ni nenda rudi? Kweli mbumbumbu mwandamizi Daraja la I mko fiti.Ujerumani imeipiga brazil 7_0,man u ilipigwa 6 na mancity,arsenal ilipigwa 8 na man..nk nk hao wote hawazungumzii hivo vipigo coz wanajua point ni 3 tu walizopata...ww mbumbu ndo unazungumzia goli 5 miaka nenda rudi alafu unasahau kwamba upo nafasi ya9..pole
Mwenye jukumu ni Yanga kama mdhamini lakini bado haikuondolei kinga kwa kuwa upo na hujafa, wala hujatoroka na unafahamika utawajibika na bank watamfuata mdhamini ambae ni Yanga na mwisho wa siku itaonekana kuna mtu amefanya uzembe atawajibishwa lakini mwisho wa siku wanarudi kwako yaani Ngasa, unless ulikuwa hulipwi mshahara vinginevyo itaonekana ni deal kati ya mchezaji na afisa wa Yanga. Na ndio maana Yanga waliamua kupeleka mshahara wake bank na makato yakaongezeka, ila kama angeingia mitini yanga wangewajibika kwa kuwa walikuwa hawapeleki mshahara wake. Sema tu kwa kuwa ni vijana na wachezaji wa mpira wanapewa heshima maalumu kama hiyo ya kukaa na kuamua kama walivyofanya Yanga, lakini ungekuwa ni Masuke au mie Jodoki ambao hatujaonyesha mchango kwa Taifa kila mwananchi atutambue, lazima methodology ya kudai deni ingebadilika ikiwa sambamba na kukamata mali zetu na wala miezi miwili isingekatika bila kutusumbua yaani mwezi wa kwanza tu mshahara umekata jamaa haoMwenye jukumu la kupeleka hizo hela benki ni nani? Je ni Ngasa au ni Yanga?
Anaongea kama mwenyekiti wa klabu, anaongea kama katibu mkuu wa klabu, anaongea kama kocha wa klabu na mbaya zaidi anaongea kama wale mashabiki wasiofuatilia soka ila ni mahili kupiga domo.jerry muro anaharibu zaidi cv yake yanga..yanga nayo inaharibiwa kwa kuonekana kama inaongozwa na afisa habari anayefoka bila sababu hata kwa hoja za kawaida kabisa. Ukweli yanga na jerry wote wamepatikana na wote wanaharibiana CV kwa kasi ya ajabu