Musiba mpaka Sasa hajaomba msamaha, Membe Shikilia hapohapo

Musiba mpaka Sasa hajaomba msamaha, Membe Shikilia hapohapo

Lakini pia vitabu vya dini vina sema
"Samehe Saba mara sabini" Yesu Kristu alitufundisha kusamehe hata kama umeumizwa kiasi gani mara ngapi.

Nahisi Musiba aliwatuma viongozi hawa wa kidini wakamuombee msamaha lakini huenda vigezo na masharti havikuzingatiwa, huenda akivizingatia atasamehewa.
Nchi inaongozwa kwa sheria, siyo kwa biblia wala msahafu.

Biblia inasema samehe hata saba mara sabini lakini usiubebe mstari huo pekee, soma biblia nzima.

Biblia pia inasema hakuna msamaha bila toba ya kweli. Biblia tena inasema ukienda hekaluni, ukataka kutoa sadaka, halafu ukakambuka ulimtendea visivyo ndugu yako, iacha sadaka yako madhabuhuni, nenda kwanza ukamwombe msamaha ndugu yako kisha uende ukatoe sadaka yako.

Pia ikumbukwe kuwa adhabu kuna wakati huwa ni sehemu ya msamaha. Ndiyo maana mtume Paulo anasema kuwa ukitaka kuonya, onya hata kwa ukali. Ukali unaotajwa hapo ni adhabu, alimradi iwe ninkwa dhamira ya kumrudi aliyepotoka na kutenda uovu.

Viongozi wa dini, wanatakiwa watambue kuwa nyumba za ibada siyo sehemu ya kuhifadhia uovu bali ni sehemu ya upatanisho baada ya kufanya toba ya kweli kwa uliyemkosea , na kwa Mungu wako.
 
Sioni kama umeielewa mantiki ya kile nilichokiandika, kwako naiona mihemko tu ya Musiba asulubiwe!.
Mwovu ni halali yake kulipia uovu wake. Tusilete mambo ya kienyeji. Kama kuombewa msamaha ndiyo kigezo cha kusamehewa basi tuwaambie wafungwa wote waende kwa Pengo na Malasusa kuwaomba wawaombee msamaha kwa Rais ili magereza yote yafungwe.

Tusijifanye tunajua sana dini, adhabu zimekuwepo wakati wote na Duniani kote. Italy kuna magereza. Mkatoliki ukienda na yaliyo kinyume na imani kwa kadiri ya mwongozo wa Kanisa, unafungiwa. Kufungiwa ni adhabu.
 
Ila Kuna watu wanamuombea msamaha. Sijui amewaambia wafanye hivyo? Sijui wanajipendekeza? Mimi hata sijui.
 
Akili yangu inanambia inawezekana musiba ana mali nyingi nyinginezo ambazo kaandika kwa majina tofauti ya umiliki, maana ni kama wamemtingisha but hajatetereka sana pengine kuna kitu kipo nyuma ngoja tuone
Alikuwa akilipwa pesa nyingi kwa uchafu aliokuwa akiufanya. Pesa aluzokuwa akipewa zilimwondoa kwenye ubinadamu mpaka kufikia hatua ya kuhamasisha watu wauawe.

Shetani alipofanya uasi alitupwa ziwa la moto.
 
hata akiomba msamaha kamwe Membe usikubali!
Shikilia hapohapo Mkuu Membe, huyu kenge alikuchafua sana!
 
Sasa kuna ubaya gani dini kuhusika kama inawahusu wote? kwanini mshangazwe?!
Cha kushangaza zaidi ni viongozi hao kupiga kelele sasa lakini kukaa kimya wakati Musiba anahamasisha watu wengine wauawe. Kwa kweli huo ni unafiki mkubwa.

Sauti za viongozi hawa zungekuwa na nguvu sana hata sasa kama wangekuwa wakati wote wamesimama katika kuuchukia uovu na kuukemea uovu wakati wote.

Wasome maandiko waone manabii wa Mungu daima walivyosimama kuutetea na kuunena ukweli wakati wote, hata mbele ya wafalme wenye nguvu waliotisha kwa mamlaka na ukatili wao.

Wewe huwezi kukaa kimya wakati watu wanauawa, wanatekwa, wanapotezwa, halafu leo unyanyue mdomo wakati mtu anapoadhibiwa kwa kufuata utaratibu wa kisheria, utegemee kauli yako itatiliwa umuhimu.
 
Membe kamwe usisikilize wahuni komaa.naye huyo bwege afilisike kabisa akitoka hapo akajitose ziwani afe.
 
Lakini pia vitabu vya dini vina sema
"Samehe Saba mara sabini" Yesu Kristu alitufundisha kusamehe hata kama umeumizwa kiasi gani mara ngapi.

Nahisi Musiba aliwatuma viongozi hawa wa kidini wakamuombee msamaha lakini huenda vigezo na masharti havikuzingatiwa, huenda akivizingatia atasamehewa.
Kwahiyo hata tutende madhambi kiasi gani tutaenda paradise maana tutasamehewa 7 mara 70!!! Msisome vitabu bila kuwa na uelewa mtajivuruga hovyo.
 
Hiyo namna yakuonyesha anajutia kosa lake itaonekana vip?..alitakiwa aende kwanza mwenyewe akaombe msamaha alafu akikataliwa ndio atume watu wakaongezee nguvu ombi lake.sasa yeye ata kwenda hajaenda alafu anatuma watu.Hivi badae akiibuka alafu akakana kua hakuwatuma hao wazee wamejituma wenyewe itakuaje?.Dini imehusika ndio kwasababu ametumia viongozi wa dini ili kulegeza moyo wa membe wakati kesi inahusu mambo binafsi.Ata angetumia wanaccm wenzake tafsiri ni ile ile.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
Mashambulizi anayopelekewa Musiba kwa sasa ndio hayo hayo yaliyokuwa yakifanywa gizani dhidi ya JPM; kwa kuwa huyu hana kinga ya kushitakiwa ndio maana waliamua kuweka hadharaani kumdhalilisha kuhalalisha tuhuma dhidi yake.

Musiba Cyprian hakufanya kosa lolote zaidi ya wengine wasiosemwa walifanya uovu gani ansulubiwa kwa sababu alikuwa akiimuunga mkono JPM wazi wazi ambapo hawakupenda

@MusibaCyprian Nenda Ngomeni haraka sana kwa Kuhani Mwacha masahibu yote yanayokukabili hutajutia ushauri huu kamwe maishani mwako.
 
Yaani ikitokea Membe amesamehe ghafla tu, nitamuona mtu wa ajabu sana!
Labda nyuma ya pazia yawezekana kuna mchezo unachezwa na hawa tissss!!

....
Na kwakwel mamba ni mtu wa hovyo "kwerikweri" ...usije shangaa anatuhadaa tu hapa kumbe hana mpango wowote wa kum-wajibisha musiba
 
Mashambulizi anayopelekewa Musiba kwa sasa ndio hayo hayo yaliyokuwa yakifanywa gizani dhidi ya JPM; kwa kuwa huyu hana kinga ya kushitakiwa ndio maana waliamua kuweka hadharaani kumdhalilisha kuhalalisha tuhuma dhidi yake.

Musiba Cyprian hakufanya kosa lolote zaidi ya wengine wasiosemwa walifanya uovu gani ansulubiwa kwa sababu alikuwa akiimuunga mkono JPM wazi wazi ambapo hawakupenda

@MusibaCyprian Nenda Ngomeni haraka sana kwa Kuhani Mwacha masahibu yote yanayokukabili hutajutia ushauri huu kamwe maishani mwako.
We nawe ni mpumbavu kumbe...yan badala ya kuwajibikia makosa yake mnataka akaombewe ? Ujinga mtu na hata huyu mungu wenu mnamnasibisha na hiz akil zenu za kipumbavu..et kuhani mwacha!! What a nonsense is this??
 
Kwa mara nyingine tena, Dhalimu baada ya kutenda udhalimu wake badala ya kuukabili uovu wake na kutake responsibility yeye anakimbilia kwa maaskofu ili wamsaidie kubeba udhalimu wake.

Iko hivi, Hakuna anayepaswa kubeba uovu wa Mwingine. Hata Kanisani mtu anapoungama, hakuna anayeungama kwa niaba ya mtu mwingine.

Leo hii Musiba pengine kwa kiburi au Jeuri anashindwa hata kuitisha press conference na kumuomba radhi ndugu Membe na wengine wote aliowakwaza, ila anakimbilia kwa maaskofu ili eti wao ndo wambebee ujinga wake.

Nawashangaa hata maaskofu, badala ya kumwambia mkosaji atake responsibility ya makosa yake, wao wanataka Mkosaji ago away kirahisi rahisi tu.

Hebu tujiulize, kwa Nini Musiba kakimbilia kwa maaskofu na siyo wazee wengine wenye heshima, ni kwa sababu anataka KUTUMIA DINI kugo away na makosa yake. Ni gemu ileile ya bosi wake wa zamani kujifanya kuwa karibu na viongozi wa dini pindi akishaharibu ili kupata huruma ya jamii.

Kitu kingine cha kujiuliza, Askofu Mwamakula huwa anawaombea laana viongozi au watu wenye kutaka kuharibu haki nchini. Aliomba hivyo wakati wa uchaguzi mkuu, kuwa atakaye iba, vuruga uchaguzi mkuu apate mapigo, Ameomba hivyo kwa atakayekwamisha katiba mpya. Leo hii kwa nini anadhani kuwa Membe shuruti awe wa rehema kwa mtu aliyemuumiza kiasi kile?


Kwa upande wa Askofu Pengo. Huyu hakuwahi kukemea ujinga na udhalimu ambao Musiba alikuwa akiufanya wakati ule. Na hajawahi kumtaka Musiba aache ujinga wake. Leo hii ana moral authority gani ya kumtaka Membe asamehe?.

Iko hivi, Tusimlazimishe Membe kusamehe au kutosamehe. Kusamehe ni haki yake na wala siyo wajibu wake.

Na mimi namshauri Membe kuwa, Mali alizopata Musiba, part ya mali hizo ni Mapesa aliyokuwa analipwa ili kuwachafua. Kwa hiyo ni jambo jema kabisa kuchukua mali hizo kama fidia.

Na hii ni muhimu kwa sababu itasaidia kutoa somo kwa watu wengine, mosi waache kutegemea binadamu aliyetoka kwa mavumbi na badala yake wamtegemee Mungu. Na pili Ubaya una consequences, Utavuna ulichopanda.

Niwakumbushe tu akina baba Askofu Pengo, kuwa huwa mnatufundisha kuwa TUTII MAMLAKA. Sasa ni wakati Muafaka wa Wao kwenda na kumwambia Musiba atii mamlaka ambayo ni Mahakama. ALIPE!
Anaanzia wapi hapa?!!
 

Attachments

  • Untitled.jpg
    Untitled.jpg
    16.4 KB · Views: 2
Kama hataki kuomba msamaha mbona mnamlazimisha!
 
Kuna makabila kuomba msamaha ni ishara yq udhaifu.
Mambo yao waachieni wenyewe .
 
Musiba anataka acheze gemu ili ionekane kuwa hajaomba msamaha na kwamba aliyoyasema dhidi ya Membe ni Kweli!.

Musiba hajutii makosa yake ila ana hofu tu ya mali yake kutwaliwa!
 
Mwovu ni halali yake kulipia uovu wake. Tusilete mambo ya kienyeji. Kama kuombewa msamaha ndiyo kigezo cha kusamehewa basi tuwaambie wafungwa wote waende kwa Pengo na Malasusa kuwaomba wawaombee msamaha kwa Rais ili magereza yote yafungwe.

Tusijifanye tunajua sana dini, adhabu zimekuwepo wakati wote na Duniani kote. Italy kuna magereza. Mkatoliki ukienda na yaliyo kinyume na imani kwa kadiri ya mwongozo wa Kanisa, unafungiwa. Kufungiwa ni adhabu.
Habari ya kujifanya sijui uliitoa wapi, concept yangu ilikuwa simple sana, siku zote msamaha hauna masharti, msamaha ni msamaha tu, kitendo chochote cha kukataa msamaha kwa kuutungia sababu ni chukizo mbele za Mungu.

Kitendo cha kuwakatalia wale viongozi wa dini kilikuwa ni kujikweza, na kujikweza hakutakiwi kwa maisha yetu, iko mistari mingi kwenye biblia inayokataza hicho kitu.
 
Cha kushangaza zaidi ni viongozi hao kupiga kelele sasa lakini kukaa kimya wakati Musiba anahamasisha watu wengine wauawe. Kwa kweli huo ni unafiki mkubwa.

Sauti za viongozi hawa zungekuwa na nguvu sana hata sasa kama wangekuwa wakati wote wamesimama katika kuuchukia uovu na kuukemea uovu wakati wote.

Wasome maandiko waone manabii wa Mungu daima walivyosimama kuutetea na kuunena ukweli wakati wote, hata mbele ya wafalme wenye nguvu waliotisha kwa mamlaka na ukatili wao.

Wewe huwezi kukaa kimya wakati watu wanauawa, wanatekwa, wanapotezwa, halafu leo unyanyue mdomo wakati mtu anapoadhibiwa kwa kufuata utaratibu wa kisheria, utegemee kauli yako itatiliwa umuhimu.
Visasi.
 
Back
Top Bottom