Muswada wa Mabadiliko ya Sheria ya Idara ya Usalama wa Taifa unaoifanya iwe chini ya Usimamizi wa Rais watua Bungeni

Muswada wa Mabadiliko ya Sheria ya Idara ya Usalama wa Taifa unaoifanya iwe chini ya Usimamizi wa Rais watua Bungeni

Mabadiliko ni muhimu,ingawa yanahitaji elites na maoni ya wadau mbalimbali kwenye nyanja za ulinzi na usalama kabla ya kuwafikia waheshimiwa wabunge.
Ni vizuri kuchakata na kupitia neno kwa neno,kifungu kwa kifungu ili kama kuna mapendekezo au mabadiliko yeyote yawe kama mbadala wakati wa mijadala ya kibunge.
 
Haya ni maandalizi ya uchaguzi ujao, jamaa hawataki kutoka madarakani kwa kura. Kumbuka ni idara hii iliyoratibu wizi wa kura katika chaguzi ziliozopita. Mbowe maridhiano yako na Samia ni kiinimacho
Sio kwamba maridhiano ni takwa la kisaisa na hayagusi Sheria ya uanzishaji wa Idara husika?
Au mnasemaje wadau....!!?
 
Mama Samia haeleweki mara baridi mara Moto. Kwa hivyo maafisa usalama wakiua mtu kwenye utekelezaji wao wa majukumu sio kosa.
 
TISS wanaomba ruhusa kuwatesa zaidi watu wanaowakamata. TISS pia wanaomba wasishtakiwe kwa makosa yoyote wanayofanya.

On the surface, it would seem to be very frightening. Lakini mimi nadhani inafaa TISS wapewe kila wanachohitaji kuilinda nchi.

Kuna sheria katika kila kitu,na hizi Security Services duniani kote zinafanya kazi according to certain fixed rules.
Mimi nashauri TISS wapewe wanachotaka. Kushauri ni serious business. Kwa sababu mambo yakiharibika watu wanauliza,"Ni nani aliyetushauri kufanya hivi?"

Imeandikwa katika Biblia_And ye shall be guiltless before the Lord and before Israel"Numbers chapter 32 verse 22. Kwamba usifanye makosa mbele ya Mungu,na usifanye makosa mbele ya Taifa lako.
 
We Una uhakika wanaotaka haya ni TISS?

Unaamini TISS walikaa Kwa umoja wao wakaona wanahitaji sheria hii?

Binafsi naamini wanaotaka haya ni wanasiasa...TISS wanapokea maagizo kutoka Kwa wanasiasa na wao wameona sasa Bora iwepo sheria ...just in case huyo mwanasiasa ikitokea hayupo wasiulizwe maswali
 
Eti eeeh , haya bhana.. uzuri malipo ni hapa hapa...
unafikiri shida ipo kwangu

Shida ipo kwa wanaotunga hayo masheria mabovu lakini hata nikipinga haisaidii bali nitajiumiza tu roho yangu bora niache hivyo hivyo

Mambo yaende yatakavyotaka kwenda potelea pote
 
TISS wanatuhumiwa kuwaua Ben Saanane, Azory Gwanda; Pamoja na kumpiga risasi Tundu Lissu.
Ikiwa ni kweli, basi hawapaswi kupewa kinga yoyote ya kutoshitakiwa.
Hakuna binadamu yeyote duniani mwenyewe mamlaka ya kuua binadamu mwenzake.
 
TISS wanatuhumiwa kuwaua Ben Saanane, Azory Gwanda; Pamoja na kumpiga risasi Tundu Lissu.
Ikiwa ni kweli, basi hawapaswi kupewa kinga yoyote ya kutoshitakiwa.
Hakuna binadamu yeyote duniani mwenyewe mamlaka ya kuua binadamu mwenzake.
Ben Saanane na Tundu Lissu waulizwe Chadema Azory Gwanda waulizwe uamsho na magazeti ya Kenya. Kubenea na Kibanda waulizwe vifo Muhimbili wakati CHADEMA wakihamasisha madaktari wagome
 
Kupitia Bunge la 12 linaloendelea Jijini Dodoma, Serikali imepeleka Bungeni Muswada unaopendeleza Mabadiliko ya Sheria ya Idara ya Usalama wa Taifa.

Pamoja na Mambo mengine, Sheria inapendekezwa kufanyiwa marekebisho katika kifungu cha 13 ili kuweka utaratibu wa kuapishwa kwa Mkurugenzi Mkuu, Naibu Wakurugenzi Wakuu, Wakurugenzi na Maafisa wa Idara.

Inapendekezwa kifungu cha 16 kifanyiwe marekebisho ili kuzuia ufichuaji wa utambulisho wa watu wanaofanya kazi katika Idara au watu wengine wanaoshirikiana na Idara na kumpa Mkurugenzi Mkuu mamlaka ya udhibiti wa watu hao. Lengo la marekebisho ni kuwalinda maafisa na watu hao kutokana na utendaii wao wa kazi za kiusalama.

Kifungu cha 19 kinapendekezwa kurekebishwa ili kuongeza kinga ya makosa ya jinai kwa Maafisa wa Idara tofauti na ilivyo sasa ambapo kinga imetolewa katika mashauri ya madai pekee dhidi ya Maafisa hao.

Lengo la marekebisho ni kuweka kinga dhidi ya makosa yanayoweza kutendeka wakati wa utekelezaji wa majukumu yao kwa uaminifu.

Vifungu vya 16(3), 17(3), 20(2) na 23 vinapendekezwa kurekebishwa ili kuongeza viwango vya adhabu kwa makosa mbalimbali kutegemeana na uzito wa kosa. Lengo la marekebisho hayo ni kuhakikisha viwango hivyo vya adhabu vinaendana na mazingira ya sasa.

Muswada unapendekezwa kuongeza vifungu vipya vya 24, 25 na 26 vitakavyoweka masharti mbalimbali ikiwemo, udhibiti wa Maafisa kutoa taarifa pindi wanapostaafu au kumaliza vipindi vya ajira, kuzuia uingiaji katika maeneo ya Idara bila idhini na masharti kuhusu vitendo vya uvunjifu wa Sheria nje ya mipaka ya Nchi.

Inapendekezwa Jedwali lifanyiwe marekebisho kwa kuongeza kiapo cha Utii pamoja na kurekebisha kiapo cha utumishi na kiapo cha kutunza siri kwa lengo la kumarisha ulinzi wa taarifa na ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ya Idara.

Pia soma: Katavi: Tundu Lissu apinga Muswada wa Sheria ya Usalama wa Taifa kuwasilishwa bungeni, adai utaleta Ukiritimba

==========

ZAIDI (Kutoka kwenye nyaraka)

Muswada huu unapendekeza kufanya marekebisho katika Sheria ya Idara ya Usalama wa Taifa, Sura ya 406. Lengo la marekebisho yanayopendekezwa ni kubadili masharti ya Sheria kuendana na mfumo wa utawala uliopo na taratibu za usimamizi wa Idara za Usalama kimataifa na kuweka masharti mbalimbali ya utekelezaji bora wa majukumu ya Idara.

Marekebisho yanakusudia kuboresha Sheria na kutatua changamoto mbalimbali zilizojitokeza wakati wa utekelezaji wake.

Muswada umegawanyika katika Sehemu Mbili. Sehemu ya Kwanza inahusu masharti ya awali ambayo yanajumuisha jina la Muswada na masharti kuhusu namna ambavyo vifungu mbalimbali vya Sheria
vimefanyiwa marekebisho.

Sehemu ya Pili ya Muswada inapendekeza marekebisho katika vifungu mbalimbali vya Sheria. Sheria inapendekeza kurekebishwa kwa ujumla kwa kubadili masharti yote kuhusu usimamizi wa Idara kutoka kwa Waziri mwenye dhamana na masuala ya Usalama wa Taifa na kuweka jukumu hilo kwa Rais.

Lengo la mapendekezo hayo ni kukidhi muundo uliopo sasa ambapo Idara ya Usalama wa Taifa inawajibika moja kwa moja kwa Rais pasipo kupitia kwa Waziri mwenye dhamana na masuala ya Usalama wa Taifa. Mapendekezo haya yamezingatia pia mfumo wa utendaji kazi wa idara za usalama duniani.

Kufuatia mabadiliko ya jumla yanayoweka usimamizi wa Idara chini ya Rais, inapendekezwa vifungu vya 11, 15, 18, 19(3) virekebishwe ili kuondoa mamlaka ya usimamizi wa Waziri wa Mambo ya Nje, Katibu Mkuu Kiongozi na Mwanasheria Mkuu wa Serikali katika masuala mbalimbali yanayohusu usimamizi wa intelijensia na usalama.

Inapendekezwa kifungu cha 4 cha Sheria kifanyiwe marekebisho kwa kuipa Idara hadhi ya Chombo cha Ulinzi na Usalama na kuiweka chini ya usimamizi wa Rais. Lengo la marekebisho hayo ni kutambua jukumu ambalo Idara imekuwa ikitekeleza kama mojawapo ya Vyombo vya Ulinzi na Usalama Nchini.

Inapendekezwa sheria ifanyiwe marekebisho katika kifungu cha 5 kwa lengo la kuipa Idara majukumu ya msingi na muhimu ya usalama inayoyatekeleza kwa sasa. Majukumu hayo ni pamoja na ulinzi binafsi wa Viongozi wa Ngazi za Juu wa Kitaifa na Kimataifa, ulinzi wa Vituo Muhimu, mamlaka ya upekuzi wa kiusalama wa Viongozi na udhibiti wa matishio ya kiusalama dhidi ya Jamhuri ya Muungano.

Kifungu kipya cha 5A kinapendekezwa kuongezwa ili kujumuisha wajibu wa Waziri katika Sheria. Lengo la marekebisho haya ni kuwezesha masuala ya kisera ya Idara yanayotekelezwa na Waziri.

Inapendekeza kifungu cha 6 cha Sheria kifanyiwe marekebisho ili kuweka sifa za uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu na kuweka masharti kuhusu nafasi hiyo baada ya utumishi. Lengo ni kupata mtendaji mwenye uwezo, sifa na weledi na kulinda maslahi ya kiusalama kwa watu ambao wamewahi kutumikia nafasi ya Mkurugenzi Mkuu.

Ili kuboresha utendaji kazi wa Idara, inapendekezwa kuongeza vifungu 6A na 6B katika Sheria ili kuweka masharti kuhusu nafasi za Naibu Wakurugenzi Wakuu kwa Tanzania Bara na Zanzibar pamoja na nafasi ya Wakurugenzi wengine katika Idara watakaoteuliwa na Rais. Pia inapendekezwa kuweka masharti kuhusu sifa za uteuzi katika nafasi hizo tajwa.

Ili kuboresha utendaji kazi wa Idara, inapendekezwa kifungu cha 7 cha Sheria kirekebishwe kwa kuweka masharti kuhusu vigezo vya ajira kwa Watumishi wa Idara. Vilevile, kifungu kinaweka sharti la matumizi ya silaha wakati wa utekelezaji wa majukumu yao kwa lengo la kutambua matumizi ya silaha na kuweka utaratibu wa nidhamu ya umiliki na matumizi ya silaha hizo.

Inapendekezwa Kifungu cha 10 cha Sheria kifanyiwe marekebisho ili kumtambua Mkurugenzi Mkuu kama Mshauri Mkuu wa Rais na Serikali katika masuala ya usalama wa Taifa. Lengo ni kutambua wajibu wa Idara katika usimamizi na udhibiti wa Usalama wa Taifa. Vilevile, kwa kuwa Mkurugenzi Mkuu ndiye Mtendaji Mkuu wa Idara, Sheria inarekebishwa kwa kumpa Mkurugenzi Mkuu mamlaka ya nidhamu kwa watumishi walio chini yake.

Kifungu cha 10A kinapendekezwa kuongezwa ili kuweka masharti yatakayo muwezesha Katibu Mkuu Kiongozi kuratibu na kuwa kiungo baina ya Rais na Idara katika utekelezaji wa masuala ya kisera na utumishi wa umma.

Sheria inapendekezwa kufanyiwa marekebisho katika kifungu cha 13 ili kuweka utaratibu wa kuapishwa kwa Mkurugenzi Mkuu, Naibu Wakurugenzi Wakuu, Wakurugenzi na Maafisa wa Idara.

Inapendekezwa kifungu cha 16 kifanyiwe marekebisho ili kuzuia ufichuaji wa utambulisho wa watu wanaofanya kazi katika Idara au watu wengine wanaoshirikiana na Idara na kumpa Mkurugenzi Mkuu mamlaka ya udhibiti wa watu hao. Lengo la marekebisho ni kuwalinda maafisa na watu hao kutokana na utendaji wao wa kazi za kiusalama.

Kifungu cha 19 kinapendekezwa kurekebishwa ili kuongeza kinga ya makosa ya jinai kwa Maafisa wa Idara tofauti na ilivyo sasa ambapo kinga imetolewa katika mashauri ya madai pekee dhidi ya Maafisa hao.

Lengo la marekebisho ni kuweka kinga dhidi ya makosa yanayoweza kutendeka wakati wa utekelezaji wa majukumu yao kwa uaminifu.

Vifungu vya 16(3), 17(3), 20(2) na 23 vinapendekezwa kurekebishwa ili kuongeza viwango vya adhabu kwa makosa mbalimbali kutegemeana na uzito wa kosa. Lengo la marekebisho hayo ni kuhakikisha viwango hivyo vya adhabu vinaendana na mazingira ya sasa. Muswada unapendekezwa kuongeza vifungu vipya vya 24, 25 na 26 vitakavyoweka masharti mbalimbali ikiwemo, udhibiti wa Maafisa kutoa taarifa pindi wanapostaafu au kumaliza vipindi vya ajira, kuzuia uingiaji katika maeneo ya Idara bila idhini na masharti kuhusu vitendo vya uvunjifu wa Sheria nje ya mipaka ya Nchi.

Inapendekezwa Jedwali lifanyiwe marekebisho kwa kuongeza kiapo cha Utii pamoja na kurekebisha kiapo cha utumishi na kiapo cha kutunza siri kwa lengo la kuimarisha ulinzi wa taarifa na ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ya Idara.
Madhara ya marekebisho ya sheria ya usalama wa taif kufanyika mwaka 2023 yameanza kuonekana bayana mwaka 2024 mtu kuruhusiwa kuvaa matendo ya kinyama dhidi ya binadamu pasipo kuhojiwa na kufanywa chochote (immunity)
 
Back
Top Bottom