Muuaji wa Kilifi Paul Mackenzie, ni vigumu kumtia hatiani vinginevyo dini zote zifutwa

Muuaji wa Kilifi Paul Mackenzie, ni vigumu kumtia hatiani vinginevyo dini zote zifutwa

Father of All

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2012
Posts
7,672
Reaction score
9,039
View attachment 2598986
_oD26GY58eQR92NDz5jdMvcPJaBJWKFlgse3jcT7TIXNxspUjECwbH7vaLGTVQjKMaQYfARsj99kvAdObUGnUc72MPYs6PBpKJtnzhY=s750


Japo nalaani mauaji ya kinyama yaliyofanyika huko Kilifi Kenya, nina wasiwasi kama sheria zetu za kiingereza zinaweza kumtia hatiani.

Zifuatazo ni sababu nuzuhu za kisheria:

Mosi, si rahisi kuthibitisha kuwa Mackenzie aliwashawishi wahanga kutokula. Na kama aliwashawishi, si kosa kumshawishi mtu kufanya kitu anachoamini binafsi kina tija. Dini zote zinaendeshwa kwa ushawishi. Ndiyo maana zimeruhusiwa kufanya uhuni wote bila kufungiwa, kuchunguzwa wala kushitakiwa. Wahusika waliamua kwa hiari yao wakiwa na akili timamu kufunga hadi kufa wakiamini walichoambiwa yaani pepo au kukutana na Bwana.

Pili, Hakuna namna waendesha mashtaka watathibitisha mashtaka yao bila wahanga kuwapo ili watoe ushahidi. Kama Mackenzie hakuwapa sumu au kuwaua kwa kuwanyonga au kwa namna nyingine zaidi ya kuwaaminisha, hana hatia hata kidogo. Rejea wanaoahidi kutenda miujiza ya kuondoa watu kwenye umaskini na kuishia kuwaibia na kuwafanya maskini na watumwa zaidi. Hata wahanga wakifufuliwa, hawawezi kuthibitisha kuwa walilazimishwa kufunga wakijua walichokuwa wakifanya na matokeo yake.

Tatu, sheria za kiingereza zinamtaka anayedai kuthibitisha madai yake. Si rahisi washitaki kuthibitisha kuwa Mackenzie aliwarubuni zaidi ya kuwahubiri nao kwa hiari yao , wakiwa watu wazima wakaamini na kutekeleza.

Nne hata akifunguliwa kwa makosa ya kuua watoto, hawampati kwa vile halikuwa jukumu lake kisheria kuangalia wale watoto zaidi ya wazazi wao. Rejea mnavyobatiza au kuingiza watoto wadogo kwenye dini zenu.

Mwisho, kwa vile dini zote zinatumia mfumo ule ule, kumpata Mackenzie na hatia, ima bunge litunge sheria mpya ambayo nayo itagonga mwamba kwa vile itakuwa illegal tokana kuwa retrospective au wafute dini kwanza ndipo mhusika ashikiwe.

Hata hivyo, itakuwa vigumu kumfunga vinginevyo wamuonee. Akipatikana na hatia si ya mauji bali uzembe au kuficha vifo na vitu kama hivyo ambavyo navyo kisheria, kama atapata wanasheria mahiri anaweza kushida.

Akifungwa, basi iwe ni kama kwenye kesi ya Mwamwindi baada ya kumuua Dk Kleruu.

Somo kubwa hapa ni kwamba tunaendeshwa na mifumo mibovu ya dhuluma
 
Kufungwa atafungwa . Japo itachukua muda
 
Huyo mchungaji atafungwa kwa sababu mbili.

1. Kuna waumini Kama kumi wamepona kwenye sakata hilo watatumika kutoa ushahidi.

2. Amewahi kuwa na kesi Kama hiyo huko nyuma ya mauaji ya watoto wawili wa waumini wake kwenye scenario Kama hiyo sema polisi waliwawahi na kumkamata na hiyo kesi bado ipo mahakamani.
 
Huyo mchungaji atafungwa kwa sababu mbili.

1. Kuna waumini Kama kumi wamepona kwenye sakata hilo watatumika kutoa ushahidi.

2. Amewahi kuwa na kesi Kama hiyo huko nyuma ya mauaji ya watoto wawili wa waumini wake kwenye scenario Kama hiyo sema polisi waliwawahi na kumkamata na hiyo kesi bado ipo mahakamani.
Shauri zao huko
 
Hyo ni kafara ya uganga kabisa kumbuka Mwamposa pale Moshi na akaachiwa leo anadunda😂😂😂...

Huyo kwa upande fulani ni mchawi tu hana jipya anatumia nguvu za giza hapo ana kesi kibao na ana ukwasi wa kutosha..
 
Amewatanguliza wenzake kwenda kukata viuno na kuimba milele huko mbinguni.
 
View attachment 2598986
_oD26GY58eQR92NDz5jdMvcPJaBJWKFlgse3jcT7TIXNxspUjECwbH7vaLGTVQjKMaQYfARsj99kvAdObUGnUc72MPYs6PBpKJtnzhY=s750


Japo nalaani mauaji ya kinyama yaliyofanyika huko Kilifi Kenya, nina wasiwasi kama sheria zetu za kiingereza zinaweza kumtia hatiani. Zifuatazo ni sababu nuzuhu za kisheria:
Mosi, si rahisi kuthibitisha kuwa Mackenzie aliwashawishi wahanga kutokula. Na kama aliwashawishi, si kosa kumshawishi mtu kufanya kitu anachoamini binafsi kina tija. Dini zote zinaendeshwa kwa ushawishi. Ndiyo maana zimeruhusiwa kufanya uhuni wote bila kufungiwa, kuchunguzwa wala kushitakiwa. Wahusika waliamua kwa hiari yao wakiwa na akili timamu kufunga hadi kufa wakiamini walichoambiwa yaani pepo au kukutana na Bwana.
Pili, Hakuna namna waendesha mashtaka watathibitisha mashtaka yao bila wahanga kuwapo ili watoe ushahidi. Kama Mackenzie hakuwapa sumu au kuwauwa kwa kuwanyonga au kwa namna nyingine zaidi ya kuwaaminisha, hana hatia hata kidogo. Rejea wanaoahidi kutenda miujiza ya kuondoa watu kwenye umaskini na kuishia kuwaibia na kuwafanya maskini na watumwa zaidi. Hata wahanga wakifufuliwa, hawawezi kuthibitisha kuwa walilazimishwa kufunga wakijua walichokuwa wakifanya na matokeo yake.
Tatu, sheria za kiingereza zinamtaka anayedai kuthibitisha madai yake. Si rahisi washitaki kuthibitisha kuwa Mackenzie aliwarubuni zaidi ya kuwahubiri nao kwa hiari yao , wakiwa watu wazima wakaamini na kutekeleza.
Nne hata akifunguliwa kwa makosa ya kuua watoto, hawampati kwa vile halikuwa jukumu lake kisheria kuangalia wale watoto zaidi ya wazazi wao. Rejea mnavyobatiza au kuingiza watoto wadogo kwenye dini zenu.
Mwisho, kwa vile dini zote zinatumia mfumo ule ule, kumpata Mackenzie na hatia, ima bunge litunge sheria mpya ambayo nayo itagonga mwamba kwa vile itakuwa illegal tokana kuwa retrospective au wafute dini kwanza ndipo mhusika ashikiwe. Hata hivyo, itakuwa vigumu kumfunga vinginevyo wamuonee. Akipatikana na hatia si ya mauji bali uzembe au kuficha vifo na vitu kama hivyo ambavyo navyo kisheria, kama atapata wanasheria mahiri anaweza kushida. Akifungwa, basi iwe ni kama kwenye kesi ya Mwamwindi baada ya kumuua Dk Kleruu.
Somo kubwa hapa ni kwamba tunaendeshwa na mifumo mibovu ya dhuluma
kisheria hana kosa , wewe na utimamu wako umeamua kufanya , hakukukaba ili ule , siungi mkono huyo mtu kufungww japo namlaumu kwa kuwateka kiakili hao marehemu
 
Hawezi kuchomoka.

Kuna lile kosa la wizi wa kuaminiwa na Hili ni Kuua kwa Kuaminiwa.
 
kisheria hana kosa , wewe na utimamu wako umeamua kufanya , hakukukaba ili ule , siungi mkono huyo mtu kufungww japo namlaumu kwa kuwateka kiakili hao marehemu
Kwahiyo uwazike watu waliokufa ambao sio ndugu zako bila kuwataarifu ndugu zao wala mamlaka za nchi.

Wewe una ushahidi gani kama walikufa kwa njaa ?
 
Ndio mana mimi nasema Waafrika tuna feli kwa kuendeshwa na Mihemko. Anaweza tokeza mtu huko akikimbia anasema fulani mchawi ukute wakati huo uchawi una kiki. Basi utashangaa watu wanaongozana nae wakikimbia na huenda wakaenda kumuua yule mtu aliyetajwa. Wakikutana nae.

Sijui hatuna au hatujazoea kufanya critical thinking. Yaani kufikiri kwa upembuzi kwenye kila neno au jambo ili kutoa uamuzi sahihi.
 
Kwahiyo uwazike watu waliokufa ambao sio ndugu zako bila kuwataarifu ndugu zao wala mamlaka za nchi.

Wewe una ushahidi gani kama walikufa kwa njaa ?
kwan walipokubali kufunga mpk kifo hawakutoa taarifa kwa ndugu zao ? kuwa wanajiandaa na umauti wa kiimani , huyo mchungaj tutamlaumu ila hana baya , uzezeta wako ndo umauti wako kama wale wa bikra 72


NB ; USHAHIDI SINA ILA KAMA ANAO USHAHIDI BASI HANA BAYA ILA KAMA NA YEYE NDO KAMA MIMI BASI AFUNGWE MPK KUNYONGWA
 
Ndio mana mimi nasema Waafrika tuna feli kwa kuendeshwa na Mihemko. Anaweza tokeza mtu huko akikimbia anasema fulani mchawi ukute wakati huo uchawi una kiki. Basi utashangaa watu wanaongozana nae wakikimbia na huenda wakaenda kumuua yule mtu aliyetajwa. Wakikutana nae.

Sijui hatuna au hatujazoea kufanya critical thinking. Yaani kufikiri kwa upembuzi kwenye kila neno au jambo ili kutoa uamuzi sahihi.
huo ndo ukwel mkuu , poor reason kwa waafrika
 
Back
Top Bottom