Kwa kweli ni upuuzi; as a matter of fact ni kana kwamba hawajui hesabu za seti! Hivi Mbunge mwanamke atakuwa anawakilisha wanawake tu kwenye hilo jimbo na Mwanaume atawakilisha wanaume watupu?
...Nakubaliana na hoja zako hapo juu, lakini siamini kuwa serikali tatu ndiyo jibu la hayo, hapana, Serikali tatu siyo jibu lakini ni hatua muhimu kuelekea kwenye jibu lenyewe, yaan Serikali Moja ya Jamhuri ya Tanganyika. Nadhani mtu yeyote makini anayetaka kugombea urais uchaguzi ujao atachagua kugombea Urais wa Tanganyika kuliko ule wa Tanzania, maana si muda mrefu baada ya uchaguzi huo Rais wa Tanzania hatakuwa na kazi, wait and see...
Ndio maana mimi nadhani Rais wa muungano asiwe mkuu wa serikali. Awe tu mkuu wa nchi tumuachie mambo ya muungano and other ceremonial amenities. Kwa muundo uliomo kwenye rasmu haiwezekani akafanya kazi ipasavyo bila mgongano na Rais wa Tanganyika. The best scenario (close to ideal) ni unakuwa na Rais wa Jamhuri na mawaziri wakuu wa Tanganyika na Zanzibar. Mawaziri wakuu wanakuwa wakuu wa serikali na Rais anakuwa mkuu wa nchi. Kwenye uchaguzi tunachagua vyama. Chama kinachopata wabunge wengi kinaunda serikali. Lakini najua hii model wazanzibari hawaitaki kwa sababu kimsingi hawa wenzetu hawataki muungano.
Hili la serikali tatu ni sawa kwa kuwa muda si muda tutakuwa na akina Yeltsin watakaowaacha akina Gorbachev bila nchi ya kutawala na hivyo Tanganyika kuwa nchi peke yake bila unyonyaji wa Zanzibar na Zinzibar kubakia peke yake bila unyonyaji wa Tanganyika. Juzi nimewasikia wakililia kiti chao UN basi tukimpata Yeltsin wetu nao watakuwa na kiti chao huko UN. Wacha zije lakini tatu hazitadumu.
maoni yangu ni kinyume kabisa na MWANAKIJIJI.. serikali ni jambo lisilokubalika kabisa mbele ya macho ya wazanzibari.
imagine!!! hizi serikali mbili mfumo ambao unawapa baadhi ya vitu vinavyowatambulisha kama taifa wanaukataa, je ukija mfumo wa serikali moja tu ambao utawapokonya hata hiki kidogo walichonacho itakuwaje?????? tafakari tafadhali.
naunga mkono hoja ya serikali mbili kama ilivyo sasa na kama sivyo labda serikali tatu kama yalivyo mapendekezo ya tume. huo ndio ushauri na maoni yangu
Sema hapana Serikali "Tatu", Sema ndiyo "Serikali moja". Nchi moja, Taifa Moja, Watu wamoja - nje ya hapo Hapana!!! Tumeshatengeneza ulaji na ukiritimba wa kutosha kwenye serikali mbili halafu tunataka kuongeza serikali ya tatu? Mizigo miwili midogo imetushinda (tunahangaika nayo) halafu magenius wetu wanataka kutupa mizigo mitatu mikubwa!? Kwanini tusiamue kutengeneza mzigo mmoja tu tukaubeba!?
Pamoja na jaribio dhaifu la Tume ya Warioba kupendekeza kuikataa majimbo, pendekezo lao la Katiba Mpya kimsingi linatengeneza majimbo yale yale (States) ambapo kutakuwa na majimbo mawili - Tanganyika na Zanzibar! Kwa sababu kama nchi mbili zimeungana na kuunda 'Shirikisho" basi zile zilizoungana haziwezi kuendelea kuwa nchi tena; zinahamisha hakimiya (sovereignty) yake kwenda kwenye federal government isipokuwa kama kilichoundwa (Shirikisho) siyo nchi!
Kwa kuanzisha mfumo wa Majimbo - Jimbo la Tanganyika litakuwa na nguvu kubwa sana kuliko jimbo la Zanzibar. Lakini kama wakiamua kufanya hali ya sawa katika kuendesha serikali ya Jamhuri ya Muungano Zanzibar itaonewa kwani ikitakiwa kuchangia nusu ya gharama za kuiendesha serikali ya Muungano italalamika mno na sidhani kama Wazanzibari watatakiwa kukubali mfumo huo.
Kwa sababu hiyo njia ya kuimarisha "Muungano" kama lengo ndio hilo basi ni kuingia Serikali Moja ya Kitaifa na Nchi Moja - siyo serikali tatu za kitaifa. Chini ya serikali hiyo moja ya kitaifa (federal government) kutakuwa na serikali za Majimbo (States) ambapo Zanzibar itabakia kama ilivyo (Visiwa vya Mafia, Bagamoyo, Pangani vinaweza kuongezwa huko... I know.. I know.. au ikagawanywa Unguja ikawa kivyake na Pemba kivyake!.) halafu Tanganyika igawanywe kwa States saba hivi ambazo zitaunda 'Regional Governments). Chini ya Regional Governments kutakuwa na "Local Governments" za Miji, Majiji, Vijiji na mifumo mingine ya kujitegemea.
Na maneno mengine mengi....
In short.. Tusikubali serikali tatu za nchi; bali serikali moja, nchi moja, taifa moja na watu wamoja.. Mapendekezo ya Tume ya Warioba kuwabebesha Watanzania mizigo hii ni ya kupingwa, kukataliwa na kupuuzwa.
Wakenya wameanzisha upuuzi huu kwenye uchaguzi uliopita. Tunalo tatizo la kuiga mambo ya kijinga na kuacha yale yenye manufaa kwa jamii.Hili linaweza kuwa baya kuliko yote,nimeangaika kutafuta kama kuna nchi duniani yenye mfumo kama huu nimekosa.Huenda Tanzania ikaweka historia kwa jambo la kipuuzi kama hilo.Mpaka hapa tulipo tunatakiwa kupunguza kwani ni gharama sana kuwalipa,unaweza ukaangalia uwiano wa wanawake bungeni duniani kwa kila nchi na Tanzania ikiwa ni ya 20;Women in Parliaments: World Classification
Kwa nini viongozi wa CCM wanang'ang'ania muungano?
Wakuu; Cuf,kule zanzbar hawataki kabisa muungano japo hawasemi wazi wazi.Uamsho ambao kwa kiasi wanaungwa mkono na Cuf hawataki muungano.CCM kule zanzbar wanataka muungano lakini wanajua vizuri kwamba njia ambayo inaweza kuwapa viti vingi vya kiungozi ni kuwa na serikali kuanzia serikali mbili na kuendelea!.Kwa sababu hiyo basi; Wazanzbar wengi hawatakubali serikali moja.
Kuhusu watu wa bara; Wengi wao bila kujali sana vyama vyao, wanataka serikali moja, nchi moja, watu wa moja, raisi mmoja, sarafu moja.Lakini ili kujaribu kuwa sawia na wenzao wa Zanzbar, ndio maana wanaamua kuwa "flexible".
Kwa mazingira haya; hatuwezi kuwa na serikali moja na pande zote zikabaki zikiwa zimeridhika licha ya kwamba nadharia ya serikali tatu nayo haina maana na wala maslahi kwa wananchi wa kawaida wa pande zote.
kwa ujumla suala hili lina kaunafiki kanako wakabili wenzetu.mimi nadhani pengine wapewe wanachotaka.mkuu hapo kwenye red natofautiana na wewe,
mosi, karume aligombana na wenzake kwenye nec akitaka wazanzibar wasikilizwe maoni yao kuhusu muungano. Akawatukana wenzake kwenye nec kuwa wana vichwa kama samaki. Je, unajua kuwa alikuwa anatetea zbar kujitenga na yeye ndo mkiti wa taifa za zanzibar mstaafu?
Pili, maalim seif ameshasema majuzi kuwa karume na kamando salmin marais wastaafu wote kutoka ccm wanaunga mkono hoja ya zanzibar kuwa serikali huru. Wenyewe hao marais mpaka leo hawajakanusha kauli maalim seif. Ccm kupitia kwa msemaji wao wakawasemea kuwa siyo kweli. Wanasema maalim seif anawagonganisha marais wastaafu na rais shein. Umeshajiuliza kwa nini hawa karume na dr salmini hawaendi public na kukanusha kauli ya maalim seif kama siyo kweli. Kiukweli wanzabar wote ccm na cuf lao ni mmoja --- zanzibar huru.
Na kwa taarifa yako, hii ndo ilikuwa siri ya kuunganisha cuf na ccm au karume na maalim seif.
Naunga mkono hoja,hakika wewe ni mzalendo,uchu wa uroho wa watu unahofia hili,mzigo wa serikali tatu haukubaliki hata kidogo mailings,serilali moja taifa moja
Hii kitu nimekua nikijiuliza tena na tena bila kupata majawabu. Pengine hawataki ku admit kuwa walifanya makosa huko awali!!...lakini kosa siyo dhambi. Hata dhambi tunaamini inasamehewa. Sasa sababu ni nini? Na hili jina Tanganyika kwa nini hawataki kulisikia?Kwa nini viongozi wa CCM wanang'ang'ania muungano?