Muundo wa Muungano: Tanganyika tunataka 'Serikali moja, nchi moja, taifa moja'!

Muundo wa Muungano: Tanganyika tunataka 'Serikali moja, nchi moja, taifa moja'!

Kwani muungano unaulazima gani kwa mtanganyika? Hasa mwananchi aliye kijijini?

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Naunga hoja serikali moja,taifa moja,nchi moja,rais mmoja!!!tueneze wito huu kwa kila mtanzania ili rasimu hii isipite na mapendekezo ya serikali 3
 
Hili la serikali tatu ni sawa kwa kuwa muda si muda tutakuwa na akina Yeltsin watakaowaacha akina Gorbachev bila nchi ya kutawala na hivyo Tanganyika kuwa nchi peke yake bila unyonyaji wa Zanzibar na Zinzibar kubakia peke yake bila unyonyaji wa Tanganyika. Juzi nimewasikia wakililia kiti chao UN basi tukimpata Yeltsin wetu nao watakuwa na kiti chao huko UN. Wacha zije lakini tatu hazitadumu.

sawa....lakini why rely on getting results by default rather than structuring it in the first place?

the point is....let's do a correct thing the first time. tuamue sasa tunataka kuwa na serikali ngapi badala ya kusubiri idadi ya serikali kupatikana by default!
 
liwalo naliwe serikali moja,taifa moja,nchi moja,rais mmoja,huo ndo muungano

Lazima ulikula jongoo ulipokuwa mdogo maana akili zako si sawa sawa za kushikiwa iweje iwe serikali moja na Zanzibar wali - keep their identity ni watanganyika tu ndio waliopoteza identity yao. sasa wana haha na katiba ya Tanganyika kabla ya uchaguzi 2015 ni dhahir ya Tanganyika itakuwa ya kuburuzwa na muda mfupi ujao itakuwa imejaa viraka.
 
si tayari wako zanzibar?? wafanye referrendum yao, wafuate taratibu na wasikilizwe ili watoke... hakuna haja ya kukaa tunalumbana na kanchi kenye kelele wakati productivity hakuna


mimi naamini kabisa kama zanzibar wangekua na nia ya dhati ya kujiondoa kwenye muungano wangeweza, ila wameishia kupiga perepete ili tu wawe wanapata watakacho, ni kama mtu mwenye gubu

kuhusu serikali tatu, nadhani itasaidia zaidi ile transition ya kuanchana na zanzibar, tutakua na migogoro mingi mno kati ya hizo serikali tatu mwisho tutafanikiwa kutengana.... ni sawa na kusema ndoa ina matatizo basi ulete mama mkwe akae hapo ndani kutatua - NDIO HIYO SERIKALI YA TATU AMBAYO ITAKUA NA MAMLAKA YA KUSADIKIKA ZAIDI, I DONT MIND UKIRITIMBA IF THAT IS WHAT IT TAKES KUVUNJA MUUNGANO

Hii nimeipenda. Kiukweli hii ni transition. Kwa wanaosema kuwa wanataka serikali moja hao ndio wanaoutaka muungano kwa dhati. Serekali mbili au tatu huo ni unafiki na kutokuupenda muungano. Kwa hili naungana na "wanafiki" ili tuuvunje kimya kimya kwani wao (wazanzibari) ndio wenye choko choko. I am sure baada ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano Watanganyika tutakaa chini tuandike ya kwetu itakayotusimamia.
 
...Sioni namna ya Wazanzibar kuridhia mfumo wowote wa Muungano, hivyo Nasema NDIYO kwa Serikali tatu kwa sababu moja kubwa, hii ni njia rahisi na ya wazi kuelekea kwenye serikali moja ya Jamhuri ya Tanganyika...

Mimi sitaki muungano. Nataka Tanganyika irudi na Zanzibar iende kwao. Tuungane EA.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
wazaninzibar mambo ya nje lazima litoke kwenye hiyo rasimu uhamiaji lazima utoke ,uraiya tutakuwa na uraiya wa tanzania huku kila nchi ikiwa na passport

yake

mfano jamuuhuri ya muungano wa tanzania au shirikisho la tanzania tangnyika passport au shirikisho la tanzania zanzibar passport

usjili wa vyama vya siasa kila nchi iasjili vyama vyake lazima litoke

sasa yaliyo baki benk kuu na hili watalijadili kwa kuliboresha sio kuliondowa kabisa

kinyume wazanzibar kuyatowa mambo ya nje basi shida na zogo la muungno halita maliza hadi kufa kwa muungano kupitia mgogoro

kwa kupitia mgogoro wa katiba

Hivi kwanini tuhangaike hivi ,kwanini tusivunje huu muungano .najua raisi anaogopa kashfa lakini huu muungano haubebeki tena
 
Baadhi ya wajukuu wa sultani ni janga kwenye Taifa letu...
Hatupaswi kuwabembeleza...ni bora tuwe na serika
 
Kwa rasimu hii tunahitaji kuwatimua na kuishitaki tume ya Warioba na pia kuwa chunguza kama zimetimia kweli

Nakuunga mkono. Ndiyo hao waliotenga bajeti ya watakaopata UKIMWI na fuel full tank kila siku. Haikubaliki. CAG aingilie mapema. Halafu kila aliposhauriwa Warioba alikuwa akibisha. May be he had a different agenda.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Tunataka serikali moja tu

Serikali ya watu wa TANGANYIKA

Hao wengine hatutaki kuwasikia, waende kupika urojo huko kwao

Ni wakati umefika Ng'ombe akatae kunyonywa na kupe mlalamishi.

Hivi kwanza wana faida gani kwa bara hawa wazenji zaidi ya kelele na udini?

Hiyo Serikali ya Tanganyika ikipatikana ule ukanda wa Pwani uliokuwa chini ya himaya ya Waarabu ikiwemo Bagamoyo na DSM itakuwa sehemu ya Tanganyika yetu au Zanzibar? King of Zamunda
 
Bado naipiti rasimu kipengele hadi kingine.
Kuhusu hili analosema Mwanakijiji kuna ukweli mkubwa sana.

Serikali ya muungano ni kubwa kuliko watu wanavyodhani. Yaani ni katiba ya sasa ambayo imevunjwa vunjwa na kupewa maneno mbadala.

Hii katiba itakuwa mzigo kwa Mtanganyika. Nikiangalia ukubwa wa serikali ya muungano nina uhakika kabisa Zanzibar hawataweza kuchangia gharama za uendeshaji wake na hilo litakuwa zigo la Mtanganyika.

Najaribu kuangalia ukubwa huo naona mambo ya kutisha kidogo. Mfano, endapo bajeti ya serikali ya muungano itakuwa trillioni 1 tu(kitu ambacho hakiwezekani) Zanzibar italazimika kchangia bilioni 500 kwa usawa.
Bajeti ya znz kwa mwaka 2013 ni bilioni 630 na mapato ya znz ni bilioni 120.
Kwa maneno mengine mapato ya znz hayawezi kuendesha kitengo kimoja cha serikali ya muungano.

Katika hali hiyo mzigo anaubeba Mtanganyika kama anavyoubeba sasa hivi.
Kitu kinachoshangaza ni kuwa nafasi zimetolewa kwa uwiano, lakini wakati wa kuchangia uwiano hautakuwepo na zigo atalibeba Mtanganyika.

Nathubutu kusema kuwa serikali ya muungano ni zigo kwa Mtanganyika, mzanzibar yupo tu kwa kudai nafasi na hana mchango wa aina yoyote kama kawaida yake. Tumesema tunataka kutua zigo la misumari

Tutaendelea kuangalia mambo mengine lakini sehemu kubwa ni mzigo kwa Mtanganyika.
 
hapa pana kitu kimejificha, na siku kikiibuka kinaweza kuleta mshangao kwa wengi.... mimi ninaamini kwa dhati kabisa kuwa muungano wetu umewachosha wote(tanganyika/zanzibar) ila tu hakuna kiongozi anayetaka kukubali umfie chini ya uongozi wake. tunashinikizwa kuungana kama jinsi mwalimu alivyoufanyia usanii mkataba wa muungano na kutokuuweka wazi hata kwa KARUME MWENYEWE....... Hatuna haja ya kulinda kwa nguvu muungano ambao pande husika haziko tayari. serikali tatu sio suluhisho na inaweza ikawa ndio muelekeo sahihi wa kuipeleka jamhuri ya muungano wa tanzania mwishoni. na serikali moja ndio janga kabisa kwa wazanzibari, hawawatakubali na watatangaza vita vya wazi(an open war) dhidi ya bara... tujiulize swali la msingi........... KAMA SERIKALI MBILI HAWARIDHIKI, HIYO MOJA WATAIPOKEAJE?????? Kwa sababu itawanyima na kuwaondolea hata kile kidogo walichonacho hivi sasa
 
Nadhani huu ndio wakati muafaka wa kuidai Tanganyika yetu,kwanini mizigo isiyo na ulazima kwetu!!!!!
Hakuna siku wazanzibar watakubali tubaki na serikali moja wavunje yao,hivyo kutaka kuwa na serikali tatu
ni kuwafurahisha wazanzibar na kutuumiza Watanganyika,ifike sasa tuseme NO'
 
Katika mazingira ya siasa za Zanzibar za sasa kwa hakika kutaka serikali moja ni "kulilia mbaramwezi"! - Halitatokea!. "Tulifanya" makosa kutunga sheria inayozuia watu wasitoe maoni yao juu ya kuwepo au kutokuwepo kwa muungano. Na haya ndio malipo yake!

Tungeanza kwanza kuwauliza watu kama wanataka kuendelea kuungana ama la, kabla ya kuwauliza mfumo wa muungano wanaoutaka. Ukitizama maoni/mapendekezo ya sasa ya baadhi ya wazanzibari, ni wazi hawataki kuendelea na huu muungano na hata watanganyika baadhi yetu hatuoni faida za wazi za muungano huu.
Yes! This would be a good starting point. Mimi sitaki muungano. Nataka Tanganyika. Hivi kweli nani aliwahi kuiona ile instrument ya muungano wa 1964? Hawa wazee walikuwa na hoja gani za msingi?


Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
  • Thanks
Reactions: SMU
mi nafikili wale Wapemba pale Kariakoo,muda umefika kuchukua maamuzi magumu....warudi Zanzibar wakaijenge Zanzibar yao....maana kama kujibembeleza tulianza zamani sana...kama ni maji sasa yako shingoni....
 
Hiyo Serikali ya Tanganyika ikipatikana ule ukanda wa Pwani uliokuwa chini ya himaya ya Waarabu ikiwemo Bagamoyo na DSM itakuwa sehemu ya Tanganyika yetu au Zanzibar? King of Zamunda
Sasa wewe unaleta mambo ya rais wa Malawi ya outdated Heligoland treaty. Tanganyika inafahamika mipaka yake. Zanzibar ni visiwa vya Unguja na Pemba. This is also known.


Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
hapa pana kitu kimejificha, na siku kikiibuka kinaweza kuleta mshangao kwa wengi.... mimi ninaamini kwa dhati kabisa kuwa muungano wetu umewachosha wote(tanganyika/zanzibar) ila tu hakuna kiongozi anayetaka kukubali umfie chini ya uongozi wake. tunashinikizwa kuungana kama jinsi mwalimu alivyoufanyia usanii mkataba wa muungano na kutokuuweka wazi hata kwa KARUME MWENYEWE....... Hatuna haja ya kulinda kwa nguvu muungano ambao pande husika haziko tayari. serikali tatu sio suluhisho na inaweza ikawa ndio muelekeo sahihi wa kuipeleka jamhuri ya muungano wa tanzania mwishoni. na serikali moja ndio janga kabisa kwa wazanzibari, hawawatakubali na watatangaza vita vya wazi(an open war) dhidi ya bara... tujiulize swali la msingi........... KAMA SERIKALI MBILI HAWARIDHIKI, HIYO MOJA WATAIPOKEAJE?????? Kwa sababu itawanyima na kuwaondolea hata kile kidogo walichonacho hivi sasa

Hukutoa maoni yako nini kifanyike notradamme
 
Back
Top Bottom