Muundo wa Muungano: Tanganyika tunataka 'Serikali moja, nchi moja, taifa moja'!

Muundo wa Muungano: Tanganyika tunataka 'Serikali moja, nchi moja, taifa moja'!

Wakuu naomba mnisikilize:

Siungi mkono muungano wa serikali mbili kwa sababu hata tukisema tutatue kero za muungano wa haina hiyo leo; kesho zitakuja nyingine na nyingine. Kwa kifupi kero zake ni endelevu!

Mimi nadhani kilichotufanya tuungane kwanza ni kutaka kuonesha njia kwa mataifa mengine ya Afrika. Kuonesha njia ambayo baadaye ingetufikisha pale ambapo Afrika nzima ingekuwa moja. Nyerere alikuwa na haki na wajibu wa kuipoteza Tanganyika ili kuidhihirishia Afrika na dunia imani yake kwenye Muungano wa Afrika! Kipindi kile ilikuwa ni sifa kubwa sana kupigania Umoja wa Afrika.

Sababu ya pili ilikuwa ni ya kuhimarisha ulinzi na usalama kwa wakati ule!

Sababu zote hizo hapo juu hazina mashiko tena kwenye zama hizi za ubepari! Sasa kwa nini tuendelee kuishi imani zisizokuwepo!

Ikumbukwe kuwa zile juhudi za kuliunganisha bara la Afrika zilikufa hata kabla hazijafika mbali kwa sababu wengi wa waliokuwa wanaamini kwenye umoja wa Afrika walitoweka na mawazo yao!

Hata zile juhudi za kuziunganisha nchi za Afrika Mashariki hazina uhai tena. Sisi ni mashuhuda wa kifo chake kitakatifu; tunasubiria tu kitangazwe rasmi siku za usoni!

Nauliza maswali hapa: Ni kwa nini kuwepo na muungano ambao mshirika mmoja anakubali kupoteza ili kumwokoa mwingine? Hata kwenye ndoa haiwezekani ndugu ni lazima walete chokochoko mwenzi mmoja akitoweka!
Eti serikali tatu haiwezekani kwa sababu Zanzibar haina uwezo! Ni kwanini nchi ijione haina uwezo wakati ilitafuta uhuru wake ili ijiendeshe?

Kama kujiendesha kwake ni kwa kutegemea taifa lingine haioni kuwa ina uhuru wa bendera tu?
Kama Zanzibar wa hofu wakiungana rasilimali zake kama mafuta n.k zitapotea; je, Tanganyika yenye gesi, mafuta, wanyamapori, makaa ya mawe, madini ndiyo iendelee kujitoa sadaka???! Basi Tanganyika itakuwa ni nchi nzuri sana ya kuishi kwa sababu haina hofu ya kuishiwa rasilimali!

Endapo atajitokeza mtu wa kuainisha pasipo shaka mipaka ya mapato na matumizi baina ya Tanzania Bara, Zanzibar na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nitafarijika sana! Nasema hivi kwa sababu ninachokiona mimi ni kuwa chochote kipatikanacho Tanzania Bara ni faida ya wote na cha Zanzibar ni kwa faida ya Zanzibar tu pekee.

Je, hii inaonesha kuwa Tanzania Bara inajiamini kuwa yenyewe ndiyo yenye uwezo wa gharamia serikali ya muungano na inaona fahari kufanya hivyo?! Au labda kuna masuala mengine Tanzania Bara inanufaika nayo ambayo sisi wananchi hatujui!
Je, Zanzibar nayo inaona fahari tu kuhudumiwa kila kitu kwenye muungano na wala haioni kuwa Tanzania Bara imebeba jukumu zito? Na je Zanzibar isipotimiziwa mambo kadhaa watakuwa radhi kulalamika ilhali wamebebwa katika mambo mengi?

Nionavyo mimi kama tatizo ni gharama za kuendesha serikali tatu ambazo ndo halali ni sharti tutafute mfumo wa kudumu kutatua tofauti zetu! Tukumbuke kuwa upande mmoja wa muungano umeingia gharama kubwa kuhudumia serikali ya muungano kwa zaidi ya miaka 49 sasa! Au iaonekana Tanganyika hajichoka kulea muungano na Zanzibar nayo haijachokaa kubebewa!

Tusijidanganye; Tanzania ni jina! Nchi ni sisi wananchi! Na wananchi wa pande zote za Muungano wamechoka kulazimishiwa muungano wa serikali mbili! Tunaowaona wanatetea ni baadhi ya watawala ambao muungano uliopo sasa unawanufaisha kwa namna fulani.
Kama wananchi wengi wanadai muungano hauwatendei sasa inabidi tuseme imetosha tutafute kitakachotupa haki na usawa. Na hiki si kingine zaidi ya nchi zote kuungana na kuwa chini ya serikali moja itakayohakikisha kila raia anakuwa na haki sawa na mwenzake bila kujali atokako!

Ingependeza tuwe na serikali tatu kila nchi ijihudumie kwani kila nchi ilidai uhuru ili iwe huru! Lakini watu wanaeneza mawazo hasi ya ukubwa wa gharama!Umaskini na uvivu wa fikra! Ikumbukwe chochote kizuri ni sharti kiwe na gharama yake; tena gharama kubwa!
Kama tunakimbilia unafuu wa serikali mbili tufahamu wazi kuwa nafuu mara zote ni ghali zaidi na mara zote hazidumu!

Muungano wa serikali mbili vilio vya unyonyaji! Muungano wa serikali tatu tunaogopa gharama! Basi muungano unaotufaa ni wa serikali moja. Kama hatuwezi muungano wa serikali moja, muungano wowote ule utakaokuwepo aidha wa serikali mbili, tatu au zaidi hautatuliza kiu ya wananchi! Narudia tena: Tanzania ni jina; nchi ni wananchi!

Nashangaa nchi zenye watu zinaogopa kujiwekea mifumo ambayo itawastawisha na kumaliza chokochoko kwa visingizio visivyoisha! Ina maana pamoja na rasili mali tulizonazo viongozi wetu wanataka kututhibitishia kuwa hawawezi kuweka mifumo ya kuliendesha taifa kwa ustawi!

Hoja ya kuwa kuna udugu wa damu kati ya Tanganyika na Zanzibar ni hoja ya kibaguzi kwani uhusiano wa damu upo pia baina ya Tanganyika na nchi nyingine. Swali hapa: Ni kwa nini tusiungane na Kenya, Uganda, Msumbiji, Burundi, Malawi, Zambia, n.k kwa sababu hata huko wapo watanganyika wana ndugu zao?
Kama hoja ni udugu ni kwanini Zanzibar wanapochagua wabunge wa kuja kwenye bunge la Jamhuri wa Muungano, upande wa Tanzania Bara nao wasichague wawakilishi wachache kwenye Baraza la Wawakilishi ili kuukuza zaidi huo unaoitwa udugu???
Udugu unaonufaisha upande mmoja zaidi ya mwingine si mzuri jamani! Tuache propaganda. Kama tunaamini umoja ni nguvu utengano ni udhaifu basi tuungane tuwe nchi moja, serikali moja, rais mmoja na Tanzania moja ili tuwe ndugu kweli!

Watasema ni chuki lakini kama hatuwezi kumaliza tofauti zetu kwa kuunda serikali tatu au moja basi ni bora kila nchi ijendee kivyake! Hata Kenya na Uganda ni ndugu zetu lakini hatujaugana nao kutengeneza taifa la kusadikika!

Litakuwa ni kosa sana kuendelea kuwa na muungano ambao upande wa Tanganyika tu ndiyo unaendelea kupoteza historia yake wakati mshirika wake Zanzibar akibakiwa na ziada hata kama ni sawa na wilaya moja ya Tanganyika!

Wakuu; naombeni kuwasilisha hoja!


Hoja imefika lakini mbona ndugu yangu hoja yako umeijenga katika mambo mengine yasiyokuwa ya kweli?
zanzibar ikiwa na serikali kamili ndiyo ya kuonewa huruma kwani inajukumu la kuwaendeleza na kuwahudumia watu wake kwa yale yanayoambiwa si ya muungano na baadae kuja kuchangia katika jungu kubwa ambalo sehemu kubwa inaliwa na walio wengi na ambao matumizi yao hayatenganishi baina ya walichozalisha wao au wenzao.
Hili la kutotafautisha baina ya kipato na matumizi ya pamoja na yale ya Tanganyika pekee ndio hufanya wazanzibari wawepo bungeni ambako hayo matumizi hufanywa. Kule zanzibar matumizi yanayopangwa na wawakilishi ni ya zanzibar peke yake sasa hiyo haja ya kuwaleta watu wasiohusika ya nini?
Hata hivyo nakubaliana nawe kuwa hakuna uwazi na hili lazima lilete manunguniko, na dawa yake ni rahisi tu, tuchukue mfano wa zanzibar wa kuwa na serikali yake na hivyo Watanganyika watajuwa nini wanachuma na nini wanatumia kwa serikali yao na kama tunahitaji tuwe na mambo fulani ya pamoja basi tufanye donation kwa mujibu wa tumbo la mtu na anavyokula!
 
Mi nadhani waasisi wa Muungano walikula yamini fulani za kipepo ambapo waliapizana kwa matambiko ya damu!
Watu wazuri kabisa wa kuungana nao walikuwa ni nchi za huku bara ambazo hatuhitaji hata usumbufu wa kupanda majahazi kufika kwao, huku uki'risk maisha kwa hofu ya kuzama baharini!
Aina ya muungano tulio nao unaleta gharama mno kwa bara na wenzetu hawariziki na chochote.
Ninachojiuliza kwanini kusiwe na referrandum ya kuhoji kuwepo au kutokuwepo Muungano kwa Bara na Visiwani ili tukate mzizi wa fitna? Ni nani mwenye hati miliki ya nchi hizi mbili hadi akataze watu kuuliza upya kama wanahitaji Muungano?
sio rahisi kuwatawala wa huku Bara, lakini wazanzibari ilikuwa rahisi. kwani kinaogopwa nini serikali tatu? Huko ndio tutakojuwa maana ya kuungana na faida zake na ni rahisi kuamuwa basi iwapo hakuna faida. Baadhi ya wazenji wanataka mkataba ,jamani hamuoni hilo ni wazo zuri zaidi kwa dunia yetu ya leo?
 
Machama mengine yamebaki kumtukana mwenyekiti na jopo lake la katiba mpya.maoni ya wananchi kuyaita ni viongozi wa tume ni opofu!!! kama serikali moja haiwezekani bac tujaribu 3 siyo mbili maana tayari madhaifu ya ni pamoja na kero na uvunjifu wa katibu ya muungan unaofanywa na upande wa pili wa muungano.g56!
muungano wa kisawa ni huu hapo chini.. sote kwa pamoja washirika wa muungano tunaongoza jeshi letu.. sote kwa pamoja tunaongoza nchi.. yako wapi leo hii... liliobakia sasa kwa sisi wana wa kizanzibari ni kuendelea kudai cha kwetuna kuwaelimisha tanganyikaz.. mlikua mnatuona machizi but now mpo kila mahala mnajadili tuloanzisha na kuendeleza sisi wazanzibari.. mnaona eihhhhh.. nyote sasa mnajadili hii kitu muungano.. angalia picha hiyoangalia step zote.. nani kamzidi mwenzake hapo.. huo ulikua usAWA.. SASA LEO IWEJE KUJIFANYA KAMIZINGA MNATAKA MPIGIWE NYINYI TUUUU NA MNAUMIA MZENJ AKIPIGIWA.. AKILI NDOGO HIZO KUTOKA KWA WASEMAJI WENU BUT IT IS WHAT IT IS.. TUKO IMARAA WAZANZIBARI TUNASONGA MBELE.. MTATUFATA TUU KUDAI CHA KWENU...
 
Binafsi huwa mara nyingi naamini muungano ni kitu kizuri, lakini nina mashaka makubwa kama nchi zetu hizi za Tanganyika na Zanzibar zimefikia hatua ya kudeal na mambo mazito tena na ambayo ni optional i.e muungano.

Kwa hatua tuliopo katika na kama kweli tuna viongozi wasio na ubinafsi wenye kutazama na kujua jinsi ya kueka priorities, basi muungano ni suala ambalo linatakiwa liondoke kabisa katika mawazo ya wananchi.Tunatakiwa tujikite zaidi katika kuboresha standard of living na kuimarisha uchumi na kuwa nchi zenye kujitegemea.

Shortly nashauri kukagawana mbawa!
 
Hesabu ya Nyerere
1+1=2 akimaanisha mbili ni serikali ya Zanzibar na Serikali ya Muungano!
Lakini maana halisi ya Muungano wetu ni
1 + 0 = 1 Yaani moja ni serikali ya zanzibar....sifuri ni nchi ya Tanganyika na Jibu ni serikali ya Muungano!

Muungano ulitakiwa kuwa hivi
1 + 1 = 2 yaani moja ni serikali ya zanzibar,moja ingine ni serikali ya Tanganyika na mbili ni serikali ya Muungano ambayo inasimamia mambo ya bara na visiwani!
Naunga mkono serikali tatu!


Mkuu!
1+1=1 ndio jibu sahihi.Hii inawezekana kwani pakiwepo na mawaziri wakuu wawili
watakaochaguliwa na wananchi/Rais awe na makamu wawili
watakaojulikana kama mawaziri wakuu mmoja kutoka Zanzibar na mwingine kutoka Tanganyika.
 
Mkuu!
1+1=1 ndio jibu sahihi.Hii inawezekana kwani pakiwepo na mawaziri wakuu wawili
watakaochaguliwa na wananchi/Rais awe na makamu wawili
watakaojulikana kama mawaziri wakuu mmoja kutoka Zanzibar na mwingine kutoka Tanganyika.

nakubaliana na wewe mkuu robert josephat

lakini nchi iwe kama ifuatavo

JINA : ZANZIBAR

CAPITAL CITY: ZANZIBAR TOWN

AGREEMENT: MUST BE 100 YEARS

MINISTERS: 50/50 TANGANYIKA/ZANZIBAR

F. EMBASSIES: MUST BE IN ZANZIBAR

ALL GOVERNMENTAL INSTITUTIONS: HQ IN ZANZIBAR

CENTRAL BANK: MUST BE IN ZANZIBAR

UHUAMIAJI: MAKAO MAKUU ZNZ

POLISI, JESHI, NAVY U NAME IT
 
Ukitaka kuwatibu waZanzibar waambie swala muungano wa serikali moja
Hatakuelewa kamwe
 
Kwetu sisi wazbr muungano c lazima,kitu cha lazima kwa upande wetu ni mamlaka kamili ya nchi yetu ikibidi muungano ni wa mkataba na nchi yoyote sio lazima iwe tanganyika,hii ni tofauti na watanganyika ambao wanaamini hawawezi kuishi bila ya muungano na muungano wao ni kwa zanzibar tu kama vile hakuna nchi nyengine duniani,zanzbr kwanza.

Hata mimi nakuunga mkono ndugu ni bora kila nchi ikabaki kivyake kuliko kuendelea kutupigia kelele humu janvini. Kwani undugu wetu utaendelea kuwepo.
 
Watanzania waishio Mtwara imesemwa waeliweshwe kuhusu umuhimu wa kusafirisha gesi kutoka Mtwara kwa bomba kuelekea Dar es Salaam. Swali ninalouliza nguvu hiyo ya uelimishaji kwa nini pia isielekezwe kwa watanzania wanaoishi Zanzibar ili wakubali tuwe na serikali moja?
 
Mwaka 2007 nilifanya research kuhusu shirikisho la Africa Mashariki katika kumalizia masomo yangu ya elimu ya juu..Ulichosema ndugu Mwanakijiji ni sahihi kabisa. Wengi walikataa hoja za shirikisho lakini tume ile ikiongozwa ( naomba nisimtaje jina) ilitoa majibu tofauti na uhalisia wa wengi.. hapa ni rasimu tuu nachoamini haki ikitendeka hata Muungano utavunjika iwapo suala la serikali 3 litapita. Ukweli lazima tufanye maamuzi kulingana na faida na hasara na ni lazima tufanye uana harakati wakuonyesha ukweli wa mambo. Kama kweli tunauihitaji muungano kwanini tuogope serikali moja? take example of Brazil, USA and other federal Governments. Mbona zina Rais Mmoja nasie ombaomba tung'ang'anie serikali 3? tena wao kila uchao wanaangalia namna yakupunguza ukubwa wa serikali...mAONI YANGU.. TUWE WAKWELI kama kwanza kama wengi wanautaka Muungano au haawataki and we should share facts about viability of such Union1

Acha kupotosha umma, USA kuna serikali 51! Yaani serikali za majimbo 50 zinazo ongozwa na magavana waliochaguliwa na wananchi kwa kura, na kuna serikali kuu ya shilikisho inayo ongozwa na Obama. Kila jimbo lina sheria zake, polisi wake, mahakama zake nk. Serikali 3 ni jibu la matatizo ya muungano.
 
Nilikuwa ndotoni. Nikaona watanzania wanaunda serikali tatu 2014. Katika ndoto hiyo nikaonaona ghafla baada ya serikali hizo tatu kuundwa Wazanzibari na Watanganyika wanajitizama na kujishangaa. Na mara wanaanza kudai katiba mpya tena ili kufanya muungano wa serikali moja. Mara ninaamka. Naitafakari ndoto yangu. Ndiyo, natamani ndoto yangu itimie katika siku chache, kabla sijafa!
 
kwani unakufa lini?...usisahau ukiota na kuona ndoto haitimii "unatakiwa urudi kulala kuitimiza ndoto yako"
 
kwani unakufa lini?...usisahau ukiota na kuona ndoto haitimii "unatakiwa urudi kulala kuitimiza ndoto yako"

nakadiria kufa kwangu kutakuwa kati ya leo na miaka 50 ijayo. Siwezi kurudi kulala kwa kuwa ndoto yangu haijatimia. Nitaendelea kusubiri itimie, nina matumaini itatimia kabla sijafa.
 
Umeota mchana.

Hapana sioti mchana, niliota usiku na nilipoamka majukumu yakanitinga, sasa ndiyo nimepata nafasi kidogo ya kuweza kuwashirikisha wenzangu hii ndoto yangu ambayo nadhani ndani yake kunaweza kuwa na unabii
 
Back
Top Bottom