Muundo wa Muungano: Tanganyika tunataka 'Serikali moja, nchi moja, taifa moja'!

Muundo wa Muungano: Tanganyika tunataka 'Serikali moja, nchi moja, taifa moja'!

HUU NDO UKWELI, NCHI MOJA SERIKALI MOJA, kama Zanzibar hawataki maana ni rahisi sana kuwa hakuna muungano
 
Watanganyika tujiulize, nini tunapata kutoka Zanzibar(Unguja na Pemba)
Wao wanapata ajira, wanapata posho 4.5%, wana serikali na jeshi, sisi tunapata nini?, maliasiri wakigundua kwao ni zao, sisi tukigungundua gesi, itachangia pato la taifa, alafu wao wapate 4.5%. hii mpaka lini. Watangyika hatuoni?

Siupendi muungano wa kinafki, kama ni muungano kila mtu achangie kwa uwiano sawa, siyo kuwabeba, kama wanataka kuedelea na muungano na wao wazanzibari wajishushe, waache jeuri wakati wanajua bila bara wamekwisha.

Waziri Dr, Khatibu amesema, Wanzibari ndo wanaohitaji muungano zaidi ya Wabara, sasa kwanini sisi wabara ndani ya ccm tunaonekana kana kwamba tunashida saana na Zanzibar. Dr. Khatibu kasema wazi, ardhi zanzibar ni ndogo, watu wakiongezeka hawana pa kwenda.

Kwa nini tuendelee kuwabeba wakati wao ndo wanatunyonya?
 
Serikali moja ndio suluhisho kama serikali mbili watu wamezichoka... Lakini serikali tatu zitaua muungano
 
sasa munajuwa wazanzibar hatutaki na kwa yakini munajuwa tunakubaguweni lakini munajitowa fahamu muungano hatuutakiwazanibar muuungano hatuutaki muuungano hatuuutaki
 
Sioni kama hawa uliowataja hapa wanataka muungano uvunjike/uvunjwe.

Mimi nimeshajaribu kuonesha ni lazima tuirudishe serikali ya Tanganyika na jina Tanganyika kama hatua ya kumaliza mazingaombwe lakini kila wanapoandika wanasema "tuwasaidie wazanzibari wajitoe"

Rai niliyotoa mimi ni kuwa tutumie rai ya mwasisi wa Muungano ya kuunda EAF. Huko tupeleke timu mbili.Serikali ya Tanganyika kivyake na serikali ya Zanzibar kivyake. Hapo ni kuwa huu muungano wa kisanii unaisha na tunaanza na Muungano wa kikweli.

Hawa dugu zangu, wananiweka njia panda.wananiona mimi UAMSHO. Bila Tanganyika na serikali ya Tanganyika ni kuendelea na kiini macho halafu tunalalamika Tanganyika inapata hasara. Entity ambayo haipo inapata hasara vipi?

Hakuna kati ya hawa anayetaka serikali ya Tanganyika.

JokaKuu unasema Tanganyika imemezwa? Imemezwa na nani?
Kama jibu ni Muungano, Muungano ni baina ya nchi ipi na nchi ipi?

Ile ngao ya adam na hawa ni nembo ya serikali ipi? Ile katiba ya Muungano imepatikana vipi?

Mkuu Nguruvi3 anasema Tanganyika ni sleeping general....alalae usimwamshe....

Jamani watanganyika tuamke!

Hawa akina mwanakijiji ni watu waongo sana,kama kweli watanganyika wananyonywa na muungano huu kwanini hawataki muungano huu uitwe ZANTANIA?yaani murejeshewe tanganyika yenu kisha zanzibar iwe ndio serekali ya muungano yenye balozi zote nje,rais wa muungano awe ndie amiri jeshi mkuu,tanganyika isipewe ruhusa ya kujiunga popote,raisi wa tanganyika akitaka kwenda nje kibali aombe zanzibar,tanganyika isiwe na kiti kule UN,makao makuu ya muungano yawepo zanzibr,wakiyakubali hayo kina mwanakijiji nitaungana nao kwenye kampeni yao ya let zanzbr go.
 
Watanganyika tujiulize tunapata nini katika muungano huu. zanzibari wanapata vingapi,ajira, ardhi, mapato ya maliasiri za bara wakati za kwao ni za kwao. mbona hatuoni ambavyo hautufaidii chochote?

sioni faida ya mungano wa kinafiki, huenda Nyerere alikuwa na sabau zake ambazo kwa sasa hazipo, kama ni muungano kila upande uchangie sawa sawa. hakuna sababu ya kuendelea na mungano unaobeba watu fulani na wengine wananyonywa.
 
MWANAKIJIJI LEO UNA HOJA LAKINI REFERENDUM INGETANGULIA MAMBO YA KATIBA HILO LINGEPENDEZA SANA.KWA SASA BUNGE LA KATIBA LIPO KAZINI NA RASIMU NDIYO HIYO,SIJUI TUTAFANYAJE,TUSHALIWA HIVYO AU KUNA MBADALA?
SERIKALI MOJA TAIFA MOJA NA NCHI MOJA!MAJIMBO NI JAMBO MUHIMU SANA NDANI YA SERIKALI MOJA!TATIZO KUBWA WALWAWLE WEZI WETU WA RASILIMALI ZETU NDIYO HAO HAO WANATUNGA KATIBA!KICHEKESHO CHA chui kutunga katiba inayohusu wanyama wafugwao kama kondoo na mbuzi na ndama!
 
kwa wenzetu wa Zanzibar kuzunjumzia serikali moja wako radhi muungano ufe,maana panga pangua wao wanachotaka lazima kuwe na serikali ya zanzibar, tatu,mbili,nne,tano kwao sio isue
 
Tusikubali kwenda serikali tatu. Kwa vile tumekatazwa kutaka kuvunja Muungano - japo waliotukataza hawana uwezo huo - na kwamba tunaweza kujadili "muundo" bora wa Muungano. Ninawasihi watu wa bara kudai "Serikali moja, taifa moja, na nchi moja". Haya mambo ya serikali mbili nchi mbili au serikali tatu nchi mbili hayaingii kichwani na ni jitihada za kujaribu kuibeba Zanzibar. Wakati umefika tudai uwepo wa serikali moja tu ya kitafa kwenye nchi moja.

Ninafahamu kabisa matokeo ya watu wa bara kutaka hili. Jambo pekee ambalo tusikubali kuuziwa (CCM na upiinzani wanataka hili) ni serikali tatu. Serikali tatu ni mzigo ambao hatuwezi kuubeba na wala hatupaswi kuubeba. Nawasihi wenzangu tukate kuongezewa mizigo. Tuwe na serikali moja, taifa moja na nchi moja. Sasa kama hili lina maana Zanzibar iwe "serikali moja, taifa moja na nchi moja" na bara iwe "serikali moja, taifa moja na nchi moja" basi na iwe.

Tuwasaidie Zanzibar watoke kwenye Muungano kama hawataki serikali moja kwani mbili hawataki na tatu tutajipa mzigo zaidi!

SAY NO TO SERIKALI TATU!!

Iambie tume ya Warioba - hatutaki serikali tatu!!
Mkuu Mzee Mwanakijiji, sijui wakati mwingine mimi ninakuwaga wapi?!, hii sikuiona ndio naiona leo!. Kumbukumbu yangu ya mwisho kwako kuhusu Zanzibar, ni ile let Zanzibar Go!.

Kwa wazo hili, tunafanana, na nimetumia nukuu hii kurutubisha uzi wangu fulani.
Thanks.
Pasco
 
Nitaendelea kuimba daima kwamba serikali moja ndio destination sahihi ambayo huu muungano ulipaswa kufikia,lakini katikati ya safari yetu kwenda huko,imejitokeza ukweli kwamba NI VIGUMU MNO KUWAUNGANISHA WATU WABINAFSI KUWA KITU KIMOJA.Kinachoendelea sasa ni revelations tu za ukweli huu.Lakini pia kuna ukweli mwingine ambao haujajitokeza bado kwa vile haujapata nafasi hiyo.Ukweli huo ni kwamba BINADAMU HAJAUMBWA AWE MBINAFSI.Kwa hiyo pale revelations za UBINAFSI zitakapotimia na UBINAFSI kutawala mifumo yote,hapo ndipo huu ukweli mwingine utapata nafasi ya kujitokeza na kutuonyesha kwamba HATUTAKIWI KUWA WABINAFSI.Wenye akili mmenielewa.
 
Nitaendelea kuimba daima kwamba serikali moja ndio destination sahihi ambayo huu muungano ulipaswa kufikia,lakini katikati ya safari yetu kwenda huko,imejitokeza ukweli kwamba NI VIGUMU MNO KUWAUNGANISHA WATU WABINAFSI KUWA KITU KIMOJA.Kinachoendelea sasa ni revelations tu za ukweli huu.Lakini pia kuna ukweli mwingine ambao haujajitokeza bado kwa vile haujapata nafasi hiyo.Ukweli huo ni kwamba BINADAMU HAJAUMBWA AWE MBINAFSI.Kwa hiyo pale revelations za UBINAFSI zitakapotimia na UBINAFSI kutawala mifumo yote,hapo ndipo huu ukweli mwingine utapata nafasi ya kujitokeza na kutuonyesha kwamba HATUTAKIWI KUWA WABINAFSI.Wenye akili mmenielewa.

Heri yako Mkuu wangu!
Hakika binadamu hakupaswa kuwa mbinafsi hata kidogo, na hakuna asiyejua hilo. Kila mtu nafsini mwake anatambua hilo, ila HULKA zetu ndizo zinazotupotosha!
UBINAFSI wetu ndio Maangamio yetu! UBINAFSI wetu ndio KIFO chetu! Hadi pale mwanadamu atakapotambua kwamba hakuna mimi bila wewe, na wewe bila mimi, hakuna kitakachokuwa salama!
Ati hoja serikali 1 wazbr watamezwa, ni Upuuzi wa wazi kabisa, tunazungumzia umoja wengine wanahofia identity yao, ni Ulimbukeni! Hatuwezi kufika kokote na watu aina hii! UBINAFSI-UMIMI ndio Angamio letu!
Mungu wetu yu tayari kutushindia vitani. Anaita sasa!
 
Kazi ipo!! Hatuwezi kumridhisha kila mtu. Maslahi ya nchi hii kwanza. Zanzibar na Jamuhuri zitakuwepo daima mpende msipende.

Watu kama kina Seif wakafie mbali kwanza mtu mwenyewe anaumwa

Tanzania kwanza!!!
 
sihitaji kabisa Serikali mbili wala zaidi kinachotakiwa sasa ni Setikali moja basi. Kama Wazanzibar hawataki wajindoe hakuna kubembelezana hapa.
 
Back
Top Bottom