Muungano mpya kati ya Burundi na Tanzania?

Kama huu wa Sasa umejaa kelele nyingi, sipati picha na Burundi ingekuwa mshirika hali ingekua tete kweli kweli.
JokaKuu Nguruvi3 Kilatha Kalamu
 
Sawa tu,tena hata Congo ya kinshasa ilitakiwa tuwe nchi moja kabisa,napenda sana tuwasaidie hao majiani zetu dhidi ya masaibu yanayowakumba mara kwa mara
Mbona cc ndo tunayo maproblem ya kushanta ni vle hawajui tu tumezoea kuvumilia, Ahahah watajutia muungano.
 
Sure
 
Unaweza ukashangaa, lakini huenda huo wa Burundi na Tanganyika ungekuwa imara zaidi kuliko huu tulionao sasa,... kwa sababu mbalimbali ambazo sitazitaja kwa sasa.
Naamini sababu ya kuwa Warundi wengi hawana uhusiano au ushawishi na watu kutoka nchi fulani ya nje ya Africa sio moja wapo.
 
Naamini sababu ya kuwa Warundi wengi hawana uhusiano au ushawishi na watu kutoka nchi fulani ya nje ya Africa sio moja wapo.
Hiyo ni sababu muhimu mojawapo, kwani hata ufadhiri wa kutafuta kuvunja muungano unaweza kuwa unapitia humo humo.
 
Hii haifai kabisa, kuungana na Burundi ili iweje?
Iwe kama ilivyotakiwa kuwa kwa Uganda mwaka 1986. Mazungumzo yakiwa katika hatua nzuri Okello akaipindua Serikali ya Obote, biashara ikaishia hapo.
 
Kabla ya huo muungano kwanza tutengeneze huu wa Zanzibar kwa maana ya kwamba ,hatutaki kuwa na Marais 2 au 3 ,ndani ya muungano ,hii inafanya maana ya muungano kuwa haieleweki!! Nini maana ya muungano Sasa Kama Zanzibar Ina wimbo wake wa taifa na bendera yake na rais wake!!? Wa burundi tunawakaribisha kwa moyo mmoja na waupendo lakini ,wakiungana na ss ,wakubali kuwa na mamlaka moja kiukamilifu yaani ,rais awe mmoja tu ,na wimbo wa taifa uwe mmoja tu,na bendera ipepee moja tu,na vyombo vya ulinzi viwe ni chini ya jeshi moja tu ,hapo ndo italeta maana halisi ya muungano, kinyume na hapo haina maana !!
 
Huu Muungano Tulonao sasa ni akil ya Ulevi kabisa, Tumeungana tu kushare faida af Mambo mengne kila mtu na utaratbu wake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…