Muungano uwe wa serikali moja tu, kama sio hivyo ufe tu

Muungano uwe wa serikali moja tu, kama sio hivyo ufe tu

Kuna uwezekano hakutakuwa na nchi inayoitwa tanzania miaka 50 ijayo....maana matatizo sugu hayatatuliki yapo tu...wameyafumbia macho
 
Faida pekee ninayoiona ya Muungano ni kuongeza idadi ya watu wetu kwenye kupata soko la ndani la bidhaa zetu na kumiliki na kudhibiti eneo kubwa bahari kiuchumi na kiulizi. Hii haina mjadala.
Sasa kama ni kwaajili ya ulinzi simngeungana na mataifa yote kwani hawawezi kupitia congo?.
 
Kuna uwezekano hakutakuwa na nchi inayoitwa tanzania miaka 50 ijayo....maana matatizo sugu hayatatuliki yapo tu...wameyafumbia macho
Jina litakuwepo tu! Siunajua tuna madini ya Tanzanite?.
 
Kuna uwezekano hakutakuwa na nchi inayoitwa tanzania miaka 50 ijayo....maana matatizo sugu hayatatuliki yapo tu...wameyafumbia macho
Ni upuuzi upuuzi tunaoambiwa tangu tukiwa watoto kuwa jina Tanzania linabeba majina ya Tanganyika na Zanzibar tayari, lakini Zanzibar bado ipo tena. Yaani Zanzibar Iko hai mara mbili ; Tanzania na Zanzibar. Ni wapuuzi TU watakaokubali hadithi kama hizo.
 
Sasa kama ni kwaajili ya ulinzi simngeungana na mataifa yote kwani hawawezi kupitia congo?.
Wakati tunaungana lilikuwa hakuna supersonic missiles na satellites za kivita. Siku hizi unaweza kupigwa kutoka Lebanon moja kwa moja. Lakini sio vizuri baharini jirani yetu kukawa na majimeli na nyambizi za kivita za adui. Usalama wa bamdari zetu ni mihimu sana.
 
Wakati tunaungana lilikuwa hakuna supersonic missiles na satellites za kivita. Siku hizi unaweza kupigwa kutoka Lebanon moja kwa moja. Lakini sio vizuri baharini jirani yetu kukawa na majimeli na nyambizi za kivita za adui. Usalama wa bamdari zetu ni mihimu sana.
Sawa mr
Seme nimda sana toka tanzania tumeshuhudia vita apa nchini.
 
Sasa kama ni kwaajili ya ulinzi simngeungana na mataifa yote kwani hawawezi kupitia congo?.
Mambo ni mengi sana, tunataka wazanzibar na watanganyika wote wawe na usawa kama watanzania kwenye nchi yao mpya Tanzania. Yaani raia wote wa Tanzania wawe kitu kimoja na fursa sawa kuliko ilivyo sasa. Mfano, Zanzibar ina watu kama 1.3m. Katika idadi hii tu ya watu ndani ya muungano lakini wana Rais, makamu 2 wa rais, waziri kiongozi, mawaziri, manaibu waziri, makatibu wa wizara, watumishi wizarani, mikoa 5, wilaya, tarafa, na kata kadhaa, shule za msingi na sekondari, vyuo vikuu, mabenki, majeshi, na mataasisi kadhaa, wabunge, wawakilishi, spika, nk. Hii maana yake kila wazanzibar 10 kuna wazanzibar 6-8 ambao wana ajira ya kudumu ya serikali na sekta binafsi. Hii nitofauti na Tanganyika kwenye nchi hiyohiyo moja ya tanzania.
 
Mambo ni mengi sana, tunataka wazanzibar na watanganyika wote wawe na usawa kama watanzania kwenye nchi yao mpya Tanzania. Yaani raia wote wa Tanzania wawe kitu kimoja na fursa sawa kuliko ilivyo sasa. Mfano, Zanzibar ina watu kama 1.3m. Katika idadi hii tu ya watu ndani ya muungano lakini wana Rais, makamu 2 wa rais, waziri kiongozi, mawaziri, manaibu waziri, makatibu wa wizara, watumishi wizarani, mikoa 5, wilaya, tarafa, na kata kadhaa, shule za msingi na sekondari, vyuo vikuu, mabenki, majeshi, na mataasisi kadhaa, wabunge, wawakilishi, spika, nk. Hii maana yake kila wazanzibar 10 kuna wazanzibar 6-8 ambao wana ajira ya kudumu ya serikali na sekta binafsi. Hii nitofauti na Tanganyika kwenye nchi hiyohiyo moja ya tanzania.
Hivi Tanganyika kwa sasa inaraisi?.
 
Mimi kinachonishangaza ni ardhi, mimi wa bara sio rahisi kupata kipande cha ardhi Zanzibar kama ilivyo wao kupata ardhi bara.
Ukiuliza hilo utaambiwa zanzibar ni ndogo, jibu la kipuuzi. Kama mtu wa zanzibar atakosa ardhi si ataenda kuipata Tanga, Mkuranga, Dar es salaam au kokote kule Tanzania? Tunataka Tanzania ya aina hii, kila mtanzania yuko huru kabisa kununua, kuuza au kuishi popote kama mtanzania popote ndani ya jamhuri.
 
Manufaa ya muungano tumeyaona, ni matamu sana kwa watanzania walio wengi. Kila kijana mzanzibar anatamani kwenda kuishi Tanzania bara, na wako watanzania bara ambao wanatamani kwenda Zanzibar kwasababu moja au nyingine. manufaa ya muungano kila mtu anaweza kuyasimulia bila kuambiwa wala kusoma pahala popote.

Mwalimu Nyerere na Karume nina uhakika wote au mmojawapo alitaka muungano wa serikali moja, na wako wazee ambao wanajua dhamira ya muungano na aina ya muungano ambayo waasisi waliukusudia lakini kwa unafiki na woga wao wamenyamaza kimya na hatimaye kufa na siri hiyo.

Wazee wa hivi hawafai kupewa heshima tunayowapa, maana ni wanafiki, waoga na wasioona mbele. Nyerere sio mjinga kuifuta serikali ya Tanganyika na asiifute ya Zanzabar, lazima kuna jambo ambalo tunafichwa na kupewa sababu za kijinga na uongo juu ya muungano wa serikali mbili. G55 hawakuwa wajinga kudai kuirudisha serikali ya Tanganyika; bila shaka ilikuwa kujibu mkwamo wa kupata serikali moja.

Wakati tunaelekea kuadhimisha sikukuu ya Muungano ni aibu nchi moja kuwa na serikali kamili mbili bila kuwepo ya Tanganyika. Wazee kama Pius Msekwa, Warioba, Butiku, Mongella, Msuya, Sumaye, Kikwete, na wengine ambao wanafahamu sababu za kweli na halisi juu ya kwanini serikali ya tanganyika ilifutwa na ya zanzibar akabakizwa waitoe siri hiyo kabla hawajaiaga dunia na kuondoka nayo hata kama kwakufanya hivyo kutaleta shida kwao. maana watoto wajao hawataujua ukweli halisi juu ya kwanini kuna serikali 2 badala ya 1 au 3.

Ni muhimu sana badala ya hivi ilivyo sasa ambavyo muungano wa aina hii utahojiwa na kila kijana wa leo na wa kesho mwenye akili timamu. Hii haitaleta afya ya muungano siku zijazo wakati wazee wote wanaoijua siri ya muungano watakapokuwa wameondoka duniani.
Absolutely
 
Kuna uwezekano hakutakuwa na nchi inayoitwa tanzania miaka 50 ijayo....maana matatizo sugu hayatatuliki yapo tu...wameyafumbia macho
Wale wazee wanaofahamu kuwa Nyerere alikusudia munngano wa aina gani na Karume alitaka muungano wa aina gani wamekaa kimya kwa faida zao binafsi. Lakini kwavyovyote vile maswali yataendelea kuulizwa na wajukuu, vitukuu na vilembwe vyao, na wakiendelea kukosa majibu watajaza majibu yao watakayoona ni sawa kwa usawa (unguided).
 
Wanasiasa ndio wanaotuzubaisha sisi raia tunaotaka full muungano. Hata Mzee karume Kuna siku alisemaga Afrika yote inahitaji kuungana kuwa nchi moja, sisi Tanzania muungano wetu umeshaenda mbele nusu na robo, bado robo moja TU kukamilisha full muungano. Sasa tangu afariki sisi tuliobaki tushindwa kumalizia Ile robo ya safari aliyoiacha.
 
Tusiongelee UK, US na miungano mingine, bali tujikite kwenye huu wa kwetu. Kuna shida gani itatokea kama serikali ya zanzibar itafutwa pia kama ile ya Tanganyika? Maana mpaka sasa hakuna sababu ya kumezana, hakuna mtu anaweza kumeza wala kuwahamisha wazanzibar kwenye makazi na majumba yao kama serikali ikiwa moja.

Shida ni kuwa Zanzibar haipo tayari kufuta serikali yao, kwahiyo muamue either iendelee kukuepo au muvunje muungano
 
Kabla hujafikia hitimisho hilo, ungejishughulisha kujua kwanini kuna aina tofauti tofauti za miungano. Mwanadamu ni yule yule na sababu ni zile zile. Usifikuri sababu za UK, US, USSR, SPAIN, FRANCE na kwingine ni tofauti na za Tanganyika na Zanzibar.
👌👍👏👊🤝🙏🆒
 
Manufaa ya muungano tumeyaona, ni matamu sana kwa watanzania walio wengi. Kila kijana mzanzibar anatamani kwenda kuishi Tanzania bara, na wako watanzania bara ambao wanatamani kwenda Zanzibar kwasababu moja au nyingine

Manufaa ya muungano tumeyaona wewe na nani ???

What a freaking Tanzania Baran dunderhead
 
Back
Top Bottom