Hivi sasa nipo katika moja ya nchi za kiarabu, nimefurahi kuona wao bado wanaendeleza utamaduni ambao tulikuwa nao hapo zamani Africa na sasa tunauacha. Majuzi rafiki yangu mmoja anasema alimpeleka mpwawe kwenda kuona mchumba aliyechaguliwa na wazazi, na mambo yote yamewekwa sawa. Ikanikumbusha mbali kipindi hicho nasi tulikuwa tukichaguliwa wachumba, lakini aah! mbona wazazi wetu waliishi tena vizuri tu na miaka mingi bila kuachana. Sisi leo tunajichagulia wenyewe wachumba hata mwaka bado kila mtu na lake, naamini baada ya kupewa mke/mume kikubwa kinakuwa huyu ndiye mwenzangu ktk hali zote. Muungano wetu unafanana na wanandoa waliooana kwa ridhaa ya wazazi, mzee wetu Karume na mzee wetu Nyerere waliamua kwa niaba yetu kama inavyosemwa na wengi. Lakini kama ndoa muungano ni kitu kizuri, iwe tumeungana kwa ridhaa na maoni yetu wenyewe au kuunganishwa kama ilivyo sasa. Kinachoonekana wenzetu wengi wa visiwani hawapendelei kuwa ktk huu muungano, na kila kasoro itakayoonekana wataitumia hiyo kuonyesha kuwa muungano si sawasawa. Nifahamuvyo mimi si kwamba bara hatuzioni hizi kasoro la, ila cha thamani ni kipi muungano au kasoro?. Kawaida vinapoungana vitu viwili kuzaa kimoja, vitu hivyo hupoteza asili yake na huo ndio muungano. Huwezi kuungana halafu ukawa tena bado vile vile, huo hautakuwa muungano ni ushirikiano. Hadithi hii nzima inanikumbusha nyumba ya rafiki yangu mmoja tuliyeshibana sana, kipindi alichooa alipata taabu sana. Mke kila leo kwao, nini mama kaniita, kesho kuna hili nyumbani, keshokutwa sababu hii. Alipata taabu kweli, alijaribu kutafuta msaada wa ushauri ikashindikana, na bahati mbaya ni ndoa ya kikristo akawa hana jinsi tena. Nyumba iliyumba sana, kwa sababu tu binti alijiona ana kwao. Hakuwa anajali lolote linaloweza kutokea kwa kuwa mama yupo, ikatokea bahati mbaya mama yake akafariki dunia ikawa safari za kwenda kwa mama zimekufa tena. Huwezi kuamini binti akatulia kweli, nyumba imekuwa na amani na sasa hata maendeleo yanaonekana, maana wanashirikiana. Inaonekana ndugu zetu wa Zanzibar wanaamini bado wanaye mama wa kumkimbilia, wanaamini kama si huu muungano saa hizi wangekuwa mbali, Mama angeshawasaidia. Kwa mwelekeo huu watakapotambua kuwa mama waliyefikiria kuwa yupo hayupo wamechelewa. Kilichotakiwa ni kutambua kuwa sisi ni ndugu na hawa wazee wetu hawakukosea kutuunganisha, kwani wameunganisha ndugu. Inaweza kuonekana walikuwa na sababu zao, lakini haitabadilisha undugu wetu. Hata tukiamua kuwa leo basi kila mtu ashike njia yake bado tutakuwa ndugu tu, ingewezekana kabisa kuwalazimisha viongozi wetu waweze kushuhughulikia kasoro zilizopo maana hakuna asiyeziona lakini kwanza iwepo nia. Na nia ni je tunautaka muungano au hatuutaki?, hizi sababu haziwezi kufanya muungano ukaonekana ni kitu kibaya hivi. Hebu fikiria wale waliooana kwa mapenzi ya wazazi, unafikiri hawakuti kasoro?. Inakuwa ni siri yao, kwao kikubwa ni ndoa yao na ndio maana wazee wetu zamani waliweza kuishi mpaka kifo ndio kikawatenganisha. Kasoro zipo na zitaendelea kuwepo, wala zisiwe sababu, mseme tu kwamba jamani eeh! kila mtu achukue ustaarabu wake tumempata mama wa kutusaidia kutoka kwenye huu umaskini!. Tutawaelewa tu, wala msiwe na hofu.
Mwiba. Wewe ni shabiki na hamna jinsi ya kukufahamisha. Watu kama nyinyi ndiyo mnaochochea maandamano na vurugu lakini hamonekani mambo yanapoiva. Watanzania bara hawahitaji wazanzibari wawapiganie. Toka awali kila mkipigana, kuchinjana kimbilio lenu limekuwa bara. Sultan wenu alihifadhiwa na Nyerere wakati Kenya ilimkataa. Wakina Babu wote walipewa hifadhi na Nyerere. Nyerere na si Karume ndiye aliyedai kuwa Zanzibar ibakize identity yake. Sisi tulio bara kwa nia njema tumekubali identity ya utanzania. Hata hivyo, msidhanie hata siku moja kuwa bara watatoa machozi kama itaamuliwa kuwa kila upande uende inakojua. Kwetu sisi tofauti haitakuwa kubwa sana maana hatuna sehemu huko Zanzibar. Ni nyinyi ambao mmekuwa huru kuhamia, kuwekeza, kuoa, kulima na hata kugombea ubunge bara ndiyo mtakaoona tofauti. Ni nyinyi mtakaotakiwa kukabili tofauti zenu (mwarabu na mswahili, munguja na mpemba n.k) ndiyo mtakuwa na kazi. Kwa wengi wetu machogo tutapumua sigh of relief. Kama walivyosema wachina: kuwa mwangalifu unachomwomba mwenyezi maana anaweza akakupatia!
Haujui unachozungumza. Nchini India kuna jimbo linaitwa West Bengal. Hili jimbo lina Chief Minister wake na serikali yake. Lina lugha yake, kibengali, ambayo ni tofauti na kihindi. Kwa muda mrefu limekuwa likitawaliwa na chama cha kikomunisti tofauti na nchi ya India. Kina mipaka yake na wananchi wake wanajitambua (identify) kama wabengali. Lakini hata siku moja hautasikia wakijiita nchi. Wakiwa nje wao ni raia wa India na si West Bengal.
Uchumi wa jimbo la California ungeifanya kama ingekuwa nchi kuwa moja ya nchi tajiri sana duniani. Lina mtawala wake, Gavana Arnold. Lina identity yake ( watu wa California wanajiona tofauti na watu wa Arkansas n.k). Lina sheria zake ambazo ni tofauti na za nchi ya marekani. Zina mahakama zake, polisi wake n.k. Lakini nako hautasikia mtu anajitambulisha ni raia wa California. Uraia ni wa nchi ya marekani, full stop. Kwa mantiki hiyo hawawezi kuingia mikataba na nchi nyingine au kujiunga na Umoja wa Mataifa au kuwa na mabalozi wake n.k.
Soverignty mnayoidai kwa kigezo cha kuwa nchi ni hiyo ya kuwapa mamlaka ya kutambuliwa kuwa mtofauti na nchi ya Tanzania. Kwa hali hiyo muweze kuingia mikataba na nchi nyingine, kujiunga na jumuia mnazotaka, kuwa na ubalozi na hatimae, ndiyo, uwezo wa kutangaza vita dhidi ya nchi nyingine. Hivi vyote ndivyo vinavyotofautisha utaifa na nchi na si hizo cultural issues ulizozingumzia. Kama alivyosema mwingine, mkipewa yote hayo basi hautakuwa muungano bali ushirikiano.
Kwa nini tumlipe na kumpa vibwagizo vyote Rais ambaye hana manufaa yeyote kwetu? Kama Tanganyika na Zanzibar zitakuwa na full sovereignty, huyo Rais wa Tanzania atakuwa wa nini? Nchi zenye ceremonial President ni nchi ambazo the federal government ina nguvu. Nchi kama India, inajulikana wazi ni nani mwenye mamlaka kati ya prime Minister na Chief Ministers wa states. Prime Minister wa Great Britain ana nguvu kuliko viongozi wa serikali za Wales, Scotland na Northern Ireland. Mfumo wa kupokezana uongozi walijaribu Yugoslavia na wote tunajua hatma yake. Ukweli ni kuwa either tuwe na Muungano wenye strong federal government au kila mmoja achukue hamsini zake.
Raza ni mtu hatari sana kwa swababu akili yake haijafikia upeo wa kujua uzito wa kitu anachokijadili. Anatakiwa kudhibitiwa haraka iwezekanavyo, la sivyo, harakati za Wazanzibari zitaonekana zina lengo baya
Nafikiri mtu wa hatari pengine ungekuwa wewe kwani Mwiba anatowa maoni yake na wala hachochei kama unavyodai. Kama uchochezi basi tusingekuwa tukijadili ufisadi na uozo mwengine. Wewe una haki yako ya kutowa mawazo yako na hivyo hivyo Mwiba na kinachojionesha ni kuwa kuna tofauti za pande mbili . Ufumbuzi si kupakana uchochezi wala kutishana bali ni kukaa na kujadili lipi la kufanywa ili kila upande uridhike na hilo likishindikana itakuwa Muungano hauna maana na MIND YOU Zanzibar itasurvive na itakushangaza.
Nimeiweka hii thread ili kuwatahadharisha ndugu zangu Wazanzibar na athari ya maneno hayo wanyoongea. Hasa huyo Raza na Shamhuna. Wasidhani kuwa kwa kuuvunja muungano watapanda vyeo au kuwa maarufu zaidi. Wajue kuwa hofu ile ile iliyofanya Mzee Karume akaamua kuungana na Tanganyika wakati ule ipo mpaka leo. Wajue kuwa mhimili mkubwa unaofanya Zanzibar kuna amani (hata hiyo kidogo iliyopo) ni huu Muungano. Kinyume chake watachinjana kama kuku. Wanalijua hilo ila ni kiburi chao tu.
Ndugu zangu watanzania na wazanzibari wenzangu naomba tuyapuuzie maneno ya Raza kwani hayaoneshi kujenga zaidi ya kubomoa.
Wanzazibari wa kawaida kabisa wamekuwa na mahusiano mema na ndugu zao wa bara kwa muda mrefu sana hata kabla ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Ni vema basi tukaona maslahi ya jamii zetu yanalindwa kwa ajili ya vizazi vijavyo na wala si vinginevyo. Tutayarishe ardhi hii ( Jamhuri ya Muungano wa Tanzania) iwe ni mahali pazuri kwa ajili ya watoto wetu. Tamaa zetu tuziweke nyuma maslahi ya taifa tuyape kipaumbele.
Leo hii sisi vijana wa Bara na Visiwani tunaishi kama ndugu moja, tumekwenda shule pamoja, tunafanya kazi pamoja na isitoshe hata familia pia tumezijenga bila ya kuzingatia maeneo tunayotoka. Sasa kwa Raza ambaye fikra zake ni kubomoa zaidi basi hatutakii mema.
Ni vema matatizo ambayo yanajitokeza kama haya tuwaachie wataalam wayazungumze na wayamalize lakini hakuna haja ya kuleta ushabiki usio kuwa na maana.
Nashindwa kufahamu Quote yako inaiacha na kurukia point nyengine. Hebu Challenge asili ya Muungano Wa Tanzania na hiyo mifano unayoieleza. Pia hebu tupe ushauri wako wa nini Zanzibar ifanye ili kuwapatia Wananchi wake Huduma. Na jee uko tayari kuitaka hiyo Soverignity iihudumie Zanzibar kwa kila hali kwa vile Zanzibar si nchi?
hicho unachokiongelea ambacho nimeki highlight kimetokezea baada ya mfumo huu wa muungano kuilazimisha zanzibar lazima iwe dependent kwa tanganyika in other way unaweza ukasema system ya muungano inamfanya tanganyika awe mtawala wa kiuchumi wa zanzibar. same thing imetokezea kwa kila nchi iliotawaliwa aidha kisiasa ,kimabavu,kiuchumi au hata kiutamaduni.mfano mzuri ni wa irish wengi walioivamia uingereza na kuwekeza wakati wakitawaliwa na muingereza na walipokubali kujipapatua nadhani unaiona ireland sasa inavyojiimarisha kiuchumi. hivyo kwa hilo usiwalaumu wazanzibari ulaumu mfumo tegemezi wa muungano wetu. itakumbukwa pia kwamba zanzibar ilipokuwa ikizitawala sehemu kadhaa za afrika mashariki basi makabila mengi ya kiafrika na ya kigeni yaliwekeza ndani ya zanzibar na hii haikuwa sababu ya kuporomoka kwao wakati zanzibar walipoporomoka.Mwiba. Wewe ni shabiki na hamna jinsi ya kukufahamisha. Watu kama nyinyi ndiyo mnaochochea maandamano na vurugu lakini hamonekani mambo yanapoiva. Watanzania bara hawahitaji wazanzibari wawapiganie. Toka awali kila mkipigana, kuchinjana kimbilio lenu limekuwa bara. Sultan wenu alihifadhiwa na Nyerere wakati Kenya ilimkataa. Wakina Babu wote walipewa hifadhi na Nyerere. Nyerere na si Karume ndiye aliyedai kuwa Zanzibar ibakize identity yake. Sisi tulio bara kwa nia njema tumekubali identity ya utanzania. Hata hivyo, msidhanie hata siku moja kuwa bara watatoa machozi kama itaamuliwa kuwa kila upande uende inakojua. Kwetu sisi tofauti haitakuwa kubwa sana maana hatuna sehemu huko Zanzibar. Ni nyinyi ambao mmekuwa huru kuhamia, kuwekeza, kuoa, kulima na hata kugombea ubunge bara ndiyo mtakaoona tofauti. Ni nyinyi mtakaotakiwa kukabili tofauti zenu (mwarabu na mswahili, munguja na mpemba n.k) ndiyo mtakuwa na kazi. Kwa wengi wetu machogo tutapumua sigh of relief. Kama walivyosema wachina: kuwa mwangalifu unachomwomba mwenyezi maana anaweza akakupatia!
kwangu mimi hii ni siasa ya propaganda, karume hakuamua kuungana kwa hilo unalolielezea , jaribu kuisoma tena historia ya zanzibar,. wazanzibari ni watu wa amani sana kama hawajatiwa vijiti vya maskio. ni mzanzibari ambae nimeishi zanzibar na kuiona hali halisi ya zanzibar na sio kuisoma magazetini.Nimeiweka hii thread ili kuwatahadharisha ndugu zangu Wazanzibar na athari ya maneno hayo wanyoongea. Hasa huyo Raza na Shamhuna. Wasidhani kuwa kwa kuuvunja muungano watapanda vyeo au kuwa maarufu zaidi. Wajue kuwa hofu ile ile iliyofanya Mzee Karume akaamua kuungana na Tanganyika wakati ule ipo mpaka leo. Wajue kuwa mhimili mkubwa unaofanya Zanzibar kuna amani (hata hiyo kidogo iliyopo) ni huu Muungano. Kinyume chake watachinjana kama kuku. Wanalijua hilo ila ni kiburi chao tu.
udugu wetu utazidi mapenzi na nguvu kama muungano huu utatenda haki sawa kwa nchi hizi 2 zilizoungana.Ndugu zangu watanzania na wazanzibari wenzangu naomba tuyapuuzie maneno ya Raza kwani hayaoneshi kujenga zaidi ya kubomoa.
Wanzazibari wa kawaida kabisa wamekuwa na mahusiano mema na ndugu zao wa bara kwa muda mrefu sana hata kabla ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Ni vema basi tukaona maslahi ya jamii zetu yanalindwa kwa ajili ya vizazi vijavyo na wala si vinginevyo. Tutayarishe ardhi hii ( Jamhuri ya Muungano wa Tanzania) iwe ni mahali pazuri kwa ajili ya watoto wetu. Tamaa zetu tuziweke nyuma maslahi ya taifa tuyape kipaumbele.
Leo hii sisi vijana wa Bara na Visiwani tunaishi kama ndugu moja, tumekwenda shule pamoja, tunafanya kazi pamoja na isitoshe hata familia pia tumezijenga bila ya kuzingatia maeneo tunayotoka. Sasa kwa Raza ambaye fikra zake ni kubomoa zaidi basi hatutakii mema.
Ni vema matatizo ambayo yanajitokeza kama haya tuwaachie wataalam wayazungumze na wayamalize lakini hakuna haja ya kuleta ushabiki usio kuwa na maana.