Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na kero zake: Je, tuuvunje?
jamani mimi nakubaliana na Mwanakijiji kwamba hiyo HIMAYA ya ZNZ iliyokuwa imepiga hatua kubwa ya maendeleo ilijengwa kwa jasho na damu ya WATUMWA kutoka TANGANYIKA.

Yuko aliyedai kwamba kuna baadhi ya watawala wa ZNZ walikuwa wa mzao wa watumwa. Mimi naomba kuelekezwa SULTANI mmoja tu wa ZNZ ambaye BABA yake alikuwa MTUMWA.

Wakati tunaungana wote Tanganyika na ZNZ tulikuwa na hali nzuri ya kiuchumi. Sote kwasababu moja au nyingine tumeanguka kiuchumi. Itakuwa jambo la msingi kama tutajichunguza wenyewe, na kutafuta sababu za ndani, kwanini, Tanganyika, au ZNZ, imeanguka kiuchumi, na kudorora kimaendeleo.

Tumekuwa tukisikia habari za ZNZ kuilalamikia TRA kwamba ndiyo "mchawi" aliyeua uchumi wa ZNZ. Lakini hii TRA imeanza kazi mwaka 1995/96. Sote tunaelewa kwamba hata kabla TRA kuanzishwa hali haikuwa nzuri ZNZ. Kinachoshangaza hakuna anayehoji suala hilo.

Wazanzibari wajichunguze wenyewe, badala ya kulalamikia kwamba kila tatizo walilonalo limetokana na muungano na Watanganyika.

Utakuwa unakosea maana Zanzibar ilikuwepo mwanzo kabla ya Tanganyika hivi ni nani mwalimu wako wa somo la historia ,kamuulize mipaka ya Zanzibar ,hivyo inawezekana kabisa kuwa wewe mwanzo ulikuwa Mzanzibari na badala yake ukabatizwa. Sasa wewe ndio wa kujichunguza.
 
Halafu kwasababu wana ccm wa zanzibar nao wanakubaliana na wale wa cuf pamoja na baadhi wa bara...Basi Zenji itakuwa nchi na mafisadi wakivuka mpaka huko kisiwani wakiwaachia bara yenu wakiwapa Tanganyika mtafanya nini?

Maana kama wakisaini pacts na nchi ya Zanzibar ambayo itakuwa Taifa la kiarabu..BASI WAKIVUKA MPAKA WAKIINGIA HAPO ZANZIBAR HAUWAGUSI WALA NINI...Say wakikubaliana na cuf na wahafidhina wengineo wa ccm kuwa wapewe zenji kwa masharti ya kuwaminya Tanganyika wasiwashitaki...Kwa hiyo ni bora mkae mzungumze ama muwape chao.

Maana ikiwa collaboration ya NRA-CUF-CCM....Basi ngoma ntolee.

Kwanza kusema Zanzibar ni waarabu ni kosa la Jinai .bara kuna waarabu wengi kuliko Zanzibar,mfano Shinyanga,Sumbawanga,Tabora Tanga na Daresalaam.
Naona Kikwete asipokazana basi hamalizi hiki kipindi chake kilichobakia ,kama Zanzibar watafanikiwa kuipapatua Tanganyika ndani ya Muungano basi itabidi ufanyike uchaguzi mwengine wa Tanganyika kitu ambacho hakijawahi kufanyika toka ipate uhuru ,pengine Kikwete akabakia kwa muda ili kuruhusu kipindi cha Uchaguzi.
 
ni wakati ambao wazanzibari wanalazimika kusahau tofauti zao za kivyama na kuungana katika kutetea taifa kwanza. sina chuki na ndugu zangu wa tanganyika lakini tunachokipigania hapa sio maslahi ya zanzibar tu bali maslahi ya pande mbili za muungano. usawa lazima upatikane baina ya mataifa 2 haya ambayo yalikuwa huru na yakaungana kwa lengo la kusaidiana na sio kukandamizana. sijaenda shule lakini hii hainifanyi kukubali kuburuzwa.mungu ibariki zanzibar ,mungu ibariki tanganyika , mungu ibariki tanzania.
 
Halafu kwasababu wana ccm wa zanzibar nao wanakubaliana na wale wa cuf pamoja na baadhi wa bara...Basi Zenji itakuwa nchi na mafisadi wakivuka mpaka huko kisiwani wakiwaachia bara yenu wakiwapa Tanganyika mtafanya nini?

Maana kama wakisaini pacts na nchi ya Zanzibar ambayo itakuwa Taifa la kiarabu..BASI WAKIVUKA MPAKA WAKIINGIA HAPO ZANZIBAR HAUWAGUSI WALA NINI...Say wakikubaliana na cuf na wahafidhina wengineo wa ccm kuwa wapewe zenji kwa masharti ya kuwaminya Tanganyika wasiwashitaki...Kwa hiyo ni bora mkae mzungumze ama muwape chao.

Maana ikiwa collaboration ya NRA-CUF-CCM....Basi ngoma ntolee.


Hivi wewe jamaa mbona mdini sana!!
 
Unaona mnavyokwenda kombo na kujichanganya, nani alisema Muungano Uvunjwe ,tatizo mnaogopa kusawazisha mambo ili yaendane na MKATABA wa Muungano,mnalazimisha mambo ambayo hayamo na yameingizwa kinguvunguvu tu.Mkataba wa Muungano ni Sheria mama ambayo haitaki kuchezewa hata kidogo,na kubadilishwa badilishwa mambo ambayo hayakuafikiwa wala kujadiliwa na pande zinazohusika na pia kama mlikuwa mnakubaliana ,tuchukulie hivyo hivyo kinyemela basi mlikuwa muwakilishe mabadiliko hayo kwenye Umoja wa Mataifa ambako ndiko kwenye kukubaliwa,tunaambiwa kwamba baada ya makubaliano ambayo ni hayo yajulikanayo kama Mkataba wa Muungano kulipigwa kura huko umoja wa Mataifa kama kuna pingamizi lakini bahati ilikuwa nzuri hakuna pingamizi ila kuna nchi moja haikupiga kura au tunaweza kusema kura moja iliharibika.
Sasa haya yote mliyoyachomekea hayajulikani ndani ya Mkataba wa awali na ndio tatizo lilipo jikita.
Na kwa asili hiyo hata atakaezaliwa baada ya miaka 100 basi atakuwa na haki ya kuchambua na kuhakiki na kuzusha madai ya Muungano huu.kusema Wazanzibari hawautaki Muungano kwa kweli sio sahihi kabisa ,nchi mbili zimeungana sawasawa ,mambo ya kusema sisi wengi tuchukue kikubwa hilo halimo,tumeungana with equal rights no one is above the other side,sasa inapotokea mmoja kutaka au kuchota ziada sio kosa ikiwa tu makubaliano yanafuatwa na kwa mchujo huo hayo yatakuwa maridhiano na yanaweza kubadilika kutokana na hali ya kila msimu,nimesema ni maridhiano lakini linaloonekana leo sio maridhiano bali ni magube au mabavu au wizi.
Nani atakubali upumbavu huo ? Tanganyika lazima irudi kama mnaoona aibu ni hiari yenu lakini Zanzibar inahitaji haki na rights zake zote kuheshimiwa kama Nchi husika katika muungano.
Kinachofanywa na Serikali ya Tanganyika ambayo imejivisha koti la Muungano ni ucowboy mnapanga kuiba pamoja mkishafanikiwa unamuua mwenzio.
Tokea Muungano huu ulipoundwa haijawahi kutokea Mzanzibari kuwa Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na hapa ndipo pia inapoongezeka ile dhana ya kuwepo Tanganyika ndani ya koti la Muungano na sasa ndio kabisa WaZanzibari wameshapoteza hata ile nafasi ya Raisi wao awe ni Makamo wa Kwanza wa Raisi ,yaani ukiangalia japo haitaleta maana sana lakini ile status ya umoja itapatikana,eti wameondoa kwa kusema kama Chama kimoja kitashinda nafasi ya Jamhuri na Upinzani utashinda Zanzibar itakuwaje ? Mnasahau kuwa unapokuwa Raisi unapoteza nafasi ya kushughulikia Chama na mambo yako yanatakiwa yawe ya Kitaifa japo ni mwenyekiti wa Chama fulani,unatakiwa ufiche sura ya Chama na kuvaa sura ya Utaifa kwa wananchi wote ,ila bado CCM wanaona wao ndio wenye hati miliki ya Nchi mbili hizi ,Napiga mbiu ya mgambo Tanganyika lazima irudi.
Good try. Hamna cha Zanzibar kutaka heshima kama nchi wala nini. Tanzania ndio nchi iliyopo pekee, la sivyo gombea kuvunja muungano, vinginevyo ni unpractical. Zanzibar si nchi tena na hilo ndio fanikio kubwa la dudu CCM, baba wa ASP na TANU. Hapo patamu, ama jaribu kuua CCM visiwani.
 
Tatizo la Zanzibar ni Karume na siyo CUF wala CCM. Karume anafikiri yeye ni mtoto wa King na CCM wamefanya makosa kumuweka huyu jamaa kwani ataipeleka Tanzania pabaya.
 
Tatizo la Zanzibar ni Karume na siyo CUF wala CCM. Karume anafikiri yeye ni mtoto wa King na CCM wamefanya makosa kumuweka huyu jamaa kwani ataipeleka Tanzania pabaya.

No, tatizo la Zenji sio Karume. Tatizo la Zenji ni Maalim Seif Shariff Hamad. Itakumbukwa kuwa baada ya Karume kuwa-assassinated mwaka 72 na Jumbe kuchukua ofisi, kuliwa na hali ya kuhitilafiana kati ya Jumbe na Mwl kuhusu suala zima la muundo wa muungano (Jumbe akitaka kuwepo serikali 3, na Mchonga aking'ang'ania zibaki 2), the same guy, Seif, alikuwa wa kwanza kumtuhumu/sell-out Jumbe—kuwa anataka kuvunja muungano. This Shariff guy is a sole looser! Mroho wa madaraka, pia! Leo anataka kujitenga na bara, kesho atataka kujitenga na unguja.
 
Nilichopata katika pekua pekua...
10ibejk.jpg

epm1e9.jpg

16ljmh1.jpg
 
No, tatizo la Zenji sio Karume. Tatizo la Zenji ni Maalim Seif Shariff Hamad. Itakumbukwa kuwa kipindi Jumbe na Mwl (in the mid-60s) walipokuwa na tofauti za waziwazi kuhusu hili suala zima la muungano (Jumbe akitaka kuwepo serikali 3, na Mchonga aking'ang'ania zibaki 2), the same guy, Seif, alikuwa wa kwanza kumtuhumu/sell-out Jumbe-kuwa anataka kuvunja muungano. This Shariff guy is a sole looser! Mroho wa madaraka, pia! Leo anataka kujitenga na bara, kesho atataka kujitenga na unguja.

Sasa unataka tukuone umezungumza ukweli ,tatizo la Zanzibar kama ulivyosema sio Karume na vilevile sio Seif ,hayo ya Jumbe yanaingia katika politics au political game na propaganda zinaweza kuwa zina ukweli au zimejaa majungu ,wanasiasa wanafahamiana si inasemwa siasa ni mchezo mchafu au ni rafu tupu ,sasa mchezo huu umeingia kikamilifu kwenye Muungano na ndio unachezwa. yaani mechi ipo uwanjani.
Umemtaja Nyerere ,ngoja nami nikueleze alivyosema Nyerere Muasisi wa Tanganyika,alisema siku moja mashoka yalikwenda msituni kutaka kuiingilia miti na kuikata kufika huko msituni miti ilichachamaa na haikuweza kukatwa ,Mashoka wakakutana wakapata shauri kuwa ili wafanikiwe kuikata miti ni lazima wapate mipini itokanayo na miti ambayo inapatikana hukohuko msituni,hivyo wakaingia kazini na kupata mipini mizuri sana,na kuanza kuingia msituni kuikata miti.
CCM wamekuwa wakiitawala Zanzibar kutokana na mipini hiyo ambayo ni Wazanzibari,Sisemi Tanganyika wameikalia Zanzibar kwani hivi sasa kuna vyama vingi matatizo haya yalianza tokea mfumo wa Chama kimoja ambacho kinaendelea kuikalia Tanganyika na Zanzibar kwa mabavu,sijui kwanza kama unakubalianza na hilo,Upinzani uliokuwepo Tanzania hauwezi kufanikiwa kama hawakuipapatua CCM katika umiliki wa nchi mbili hizi,ni lazima kwa hali yeyote ile CCM ipapatuliwe katika kuzikalia nchi mbili hizi kimabavu,na utajua kama nchi hizi zinakaliwa kimabavu na kikundi kikubwa kutokana na aina ya matatizo yanayo au yaliyomo ndani ya Tanzania ,ndani ya CCM kwa muda huu tulionao kuna matatizo kuna makundi kuna mitandao ukiangalia yote hayo na kuyapima utaona TANZANIA inaongozwa na makundi ya CCM wakati kila kundi likitaka kumkomoa mwenziwe ,usitegemee kuondokana na hali ya maisha duni na kupelekwa kwenye maisha bora,hiyo ni ndoto,Jakaya aliahidi kupambana na matatizo lakini sasa ni miaka mitatu hakuna mafanikio ambayo ameyapata na kila siku tunasikia wanakurupushana na vidole machoni , wanaogopana wanatishana na wanauwana, watu hawa CCM hawajali maisha ya Mtanganyika wala Mzanzibari ,hivyo kuendelea na Muungano au kuulinda Muungano ni kudanganyana na ni kuwapa nafasi mafisadi kuzidi kuzinyonya nchi mbili hizi kwa manufaa yao binafsi na kwa manufaa ya makundi yao.
Ikiwa maanadamano ya Zanzibar yatafanyika na kufanikiwa basi sehemu ya pili ya Maandamano itabidi yafanyike upande wa Tanganyika na ili kuwahi ni lazima vyama vya upinzani viandae maandamano makubwa kwa Tanganyika yote mara tu baada ya kumalizika yale ya Zanzibar kuidai Tanganyika ijivue ndani ya koti la Muungano ,na hata Mataifa ya nje hayatashangaa yataona ni ukweli ambao ulikuwa umejificha au umefichwa ,Tanganyika haikufa ipo ila serikali yake imetekwa na kundi ndani ya makundi ya CCM na kuifanya ionekane ya Muungano.
Ni lazima serikali hii ya Tanganyika ipapatuliwe na kuvuliwa ndani ya serikali ya Muungano na huo ndio utakuwa mwisho wa ukiritimba wa CCM dhidi ya nchi mbili hizi.
Nimekuwa nikijaribu kuonyesha kuwa Muungano hauna tatizo ila matatizo yapo katika uendeshaji na waendeshaji ambao ni CCM,hawa hawana wanalolifanya kwa faida ya nchi mbili hizi,hawa ni makundi yanaozimaliza nchi mbili hizi kwa faida yao binafsi na makundi yao,makundi haya yanapatikana ndani ya CCM ,kuipapatua Tanganyika ni kuyaanika makundi haya na kuyaweka pakavu ,sheria zitakuwa msumeno ,sheria zitafuatwa ,amri zitafuatwa na ukweli utakuwa sio siri tena, sasa hivi hakuna cha makubaliano ya mkataba,wala hati ya mkataba wala nani na nani walisaini mambo ni mbele kwa mbele lazima ziwepo serikali tatu.
Na sasa tupo kwenye wakati mzuri kwani vyama vyetu vya siasa vinaruhusika kufanya siasa katika Nchi zote mbili Tanganyika na Zanzibar ,Zanzibar ambayo inaendesha Uchaguzi wake tokea ipate uhuru haina kazi kubwa kukaa sawa ila Tanganyika kidogo itakuwa na kazi kwani haina Raisi wala waziri hawa mafisadi waliojikita ndani ya serikali ya Muungano wote watapoteza ulaji na kurudi katika Chama chao ambacho kitawapa wakati mgumu kutokana na makundi yaliomo ,makundi ambayo itabidi yasambaratike.
Muungano hauvunjwi hilo sina wasi wasi nalo ,ila Tanganyika ndio itakayorudishwa kama Nchi,kwani karibu vyama vyote vya upinzani vinakubaliana na serikali Tatu na vimeona hilo ni jambo muhimu,sasa ukiritimba wa Chama kimoja tu kutaka serikali mbili au moja ni jambo la kulitilia shaka.
CCM kama utawasikia siku hizi wamekazania anaetaka kuvunja Muungano ni haini ,anaesema Zanzibar ni Nchi nae pia ni haini ,naamini anaesema Tanganyika nayo ni Nchi huyo pia atachanganywa na kutiwa ndani ya kapu la uhaini ,hawa mafisadi wanatafuta pa kushika (Samahanini CCM mliokuwa si mafisadi ,tunamsemo wa kiswahili usemao akioza samaki mmoja basi wote watakuwa wameoza) ,CCM wanatafuta pa kushika ili kuendelea kuzikalia nchi mbili hizi na kuzitapeli.
Ni lazima vyama vya upinzani kushirikiana ili kuidaia Tanganyika hadhi yake kama nchi yenye serikali msiwaachie WaZanzibari peke yao kwa kuogopa kuitwa wahaini.
Tanganyika na Zanzibar zimetekwa na CCM ,hivyo vyama vilivyobakia ambavyo vina imani na kuwepo kwa serikali tatu ni lazima visimame kidete kupambana na CCM naamini kabisa vita hii tutashinda ,na hapo ndipo kutapatikana Katiba mpya itakuwepo kwa upande wa Tanganyika na vilevile kwa upande wa Zanzibar na vilevile kwa upande wa Muungano.
Lakini hivi vitisho vya CCM kuwaita watu wahaini wanapoulizia Nchi yao visikubalike ,na kama utachunguza kwa kina wanaolipinga suala hili na kulivalia njuga na kuwaita watu wahaini ni maneno kutoka Chama kimoja tu cha CCM , na Zanzibar wameshaanza kupigwa ngwara kwani wale woga waliomo ndani ya CCM huko Zanzibar sasa woga umeshawaondoka na kuona ukweli wa kuwa wanatawaliwa kimakundi na mafisadi waliojikita ndani ya CCM.
Mtanganyika unasubiri nini ungana na WaZanzibari kuipapatua Tanganyika ili tushinde vita dhidi ya mafisadi.
 
Sasa unataka tukuone umezungumza ukweli ,tatizo la Zanzibar kama ulivyosema sio Karume na vilevile sio Seif ,hayo ya Jumbe yanaingia katika politics au political game na propaganda zinaweza kuwa zina ukweli au zimejaa majungu ,wanasiasa wanafahamiana si inasemwa siasa ni mchezo mchafu au ni rafu tupu ,sasa mchezo huu umeingia kikamilifu kwenye Muungano na ndio unachezwa. yaani mechi ipo uwanjani.
Umemtaja Nyerere ,ngoja nami nikueleze alivyosema Nyerere Muasisi wa Tanganyika,alisema siku moja mashoka yalikwenda msituni kutaka kuiingilia miti na kuikata kufika huko msituni miti ilichachamaa na haikuweza kukatwa ,Mashoka wakakutana wakapata shauri kuwa ili wafanikiwe kuikata miti ni lazima wapate mipini itokanayo na miti ambayo inapatikana hukohuko msituni,hivyo wakaingia kazini na kupata mipini mizuri sana,na kuanza kuingia msituni kuikata miti.
CCM wamekuwa wakiitawala Zanzibar kutokana na mipini hiyo ambayo ni Wazanzibari,Sisemi Tanganyika wameikalia Zanzibar kwani hivi sasa kuna vyama vingi matatizo haya yalianza tokea mfumo wa Chama kimoja ambacho kinaendelea kuikalia Tanganyika na Zanzibar kwa mabavu,sijui kwanza kama unakubalianza na hilo,Upinzani uliokuwepo Tanzania hauwezi kufanikiwa kama hawakuipapatua CCM katika umiliki wa nchi mbili hizi,ni lazima kwa hali yeyote ile CCM ipapatuliwe katika kuzikalia nchi mbili hizi kimabavu,na utajua kama nchi hizi zinakaliwa kimabavu na kikundi kikubwa kutokana na aina ya matatizo yanayo au yaliyomo ndani ya Tanzania ,ndani ya CCM kwa muda huu tulionao kuna matatizo kuna makundi kuna mitandao ukiangalia yote hayo na kuyapima utaona TANZANIA inaongozwa na makundi ya CCM wakati kila kundi likitaka kumkomoa mwenziwe ,usitegemee kuondokana na hali ya maisha duni na kupelekwa kwenye maisha bora,hiyo ni ndoto,Jakaya aliahidi kupambana na matatizo lakini sasa ni miaka mitatu hakuna mafanikio ambayo ameyapata na kila siku tunasikia wanakurupushana na vidole machoni , wanaogopana wanatishana na wanauwana, watu hawa CCM hawajali maisha ya Mtanganyika wala Mzanzibari ,hivyo kuendelea na Muungano au kuulinda Muungano ni kudanganyana na ni kuwapa nafasi mafisadi kuzidi kuzinyonya nchi mbili hizi kwa manufaa yao binafsi na kwa manufaa ya makundi yao.
Ikiwa maanadamano ya Zanzibar yatafanyika na kufanikiwa basi sehemu ya pili ya Maandamano itabidi yafanyike upande wa Tanganyika na ili kuwahi ni lazima vyama vya upinzani viandae maandamano makubwa kwa Tanganyika yote mara tu baada ya kumalizika yale ya Zanzibar kuidai Tanganyika ijivue ndani ya koti la Muungano ,na hata Mataifa ya nje hayatashangaa yataona ni ukweli ambao ulikuwa umejificha au umefichwa ,Tanganyika haikufa ipo ila serikali yake imetekwa na kundi ndani ya makundi ya CCM na kuifanya ionekane ya Muungano.
Ni lazima serikali hii ya Tanganyika ipapatuliwe na kuvuliwa ndani ya serikali ya Muungano na huo ndio utakuwa mwisho wa ukiritimba wa CCM dhidi ya nchi mbili hizi.
Nimekuwa nikijaribu kuonyesha kuwa Muungano hauna tatizo ila matatizo yapo katika uendeshaji na waendeshaji ambao ni CCM,hawa hawana wanalolifanya kwa faida ya nchi mbili hizi,hawa ni makundi yanaozimaliza nchi mbili hizi kwa faida yao binafsi na makundi yao,makundi haya yanapatikana ndani ya CCM ,kuipapatua Tanganyika ni kuyaanika makundi haya na kuyaweka pakavu ,sheria zitakuwa msumeno ,sheria zitafuatwa ,amri zitafuatwa na ukweli utakuwa sio siri tena, sasa hivi hakuna cha makubaliano ya mkataba,wala hati ya mkataba wala nani na nani walisaini mambo ni mbele kwa mbele lazima ziwepo serikali tatu.
Na sasa tupo kwenye wakati mzuri kwani vyama vyetu vya siasa vinaruhusika kufanya siasa katika Nchi zote mbili Tanganyika na Zanzibar ,Zanzibar ambayo inaendesha Uchaguzi wake tokea ipate uhuru haina kazi kubwa kukaa sawa ila Tanganyika kidogo itakuwa na kazi kwani haina Raisi wala waziri hawa mafisadi waliojikita ndani ya serikali ya Muungano wote watapoteza ulaji na kurudi katika Chama chao ambacho kitawapa wakati mgumu kutokana na makundi yaliomo ,makundi ambayo itabidi yasambaratike.
Muungano hauvunjwi hilo sina wasi wasi nalo ,ila Tanganyika ndio itakayorudishwa kama Nchi,kwani karibu vyama vyote vya upinzani vinakubaliana na serikali Tatu na vimeona hilo ni jambo muhimu,sasa ukiritimba wa Chama kimoja tu kutaka serikali mbili au moja ni jambo la kulitilia shaka.
CCM kama utawasikia siku hizi wamekazania anaetaka kuvunja Muungano ni haini ,anaesema Zanzibar ni Nchi nae pia ni haini ,naamini anaesema Tanganyika nayo ni Nchi huyo pia atachanganywa na kutiwa ndani ya kapu la uhaini ,hawa mafisadi wanatafuta pa kushika (Samahanini CCM mliokuwa si mafisadi ,tunamsemo wa kiswahili usemao akioza samaki mmoja basi wote watakuwa wameoza) ,CCM wanatafuta pa kushika ili kuendelea kuzikalia nchi mbili hizi na kuzitapeli.
Ni lazima vyama vya upinzani kushirikiana ili kuidaia Tanganyika hadhi yake kama nchi yenye serikali msiwaachie WaZanzibari peke yao kwa kuogopa kuitwa wahaini.
Tanganyika na Zanzibar zimetekwa na CCM ,hivyo vyama vilivyobakia ambavyo vina imani na kuwepo kwa serikali tatu ni lazima visimame kidete kupambana na CCM naamini kabisa vita hii tutashinda ,na hapo ndipo kutapatikana Katiba mpya itakuwepo kwa upande wa Tanganyika na vilevile kwa upande wa Zanzibar na vilevile kwa upande wa Muungano.
Lakini hivi vitisho vya CCM kuwaita watu wahaini wanapoulizia Nchi yao visikubalike ,na kama utachunguza kwa kina wanaolipinga suala hili na kulivalia njuga na kuwaita watu wahaini ni maneno kutoka Chama kimoja tu cha CCM , na Zanzibar wameshaanza kupigwa ngwara kwani wale woga waliomo ndani ya CCM huko Zanzibar sasa woga umeshawaondoka na kuona ukweli wa kuwa wanatawaliwa kimakundi na mafisadi waliojikita ndani ya CCM.
Mtanganyika unasubiri nini ungana na WaZanzibari kuipapatua Tanganyika ili tushinde vita dhidi ya mafisadi.

Mwiba umesema kweli tupu,

Kumbe ni Tanganyika ambayo inatakiwa kudaiwa kuwa ni nchi sio Zanzibar kama ambavyo watu wanaamini. I am waiting eagerly for my Tanganyika.

Njimba
 
No, tatizo la Zenji sio Karume. Tatizo la Zenji ni Maalim Seif Shariff Hamad. Itakumbukwa kuwa kipindi Jumbe na Mwl (in the mid-60s) walipokuwa na tofauti za waziwazi kuhusu hili suala zima la muungano (Jumbe akitaka kuwepo serikali 3, na Mchonga aking'ang'ania zibaki 2), the same guy, Seif, alikuwa wa kwanza kumtuhumu/sell-out Jumbe—kuwa anataka kuvunja muungano. This Shariff guy is a sole looser! Mroho wa madaraka, pia! Leo anataka kujitenga na bara, kesho atataka kujitenga na unguja.

Kamanda, Sio Jumbe wala Maalimu waliokuwa kwenye nyazifa za kuongea na Marehemu Nyerere katika miaka ya 60

Huu ni upotoshaji mkubwa wa historia ya Tanzania
 
No, tatizo la Zenji sio Karume. Tatizo la Zenji ni Maalim Seif Shariff Hamad. Itakumbukwa kuwa kipindi Jumbe na Mwl (in the mid-60s) walipokuwa na tofauti za waziwazi kuhusu hili suala zima la muungano (Jumbe akitaka kuwepo serikali 3, na Mchonga aking'ang'ania zibaki 2), the same guy, Seif, alikuwa wa kwanza kumtuhumu/sell-out Jumbe—kuwa anataka kuvunja muungano. This Shariff guy is a sole looser! Mroho wa madaraka, pia! Leo anataka kujitenga na bara, kesho atataka kujitenga na unguja.

Gustanza,

Hiyo ilikuwa early 80s na sio mid 60s
 
Tatizo la Zanzibar ni Karume na siyo CUF wala CCM. Karume anafikiri yeye ni mtoto wa King na CCM wamefanya makosa kumuweka huyu jamaa kwani ataipeleka Tanzania pabaya.

No, tatizo la Zenji sio Karume. Tatizo la Zenji ni Maalim Seif Shariff Hamad. Itakumbukwa kuwa kipindi Jumbe na Mwl (in the mid-60s) walipokuwa na tofauti za waziwazi kuhusu hili suala zima la muungano (Jumbe akitaka kuwepo serikali 3, na Mchonga aking'ang'ania zibaki 2), the same guy, Seif, alikuwa wa kwanza kumtuhumu/sell-out Jumbe—kuwa anataka kuvunja muungano. This Shariff guy is a sole looser! Mroho wa madaraka, pia! Leo anataka kujitenga na bara, kesho atataka kujitenga na unguja.
tatizo la zenji sio karume wala maalim seif, muasisi wa tatizo la zenji anajulikana takriban na wazenji wote ila huu mfumo wa sera za chama kimoja kutawala bara na visiwani (asp + tanu= ccm) ndio unaowafanya baadhi ya wazenji kuogopa hata kumtaja huyo mchawi wao ilhali wanamjua, aliasisi matatizo yanayoikabili zenji leo na sasa lililobaki ngoma ishapigwa na kilichosalia ni kwamba wazenji tunaicheza hiyo ngoma.lakini ipo siku! maneno ya kamando salmin.
 
Kamanda, Sio Jumbe wala Maalimu waliokuwa kwenye nyazifa za kuongea na Marehemu Nyerere katika miaka ya 60

Huu ni upotoshaji mkubwa wa historia ya Tanzania

You're right mkuu. Asante kwa kuona hilo kosa. Nimechanganya digits hapo juu (nita-edit baadaye). You know, wakati na-submit reply, kilichokuwa akilini mwangu ni digits za Muungano (you know 64 and...)

Ila Point niliyokuwa nataka ku-make hapa ni hii: baada ya Karume kuwa-assassinated mwaka 72, na Jumbe kuchukua ofisi; Jumbe alianza kuhitilafiana na Mwl kuhusu suala zima la muundo wa muungano (Serikali 3 au 2?). Kidampa Sharrif, akawa wa kwanza kumtuhumu Jumbe akidai kwamba--"Jumbe anataka kuvunja muungano."
 
tatizo la zenji sio karume wala maalim seif, muasisi wa tatizo la zenji anajulikana takriban na wazenji wote ila huu mfumo wa sera za chama kimoja kutawala bara na visiwani (asp + tanu= ccm) ndio unaowafanya baadhi ya wazenji kuogopa hata kumtaja huyo mchawi wao ilhali wanamjua, aliasisi matatizo yanayoikabili zenji leo na sasa lililobaki ngoma ishapigwa na kilichosalia ni kwamba wazenji tunaicheza hiyo ngoma.lakini ipo siku! maneno ya kamando salmin.

Ni kweli kabisa kuwa tatizo la Zanzibar si Seif wala Karume bali ni nguvu ya upande mmoja wa Muungano. Seif alitumiwa na Nyerere kumuangamiza Jumbe ambaye hapo awali alikuwa mjumbe mzuri wa matakwa ya Nyerere hadi alipobaini ukweli. Seif nae alitumiwa na Nyerere kwa wakati wake na ayeye allianza kubadilika mapema na hivyo akatemwa.
Karume yeye alipewa madaraka na Bara ili aendeleze maslahi ya Bara na bahati mbaya suala la Muwafaka likaleta mfarakano na hivyo anaonekana hafai kwa maslahi ya Bara nae kwa upande wake anataka aonyeshe nguvu zake.
Kitachowasaidia Wazanzibari ni harakati zao wenyewe na sio viongozi waliomo madarakani kwani wao huangalia maslahi yao. Nguvu za Wananchi ni uchaguzi wa 2010 na kwa bahati nzuri JAHAZI bado lipo!
 
Na Salma Said, Zanzibar .
Jeshi la Polisi Zanzibar limepinga kufanyika kwa maandamano ya Chama cha National Reconstruction Alliance (NRA) yenye lengo la kumpinga Waziri Mkuu Mizengo Pinda katika maandamano amabyo awali yalipewa kibali na jeshi hilo .
Sambamba na hilo Jeshi hilo limesisitiza agizo la awali la kutokuwepo kwa mabango ya aina yoyote yenye kuzungumzia Zanzibar nchi au si Nchi katika maandamano hayo amabyo yamepangwa kufanyika Agosti 10 Mjini Unguja.
"Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi ilipokea barua ya maombi ya maandamano ya chama cha NRA yenye kumbukumbu NRA/007/12/2008 ya tarehe 06 Agosti, 2008 baada ya kupokea barua hiyo Polisi tuliishughulikia katika taratibu zetu za kawaida baada ya viongozi wa NRA kuitwa na kuwapa maelekezo ambayo waliyakubali" ilisema barua hiyo ambayo Mwananchi imepata nakala yake.
Katika taarifa yake jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, Bakari Khatib Shaaban alisema Jeshi lake halijaruhusu maandamano yenye maudhui ya kumpinga Waziri Mkuu wala hoja ya Zanzibar kuwa nchi au si nchi.
"'Kwa hivyo basi taarifa zilizotolewa katika vyombo vya habari vinavyosema kwamba eti Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi wametoa ruhusa kwa Chama cha NRA ya kufanyika maandamano na mkutano ya kumpinga Mheshimiwa Waziri Mkuu Mizengo Kayanza Peter Pinda sio sahihi" Alieleza Kamanda Bakari katika barua yake yenye kurasa moja tu.
Kamanda Bakari pia alisema kwamba baada ya kupokea maombi ya Chama cha NRA katika barua yao ya Augosti 6 mwaka huu ilikaa pamoja na viongozi wa Chama hicho na kuwapa maelekezo ambayo waliyakubali ambayo yaliyowataka wafuasi wao kutobeba mabango ya aina yoyote yanayozungumzia Zanzibar ni Nchi au si Nchi.
Alisema kwamba pamoja na agizo hilo la kutobeba mabango hayo yenye ujumbe wa wowote pia wamekitaka Chama hicho katika mkutano wake na maandamano yao kutotumia lugha ya matusi kwa Serikali au Vyama vyengine vya Siasa vitavyoashiria fujo na kuhatarisha amani na utulivu uliopo hivi sasa.
"Kwa kuzingatia kifungu namba mbili na sita vinatoa taswira sahihi kuwa Polisi haijaruhusu maandamano na mkutano wenye maudhui yaliyotolewa na vyombo vya habari…Kama nilivyosema Kifungu cha sita kinawataka wasichukue mabango ya aina yoyote yanayozungumzia Zanzibar nchi au si nchi" Alisisitiza Kamanda Bakari.
Hata hivyo Kamanda Bakari alisema kwamba kimsingi Polisi imeruhusu kufanyika kwa maandamano yasiyokuwa na maudhuwi ya kumpinga Waziri Mkuu Mizengo Pinda pamoja na kuzungumzia Zanzibar ni nchi na si vyenginevyo.
Juzi Jeshi la Polisi kupitia Mkuu wa Polisi Wilaya ya Mjini Mkadam Khamis Mkadam lilitoa ruhusa kwa Chama Cha NRA kufanyika maandamano sanjari na kuwapa masharti ya kutochukua mabango ya aina yoyote katika maandamano yao ambayo yalipangwa kuanzia Komba wapya adi Kibanda Maiti na kuhutubiwa katika Uwanja wa Demokrasia.
Naibu Katibu Mkuu wa NRA, Suleiman Gaddafi amesema chama chake kimeshaandaa matayarisho ya maandamano hayo sanjari na kuwaalika viongozi mabli mbali wa vyama vyote vya kisiasa vilivyopewa usajili nchini na kimsingi wamekubali kushiriki katika maandamano hayo isipokuwa CCM ambao wametoa sababu ya kutoshiriki kutokana na suala hilo kushughulikiwa na serikali mbili.
---------------------------------------------------
Katika hatua nyengine Kampuni ya Legal Authoriesed For High Court Zanzibar, and Other Legal Matters Relating Thereto&Legal Consultants ya Ali Omar Juma imeliandikia Jeshi la Polisi barua ya kutaka kufanya mkutano na maandamano ya amani Visiwani hapa.
Kwa mujibu wa barua hiyo yenye kumbukumbu namba Z/20/35/120/VOL.16/08 ambayo ina orodha ya majina ya wateja hao wa mikoa mitano imesema "Kwa kuzingatia kuwa wateja wangu ndio viongozi wa maandamano hayo na mkutano wa hadhara na kuwa wanawakilisha wazanzibari wa mikoa mitano ya Zanzibar na kuwa wana haki ya katiba" imesema barua hiyo na kuongeza kwamba .
""Maandamano hayo yana lengo la kuunga mkono katiba ya zanzibar ya mwaka 1984 ibara ya 9(1),(2),(a),(b),(c) pamoja na kufnaya mkutano wa hadhara wenye lengo la kuweka wazi msimamo wao wa kutambua Zanzibar kuwa ni nchi kamili" imenukuu barua hiyo.
Kulingana na barua hiyo maandamano hayo yataanzia viwanja vya Demokrasia Kibanda Maiti, kupitia barabara za Mikunguni, Mwembeledu, Biziredi, Kariakoo, Michenzani Ksiwandui, Hailesellasie, Karume Housena kuishia Viwanja vya Mnazi Mmoja kwa ajili ya mkutano wa hadhara ambao utahutubiwa na viongozi hao wa mikoa mitano.
"Napenda kutoa taarifa kwa jeshi la polisi kutoa ushirikiano wa dhati kwa ajili ya kuruhusu maandamano na mkutano wa hadhara yenye lengo la kufikisha sauti zao aidha lolote linalohusiana na taarifa ya maandamano na mkutano wa hadhara ni vyema tukawasiliana kupitia ofisi yangu" imesema barua hiyo amabyo imesainiwa na Wakili Ali Omar Juma.
Suala la Zanzibar Nchi au si Nchi liliibuka Mjini Dodoma Juni 26 wakati Waziri Mkuu Mizengo Pinda kujibu swali ya ana kwa ana kwa wabunge ambapo Mbunge wa Chakwa Yahya Kassim Issa, alitaka kujua kwamba Zanzibar nchi au si nchi ndipo Waziri Mkuu alipojibu kwamba kwa mujibu wa Katiba, Zanzibar si nchi bali ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Majibu hayo ya Waziri Mkuu Pinda yaliibua mijadala mikali Visiwani Zanzibar ambapo Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar,Idd Pandu Hassan alisisitiza kwamba Zanzibar kuwa ni nchi huku akiungwa mkono wa baadhi ya wajumbe wa baraza la wawakilishi wa kambi ya upinzani na wale wa CCM kwa nyakati tofauti licha ya mjadala huo kupingwa marufuku zaidi ya mara mbili na Spika wa Baraza la Wawakilishi, Pandu Ameir Kificho kwamba usiendelee.
Julai 24 mwaka huu Naibu Waziri Kiongozi na Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Ali Juma Shamhuna pia aliwaambia wajumbe wa baraza hilo wakati akifanya majumuisho ya bajeti ya wizara yake alisema Zanzibar ni Nchi yenye mamlaka kamili na wakati wa kutishana umepitwa na wakati
-------------------------------------------------
MWISHO---
Hii ni barua ya mwisho iliyopatikana jioni jana inayohusu maandamano ya Jumapili.
"Kutokana na hali halisi iliyojitokeza katika vyombo vya habari kuhusiana na dhamira ya maandamano na mkutano wenu mliokusudia kuufanya siku ya jumapili ya tarehe 10 Agosti polisi mkoa wa mjini magharibi imebaini kwamba dhamira ya mkutano wenu huo haitakuwa kama tulivyokubaliana, aidha kwa taarifa zilizopo kwamba vyama vya vyote vya siasa mlivyovialika na wananchi wanaoshabikia kuwa zanzibar nchi au si nchi kuna uwezekano mkubwa wa kushiriki kwneye maandamano na mkutano wenu jambo ambalo jeshi la polisi halijajipanga kukabiliana na shughuli hiyo kwa siku hiyo, na kwa maana hiyo kuna dalili na ishara zote kuwa kutakuwepo na uvunjifu wa amani kwa msingi huo polisi mkoa wa mjini magharibi inazuia kufanyika kwa maandamano pamoja na mkutano mpaka hapo baadae" imesema barua hiyo yenye Kumbukumbu namba W/MJN/SO.72/A/108 iliyosainiwa na Mkuu wa Polisi Wilaya ya Mjini, Mkadam Khamis Mkadam kwenda kwa Naibu Katibu Mkuu wa NRA.
 
Yale yamezimwa kijanja ili kuruhusu haya yanayofuata mkondo wa Katiba ambao sio yatajumuisha Chama bali yameandaliwa kupitia Nchi Nzima ya Zanzibar na yamewahusisha watu wa mikoa yote iliyokuwepo Zanzibar,tofauti na maandamano ya mwanzo ambayo yalijikita kichama haya ni hatari zaidi katika kuipapatua Tanganyika maana wazalendo wote wa Zanzibar watatupa tofauti zao na kuwa kitu kimoja ,sijui lini waTanganyika nao wataungana na wezao wa Zanzibar kuidai Tanganyika ili kuwatokomeza mafisadi.
 
Yale yamezimwa kijanja ili kuruhusu haya yanayofuata mkondo wa Katiba ambao sio yatajumuisha Chama bali yameandaliwa kupitia Nchi Nzima ya Zanzibar na yamewahusisha watu wa mikoa yote iliyokuwepo Zanzibar,tofauti na maandamano ya mwanzo ambayo yalijikita kichama haya ni hatari zaidi katika kuipapatua Tanganyika maana wazalendo wote wa Zanzibar watatupa tofauti zao na kuwa kitu kimoja ,sijui lini waTanganyika nao wataungana na wezao wa Zanzibar kuidai Tanganyika ili kuwatokomeza mafisadi.


..yetu macho, tunasubiri tuyaone!
 
Tusubiri tuone lakini nafikiri na haya yatazimwa kwani tunasikia wawakilishi wa ccm wa baraza la wawakilishi wameshaitwa Dodoma hatujui safari hii watawatia nini maana wapo wazi Watangayika wasemalo wao wapo tayari kutii kama mbwa aloana chatu.
 
Back
Top Bottom