Wana JF tunatakiwa kuwa makini na watu wanaopost comment kama "MWIBA", watu kama hawa ambao wanashindwa kuchambua na kuelewa ukweli na pumba hatuwataki.
Mheshimiwa Mwakyembe amesema kweli tupu na kama tutapata watanganyika kama hao 50 ndani ya bunge letu mambo yengukuwa tofauti leo hii, nadhani hata Mheshimiwa rais angesema kwa sauti kubwa ZANZIBAR SIYO NCHI.
Huyu waziri wa zenji anakesi ya kujibu mbele ya watanganyika.
Mwiba: kama unachuki binafsi na Mwakyembe sema ili wana JF wakusaidie, tupo tayari kukurekibisha ili uende kwenye mstari.
Ana kesi ya kujibu mbele ya WaTanganyika iweje waTanganyika ? na Sio WaTanzania hivi unaelewa ya kwamba Tanganyika imezirai na Zanzibar bado inatuta ? Unaweza kukariri mstari ambao wewe unauona kuwa ni kweli tupu,halafu tuone kama Mwakyembe hakuvunja Katiba kwa kuzuia haki na kutaka Shamhuna asulubiwe ,maana ndivyo ilivyozoeleka ndani ya CCM ukisema ukweli unaitwa mhaini,unaitwa mpinzani unaonekana si mwenzetu ,unaekewa kikao na wafuata upepo wote wanakuzamisha kwa kuwa tu umepinga kauli,jamani mambo ya Ndio Mkuu yamepitwa na wakati wakuu wenyewe sasa hawajui hata dira ya Tanzania ilipoekea wanahitaji msaada wa hali ya juu na sio kila wanakotuongoza tuseme ndio huko huko mbele kwa mbele ,huu ni wakati wa kuekana sawa awe Raisi,Waziri Mkuu,au Waziri yeyote au kiongozi yeyote yule Jeshi au Polisi si wakati wa kunyamaziana na anapopingwa mtu wengine wakaruka na kusema unakosa adabu ,huna nidhamu ,kila mtu tapewa heshima yake na kuheshimiwa lakini linapokuja suala la kujadiliana hapo hapatakiwi usawa nani Mkuu nani mtawala nani mtawaliwa panatakiwa hoja kujadiliwa kupingwa kukosolewa isiwe akipingwa mtu aseme fulani inafaa adhibitiwe,inafaa achuliwe hatua ,inafaa aadhibiwe, ukisikia mtu anasema hivyo basi huyo ni adui wa haki tena ni mtu ambae inaonyesha ubaya wake upo ndani kwa ndani.
Shamhuna hana uhusiano na serikali ya Muungano wala CCM kama sikosei,ni kiongozi katika serikali ya Zanzibar ,hivyo alikuwa anawajibika kusema lolote iwe amesema alivyosema Pinda ni sahihi au alivyosema Pinda si sahihi ,natumai anayo haki hiyo ,sasa kilichowatonesha akina Mwakiyembe ni kwa nini Shamhuna amesema au ameipinga kauli ya Pinda hata kama kauli hiyo ilikwishatolewa maelezo lakini ifahamike ni wapi ilipotolewa maelezo ni Bungeni kwenye chombo cha Muungano na Shamhuna nae ametolea maelezo kwenye Baraza la wawakilishi Chombo chao huko Zanzibar ,kosa lipo wapi ? Bahati mbaya Shamhuna amesimamia Uzalendo wa Taifa lake na Katiba ya Zanzibar ambayo inatamka wazi Zanzibar ni nchi ,na yeye yupo sahihi zaidi kuliko Pinda kwani hakuna sehemu katika Katiba ya Muungano palipoandikwa Zanzibar si Nchi.
Jaribuni mnaposoma na kutoa hoja msiwe na jazba aidha kama wewe ni CCM hapo nitakuwa sina la kukufanya ,vilevile ukiwa ni Mtanganyika pia nitakuwa nakuangalia tu.Ila Kama unajihesabu ni Mtanzania basi itabidi uwe katika njia inayotakiwa kuwepo ,japo upo na Chama usijaribu kukilinda chama kinapokosea ni lazima ukiulize,ukihoji ili kupata maelezo na kama yanahitajika kupingwa basi usisite kupinga ,kuliko kuogopa kuambiwa unadharau au huna adabu ni aibu kwa DR>Mwakiyembe kusema maneno alisema ya fulani adhibitiwe au sijui atiwe adabu na wengine mnarukia na kumuona ni shujaa sijui kwa kigezo kipi.