Kilichowapa wasiwasi wenzetu wazanzibari ni muda ulioteuliwa kufanya mapendekezo ya mabadiliko katika yale masuala ya muungano na yasiyo ya muungano. Kabla ya tetesi za kuwapo mafuta Zanzibar, hiyo oil and gas resources halikuwa suala la muungano. Baada ya tetesi kuashiria kuwa mafuta huenda yapo Zanzibar na tena kwa wingi, zikaanza juhudi za kufanya kuwa mafuta liwe suala la muungano. Ndio wale wanaokuwa suspicious haraka wakahisi kuna jambo hapa! Wakaanza kupinga. Sasa leo hii mtaalamu anadai mafuta yale yaliyosemwa yapo, kumbe ni kama hayapo maana hata kazi ya kuyatafiti tu kuona ni kiasi gani inaonekana ni ya hasara, ni kidogo sana hayo mafuta. Wengine wanaona hapana, kwa nini hili la kukosekana mafuta lisemwe leo tunapokataa yasiwe ya muungano? Pengine bado kuna tusilolijua! Ndio wasiwasi ulioko hapo wakuu, lakini ripoti ya wataalamu ndio kama hivyo, hakuna mafuta ya kutosha kuendesha uchimbaji hata wa matumizi tu ya kawaida, acha wa kibiashara!