Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na kero zake: Je, tuuvunje?
Sasa wanasema tunauza mbuzi!

Mbuzi yupo ktk gunia!!!

Fungua basi gunia mbuzi tumwone???

Je kuna mafuta kweli????

Yaani mnasahau hata lugha ya Taifa na misemo yake ,nikiwakumbusha labbda mtafunguka masikio , ...Panapofuka moshi panaficha moto. Sasa hizi kelele unazosikia au mnazozisikia hazikuzuka tu kama uyoga , mafuta yapo ya uhakika sio mchezo na hayakugunduliwa jana wala juzi ,tokea wakati wa Mfalme ,na nyaraka za wakati huo zipo ,ila kutokana na utajiri wa Zanzibar enzi hizo mfalme aliposhauriwa kuyachimba alisema haina haja anawawachia generation zijazo ni hazina yao ,Mfalme ,kwa kiswahili sanifu tunasema alikuwa hana shida ya kuchimba mafuta ,serikali yake ilikuwa na feza kedekede iliyotokana na ushuru waliokuwa wakilipa WaTanganyika waliokuwa wakileta wenzao kuwauza (Ni wakati wa utumwa) na wengine wakileta mazao kuuza yaani Zanzibar ilikuwa ni Hub ya kibiashara kwa east & central east ya Afrika Hebu kasomeni kitabu kijulikanacho kama Modern Tanganyika kinapatikana kwenye mtandao humo mtafaidika sana na haya Mambo ya Zanzibar na hata kuwajua ni akina nani wakipelekana kuuzana Zanzibar ,naona mkisoma si lazima kitabu chote lakini fukua tu na hutakosa kufaidika na kuja hapa na heshima na adabu kama alivyosema Mwakiembe iwepo heshima.Maana mnavyosema mtafikiri Tanganyika ilikuwepo mwanzo kabla ya Zanzibar kumbe ni kajinchi cha juzijuzi tu ,hilo nalo mnatakiwa mlielewe tena mlielewe sana ili mjue nyinyi wenyewe ni akina nani.

Kile kiwanda cha kusafishia mafuta ghafi kilijengwa kwa kutegemeakusafisha mafuta ya Zanzibar ,sijui kama hilo mliwahi kuambiwa na Baba yenu Nyerere lakini WaZanzibari wakamwambia baba kwa hilo tutasameheana mwanangu ,tutasafisha mafuta yetu pale ambapo tutapata kwa bei poa , Oman inachimba mafuta lakini nimeambiwa kuwa mafuta yanayotumika ndani ya nchi hiyo yananunuliwa kutoka nchi nyengine yao wao huwa ni grade nzuri na wanayauza kwa bei ya juu ,sijui kama ni ukweli au jamaa alikuwa kashiba tende kutoka huko kwao ,alinikuta pale Tabora nikiwa natengeneza baiskeli mbovu na zingine nakodisha.
 
Hapa ndo pa kumshukuru Prof. Baregu kwa kusema kile sikuzote watu wanaogopa kukisema ambacho kina maanisha Zanzibar si nchi katika muungano bali ni koloni la Tanganyika. Hata mm nashangaa nguvu gani ya kidola anayoimaanisha Prof. wakati akihusisha suala la mafuta?
 
Sasa wanasema tunauza mbuzi!

Mbuzi yupo ktk gunia!!!

Fungua basi gunia mbuzi tumwone???

Je kuna mafuta kweli????
Mbona mnaogopa kusema kila mtu anamrushia mwenziwe mpira, semeni basi, mtu wetu wenyewe kajitia kimbelembele kashika adabu yake, mnasubiru bunge na sisi tunasubiri maana hatutakaa nje kusubiri mtachosema na kuamua,tutasema na kuamua sote...time will tell.
 
Yaani mnasahau hata lugha ya Taifa na misemo yake ,nikiwakumbusha labbda mtafunguka masikio , ...Panapofuka moshi panaficha moto. Sasa hizi kelele unazosikia au mnazozisikia hazikuzuka tu kama uyoga , mafuta yapo ya uhakika sio mchezo na hayakugunduliwa jana wala juzi ,tokea wakati wa Mfalme ,na nyaraka za wakati huo zipo ,ila kutokana na utajiri wa Zanzibar enzi hizo mfalme aliposhauriwa kuyachimba alisema haina haja anawawachia generation zijazo ni hazina yao ,Mfalme ,kwa kiswahili sanifu tunasema alikuwa hana shida ya kuchimba mafuta ,serikali yake ilikuwa na feza kedekede iliyotokana na ushuru waliokuwa wakilipa WaTanganyika waliokuwa wakileta wenzao kuwauza (Ni wakati wa utumwa) na wengine wakileta mazao kuuza yaani Zanzibar ilikuwa ni Hub ya kibiashara kwa east & central east ya Afrika Hebu kasomeni kitabu kijulikanacho kama Modern Tanganyika kinapatikana kwenye mtandao humo mtafaidika sana na haya Mambo ya Zanzibar na hata kuwajua ni akina nani wakipelekana kuuzana Zanzibar ,naona mkisoma si lazima kitabu chote lakini fukua tu na hutakosa kufaidika na kuja hapa na heshima na adabu kama alivyosema Mwakiembe iwepo heshima.Maana mnavyosema mtafikiri Tanganyika ilikuwepo mwanzo kabla ya Zanzibar kumbe ni kajinchi cha juzijuzi tu ,hilo nalo mnatakiwa mlielewe tena mlielewe sana ili mjue nyinyi wenyewe ni akina nani.

Kile kiwanda cha kusafishia mafuta ghafi kilijengwa kwa kutegemeakusafisha mafuta ya Zanzibar ,sijui kama hilo mliwahi kuambiwa na Baba yenu Nyerere lakini WaZanzibari wakamwambia baba kwa hilo tutasameheana mwanangu ,tutasafisha mafuta yetu pale ambapo tutapata kwa bei poa , Oman inachimba mafuta lakini nimeambiwa kuwa mafuta yanayotumika ndani ya nchi hiyo yananunuliwa kutoka nchi nyengine yao wao huwa ni grade nzuri na wanayauza kwa bei ya juu ,sijui kama ni ukweli au jamaa alikuwa kashiba tende kutoka huko kwao ,alinikuta pale Tabora nikiwa natengeneza baiskeli mbovu na zingine nakodisha.
Kule Pemba jamaa yanafukuta baharini, hatuitaji wataalamu wanafiki kama kina Reading ambao weshayaweka makampuni yao huko kwa standa by, wanasubiru wazanzibar walegee tu, wawape dili mafisadi.
 
Mwenye macho haambiwi tazama! Mafuta hakuna Zanzibar lakini kwa tamaa zao wanangangana nayo. Nini kitapotea kwa kuwaambia sawa chukueni hayo mafuta. Basi!!.
Kwanini iwe issue na iwe tishio kwa Muungano? Tishio lilikuwa lile la kudai kuwa Zanzibar ni nchi pengine lingekuwa tishio kwa Muungano lakini la upande mmoja kudai haki yake si tishio bali ni nyenzo muhimu kwa Muungano. Isitoshe upande mmoja unaendelea kuvuna chake bila kugawana na upande mwengine. Sasa tabu iko wapi hapa, Muungano upo pale pale wala hauna mtikishiko wowote kwani pande zote si za Waungwana? Waungwana wanakuwa na kauli moja. tumia chako nitunie changu Basi.
si mafuta tu..........
 
Sisi watanganyika tu wabinafsi sana! Inapokuja raslimali basi kadi ya Muungano tunaiweka mbele hali tukijua wazi mapungufu ya muungano. Ndio maana baregu anasema turudi kwenye makubaliano ya muungano ilituelewe yamebeba nini! kwa hali ya wazi hilo la mafuta halimo kwenye Tanzania! Na ndipo hapa Baregu anapotoa onyo kufutia hali halisi ya siasa za mafuta dunia, Zanzibar ikiamua kuingia kwenye mafuta yenyewe itakuwa laana... si kwa kudhulumiwa na wageni tu, mgongano wa bara na visiwani ndio utakapoanza! Mama yangu! Kama naiona Tanzania inavyomshughulikia zanzibar ikisahau kabisa kwamba ni sehemu yake ya muungano!
 
BARAKA SHAMTE of all persons? Hapa dada yangu hapana kitu, tafadhali tafuta profile yake itasum up everything.
Mimi siku zote nasisitiza kuwa Hakuna mgogoro wa kisiasa Zanzibar haya mambo yanapandikizwa kutoka bara,kwa lengo la kulazimisha CCM ibaki madarakani hata kama wazanzibar hawataki, kama mpasuko wa kisias kwa nini siku zote uanzie katika uchaguzi? mbona wazanzibar wa unguja na pemba wapo pamoja sikuzote ila wakati wa uchaguzi tu, wakishaletewa mgomboea kutoka bara, na majeshi ya kumlinda na kundi la wapiga kura wa kupandikiza, matokeo ya kughushi ya uchaguzi n.k makusudi haya yote kuifanya zanzibar iendelee kubakia na katika "ukoloni",na chombo pekee cha kufanikisha hilo ni CCM, ambayo inaandelea kubakishwa madarakani zanzibar kwa gharama ya damu ya wazanzibar.
 
Kosa la Baregu ni kusema Zanzibar ina nguvu ndogo kidola ,hili ni kosa na kisheria alitakiwa afute usemi huu ,Nguvu za Dola ni za Muungano haziwezi kuwa za Zanzibar wala Tanganyika ,japo Zanzibar ni nchi ndani ya Tanzania na ni Tanzania nje ya Tanzania.
 
Yaani mnasahau hata lugha ya Taifa na misemo yake ,nikiwakumbusha labbda mtafunguka masikio , ...Panapofuka moshi panaficha moto. Sasa hizi kelele unazosikia au mnazozisikia hazikuzuka tu kama uyoga , mafuta yapo ya uhakika sio mchezo na hayakugunduliwa jana wala juzi ,tokea wakati wa Mfalme ,na nyaraka za wakati huo zipo ,ila kutokana na utajiri wa Zanzibar enzi hizo mfalme aliposhauriwa kuyachimba alisema haina haja anawawachia generation zijazo ni hazina yao ,Mfalme ,kwa kiswahili sanifu tunasema alikuwa hana shida ya kuchimba mafuta ,serikali yake ilikuwa na feza kedekede iliyotokana na ushuru waliokuwa wakilipa WaTanganyika waliokuwa wakileta wenzao kuwauza (Ni wakati wa utumwa) na wengine wakileta mazao kuuza yaani Zanzibar ilikuwa ni Hub ya kibiashara kwa east & central east ya Afrika Hebu kasomeni kitabu kijulikanacho kama Modern Tanganyika kinapatikana kwenye mtandao humo mtafaidika sana na haya Mambo ya Zanzibar na hata kuwajua ni akina nani wakipelekana kuuzana Zanzibar ,naona mkisoma si lazima kitabu chote lakini fukua tu na hutakosa kufaidika na kuja hapa na heshima na adabu kama alivyosema Mwakiembe iwepo heshima.Maana mnavyosema mtafikiri Tanganyika ilikuwepo mwanzo kabla ya Zanzibar kumbe ni kajinchi cha juzijuzi tu ,hilo nalo mnatakiwa mlielewe tena mlielewe sana ili mjue nyinyi wenyewe ni akina nani.

Kile kiwanda cha kusafishia mafuta ghafi kilijengwa kwa kutegemeakusafisha mafuta ya Zanzibar ,sijui kama hilo mliwahi kuambiwa na Baba yenu Nyerere lakini WaZanzibari wakamwambia baba kwa hilo tutasameheana mwanangu ,tutasafisha mafuta yetu pale ambapo tutapata kwa bei poa , Oman inachimba mafuta lakini nimeambiwa kuwa mafuta yanayotumika ndani ya nchi hiyo yananunuliwa kutoka nchi nyengine yao wao huwa ni grade nzuri na wanayauza kwa bei ya juu ,sijui kama ni ukweli au jamaa alikuwa kashiba tende kutoka huko kwao ,alinikuta pale Tabora nikiwa natengeneza baiskeli mbovu na zingine nakodisha.

Mzee usitufunge kama hapa. Sasa unataka kusema waingereza nao waliyaona wakayaacha?? ZNZ wanajua yalipo lakini wanasubiri kizazi kijacho pamoja na ufukara uliopo kule??? Au unataka kusema ramani za sehemu za mafuta zimefichwa?? Je kwa nini walileta consultant kuangalia kama wana mafuta au hawana wakati wanajua yalipo. Hicho kitabu kinaukweli gani kuhusu mafuta kuliko utaalamu uliopo sasa???? Hivi kwa nini makapuni yananunu leseni za exploration tu badala ya ku-negotiate uchimbaji wa mafuta au unataka kusema hawafahamu isipokuwa mfalme tu???
 
Kosa la Baregu ni kusema Zanzibar ina nguvu ndogo kidola ,hili ni kosa na kisheria alitakiwa afute usemi huu ,Nguvu za Dola ni za Muungano haziwezi kuwa za Zanzibar wala Tanganyika ,japo Zanzibar ni nchi ndani ya Tanzania na ni Tanzania nje ya Tanzania.

sioni kosa la beregu! Nguvu za serikali zinapishana inategemea unaliganisha nini? Nguvu ya dola ya kijeshi ya marekani ni kubwa zaidi ya tanzania, lakini uhujumu uchumi wa dola wa tanzania yawezekana umezidi marekani, na kutufanya tuwedhaifu zaidi.

Sioni kosa la beregu, kwani zanzibar inaserikali yake! Na ukilinganisha nguvu za serikali ya zanzibar na tanzania, ambayo tanganika imetoweka, nguvu ya serikali ya zanzibar ni ndogo - kijeshi, na kwa kuhujumu uchumu, watu, eneo, - kila kitu. Labda yakwao inautu zaidi ya yakwetu!
 
Hapa napo suluhisho ni sera ya CHADEMA ya mfumo mpya wa utawala almaarufu kama Sera ya Majimbo. Mamlaka ya kuamua kuhusu rasilimali na kunufaika na rasilimali lazima yashirikishe wananchi wa eneo ambalo rasilimali zinatoka

Asha
 
Mwenzenu mpaka sasa sielewi kwa nini wanapoteza pesa za walipa kodi kukaa vikao kuzungumzia rasilimali ambayo haipo (mafuta) na kuacha kufocus kwenye rasilimaliambayo tunaibiwa (madini). Kweli wadanganyika ndiyo waliwao!!!! Kama nguvu nyingi hivi zinatumika kwenye mafuta tusiyonayo, je yakipatikana itakuwaje??? Mungu iepushe TZ kwenye haya majanga. Wananchi wa TZ wanasota na ni mafukara utafikiri walikuwa na vita vya miiak arubaini sasa ikija vita ya ukwelikweli sijui itakuwaje? Naogopa hata kufikiria................!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Hapa napo suluhisho ni sera ya CHADEMA ya mfumo mpya wa utawala almaarufu kama Sera ya Majimbo. Mamlaka ya kuamua kuhusu rasilimali na kunufaika na rasilimali lazima yashirikishe wananchi wa eneo ambalo rasilimali zinatoka

Asha

Asha,

Tunahitaji kuweelewa hizo sera za majimbo! na kuone uhalisi wake katika uzalishaji mali! Nani atakuwa na nguvu ya soko ni Tanzania ama jimbo! Mahusiano ya jimbo na taifa yatakuwa vipi? jimbo ambalo halina malighafi linakuwaje? Hawa viongozi wa majimbo watachaguliwaje, wanaingia vipi bungeni!

Tatizo langu kwa sasa sio sera tu, ni watu pia! CCM inatoka jamii ile ile ambayo chadema inaishi, tusipokuwa makini tutabaki kubadiisha majina tu na ufedhuli ukaendelea pale pale!
 
Kosa la Baregu ni kusema Zanzibar ina nguvu ndogo kidola ,hili ni kosa na kisheria alitakiwa afute usemi huu ,Nguvu za Dola ni za Muungano haziwezi kuwa za Zanzibar wala Tanganyika ,japo Zanzibar ni nchi ndani ya Tanzania na ni Tanzania nje ya Tanzania.
Al Ustaadh Mwiba, kosa gani kisheria?. Mbona Prof. Beregu ameipendelea Zanzibar kusema Zanzibar ina nguvu ndogo kidola, hata hiyo kidogo ni upendeleo, Zanzibar ina dola?.
Aliyetamka rasmi Zanzibar sio dola ni Nani?. Ni Mahakama Kuu ya Zanzibar kwenye kesi ya uhaini baada ya kubainika, kosa la uhaini haliwezi kufanywa mahali ambapo hakuna dola. Kimataifa Zanzibar ni kama Tandahimba au Mafia au Kilwa.
Alichosema Profesa, akhad ya mafuta ya 'Kinibu' yaliyopo
Zanzibar, yasiwavimbishe kichwa kuutikisa Muungano, kwani ni nguzo muhimu kwa ustawi na usalama wa Zanzibar ambayo haina dola. Msamaha wa nini?.
Kitu kimoja ninakubaliana na mtoa mada, baadhi ya wasomi wetu, wanazungumza kisomi mno kiasi kwamba sisi malaymen wakati mwingine, hatuwaelewi, ili umwelewe vizuri Prof. Beregu, unahitajika angalau uwe na level ya uelewa huo.
Nasisitiza umuhimu wa kukosoa mada kwa kuibomoa ama kwa kujenga hoja mbadala, sio busara kukejeli accademic credentials ambazo hazina ubishi kama Prof. Beregu.
Mwisho naungana na wewe Mwiba, mafuta ni ya Wazanzibari hata kama ni kujaa kwenye kinibu, ni yao, hakuna sababu ya kuyapigia kelele siye wabara, na kama yapo, si watatuuzia kwa bei poa kuliko Waarabu?. Au kwa vile nako walikuwa hao hao Waarabu, kabla ya wabantu masalia ya watumwa waliokosa soko, hivyo kuna uwezekano wakatukamua kama 'Waarabu wa Pemba wanavyojuana kwa Vilemba'?.
 
Mzee usitufunge kama hapa. Sasa unataka kusema waingereza nao waliyaona wakayaacha?? ZNZ wanajua yalipo lakini wanasubiri kizazi kijacho pamoja na ufukara uliopo kule??? Au unataka kusema ramani za sehemu za mafuta zimefichwa?? Je kwa nini walileta consultant kuangalia kama wana mafuta au hawana wakati wanajua yalipo. Hicho kitabu kinaukweli gani kuhusu mafuta kuliko utaalamu uliopo sasa???? Hivi kwa nini makapuni yananunu leseni za exploration tu badala ya ku-negotiate uchimbaji wa mafuta au unataka kusema hawafahamu isipokuwa mfalme tu???

Wewe hufahamu kitu muingereza alikuwa kama watchman ,maana sijui kama unaelewa historia ya vita vya majimaji,kuna msudani ambae alikuwa ni askari aliyewahi kuwa katika jeshi la sudani huyu alisema kama risasi itageuka maji maji atajiua na kuelekea kwenye mapambano, hebu kasomeni hapa
A modern history of Tanganyika - Google Book Search
 
Ndugu Mlalahoi, Kwa heshima kubwa napenda urudi kusoma tena maandishi yako. Inaonekana wazi kuwa wewe na profesa wako munawadharau sana wazanzibari. Hivi ni kwamba bila ya bara, Zanzibar haiwezi kujiendesha?. Kwani kinacho rudisha maendeleo nyuma zanzibar ni huu muungano "FEKI" tulionao. Nataka kukujulisha kuwa kabla muungano, Zanzibar kulikuwepo na baada ya muungano pia Zanzibar itakuwepo. Sisi sio watu wavivu kabisa. Sisi ni watu wenye uwezo mkubwa wakuendesha mambo yetu. Sisi hatutaki ufisadi mulionao huko bara kutuletea huku. Siku zote dhahabu yashinyaga, almasi za mwadui, misaada kutoka nje, yooote mumekumbatia nyinyi. Sisi tnawadai hata pesa za kujenga benki kuu ya tanzania. Iko haja takaeni chini tufanye hesabu za mali muliochukua kinyemala badala ya kukaa mukipiga kelele za ovyo. Sisi wazanzibari tumechoshwa na muungano huu wakuburuzwa. Muungano uliokosa dira na muelekeo.
 
taarifa zilizotufikia hivi punde zinasema bunge la wawakilishi znz lilikutana ghafla kwa kificho katika hotel ya serena zanzibar jana usiku , katika mkutano huo kulikuwa na wazungu kadhaa waliokuja na magari ya kufahari lakini wakaondoka na magari ya kawaida baada ya kuona watu wameanza kuwa na wasiwasi nao haijulikani walijadili nini katika mkutano huo inawezekana ni suala la muungano na mengine yanayohusiana mafuta
 
Shy, unaweza kuiweka hii habari vizuri. Hao wazungu nao walikuwa miongoni mwa wajumbe katika hicho kikao cha wajumbe wa baraza la wawakilishi ama?. Hii ndio miungano inayofanyika bila kupata ridhaa ya watu wa pande zote, kama mambo ya muungano yanabadilishwa na kikundi fulani cha watu, tutegemee nini?, ni haki yao kukutana na kuzungumza wanayotaka.
 
taarifa zilizotufikia hivi punde zinasema bunge la wawakilishi znz lilikutana ghafla kwa kificho katika hotel ya serena zanzibar jana usiku , katika mkutano huo kulikuwa na wazungu kadhaa waliokuja na magari ya kufahari lakini wakaondoka na magari ya kawaida baada ya kuona watu wameanza kuwa na wasiwasi nao haijulikani walijadili nini katika mkutano huo inawezekana ni suala la muungano na mengine yanayohusiana mafuta
Wewe acha mambo ya udaku Bwana. Baraza la wawakilishi lina pahala pake pa kukutana napo ni katika Ukumbi wa Baraza la wawakilishi. Vyenginevyo linaweza kukutana pengine katika mfumo wa Semina maalum. Sasa kama wajumbe fulani binafsi umewaona Serena acha kukipakazia hicho chombo chetu tukufu -BARAZA LA WAWAKILISHI.
 
Back
Top Bottom