Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na kero zake: Je, tuuvunje?
sasa Namwamini Mchungaji Mtikila, alipodai Tanganyika watu walimcheka wakasema ni chizi lakini kumbe alikuwa anapanda mbegu ambayo sasa inaota Big up rev. Mtikila tuko nyuma yako bro.
 
sasa Namwamini Mchungaji Mtikila, alipodai Tanganyika watu walimcheka wakasema ni chizi lakini kumbe alikuwa anapanda mbegu ambayo sasa inaota Big up rev. Mtikila tuko nyuma yako bro.

I can no longer rally behind Mtikila. He's corrupt. He had been financed by RA. He has won big cases but he makes no follow up. He is a lier. I only like his slogan "saa ya ukombozi sasa Tanganyika"
 
Come rain!!... Come sun!!... one day... TANGANYIKA will return triumphantly!!!

Nasikitika haijaja chini ya CCM na nimekata tamaa kabisa baada ya kuwasikia CHADEMA wakilia eti Zanzibar inavunja Katiba kujitangaza kuwa ni nchi. Ajabu ni kuwa Katiba hiyo ni nzuri kwa kuikalia Zanzibar tu na kwa mengine iondolewe!
 
sasa Namwamini Mchungaji Mtikila, alipodai Tanganyika watu walimcheka wakasema ni chizi lakini kumbe alikuwa anapanda mbegu ambayo sasa inaota Big up rev. Mtikila tuko nyuma yako bro.

Jee tunampinga Baba wa Taifa?
 
Tanganyika tanganyika tanganyika nakupenda kwa moyo wote....... Wimbo waliotohoa toka tanganyika na kuufanya wa tanzania kwa tanganyika ipo kila unapoimba wimbo wa taifa basi ujue unauimba huo wa tanganyika.
 
Tanganyika tanganyika tanganyika nakupenda kwa moyo wote....... Wimbo waliotohoa toka tanganyika na kuufanya wa tanzania kwa tanganyika ipo kila unapoimba wimbo wa taifa basi ujue unauimba huo wa tanganyika.

Usisahau Mungu ibariki Tanganyika.......ndio ulikuwa wimbo wetu wa taifa......
 
there are few associations that kept the word Tanganyika and it reminds me that Tanganyika just exists and soon it will regain independence from Tanzania.


On my list
  1. Tanganyika Farmers Association
  2. Tanganyika Law Society
  3. Tanganyika Instant Cofee Ltd

Muulize aliyeua Tanganyika Mwalimu Nyerere na sababu anazo.
 
Chadema anzeni kudai Uhuru kabla ya kudai umeya, hapo ntawaelewa:

Zanzibar, wana Rais wao, Tanganyika haina.

Zanzibar wana Baraza lao la wawakilishi, Tanganyika haina.

Zanzibar wana Bendera yao, Tanganyika haina.

Zanzibar wana wimbo wao wa Taifa, Tanganyika haina.

Zanzibar wana Serikali yao, Tanganyika haina.

Zanzibar wana jina lao, Tanganyika haina.

Nani hapa aliekuwa huru?
 
Nawapenda sana Watanzania maana yake ukijumlisha Watanzania Bara Watu wa Tanzania Visiwani (Wazanzibar) lakini pamoja na hayo,mimi napata shida kutambua faida ya muungano hasa kwa Tanzania Bara,japokuwa najua umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu lakini unapojenga umoja na mtu asiyeutaka umoja sidhani kama utakuwa nguvu tena.Zanzibar chini ya raisi wao kipindi kile cha kuungana wao ndiyo walitaka faida ya kulindwa ili wasije wakapinduliwa na adui zao,lakini leo adui hayupo tena maana wanadhani wamepatana hivyo hawataki tena Muungano,ingawa siamini kama hakuna adui tena.
Lakini pia inaonesha Zanzibar inazofaida nyingine nyingi ktk Muungano ukiondoa ulinzi kama vile kupata gawio ktk kila pato la Tanzania Bara wakati ktk pato la Zanzibar,Bara hawapati gawio.
Naomba wana JF kujulishwa muungano huu tulionao ni wa nini kama wanaoufaidi hawautaki?na je tukiubadili muundo wake utaleta manufaa kwa wote?na ukivunjika kuna hasara gani kwa Bara zaidi ya kukaribisha magaidi?
 
Tanzania bara ni wapi na Tanzania visiwani ni wapi ? Kabla hujafikiria mbali Kilwa itakuwa upande gani !! Katika katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar (Tanzania) ni wapi kumetajwa Tanzania Bara na wapi imetajwa Tanzania visiwani ? Pato la Tanzania Bara lipo nchi gani ? Na hii Tanzania bara ni nchi ya wapi ? Utaifa wake uhuru wake na mipaka yake ni ipi ,mimi sijawahi kusikia kama kuna Nchi inaitwa Tanzania Bara na hata Raisi sijui kama yupo wa Tanzania bara.
 
hakuna tanzania bara, bali kuna tanganyika na uhuru wa tanganyika ulipatikana tar 9 dec 1961, hivyo basi kuna kila haja ya kuidai na kuirudisha tanganyika yetu kwanza, kuhusu faida za muungano kwa upande wa tanganyika hakuna hata moja ila viongozi mafisadi wa ccm wanashinikizwa na mabwana zao wamarekani na umoja wa ulaya ili kuidhibit zanzibar na magaidi wa kiislam ambao kuna uwezekano mkubwa sana kama wakijitenga alqaeda,alshabab pamoja na hizbulah wanaweza wakaweka matawi yao hapo na kuhatarisha maslah ya wamarekani, mi binafsi nauchukia sana huo mungano napenda hata leo uvunjike na sisi watanganyika tuwe na nchi yetu huru.
 
Jee Muungano una faida au hasara kwa Zanzibar YES/NO?

Hii ni haki ya kila Mzanzibar kujiuliza na kutowa rai ya kufanya ili tutatuke katika jambo gumu hili? Wznz tuweke pembeni utashi wa vyama kwa vile vyama vyote vina wafuwasi Zanzibar na Tanganyika?lakini jambo la Utaifa na Uzanzibar unawahusu Wzanzibar tu na hatma ya nchi yao na kizazi chao cha baadae.
Kwa maoni yangu mimi binafsi ukiniuliza faida na hasara nitakwambia hasara ni nyingi kuliko faida, na nasema hivi sio kwamba sipendi tungane au siwapendi Wtanganyika no. Mimi naona Wzanzibar tuna mapenzi zaidi kuliko ndugu zetu waTanganyika walivyo, na kuna mifano mingi hai inaonyesha sisi tuulivyoo wastahamilivu na kuvumilia mengi ? Lakini inaonekana upole wetu na ukarimu wetu wenzetu ndio hushukuwa advantage ya kuimeza nchi yetu kidogo x2 kwa kutumia kigezo cha Muungano na katiba ya Tanganyika ambayo ndio hii ya Tanzania imefanyiwa marekebisha kidogo tu.
Kama kwela ndugu zetu wa Tanganyika wangekuwa na nia safi na Muungano wangeweza Kuufuata makubaliano halali ya Muungano(Artcle of Union) waliokubaliana wasisi wawili Rais wa Tanganyika Julias Kambarage Nyerere na Rais wa Zanzibar Mh Abedi Amani Karume lakini wapi?.
Nikipindi kifupi tu bada ya kufariki Mh Abedi Amani Karume ndipo Rais wa Watu wa Tanganyika akanza kutubadilikia na kujifanya Super power Baba wa Taifa Mama Kafaa?.
Jambo kubwa Wzanzibar lililo tutia shaka na kutushtuwa ni pale Wenzetu Ndugu zetu Wtanganyika walipo itana na kuwa kitu kimoja na kuitisha Bunge lao la Tanganyika likiongozwa na Rais wa Tanganyika Julias, Na kwa nia yao mbaya ya kutaka kutukolonazi na kuimeza Zanzibar kimipango, ni kumsikiliza Nyerere kuwa kila balipo andikwa Tanganyika andikeni Tanzania na Tanganyika ikavaa Koti la Tanzania na Katiba ya Tanganyika ikafanyiwa marekebicho ikawa ndio hii ya Tanzania na nembo zote za Tanganyika kineme Adam na Hawa ndio hizi za Tanzania.
Huu ndio ujanja wao waliohisi Utafanyaa kazi kuimeza Zanzibar ktka Tumbo la Tanganyika ambayo ndio hii Tanzania kilisho badilika ni jina tu Nisawa na Zaire kuita Kongo au Kusema Paka kanywa mchuzi,mchuzi umenywewa na Paka ni imla hio hio tu.
Kuanzia hapo Nyerere akatukuzwa na watu wake kuwa Papa wa Taifa la Tanzania ambayo ni Tanganyika na Mipaka ya Tanzania ikawa ni Tanganyika Bara na Tanganyika visiwani?.
Baada ya hapo ikawa Zanzibar inanyoyolewa kwa kutumia katiba ya Tanganyika kwa faida ya Watanganyika na Wzanzibar tukaanza kugonganishwa vishwa vya Usultani,uwarabu,upemba na Unguja na mwisho mapinduzi daima lakini wenzetu wana lengo jengine.
Kwa hio hivi sasa Wzanzibar tumeungana na tumejifunza mingi na hatuko tayari kukaribisha fitna zakutugawa hazina nafasi tena na kiwiliwili cha kila Zanzibar hivi sasa nikimoja tu na nikupigana na aduwi fitna na kudai maslahi ya nchi yetu kwanza kwa faida ya kizazi shetu.
Ukitaka ujuwe kuwa Wtanganyika lao moja awe ccm,awe cuf awe Chadema,awe Muislam awe mkristo lao moja, mimi nashangazwa na Chadema eti wanasema cuf wamevuja katiba ya Muungano ambayo sera yake ni Serekali mbili kuelekea moja 2-1? Na hivi juzi ktk Kongamaano la Prof Shevi na Jeneral Ulimwengu wanasema Zanzibar imeshavunja makubaliano ya Muungano ni pale ilipobadilisha Katiba kifungu no 10 kinasho sema Rais wa Zanzibar ni Rais na mipaka yake ya nchi na mikowa yake? Kwa hio imevunja Muungano tayari. Sasa Wzanzibar tunasema kidogo ya Wzanzibar ni udogo wa Nyuki kujenga asali na wingi wenu ni Wanzi hauna faida yoyote ile.
Njoni Zanzibar tuwafundishe maisha, na ikiwa tumeshavunja Muungano na katiba ya Muungano Jee nyiyi mumefanya nini?nyiyi mumejisahau na Papa wenu wa Taifa na kuiuwa Tanganyika yenu na katiba ya yenu kwa Zamira yakuimeza Zanzibar kirahisi? Yaguuju Zanzibar ipo kabla ya Tanganyika na historia ya Zanzibar katu kufa na ndio itakayo wasuta. Kama uhuru wa Tanganyika ndio wa Tanzania muta jiju.sisi hivi sasa tunavuta kamba moja na ishaallah M/mungu atatusaidia kwa haki yetu kututoka.Mungu ibariki Zanzibar.

Jee nembo hii ya Adam na Hawa si ile ya Tanganyika kabla ya Muungano?huyu ni Rais wa Tanganyika na katiba mulionayo ni ile ile ya Tanganyika musitudanganye

 
Jee nembo hii ya Adam na Hawa si ile ya Tanganyika kabla ya Muungano?huyu ni Rais wa Tanganyika na katiba mulionayo ni ile ile ya Tanganyika musitudanganye

yakhee..... kwanza hujui historia ya nembo na alama za nchi.... nembo hii ya bibi na bwana inaonyesha bendera ya Tanzania ambayo ni muungano wa Tanganyika na zanzibar....cha ajabu wewe unasema nembo hii ni ya Tanganyika kabla ya muungano.... wakati bendera ya tanganyika ndio hii hapa chini..... haipo kwenye nembo ya bibi na bwana kama National emblem ya Tanzania


tanganyika.jpg ................................ emblem.jpg
Tanganyika flag .........................................Tanzania emblem with Tanzanian Flag

haya compare vitu ambavyo umejichanganya wewe mwenyewe

usipende kukurupuka utaumbuka humu JF,,,,
 
abdulahsaf .... laiti ungejua muungano ni nini na kwanini kuna wimbi la federations and unions even in rich countries usingezungumzia upupu wako hapa... in principle inchi maskini za kama zetu ambazo ni poor counties ndio tunaotakiwa kulilia muumgano ... tunabahati waasisi wetu waliyaona haya in advance... nikuulize swali moja..muungano ukifa... je tanzania bara watakuja zanzibar kuomba yafuatayo...?

mahindi, nyama, umeme, dhahabu, tanzanite, rubby, chuma, shaba, almasi, gesi, umeme, maji, mbuga za wanyama, bandari, mlima kilimanjaro, maziwa makuu, mipaka na nchi takriban saba, vyuo vikuu, viwanja vya ndege, majeshi, kahawa, korosho, matunda, mbao, samaki,

kwa kifupi tutakuja kuomba karafuu tuu
 



Mimi sizani kwamba Tanganyika imekufa au kuwa haipo kama wasemavyo wenyewe Wtanganyika kuwa Tanganyika imekufa lakini Zanzibar baado ipoo?. Huu ni uongo na unafikii wakuzibwa macho Wazanzibar watotezwe ktk muelekeo na kufanywa(BLIND) tuelekezwe kizani wapate kututawala na kuvishonza visiwa vyetu , Kama kwela Tanganyika imekufa au haipo hebu tujiulize ni nani alio iuwa Tanganyika ni Wazanzibar au Watanganyika wenyewe? na kwa mazumuni gani Tanganyika ifee? Mimi nasema hapa pana mipango ya muda mrefu na mite go mingi nilazima tuhoji kifo hishi cha Tanganyika.
Kwa sababu haingii akilini kabisa kabisa Tanganyika ifee hali ya kuwa ni nchi yenye historia yake ya ya watu wake na rasilimali zake na walitumia jacho kubwa na nguvu nyingi ili kuigombowa kupata uhuru wake wa December 9,1961?. Vipi leo waseme Tanganyika imekufaa haipo?. Na sikweli kuwa wameeiuwa Tanganyika kwajili ya Muungano?hii sio Kwelii na haingii akilini, Muungano ni urafiki tu wa mkke na Mumme unaweza kukatika wakati wwte? Sasa ukikatika vipi itakuwa Tanganyika au itabakia kuwa Tanzania na (9 December 1961) itakuwa sherehe za uhuru wa Tanganyika au zitapaki za Tanzania kama mulivyo zowea kujipiga shindano yakupoteza fahamu?.
Mimi nasema hili halingii akilini na Wzanzibar tusije tukaanowa steep tutapotea vibaya sisi na nchi yetu na kizazi shetu katakana kutusuta na kutukaa rohoni kwa upumbavu huu wa kuiuza kwa bei ya jumla Nchi yeo. Maana wenzetu nia yao ni kututawala kimbinu na kirai haiwezekani kufanya watakavyo na sisi viongozi wetu wa Baraza la Uwakilishi wapo wanatumbua macho tu bila ya kulizungumzia hili? Hii ni haki yetu ya kutaka kujuwa hatma ya nchi. Vyama,mtu,uongozi vyote vinapita tu? Jee BLW vipi hatma ya watoto wako na wajuukuu zako?
Kwa hili Wzanzibar tuvute kamba moja na Ishaallah M/Mungu atakuwa pamoja na sisi kwa vile nihaki yetu. Hawa jaa wamekaa vibaya mshirika wa Muungano ni Nyerere na Karume yani Tanganyika na Zanzibar Vipi leo tuambiwe Tanganyika haipo na sisi na sisi Wzanzibar bado tugaganie kuwepo? Wakati mshirika mmoja wa Muungano ameshavunja makubaliano ya Muungano?.
(Wake up) BLW na Wzanzibar wote kwa hili tuamke na susioneane haya Tanganyika ipoo na ndio hii Tanzania iliovaa Koti la Tanganyika na kujitambulicha kiimataifa shuhuli zake na kazi zake na ndio ukaona nembo na alama zote za Tanzania ni zile zile za Tanganyika hawakubadilisha kitu ispokuwa ni Zaire kuita Kongo na Sherehe zao hujifanya sherehe za uhuru wa Tanzania ,Katiba ya Tanganyika ndio katiba yao inayosimamia mambo yao ya Tanganyika zikiwemo meneral Tanzanet,Zahabu,Almasi,Makaa ya mawe -gesi ya Songo songo na TRA kusimamia rasilimali za Wzanzibar na Maputo jioni kuondoshwa kupelekwa Tanganyika huu ni ujinga na upumbavu Wzanzibar tuufanyao na upole na ukarimu wetu ndio adventege ya wenzetu kutufunga makoli sisi tumeebakia tulinde na tuuenzi Muungano wetu wakati wenzetu wameshauvunja tayari kwa maslahi ya kutunyonga wake up BLW.
Mimi hushangazwa na Wtanganyika kusema kuwa Zanzibar imeshavunja Muungano ktk marekebisho ya kifungu cha kumi kusema Zanzibar ni nchi na ina mipaka yake? Sasa tujiulize kabla ya Muungano Zanzibar ilikuta ni Mkowa? Na kwaroho mbaya Zao za udini Chadema hivi karibuni wanasema kuwa Zanzibar imevunja mkataba wa Muungano na Katiba ya Muungano ambayo ilani yake ni Serekali mbili kuelekea moja/ yagujuu Chadema. Wzanzibar wasasa sio wale wa nyuma ni Damu mpya na nguvu mpya za Ukweli na uwazi.
Ikiwa nyiyi Chadema na Ccm/Tanganyika lenu moja kuimeza Zanzibar ktk Tumbo la Tanzania ambayo ndio hio Tanganyika kuwa muelekeo ni Serekali moja yaguujuu mutaotaa? Katu Wzanzibar hatuto kubali kuambiwa (REPLIC OF TANZANIA) NO,NO kuku Bali hivi ni kula matapishi yetu wenyewe yani mufanye Serekali ya Watu wa Tanzania(Tanganyika) iwe ni 1. Hili hatulikubali katu katu mwataka kujirekebisha ni kuwa na Serekali 3. Ndio ulimwengu wa nchi zilizo ungana yani (REPLIC OF TANGANYIKA AND ZANZIBAR)Sio sere kali ya watu wa Tanzania tuingie ktk tumbo la Tanganyika yagujuu tutadaa haki zetu kwa bei yoyote ile.Wazanzibar kidogo lakini ya Nyuki sio nyiyi wingi lakini wa Nzii, Ameshawambia Mh Hamadi Rashi kuwa nyiyi siasa hamujuwi njoni Zanzibar mufundishwe siasa? Ama nyie watu wabaya sana Chadema walipokuwa wakiona damu ya ki-Zanzibar inamwagika Zanzibar wao wakishekelea, Wawakilishi kususia vikao wao wakizihaki na kujejea sasa ngoma imewageukia wao na hivi sasa wanapita katika guwa la Cuf sehemu iliokwisha pitwa na Cuf. Chadema washeni udini daini Tanganyika yenu na sisi tutawapiga tigh,sio kuleta ubaguzi wakidini na choyo cha kusema sasa cuf wameshaungana na ccm upinzani umekufaa,sijuwi marekebisho ya Zanzibar ni asari za Muungano nyoko nyoko. Kama kwela Muungano munaopenda musike itana Bunge la Tanganyika kumsikiliza Papa wenu kuua nchi yenu ya Tanganyika na Katiba yenu in Yolinda rasilimali zenu na historia ya nchi yenu, lakini muligeuka kuwa Majambazi na koruna makubaliano halali ya Muungano(Artcle of Union) kwa lengo la kuimeza Zanzibar yagujuu. Wazungu mbinu zao zote wakishirikiana na Nyerere walishindwa kuiuia hitoria ya Zanzibar itakuwa leo Kikwete?.
Nyiyi itabaki nyimbo zenu hizo hizo za siku zote Muungano ukivunjika Maduka Kariakoo mutayakosa,sijuwi mumejenga Majumba ya Gorofa mutayakosa sijuwi viazi vibovu na mbatata mbovu mutazikosa yokox2 nyiyi hamuna mpya mumezowea kuongozwa na ndio mukawa wengi lakini wa Nzii. Laiti ingekuwa Wzanzibar tuko wingi kama huo wenu na Ardhi kubwa kama hio yenu basi Tanganyika ingekuwa Tajiri kuliko nchi yoyote Africa lakini muko tu kama midudu mwaongozwa na ccm mukivishwa Mabakasha na makaunda yakijani. Mungu ibariki Zanzibar na Kizazi cha Wzanzibar.
Wziri wa Sheria na Katiba wa Z'bar Mh Abubakar Khamis Bakari

[caption id="attachment_27134" align="alignnone" width="294" caption="TANGANYIKA IPO KWA SABABU YA NEMBO HII YA TANGANYIKA. "]
 
Fadhili ya punda ni
MISHUZII
Endelea kubip watg dola ipo
TUTAWAPIGIA DOGO!
 
Back
Top Bottom