Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na kero zake: Je, tuuvunje?
FIKIRIA unahisi vipi unapokuwa unapita katika vichochoro vya mitaa ya Zanzibar na kumkuta mtoto mdogo amekaa nje ya nyumba yao anachezea mchanga na wenzake.
Inawezekana wakati huo mzazi au mlezi wake huwa anafua nguo za huyo mtoto au anamtayarishia chakula chake kabla ya kuanza kulia, kama ishara ya kuonyesha kuwa ana njaa.
Ukifikiria zaidi utaweza kukumbuka, ijapokuwa kwa mbali, kuwa na wewe ulipokuwa mdogo kama yeye, ulifurahia sana mchezo kama alivyokuwa yule mtoto aliyekuwa anachezea mchanga kwani kwa mtoto mdogo mchezo ndio furaha yake ya maisha.
Lakini mara baada ya kuachana nacho hicho kitoto, mara unasikia kelele za mtoto analia na unaporudi nyuma kuangalia unakikuta kile kitoto uliokuwa ukikiangalia na kujikumbusha zama za utoto wako, kinagaragara chini na damu imetapakaa mkononi mwake.
Unashangaa kwa vile sekunde chache kabla ulikiona kile kitoto kinachezea mchanga kwa kuutia kwenye kifuu na kumimina chini na kurudia hivyo mara mbili au tatu.
Kwanza unafikiria labda amejikata na kitu kikali. Kumbe si hivyo, bali katokea kiumbe katili na jahili aliyeamua si tu kumnyima raha ya mchezo yule mtoto kwa wakati ule, bali raha katika maisha yake yote. Kilichotokea ni kwa huyo jahili kumdunga yule mtoto sindano iliyokuwa haina damu salama, ili amuambukize virusi vya ukimwi.
Huu ndiyo unyama na ujahili wa aina yake unaosemekana kutokea katika baadhi ya sehemu za mji wa Zanzibar katika siku za hivi karibuni. Kwa mujibu wa taarifa ya kipindi cha matukio mbalimbali kijulikanacho kama ‘Mawio’ cha Sauti ya Tanzania Zanzibar, matukio mawili ya aina hii yameripotiwa.
Wazimu huu mpya wa baadhi ya vijana ni unyama usiokuwa na kifani na tabu kuufikiria na kuamini. Hivi watoto wa miaka miwili au mitatu wamefanya kosa gani hata kupewa hiki unachoweza kukiita adhabu ya kifo?
Lakini ukichunguza kwa undani utagunduwa kuwa huu ni mtiririko wa kuendelea kwa kasi kuporomoka kwa utu, imani, huruma na maadili Visiwani. Lakini kiwango cha mporomoko huo kilichoonekana hivi karibuni si tu ni cha kusikitisha, bali ni cha kutisha.
Iwapo haitadhibitiwa haraka hali hii, na iwapo itafanyiwa mzaha wa kuonekana kama mchezo wa kuigiza, inaweza kuwa na athari kubwa hapo baadaye kwa Zanzibar. Kwanza inawezekana ikasababisha watoto wengi Visiwani kuambukizwa virusi vya ukimwi na hawa wendawazimu wanaosaka watoto wadogo ili wawadunge sindano za damu yenye virusi vya ukimwi.
Kwa vyovyote vile, matukio haya yatasababisha wazazi kuanza kufungia watoto wao majumbani kama ndege waliomo kwenye tundu, hali ambayo itawakosesha watoto wadogo raha yao ya kucheza kutokana na wazazi kuhofia kwamba hata nje ya nyumba zao si tena salama.
Hili suala ni zito sana na linahitaji kushughulikiwa kwa haraka sana na kwa nguvu zote, si tu za kisheria, bali pamoja na wana jamii wa Visiwani kushirikiana kuwabana hawa majahili wanaofanya unyama huu wa kuhatarisha maisha ya watoto wadogo.
Kwa muda mrefu imani na maadili ya watu wa Visiwani yamekuwa yakiporomoka kwa kasi ya aina yake na kuja kwa huu unaoitwa unga, yaani mihadarati, ndio kumeongeza zaidi hiyo kasi.
Hivi sasa katika kila pembe ya mji wa Zanzibar wapo vijana walioathirika na dawa hizi hatari na wanaonekana wakisinzia ovyo na udenda kuwatoka kama kuku wenye kideri. Maeneo mengi wanayokaa vijana hawa wanaotumia dawa hizi hatari na kuitwa Colombia, Peshawar, Kandahar na Jalalbad yanaeleweka vizuri.
Kama vijana wanaotumia mihadarati wanajua wapi wanaweza kuzinunua, inakuwaje iwe shida kwa askari polisi kufahamu dawa hizi hatari zinauzwa wapi?
Lilio baya zaidi, kama matukio ya kuwadunga sindano za damu yenye virusi vya ukimwi hawa watoto wadogo wasiokuwa na hatia, ni kuwa baada ya hawa vijana waotumia mihadarati kuathirika na maisha yao kuvurugika, wao sasa wameamua kumaliza maisha ya watoto wadogo.
Kama watu wa Visiwani wamekuwa wakiona taabu kuwabana wanaoziingiza dawa hizi nchini, wanaoziuza na wanazozitumia kwa vile ni jamaa, ndugu na marafiki zao, sasa waelewe kuwa mbali ya kuwa na vijana wengi kuharibikiwa akili madhara ya dawa hizi sasa yanahatarisha maisha ya hata watoto wadogo ambao hata hayo maisha yenyewe bado hawayajui.
Jamii inapaswa ielewe kuwa kama upo wakati wa kusema adui mkubwa wa Zanzibar hivi sasa ni hizi mihadarati na si jambo jingine lolote lile basi ni huu. Ni lazima mapambano dhidi ya dawa hizi hatari yakolezwe moto na pasiwepo na huruma kwa vile hao wanaoonewa huruma sasa wanafanya ujahili na unyama wa hali ya juu.
Katika miaka ya nyuma, mtoto Visiwani alilelewa na watu wote mtaani na mzee aliweza kumuacha mwanawe nyumba ya jirani bila ya wasiwasi na kuangaliwa ipasavyo na majirani na wapita njia. Kinachoonekana sasa ni kuwa kumuacha mtoto acheze nje ya nyumba ni kosa na kuhatarisha maisha yake.
Ni vizuri kwa Wazanzibari kuitafakari hali hii ya kusikitisha na kutisha kwa makini na kuchukuwa hatua madhubuti za kuwabana wanyama hawa wanaohatarisha maisha ya watoto kabla ya kila mzazi katika nyumba kubaki analia.
Hii ni changamoto nyingine kwa Jeshi la Polisi. Ni kweli hivi sasa Jeshi la Polisi lina kazi kubwa ya kulinda usalama wa raia na mali zao, lakini huu usalama wa watoto wadogo unapaswa kupewa umuhimu mkubwa.
Lakini itakuwa ni kosa kutegemea askari polisi peke yao kuweza kuifanya kazi hii kwa uadilifu na ukamilifu. Wanajamii lazima watoe ushirikiano na wao wenyewe wafanye juhudi za kuwasaka wanaofanya ushenzi huu.
Tukumbuke kuwa watoto, kutokana na umri wao mdogo, akili zao zikiwa bado hazijakamilika na udhaifu wao wa mwili, hawawezi kujilinda wenyewe. Ni wajibu wa kila mtu kuchangia kuwalinda kwa hali na mali.
Hili ni jukumu la kila mtu, mzazi na kila mwenye kuthamini maisha. Unyama huu lazima ukomeshwe haraka.
 
Mkimkamata aliemchoma mtoto sindano yaukimwi auawe palepale achomwe moto,mkiwachoma moto kama 5 tu wataogopa,ila awe kweli kamdunga mtoto sindano yakumuuakwa ukimwi,dawa ya moto nimoto.
 
Samahani ndugu mtoa mada, naona hapo umemix madesa.... heading haiendani kabisa na mada :twitch: muungano na unga wapi na wapi au ulitaka kusema kuwa wauza unga ni wa tanganyika sielewi kabisa hii kitu :thinking:
 
Unga unaouzwa Zanzibar unatoka Pakistan na Afghanistan. Na wanaouingiza na kuuza ni Wazanzibari wenyewe. Don't look beyond your noses for the sources of your own problems.
 
Kwani huelewi kama watanganyika ndio mafundi wa unga?

Likely mtoa mada and you ni watumiaji wakubwa wa huu unga, bt 'mnapopendeza' nyie badala ya kudunga watoto mnakuja kudunga watu wazima humu jf siyo? Shame on you!
 
Jamani napita ila wa zenji nisalimieni wajna wangu Mohammed Raza naona siku hizi hasikiki amepatwa na nini? au anaridhika na mwenendo wa chama?
 
Ikiwa ungia Zanzibar basi wa kulaumiwa ni vyombo vya ulinzi, migration && police.Si dhani kama Zanzibar ina vyombo vyake vya ulinzi.....well i guess you can see where this is goin
 
..Polisi na Majeshi ni vyombo vya muungano.

..lakini watendaji wakuu na makamanda kwa vikosi vilivyoko Zanzibar ni wenyeji wa hukohuko.

..vilevile hili tatizo linaweza kuwa kubwa huku Tanganyika kuzidi hata Zanzibar.

..kinachofanya lionekane kubwa huko Zanzibar ni udogo wa eneo lake.

NB:

..vilevile tatizo hili nalisikia linazungumziwa zaidi kwa eneo la Unguja.

..je, Pemba hawana matatizo haya? how come wao wameweza kuyaepuka madawa ya kulevya wakati wenzao wa Unguja wameathirika?
 
Tatizo la madawa ya kulevya ni kubwa sana hapo Zenj, aidha kumekuwepo na njia nyingi za utumiaji wa madawa hayo. Miaka ya hivi karibu vijana watumiao madawa hayo walikuja na njia nyingine waitayo Flush blood ambapo aliyetumia madawa hutoa damu yake na kumpa mteja mwingine ambae hana uwezo wa kununua madawa hayo.

Ukosefu wa ajira kwa vijana wengi hapo visiwani kumetajwa kuwa ni sababu kubwa inayowafanya vijana wengi kutumia madawa hayo. Aidha kusema Muungano umechangia /umesababisha hayo ni uongo usio na mfano.

Awali, Zanzibar ilikuwa ni pepo ya wasafiri watumiao Bangi. Hii ilitokana na urahisi mkubwa wa kupatikana kwa bangi visiwani humo. Taratibu madawa mengine ya kulevya yalianza kuingia visiwani na kufikia kilele katika miaka ya tisini.

Hadi kufikia mwaka 2001, Zanzibar ilikuwa tayali imepata umaarufu mkubwa wa kuwa bandari ya kupitishia madawa ya kulevya. Umaarufu huu ulisadikiwa kufunika hata umaarufu wa soko la watumwa uliotokea miaka mia mbili iliyopita. Ukuuaji wa biashara ya ya madawa ya kulevya katika Zanzibar ulikwenda sambamba na uporomokaji wa bei ya karufuu katika soko la dunia na kupanda chati kwa biashara ya utalii.

Zanzibar kuwa pitisho kubwa la madawa ya kulevya katika ukanda wa Afrika ya Mashariki, kunahusishwa sana na mabadiliko ya ya kiutawala huko Afrika ya Kusini, ambapo utawala wa kibaguzi ulifikia kikomo. Ulinzi mkali katika bandari ya Mombasa baada ya ulipuaji wa balozi za USA huko Nairobi na Dar es Salaam ni sababu nyingine inayotajwa ya Zanzibar kuwa kimbilio la kupitishwa kwa madawa hayo. Aidha ubinafishwaji wa Uwanja wa ndege wa Zanzibar katika miaka ya mwishoni ya tisini umetajwa kuchangia kwa kiasi kikubwa kukua kwa upitishaji wa madawa hayo katika Zanzibar.

Matumizi ya madawa ya kulevya yamekuwa yakienda pamoja na uongezekaji wa maambukizi ya virusi vya ukimwi. Hii hasa kwa wale wanaojidunga sindano. Uchunguzi unaonyesha kuwa asilimia 46 ya watumiaji wa madawa hayo hushare sindano, huku zaidi ya asilimia 50 wakifanya ngono (group sex na anal sex) ili kupata madawa hayo. Baadhi ya vijana huweza kutumia hadi US$ 240 kwa mwezi kupta madawa hayo.
 
Sidhani kama kuna umuhimu wa kuogopa tena ukaribu na umbali na adui katika dunia ya sasa, kwani hata wakiwa mbali wanaweza kukufyatua. Mi nadhani tuuvunje tu
 
kuna haja wa Tanzania kupiga kura ya kuijitenga na kutengeneza nchi mbili Zanzibar na Tanganyika maana serikali ya mapinduzi zanzibar sasa haina upizani tena bali selikali ya umoja wa kitaifa kazi imebaki Tanganyika ambako chama tawala ni ccm. huku kwa mtazamo wangu Watanganyika mnaonaje tukawa taifa huru.Ni pendekezo langu katika mswaada wa katiba mpya.
 
Kwa yaliyotokea jana bungeni nafikiri sasa ni wakati muafaka wa kuwa na serikali tatu. Ya zanzibar, ya tanganyika na ya shirikisho
 
Mkuu hiyo ni kweli serikali mbili hazima maana kwa sasa!
 
Ni wakati muafaka kabisa kutafuta utaratibu wa kupata maoni ya wananchi kama wanataka muungano au la. Ushahidi wa kihistoria unaonyesha hilo halikuwahi kufanywa. Ni viongozi wao waliouamu huu muungano kwa niaba ya wananchi. Yawezekna walifanya hivyo kwa kuwa ulewa wa wananchi wa wakati ule ulikuwa mdogo wakaona ni muhimu wa waamulie. Ila sasa tunaelewa tunataka tuamue wenyewe. Itapendeza kama hili litafanyika kabla ya katiba mpya.
 
Wazanzibar
1.tunaburuzwa kwenye muungano
2.Tunachaguliwa rais wa zanzibar (kimkakati kwani CCM inawapitishia wagombea urais)
3. Dai jipya: TUMECHEZEWA RAFU MATOKEO YA FORM FOUR 2010 (wanataka baraza lao la mitihani)na malalamiko kibao.TUJITOE KWENYE MUUNGANO

BARA:tudumishe muungano jamani na misemo kibao ya Mwalimu.

My take:Tuwaachie zanzibar yao waone watafika wapi na siasa zao zisizo na hoja wala mashiko bali visasi vya kihistoria mara HANGA,ushiriki wa SEIF kumdhalilisha JUMBE,sijui mara Sultan alifanyaje yaan ajabu bin ajabu.

Vijana wa BARA tunataka siasaleo (sio siasahistoria ya CUF+-CCM)inayochipua hoja bila woga kwa maslahi ya taifa.Tumeingia kwenye ulingo mwingine wa kuikomboa nchi kutoka kwa Mafisadi.
 
Pamoja na mapungufu mengi ya mchungaji mtikila, lazima nikiri kuwa aliona mbali sana kudai serikali ya tanganyika. Madhara ya kutokuwa na serikali ya tanganyika ni pamoja na hayo tuliyoshudia live bungeni jana.
 
Back
Top Bottom