Mwiba,
Mkuu do really buy that?..
Zoezi hilo ni kuwaonyesha Wazanzibar wenye mawazo tofauti kwamba Jeshi letu lipo tayari kukabiri vikundi vidogo vidogo vinavyojenga na KUENEZA Fitna ktk Muungano. Hata siku moja usifikirie kwamba jeshi hilo lipo upande wa Visiwani, jeshi linaongozwa na Serikali ya Muungano na amri Jeshi mkuu ni rais wa Jamhuri. Mkuu hii ni nchi ya Kiafrika Ogopa sana nguvu ya Dola na nakuombeni msifikie kufikiria hivyo!.
Kitu kimoja binafsi nachokubaliana na Zanzibar ni kuwepo kwa nchi au Taifa inategemea na kipi kinachotangulia. Iwe NCHI au TAIFA ndio neno linalopaswa kutumia kuzitambulisha sehemu hizi mbili nje ya Muungano. Zanzibar ina sovereign yake ktk territory za visiwa vyake na ndio maana tuliunda MUUNGAMO. Sh. Abeid Karume alikuwa President wa Zanzibar siku na kabla ya Muunngano huwezi kuondoa hilo ktk Muungano na ndiye aliyeweka sahihi na kuchanganya mchanga. Pamoja na yote hayo still mtu unawqeza kuona tofauti ya mchanga ktk lundo la mchanganyiko kuwa upo mchanga wa sehemu mbili tofauti.
Neno, MUUNGANO haliji bila kuwepo makubalianano kati ya nchi mbili HURU..kwa hiyo hao viongozi wa Bara ni lazima wafahamu ukweli huo ambao haupingiki.
Sasa ni jinsi gani nchi zetu zinaweza kutumia rasilimali zetu ktk Muungano huu ni swala ambalo LAZIMA litazamwe upya kwa sababu wakati wa Muungano wa kwanza nchi zetu zote zilichukua mfumo wa UJAMAA ambao kila kitu kilikuwa centralised ktk serikali kuu. Mfumo huo tumeuacha miaka mingi sasa na ajabu swala la mgao wa pato la Taifa haukufanyiwa marekebisho isipokuwa UFISADI wa Azimio la Zanzibar kuwapa nafasi viongozi kujijenga wao.
Hapa inatueleza nini kwetu sisi wananchi?.. ni kwamba serikali zetu, viongozi wetu na hasa chama cha Mapinduzi ni chama kilichoingiliwa na Majambazi!.. Leo hii nina mashaka makubwa kama wapo wazee waliopigania UHURU wa nchi zote hizi mbili ktk madaraka kuwaelekeza hawa vijana viongozi. Sidhani kama wapo wazee viongozi wenye sauti ktk serikali hiii ya Muungano ambao walihudhulia mazungumzo ya awali kuhusiana na Muungano, Pengine wengi wameisha kufa ama ndio hawashirikishwi kabisa...
La muhimu kabisa kwanza ni kutambua umuhimu wa Muungano wetu, msiwe na fikra zinazotanguliwa na umaskini yaani nikiwa na maana ya NJAA!.. Uchumi wa nchi zetu umekuwa ukigawanywa kama vile maskini anavyopata.. Ni kweli Bara walipopata Gas na Madini waliona wameuchinja wakajitenga lakini ni akina nani haswa?.. Utakuta ni viongozi hawa vijana ambao Hata Bara kwenyewe wameikimbia Familia yao (Bara) kutafuta makazi mapya.. Haya ndiyo maisha ya mtu maskini siku akipata huikimbia hata Familia yake akajitenga kabisa kuogopa fedha zake zitakwisha kujaribu kuokoa ndugu zake.
Sasa tatizo jingine ni Zanzibar, maskini mwingine ambaye pia kaona kuna dalili za Utajiri! Kwa akili ya kimaskini anatafuta naye kujitenga mapema na hakika wanaoshinikiza swala hili ni viongozi maskini. Viongozi ambao nina hakika siku Zanzibar wakipata Utajiri huo watachukua kila kitu na kujitenga na Familia yao (Zanzibar) kutafuta makazi mapya pengine Arabuni ama Bara. Hawa ndio viongozi Mafisadi wasiokuwa na haya ambao wanasubiri tu nafasi za kuibia wananchi wake.
Kwa hiyo wajomba sisi wananchi, wa bara na visiwani ni muhimu kutazama kwanza ADUI wa maendeleo wa pande zote hizi ni nani? nani adui wa maendeleo ya visiwani na Bara utakuta ni viongozi wetu wenyewe!.. Visiwani wakitaka kujitenga ili wapate kuvuta kirahisi na Bara nako viongozi wetu ambao tayari wameisha kamata Bara sasa Uroho wa Utajiri umevuka bahari na kutazama Zanzibar!.. Huko Zanzibar nako viongozi wanaona duh.. wakuu hizi zangu mimi nyie mnavuta Bara na sisi tuachieni huku, hakuna kiongozi mwenye kutazama maslahi ya nchi.. HAKUNA!
Ikiwa leo Bara pamoja na rasilimali zote hizo bado tupo nyuma kiuchumi hata Rwanda imeshaanza kutukimbia kweli jamani bado mna imani na viongozi wetu.. Kikwete alikuwa tegemeo la wengi lakini hadi leo hiii ameonyesha HAWEZI kuwa kiongozi bora! Pengine kiti cha IKULU hakihitaji MUUNGWANA kwani ktk mazingira yetu ya Umaskini ni moja ya udhaifu wa kiongozi.
Ushauri wangu wa Mwisho ni kwamba bado tuna wakati na nafasi kubwa ya kufanya Marekebisho.. Tuzitazame nchi nyingine na hasa Canada Muungano wao umejengwa vipi. Kuna Nchi kama Alberta ambazo ni tajiri kwa mafuta na uchumi wake unapanda juu kuliko sehemu nyingine zote, lakini bado kuna fungu huchangia ktk maendeleo ya sehemu maskini. Hivi majuzi Jimbo (nchi) jingine ambalo lilikuwa maskini ktk rasilimali wamevumbua pia mafuta (Saskachewan) na uchumi wake ghafla umepanda lakini hata siku moja hawakulalamikia umaskini wao kwa kuutazama Muungano na mfumo mzima wa Kiuchumi...
Pengine swala la Zanzibar ni zaidi ya hayo kama lilivyo jimbo la Quebec (jimbo la Kifaransa) ambao wao hujiona tofauti na wanataka UHURU wao wenyewe. Uhuru ambao unasukumwa na wanasiasa hali wananchi wake kwa hesabu kubwa wanataka kuwa ndani ya Muungano. Na kwa bahati mbaya kutokana na kujitenga kwao wao ndio maskini kupita province nyinginezo, uchumi wao ulianguka toka siku waliotangaza kutaka kujitenga..They never recovered!
Mkuu do really buy that?..
Zoezi hilo ni kuwaonyesha Wazanzibar wenye mawazo tofauti kwamba Jeshi letu lipo tayari kukabiri vikundi vidogo vidogo vinavyojenga na KUENEZA Fitna ktk Muungano. Hata siku moja usifikirie kwamba jeshi hilo lipo upande wa Visiwani, jeshi linaongozwa na Serikali ya Muungano na amri Jeshi mkuu ni rais wa Jamhuri. Mkuu hii ni nchi ya Kiafrika Ogopa sana nguvu ya Dola na nakuombeni msifikie kufikiria hivyo!.
Kitu kimoja binafsi nachokubaliana na Zanzibar ni kuwepo kwa nchi au Taifa inategemea na kipi kinachotangulia. Iwe NCHI au TAIFA ndio neno linalopaswa kutumia kuzitambulisha sehemu hizi mbili nje ya Muungano. Zanzibar ina sovereign yake ktk territory za visiwa vyake na ndio maana tuliunda MUUNGAMO. Sh. Abeid Karume alikuwa President wa Zanzibar siku na kabla ya Muunngano huwezi kuondoa hilo ktk Muungano na ndiye aliyeweka sahihi na kuchanganya mchanga. Pamoja na yote hayo still mtu unawqeza kuona tofauti ya mchanga ktk lundo la mchanganyiko kuwa upo mchanga wa sehemu mbili tofauti.
Neno, MUUNGANO haliji bila kuwepo makubalianano kati ya nchi mbili HURU..kwa hiyo hao viongozi wa Bara ni lazima wafahamu ukweli huo ambao haupingiki.
Sasa ni jinsi gani nchi zetu zinaweza kutumia rasilimali zetu ktk Muungano huu ni swala ambalo LAZIMA litazamwe upya kwa sababu wakati wa Muungano wa kwanza nchi zetu zote zilichukua mfumo wa UJAMAA ambao kila kitu kilikuwa centralised ktk serikali kuu. Mfumo huo tumeuacha miaka mingi sasa na ajabu swala la mgao wa pato la Taifa haukufanyiwa marekebisho isipokuwa UFISADI wa Azimio la Zanzibar kuwapa nafasi viongozi kujijenga wao.
Hapa inatueleza nini kwetu sisi wananchi?.. ni kwamba serikali zetu, viongozi wetu na hasa chama cha Mapinduzi ni chama kilichoingiliwa na Majambazi!.. Leo hii nina mashaka makubwa kama wapo wazee waliopigania UHURU wa nchi zote hizi mbili ktk madaraka kuwaelekeza hawa vijana viongozi. Sidhani kama wapo wazee viongozi wenye sauti ktk serikali hiii ya Muungano ambao walihudhulia mazungumzo ya awali kuhusiana na Muungano, Pengine wengi wameisha kufa ama ndio hawashirikishwi kabisa...
La muhimu kabisa kwanza ni kutambua umuhimu wa Muungano wetu, msiwe na fikra zinazotanguliwa na umaskini yaani nikiwa na maana ya NJAA!.. Uchumi wa nchi zetu umekuwa ukigawanywa kama vile maskini anavyopata.. Ni kweli Bara walipopata Gas na Madini waliona wameuchinja wakajitenga lakini ni akina nani haswa?.. Utakuta ni viongozi hawa vijana ambao Hata Bara kwenyewe wameikimbia Familia yao (Bara) kutafuta makazi mapya.. Haya ndiyo maisha ya mtu maskini siku akipata huikimbia hata Familia yake akajitenga kabisa kuogopa fedha zake zitakwisha kujaribu kuokoa ndugu zake.
Sasa tatizo jingine ni Zanzibar, maskini mwingine ambaye pia kaona kuna dalili za Utajiri! Kwa akili ya kimaskini anatafuta naye kujitenga mapema na hakika wanaoshinikiza swala hili ni viongozi maskini. Viongozi ambao nina hakika siku Zanzibar wakipata Utajiri huo watachukua kila kitu na kujitenga na Familia yao (Zanzibar) kutafuta makazi mapya pengine Arabuni ama Bara. Hawa ndio viongozi Mafisadi wasiokuwa na haya ambao wanasubiri tu nafasi za kuibia wananchi wake.
Kwa hiyo wajomba sisi wananchi, wa bara na visiwani ni muhimu kutazama kwanza ADUI wa maendeleo wa pande zote hizi ni nani? nani adui wa maendeleo ya visiwani na Bara utakuta ni viongozi wetu wenyewe!.. Visiwani wakitaka kujitenga ili wapate kuvuta kirahisi na Bara nako viongozi wetu ambao tayari wameisha kamata Bara sasa Uroho wa Utajiri umevuka bahari na kutazama Zanzibar!.. Huko Zanzibar nako viongozi wanaona duh.. wakuu hizi zangu mimi nyie mnavuta Bara na sisi tuachieni huku, hakuna kiongozi mwenye kutazama maslahi ya nchi.. HAKUNA!
Ikiwa leo Bara pamoja na rasilimali zote hizo bado tupo nyuma kiuchumi hata Rwanda imeshaanza kutukimbia kweli jamani bado mna imani na viongozi wetu.. Kikwete alikuwa tegemeo la wengi lakini hadi leo hiii ameonyesha HAWEZI kuwa kiongozi bora! Pengine kiti cha IKULU hakihitaji MUUNGWANA kwani ktk mazingira yetu ya Umaskini ni moja ya udhaifu wa kiongozi.
Ushauri wangu wa Mwisho ni kwamba bado tuna wakati na nafasi kubwa ya kufanya Marekebisho.. Tuzitazame nchi nyingine na hasa Canada Muungano wao umejengwa vipi. Kuna Nchi kama Alberta ambazo ni tajiri kwa mafuta na uchumi wake unapanda juu kuliko sehemu nyingine zote, lakini bado kuna fungu huchangia ktk maendeleo ya sehemu maskini. Hivi majuzi Jimbo (nchi) jingine ambalo lilikuwa maskini ktk rasilimali wamevumbua pia mafuta (Saskachewan) na uchumi wake ghafla umepanda lakini hata siku moja hawakulalamikia umaskini wao kwa kuutazama Muungano na mfumo mzima wa Kiuchumi...
Pengine swala la Zanzibar ni zaidi ya hayo kama lilivyo jimbo la Quebec (jimbo la Kifaransa) ambao wao hujiona tofauti na wanataka UHURU wao wenyewe. Uhuru ambao unasukumwa na wanasiasa hali wananchi wake kwa hesabu kubwa wanataka kuwa ndani ya Muungano. Na kwa bahati mbaya kutokana na kujitenga kwao wao ndio maskini kupita province nyinginezo, uchumi wao ulianguka toka siku waliotangaza kutaka kujitenga..They never recovered!