Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na kero zake: Je, tuuvunje?
Ingawa nina malalamiko mengi na muungano wa sasa, lakini bado sidhani kama ni wazo zuri kuvunja muungano. Hii mipaka mingi iliwekwa na wakoloni. Waafrika kabla ya wakoloni wa kiarabu na kizungu, tulikuwa tukiishi pamoja.

Kutengana sio suluhisho katika mgogoro wa sasa!

Nakubali 100%. Tena tukianzisha 'Jamhuri ya Afrika' ni poa zaidi Mwafrika wa Kike. (Japo ni ndoto, ukifikiria nani atakuwa nani kati ya Mugabe, na Ghadafi na Kibaki. Na Dafur, na Comoro, na Congo. Na Chenge na Billal na Mkapa na Mkono na Karamagi na Rostam).

Swali langu dogo sana. Mkataba wa Muungano uko wapi? Siombei usiwepo. Na sisemi haupo. Na hata kama haupo haimaanishi hatujaungana. Na kama tumeungana na mkataba haupo sidhani tuuvunje!

Najifunza historia tu. Mkataba uko wapi?
 
I wish wakati wa sherehe za mwaka huu wangeupeleka pale makumbusho ili kila anyetaka aweze kuuona ukiwa kwenye kioo atreast watu waweze kujilizisha kuwa upo. Maana tunapoelekea watu watakubali kuwa haupo.
 
Ingawa nina malalamiko mengi na muungano wa sasa, lakini bado sidhani kama ni wazo zuri kuvunja muungano. Hii mipaka mingi iliwekwa na wakoloni. Waafrika kabla ya wakoloni wa kiarabu na kizungu, tulikuwa tukiishi pamoja.

Kutengana sio suluhisho katika mgogoro wa sasa!
hivi ni lazima kuchangia kila mada japo huna ufahamu nayo? hili la muungano hebu kaa pembeni...
 
wanaJF kama mnataka kufahamu kuwa huu umerekebishwa au la angalieni kwenye katiba ya jamhuri ya muungano wa tanzania 1977 as amended from time to time pages flani za mwisho mtaona the amended version ya articles of the union.
 
Muungano ni kama ndoa..na kama ikishindikana kuishi pamoja basi tupeane talak kila mmoja atazame ustaarabu wake.

Muungano haukuwepo na unaweza usiwepo.Kwa wazanzibari wengi wao be it CUF au CCM deep down wanaamini kuwa muungano hauna faida kwao, na zaidi ule mkutano wa Butiama ambao CCM ZNZ walimtisha JK kuwa kama anataka kuwasikiliza hao CUF basi na wao watarudi ZNZ kivyao.Na hapo bado hatujazungumzia 60/40

Bara nao wanaona kuwa watu wa ZNZ wanaishi kwa income support ya kodi wa watu wa Bara sasa je mnasemaje wana JF tuuvunje huu muungano?

Maoni yenu Tafadhali


JAMBO FORUMS WHERE WE DARE TALK OPENLY
 
Wenye uwezo wa kufanya hili ni serekali ya CCM iliyopo madarakani and we all know what they will say, we have heard it before- 'tupate ridhaa ya wananchi!' as if wakati wa kuunda huo muungano kulikuwa na kitu kama hicho.
 
... inanikumbusha lile jaribio la G55 miaka ya 1990's.

Wakati huo naona kulikuwa na demokrasia kuliko huu usanii tunafanyiwa sasa hivi.
 
Hakuna sababu za msingi za kuvunja muungano, ila zipo kero ambazo zinapaswa kushughulikiwa siyo kuvunja muungano. nadhani yangekuwa yanatolewa mapendekezo yatakayopelekea kudumisha muungano. Hata katika mfano ulioutoa wa ndoa, si vema kuvunja ndoa kwasisi Wakristo Biblia inasema 'Mungu anachukia wanandoa kuachana' Mtu mzima akiona ndoa inayumba anapaswa kutatua matatizo au changamoto za ndoa siyo kutoa taraka.
 
cha ajabu wanaotaka muungano na hasa toka bara hawako tayari kueleza kwa nini tuendelee kuwa na hili jambo

Hii ni kama ndo ikishindikana kila mmoja anatazama lwake

 
Muungano si vizuri kuuvunja ila tunahitaji kurekebisha katiba na muundo wa muungano ili uendane na hali ya sasa ya siasa. Tutahitaji seikali tatu na hilo liko wazi na nilazima litakuja kuwa ila kwa sasa tunaliahirisha tu.
 
Muungano si vizuri kuuvunja ila tunahitaji kurekebisha katiba na muundo wa muungano ili uendane na hali ya sasa ya siasa. Tutahitaji seikali tatu na hilo liko wazi na nilazima litakuja kuwa ila kwa sasa tunaliahirisha tu.

You are true, huu ni mtazamo wangu pia.
 
cha ajabu wanaotaka muungano na hasa toka bara hawako tayari kueleza kwa nini tuendelee kuwa na hili jambo

Hii ni kama ndo ikishindikana kila mmoja anatazama lwake


wengine tuna wachumba wa kiunguja ebo!! mambo ya kusubiria visa si utakuta mchumba ameshachukuliwa na mwingine.

Imefikia wakati huu muungano tuujadili kwa mapana na marefu wanancho wote washirikishwe kama ni kuunda upya tufanye hivyo.
 
unanikumbusha mambo ya sports wamakunduchi hawavundi, wanasema kina mama wa kibongo si mzaha wao ukiwauliza watasema udumu tu
 
Hapana hatutakiwi kuuvunja Muungano kwani amini usiamini Wapemba wataleta mapinduzi makubwa ambayo yatatuokoa hadi sisi wa bara kutoka mikononi mwa Chama Cha Mafisadi kwani wananchi wa kule wameshaelewa kuliko wa huku Bara amao wengi bado hawajazinduka.
 
Back
Top Bottom