Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na kero zake: Je, tuuvunje?
Acheni jazba ,inaonekana hata humu mumepoteza muelekeo na sasa ni wazi uzalendo wa Utanganyika unawaandama japo wengine mnaota kuwa Tanganyika ilikwisha kufa,hao siwezi kuwaelewesha ni sawa na kumtambua mwendawazimu aliepona na kumpa uhuru.
Hizi serikali mbili ni tofauti ,na kila serikali ina mamlaka yake na mipaka yake ,sasa inapohojiwa kuwa Je serikali ya Muungano ina mamlaka juu ya serikali ya Zanzibar ,msiwe na pupa na kukurupuka na kujijibu wenyewe ,maana mnajiuliza halafu mnajijibu ,kwa nini msitazame mipaka ya serikali hizi ? Mimi sitaki kuweko upande wenu kwa mnayoyaona mambo haya ni mepesi na hivyo mnajibu vile mnavyojiuliza wenyewe ,very interesting !
Sijui Mwakiyembe ni Mwanasheria atulie na hawezi kujibu hoja hizi za viongozi wa Zanzibar maana ni za kipumbavu, nilisema katika ile topik ya Mwakiyembe ndie aliekuwa hana adabu ,maana amevunja hata amri ya Spika ,mnakuja na kuhoji eti nikatazame nukuu za Bunge , mimi si mwana siasa wala mwanasheria ni mlala hoi tu,lakini kauli ya Mwakiyembe at the first hearingi niliiona amekwisha kosea kwa maneno aliyotumia ,haihitaji misamiati mingi kuielezea na nilisema Mwakiyembe akibanwa basi atakuwa matatani kwa kauli aliyotumia hasa maneno au lugha chafu ,nikatoa Chalenge ,yatazamwe maneno aliyosema Shamhuna na aliyosema Mwakiyembe ,mnaposikia kila ngoma ikivuma ndipo inapokaribia kupasuka ,Mwakiyembe amepasuka na sasa hafai na ametoa mtihani mwengine kwa Bunge na Raisi Kikwete ,japo kwa mtazamo wenu mnaona hana kosa ,lakini sivyo Mwakiyembe ametenda kosa tena baya zaidi hata kuliko wale wanaosema Zanzibar si nchi.
Ninachowataka msiingie katika kujigawa mkaona labda Mwiba niMpemba Mzanzibari anatetea WaZanzibari na Mwakiyembe ni mwenzetu Chogo basi tumlinde ,mtakuwa mnakosea , mimi ninaweza kuwa bora kwa Mwakiyembe kuliko nyinyi mnaojidai kumlinda na kumkazania ashike na kusimamia msimamo wake ,hamumtakii mwema Mwakiembe , mmesikia mmoja alipohojiwa kuhusu madai ya Zanzibar na kauli ya Mwakiyembe na taratibu za Bunge ,jamaa alijibu waandishi nendeni katafuteni ,soma hiki kipande :-
...Naye Naibu Spika wa Bunge, Bibi Anne Makinda alipoulizwa kuhusu kanuni za Bunge zinasemaje kuhusu shinikizo anazopewa Dkt. Mwakyembe, alimtaka mwandishi azitafute ili ajionee mwenyewe... Umeona ustadi wa kukwepa suala ,huyu Bibi Anne ameshaona tatizo linalomnyemelea Mwakiyembe.
Ushauri wa bure kwa Mwakiyembe ,awaombe radhi ikiwa anajiona ana kosa au hana kosa na atakuwa amefunga mjadala kiustaarabu kabisa.Mwakiyembe afahamu kuwa yeye ni mbunge na natumai anaifahamu CCM vilivyo ,Mwakiyembe amegusa sega ,sega ambalo linawanufaisha magogo wa CCM bara , natumai mtaiona factor na hatari inayoplay kwa Mwakiyembe.


'Anger is a condition whereby the mounth works faster than the brain'

Inaelekea ulikwa unaandika kama vile unvyoongea upupu huko Bungeni. Rekebisha hiyo text tuweze kuisoma .Otherwise semi iliteracy may just mean it.
 
Kuna mchangiaji humu anajibu hoja ki-mdebwedo. When it comes to worse, the Constitution prevails. Not hearsay, not opinion. Ukisoma jinsi Jaji A Ramadhani na wenzake walivyochambua vifungu hadi kufikia maamuzi kwamba hakukuwa na uhaini Zanzibar, ndio mfumo huo huo utakaotumika kuamua nani mkubwa: Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zenj, au Waziri Mkuu..

Kama hoja ni kuvunja muungano... basi hoja na iwe kuvunja muungano. Tatizo, wanaotaka kuvunja muungano hawana ujasiri, wanatumia vi-hoja vyepesi vyepesi, typical Zanzibari. Muda wa kupiga Kiswahili umekwisha, ndiyo maana Waziri Pinda mpaka leo hajabadili kauli kwamba Zanzibar si nchi, that's how the books say.

My vote: Let Zanzibar Go, Its Been a Pain all Along. Tanganyika has enough problems to focus on, Umaskini, Mafisadi n.k
 
Tatizo la Watanganyika ni bullies, mnawalazimisha Wazanzibari wabaki kwenye ndoa ambayo wenzenu wameichoka.

Wakisema Zanzibar ni nchi, je inaongeza au kupunguza nini kwenye tija ya mwananchi wa kawaida? Sana sana ni feel good factor tu kwa Wazanzibari kujisikia nao wana nchi yao.

Kwa mfano hapa UK, mara nyingi tu Scotland wanajiona kama ni nchi, lakini sijawahi kusikia waziri akilalamika wao kusema si nchi. Katiba iko wazi na inaeleza wajibu wa kila serikali.

Huu mjadala wote mimi naona ni kupoteza muda tu kuongelea mambo ambayo hatuna uwezo wa kuyatatua zaidi ya kuwaachia majaji kuamua. Mjadala huu hauna tofauti na mijadala ya dini, mtu akiwa na imani yake hata siku moja huwezi kumbadili. Muhimu ni kila mtu kuishi kwa amani kwa kuzingatia sheria na taratibu zilizopo.

Haya mambo ya nani mkubwa zaidi ya mwenzake hayana maana yoyote. Kama mmoja ni mkubwa, basi ukubwa wake uongozane na delivery ya services za maana kwa hao waliochini. Nini maana ya kuwa mkubwa huku kuwepo au kutokuwepo kwako hakuongeze tija yoyote?

Watu wanahangaika kwa umaskini na maradhi, nchi nzima inahangaikana kupandisha misuri ili kujua nani mkubwa kuliko mwenzake?

Sitashangaa tunakoenda ni kutwangana risasi shauri ya kutaka kuonyeshana nani mkubwa, baada ya hapo tunarudi hatua 20 nyuma kwa umaskini. Angalia yale ya Georgia.

Give me peace! I don't care Zanzibar ni nchi au sio nchi, Muhimu ni wananchi wetu kupata huduma muhimu na kuendelea kuishi kwa amani na utulivu kama binadamu wengine wa dunia hii. Kama wanaweza kuishi hivyo ndani ya muungano sawa, wakiamua kujitenga pia sawa. Hakuna sababu ya kutumia mtutu kulazimisha ndoa iliyochuja.

You are a real MTANZANIA. Hongera sana. Nakubaliana nawe moja kwa moja. Tuna shida nyingi zinahitaji kutatuliwa. Na tuchangiane mawazo katika hili.
 
Sekenke,

Ni vizuri ukamtaja tu kama ni Mwiba au huyu Ngekewa. Kwa kweli wanachoandika ni purely kutoka kichwani mwao na si katika maandiko ya katiba na uamuzi wa mahakama.

Ukiwauliza maswali madogo kama Pinda ni waziri mkuu wa wapi, Hawana majibu.

Ngoja nijadiliane na wengine, ndio maana nimesema kuwa hii ni kama Palestine na Israel.
 
Acheni jazba ,inaonekana hata humu mumepoteza muelekeo na sasa ni wazi uzalendo wa Utanganyika unawaandama japo wengine mnaota kuwa Tanganyika ilikwisha kufa,hao siwezi kuwaelewesha ni sawa na kumtambua mwendawazimu aliepona na kumpa uhuru.
Hizi serikali mbili ni tofauti ,na kila serikali ina mamlaka yake na mipaka yake ,sasa inapohojiwa kuwa Je serikali ya Muungano ina mamlaka juu ya serikali ya Zanzibar ,msiwe na pupa na kukurupuka na kujijibu wenyewe ,maana mnajiuliza halafu mnajijibu ,kwa nini msitazame mipaka ya serikali hizi ? Mimi sitaki kuweko upande wenu kwa mnayoyaona mambo haya ni mepesi na hivyo mnajibu vile mnavyojiuliza wenyewe ,very interesting !
Sijui Mwakiyembe ni Mwanasheria atulie na hawezi kujibu hoja hizi za viongozi wa Zanzibar maana ni za kipumbavu, nilisema katika ile topik ya Mwakiyembe ndie aliekuwa hana adabu ,maana amevunja hata amri ya Spika ,mnakuja na kuhoji eti nikatazame nukuu za Bunge , mimi si mwana siasa wala mwanasheria ni mlala hoi tu,lakini kauli ya Mwakiyembe at the first hearingi niliiona amekwisha kosea kwa maneno aliyotumia ,haihitaji misamiati mingi kuielezea na nilisema Mwakiyembe akibanwa basi atakuwa matatani kwa kauli aliyotumia hasa maneno au lugha chafu ,nikatoa Chalenge ,yatazamwe maneno aliyosema Shamhuna na aliyosema Mwakiyembe ,mnaposikia kila ngoma ikivuma ndipo inapokaribia kupasuka ,Mwakiyembe amepasuka na sasa hafai na ametoa mtihani mwengine kwa Bunge na Raisi Kikwete ,japo kwa mtazamo wenu mnaona hana kosa ,lakini sivyo Mwakiyembe ametenda kosa tena baya zaidi hata kuliko wale wanaosema Zanzibar si nchi.
Ninachowataka msiingie katika kujigawa mkaona labda Mwiba niMpemba Mzanzibari anatetea WaZanzibari na Mwakiyembe ni mwenzetu Chogo basi tumlinde ,mtakuwa mnakosea , mimi ninaweza kuwa bora kwa Mwakiyembe kuliko nyinyi mnaojidai kumlinda na kumkazania ashike na kusimamia msimamo wake ,hamumtakii mwema Mwakiembe , mmesikia mmoja alipohojiwa kuhusu madai ya Zanzibar na kauli ya Mwakiyembe na taratibu za Bunge ,jamaa alijibu waandishi nendeni katafuteni ,soma hiki kipande :-
...Naye Naibu Spika wa Bunge, Bibi Anne Makinda alipoulizwa kuhusu kanuni za Bunge zinasemaje kuhusu shinikizo anazopewa Dkt. Mwakyembe, alimtaka mwandishi azitafute ili ajionee mwenyewe... Umeona ustadi wa kukwepa suala ,huyu Bibi Anne ameshaona tatizo linalomnyemelea Mwakiyembe.
Ushauri wa bure kwa Mwakiyembe ,awaombe radhi ikiwa anajiona ana kosa au hana kosa na atakuwa amefunga mjadala kiustaarabu kabisa.Mwakiyembe afahamu kuwa yeye ni mbunge na natumai anaifahamu CCM vilivyo ,Mwakiyembe amegusa sega ,sega ambalo linawanufaisha magogo wa CCM bara , natumai mtaiona factor na hatari inayoplay kwa Mwakiyembe.

Pengine hukutaka kuwafungulia lakini mimi nitajaribu kuwafungulia. Tatizo la wenzetu huwa hawayaelewi mambo ya Zenji na kukurupuka kwa habari za waandishi uchwara wasioijuwa Zenji.
Umaarufu na nafasi aliyonayo Mwakyembe unatokana na nguvu za Zanzibar na sasa ameshawakanyaga basi na tuangalie kama atarejea tena Bungeni. Mwakyembe aliwashinda Mtandao ka backing ya Zanzibar, katika kinyanganyiro cha ubunge. Backing ya Zanzibar kwa Mwakyembe ilianzia na midahalo iliyokuwa ikifanywa ndani ya TVZ (TV ya serikali ya Zamzibar). idahalo hiyo ikifanywa kati yake na waasheria wengine wa Bara akiwemo DR Mvungi wa NCCR na Dr. Kabodi (kama nimelipatia vizuri jina). Kwenye midahalo hii Mwakyembe alionekana moja kwa moja kuipigia debe Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na hivyo SMZ ikamzawadia kuwa mjumbe wa Kamati ya Mwafaka wa CCM na CUF(yeye alikuwa mjumbe pekee kutoka Bara)/

Uhusiano huo ndio uliompa umaarufu na kumfanya awe na Gutts za kuomba ubunge na akaweza kuvuka wikwazo vya Mtandao kwa backing ya Zanzibar. Fadhila zake ni hizi na hivyo tungojee.
 
ama Kweli Tanzania Tuna Viongozi...




kweli Mkuu Mwiba Unataka Dr Mwakyembe Na Elimu Yake Yote Awaombe Hawa Watu Wasiojua Katiba Wala Maana Ya Muungano Msamaha. Hii Nithamu Ya Woga Imepitwa Na Wakati, Jk Anatakiwa Atoe Onyo Kali Kwa Karume Kuwa Awafundishe Nithamu Viongozi Wa Visiwani La Sivyo Awaathibu Yeye Kwa Nguvu Alizonazo Kama Kiongozi Wa Jamhuri.

Hizi Kauli Huwa Zinachimba Mashimo Ambayo Kuyafukia Sio Rahisi.

Ubavu Anao Au Hataki Kurejea 2010?
 
Kauli ya SMZ inatoa picha hii moja kubwa ama SMZ haitambui Katiba ya Jamhuri ya Muungano au SMZ ina wajinga wasiojuwa wajibu wao au kuifahamu Katiba.

Katiba ya Jamhuri inazungumza Waziri Mkuu kama nafasi ya tatu kutoka Rais na makamu wa Rais.

Waziri mkuu huteuliwa na Rais na kisha hidhinishwa kwa kura za Wabunge ambao ni kutoka pande zote za Muungano.

Maamuzi ya bunge la Muungano ni ya Tanzania si ya Tanganyika (Tanzania bara).

Sasa kama Waziri Mkuu anapewa kura ya kuhalalishwa na Wabunge kutoka Zanzibar, je hicho kitendo maana yake ni nini?

Je SMZ leo inawakana wabunge wa Zanzibar katika Bunge la Muungano? Je SMZ inaikana Katiba ya Jamhuri wa Muungano? Je huo si Uhaini?

Mseto si lazima uwe wa chakula fulani na unaweza ukachanganya mtiririko wa vyakula na ukabaki kuwa mseto . Muungano unavyouona wewe sio ulivyo bali ni mchanganyiko usioeleweka hivyo tunahitaji recipe iliyo wazi na hili ndilo wanalogombania Wazanzibari. Huu mtindo wa mkubwa ndie sahihi na mkubwa achukuwe chake na cha mwenziwe ndio unaokupeni tabu ndugu zetu.

TANBIHI: Mwwerevu kuelimishwa na Mjinga ndiko huku.
 
Wakuu tusichanganye mambo hapa, straight to the point Zanzibari ni Mkoa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa maneno mengine ni only a State kama Rukwa na Manyara kama kuna asiyetaka dawa ni kubadili katiba ili Zanzibar iwe Nchi ndani ya Muungano wa Tanzania.

Rais wa Zanzibar ni RC, kama ma-RC wengine wa Rukwa na Manyara, kama sio Mtwara, rais anapokuwa hayupo katiba iko very clear anakaimiwa na Makamu wa Rais Shein, na yeye akiwa hayupo nafasi ya Rais inakaimiwa na Waziri Mkuu, na yeye akiwa hayupo inakaimiwa na Spika wa bunge,

Rais wa Zanzibar is no where in the picture, sasa kama sio RC wa mkoa ni nani huyu? Kama wa-Zanzibari wana tatizo hapo basi waende kwenye katiba, tumechoka sana na nonesense! no solution so far wanaonekana kuamua kuwa part of the problem, badala ya kuwa part of the solution sasa sisi Bara hatuwezi kuwasaidia kwa hili, ni uamuzi wao kusuka au kunyoa!


Sisi Bara tunaondoka!

MAMBO sivyo yalivyo BABA, MATAKWA YAKO YAWEKE KWAKO.
 
Tunachopinga wengi ni hypocrisy ya hawa wenzetu. Utadaije sovereignty ndani ya muungano? Si watamke wazi kuwa Muungano kama ulivyo haukidhi mahitaji yao kwa hiyo uvunjwe ili tubaki na ushirikiano wa nchi mbili zilizo na full sovereignty! Kigugumizi cha nini?
 
KWA TAARIFA HIYO: SERIKALI YA ZANZIBAR IMEJIMALIZA YENYEWE
Wakuu nimekuwa consistent toka juzi kuwa hoja alizozi"raise" Dk. Mwakyembe ni zamsingi mno ukiziangalia kwa makini. Angalia sasa statement kutoka Serikali ya Zanzibar:
(a) kwamba PM hana authority over Zanzibar, mwenye authority ni huyo Chief Minister wao! PM na Chief Minister ni level moja!
(b)hawawajibiki kwa Bunge wala Serikali ya Jamhuri ya Muungano;
(c)ina vikosi vya majeshi!
Hii ni nini kama si uasi! PM anapigiwa kura kwenye Bunge na wabunge wanaochaguliwa na Wazanzibari na Watanzania BARA. Ana direct authority Zanzibar kwenye masuala yote ya Muungano ambayo ni mengi: mambo ya nchi za nje, ulinzi na usalama, polisi, emergency matters, citizenship, immigration, loans and foreign trade, income tax, customs, bandari, usafiri wa anga, posta, simu, sarafu (fedha), leseni za viwanda, takwimu, elimu ya juu, mafuta, gesi asilia, mitihani ya taifa, utafiti, utabiri wa halio ya hewa, mahakama ya rufaa, vymana vya siasa n.k. (Ibara ya 4 ya Katiba ya Muungano na Nyongeza ya kwanza ya Katiba) Sasa hiyo "sovereign" state ya Zanzibar imebaki na nini cha msingi kutukoromea kila kukicha na kudai wimbo wao wa taifa na bendera?
Kwa hiyo Kikwete ni Rais wa wabara tu? Makubwa!

Serikali ya Zanzibar leo inadiriki kutamka kuwa ina majeshi ya kwake? Mbona wanainajisi Katiba? Ibara ya 147 inasema ini marufuku yeyote yule kuunda au kuweka jeshi la aina yeyote isipokuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania! Ndiyo maana Shamhuna alitamka kuwa "kipindi cha kutishana kimepita", kwa maana ya kwamba sasa wamejizatiti, Bara tukileta ujinga watatudhibiti hata kijeshi!
Nimeisoma taarifa ya Serikali ya Zanzibar mara sita, ni hoja za kitoto zinazokwepa hoja ya msingi aliyoi"rasie" Mbunge Mwakyembe: Shamhuna ana mamlaka gani kum"criticise" na kumpinga PM, bosi wake, na kuacha kutumia vyombo vya kiserikali vya ku"handle" misuguano ya kimuungano, kaka huo si utovu wa nidhamu? Sasa kuna haja gani kuwa na Makamu wa Rais (Mzanzibari)na Waziri specifically for Muungano ambao kwanza ni Wazanzibari na ni kiungo kikuu cha kikatiba cha Serikali ya Muungano na Zanzibar?
Nilicheka sana juzi wakati Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Kiongozi, Bw. Hamza Hassan Juma, alipoongea na waandishi wa habari na kukataa kujibu maswali ya ziada. Mwandishi mmoja wa Zanzibar (jina silisemi sasa) akanieleza: "angejibu nini mtu mwenyewe hata taarifa yenyewe alikuwa hajaielewa, alikuwa anasoma tu kama kasuku. Unawajua mawaziri wa Karume - huyo jamaa ni darasa la saba na profession yake fundi cherehani". Sijui kama ni kweli, lakini washikaji you are free to cross-check. lakini hawa ndo waobeba hatma ya maisha yetu!

Mkuu najisi ya mmoja si najisi kwa mwengine. Hiyo najisi unayoiona wewe si najisi kwa Viongozi wa Zanzibar na wa Muungano hata Nyerere wakati wa uhai wake. Kama ulikuwa hujui kama wana vikosi viongozi wanajuwa na wao wangekuwa na uwezo wa kuchukua hatuwa kwa vitendo na si kuropoka tu kama wewe. Kwa nini hawajachukua hatuwa labda najisi hii kwao ni halali.
 
mwakyembe yuko sahihi. kumbuka tena huyu ni mtaalamu ya constitutional law. someni kitabu chake.

Hata awe na vitabu Mia. Tunampima sasa kwa utumbo wake anaoeleza Bungeni. Upo hapo.
 
Tunafanya kosa kufikiri kwamba tutaendelea kuwang'ang'aniza wazanzibar wabaki kwenye muungano huku tukiwatukana. Ipo siku CCM na CUF huko Zanzibar watatufanyia kitu mbaya na ndio utakuwa mwisho wa huu muungano.

Haya ni maneno ya busara.
 
Ngekewa,

Ukisha ruka ruka weeeeeeeee, naomba ujibu maswali yangu ukitulia.

Asante
 
Lakini kisichofahamika hapa Wazanzibari si WANA HAKI ya kuamuwa wanachotaka basi na waachiwe waamuwe. Mtaendelea kuwaamulia mpaka lini?
Kwa akili yangu ndogo nahisi kutokana na wasifu mnaowapa Wazanzibari ni bora kuwaepuka na sio kuwangangania. Mmekuwa nao kwa miaka 44 mmeshindwa kuondowa ujinga wao, udini wao, uharamia wao, kutothamini fadhila mnazowapa, kuwalinda mnakowalinda na faida chungu mzima mnazowapa lakini bado wana msimamo mwengine BASI BORA KUWAACHIA WATOKOMEE.
Kuendelea kuwangangania huko mkiwatukana SI USTAARABU ambayo ni tabia yenu.

Kwa nini wangoje ruhusa au kuachiwa na hao watanganyika? Wao wanaoona wanaonewa na hawapendwi si waseme tu wazi kuwa huu Muungano sell-by date yake imeishapita! Si kujificha nyuma ya vijineno visivyo na maana. Watamke, na kama kweli wanawazungumzia wazanzibari walio wengi, sioni sababu hoja yao ishindwe. Sidhani kama watanganyika wana ubavu wa kuwang'ang'ania wazanzibari walioamua kuondoka. Si zama hizi!
 
Reverend na wenzio (wakiwemo Dr. Mwakiyembe na waheshimiwa wengine) na nyinyi mnaonyesha dhahiri kuwa hamuelewi Katiba ya Zanzibar. Hamuelewi Nini wajibu wa Baraza la Wawakilishi na majumbe wa Baraza la Wawakilishi, Hamuelewi nini wajibu na majukumu ya Rais wa Zanzibar na Baraza lake la Mawaziri kwa wananchi wa Zanzibar. Jifunzeni hayo kabla ya kushupalia kupayuka tu na kusisitiza misimamo yenu. Jamhuri ya Muunagno wa Tanzania ina madaraka yake nba mipaka yake, Na Zanz\ibar ina mipaka yake na madaraka yake. Sijui Tanganyika (Tanzania Bara) ambayo hamuelewi kama ipo ama imezimia.
 
Unajua sometimes Kikwete huwa anajaribu kufikiri sawa ingawa sio wakati wote, siku moja alimuambia Shamuhuna kuwa atamnyanga'nya vingora maana inaonekana vinampa taabu sana, kumbe alikuwa na ukweli,

Sasa anajua kuwa Muungwana yuko kwenye line na Bilali, kwa hiyo yale ya yeye na mtandao yameisha, amesahahu kuwa hata nafasi ya Deupty Waziri Kiongozi haipo kwenye katiba za Jamhuri au Visiwai, ila kilianzishwa tu kwa makubaliano kati ya Muungwana na Karume, kumsitiri Shamuhuna baada ya Mkapa kumgomea kuwa Makamu wa Rais wa Bara,

Mwakyembe anahitaji hongera kwa kuweka ukweli wazi bila kumuogopa huyu former Mtandao, can you imgine huyu ndio angkeuwa makamu wa rais wa Jamhuri? Damn! Halafu eti antaka kuwa rais wa Visiwani?

Mkuu wa Medani! Shamhuna VP?!!!!!!!!! Was it planned by JK and his Team or?

Tunashukuru kusikia haya ila bado hilo halimnyimi nguvu ya kupiga kelele , mind u mtaalam ana machungu ya kutoswa NEC hivyo the only way ya yeye ku survive ktk siasa za Zenj ni kugusa area zote sensitive kila anapopata mwanya.

Tuipende nchi yetu kwa hoja za kujenga na si kutishana.
 
Mkuu Field Marshall ES.

Nakuongezea... President wa Zanzibar... ni mjumbe wa Baraza la Mawaziri la Muungano.

Mkuu Kasheshe,

Hivi ndivyo nijuavyo siku zote, na ndio maana Salimin alipokuwa rais wa Zanzibar kwa kushauriwa na Raza, hakuhudhuria kikao hata kimoja cha Baraza la Mawaziri kwa kutokubaliana na hiki kipengere cha kwenda cabinet kama waziri, lakini hakujaribu hata mara moja kuibadili hii sheria,

Wa-Zanzibari wasitutingishie kibiriti sisi wananchi wa bara on this ishu ya Muungano, kwa sababu we have absolutely nothing to do na hiyo misery yao na Muungano, sisi wananchi sio viongozi kwamba watatu-bully kama walivyowafanyia viongozi wa CCM Butiama,

Nyinyi wananchi wa Visiwani, get this straight kwamba Zanzibari ni mkoa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kama mnataka kuibadili hiyo inabidi mtumie sheria sio kupiga piga makelele kwenye migahawa na kashata, sisi huku forum hatuwezi kuwasaidia anything, kwa sababu hapa tuna mawe tu na fimbo hatuna peremende, wala tende, nendeni mkapigie kelele viongozi wa juu huko CCM.

Ahsanteni Sana.
 
MAMBO sivyo yalivyo BABA, MATAKWA YAKO YAWEKE KWAKO.

Mkuu it not about matakwa yangu au yako, ni about sheria kupiga kelele zako hapa forum ni the wrong place, sisi wananchi wa Bara pia tumechoshwa na never ending nonesense, matakwa yako kwenye muungano hayawezi kutatuliwa hapa forum hata urushe maneno kiasi gani, hapa utapewa facts tu za muungano kama zilivyo,

Nazo ni kwamba nchi yako ni mkoa ndani ya muungano, FULL STOP!
 
Back
Top Bottom